Wednesday, May 21, 2008

Kifo cha Ballali kichunguzwe - Dk. Slaa

Dk. Wilibrod Slaa, Mwanasiasa wa kwanza kuzitaja hadharani tuhuma zilizokuwa zinamkabili aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), marehemu Daudi Ballali, ameibuka na kutaka uchunguzi wa kina ufanyike dhidi ya kifo alichokiita cha kutatanisha cha Ballali.
Dk. Slaa anasema kuwa mazingiya kuugua, kuondoka nchini, kulazwa nje na hatimaye kifo cha Ballali, yanatatanisha na kuacha maswali mengi sana yanayohitaji majibu ya uhakika ili kuondosha wingu la wasiwasi kutokana na kifo hicho.
Dk. Slaa, ambaye ni Mbunge wa Karatu ambaye akiwa Bungeni aliwahi kuziorodhesha tuhuma dhidi ya Ballali na mkewe Anna Muganda, alisema kuwa anaamini kuwa Ballali alipelekwa Marekani kwenda kufichwa ili asitoe siri ambazo iwapo angezisema hadharani, zingewaweka pabaya viongozi wengi pamoja na serikali yenyewe.
Kwa maana hiyo, alisisitiza kuwa kifo cha Ballali, bado kinaielemea serikali, ambayo mlolongo wa matukio, unaonyesh kuwa haikuwa tayari kutoa habari za uhakika kuhusiana na mtumishi huyo wa ngazi za juu serikalini.
Alisema inashangaza kuwa kifo hichokimetokea wakati rekodi zikionyesha kuwa serikali haifahamu Ballali alikuwa wapi hasa, lakini wakati huohup kukiwa na taarifa kwa serikali hiyo hiuyo ilituma makachero wake Marekani kwenda kuchunguza nyendo za maisha ya Ballali.
Aidha, Dk Slaa alisema serikali hadi sasa haijakiri hadharani iwapo kweli iliwatuma makachero hao hasa ikizingatiwa kuwa taarifa byibgibe zilibainisha kuwa kamati iliyopewa kazi ya kuchunguza wizi wa shilingi bil 133 za EPA, nayo iliripotiwa kwenda Marekani kumhoji Ballal.
"Haiwezekani katika kipindi cha wiki moja ,akachero waende kumfuatilia Ballali, halafu katika kipindi cha wiki hiyo hiyo Kamati iende kumhoji na baadaye zikavuma taarifa kupitia katika mtandao kuwa Ballali amefariki kabla haijathibitishwa kuwa kweli amefariki.
"Hapa lazima kuna kitu fulani kimefanywa na kinafichwa ili watanzania wasikifahamu. Na ndio maana nasisitiza uchunguzi wa kina ufanyike dhidi ya kifo hiki cha kutatanisha," anasema Dk. Slaa.

Ballali afariki

(Habari hii ni kwa hisani ya Tanzania Daima)

*Kuzikwa huko huko Marekani Ijumaa hii
*Serikali kutoa taarifa rasmi ya msiba leo
*Baadhi wanahofia huenda alilishwa sumu

Na Absalom Kibanda


ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) amefariki dunia mwishoni mwa wiki nchini Marekani, Tanzania Daima imethibitisha.

Habari ambazo gazeti hili limezipata kutoka Marekani na Dar es Salaam zinaeleza kwamba, Ballali alifariki dunia Ijumaa iliyopita nyumbani kwake Washington alikokuwa akiishi.

Jamaa wa karibu wa Ballali walioko Dar es Salaam na Washington walilithibitishia Tanzania Daima kuhusu kutokea kwa msiba huo.

“Ni kweli amefariki nyumbani kwake Ijumaa usiku. Na sasa hivi tuko katika maandalizi ya kwenda funeral home (taasisi ya kuandaa shughuli zote za mazishi) kwa ajili ya kuanza kufanya maandalizi kwa ajili ya msiba,” alisema ndugu wa karibu wa Ballali kutoka Washington.

Habari zaidi zinaeleza kwamba, tayari familia ya gavana huyo wa zamani wa BoT imeshaitaarifu serikali kuhusu kutokea kwa msiba huo na kwamba taarifa rasmi kuhusu kifo hicho zitatolewa leo hii.

Ndugu mwingine wa karibu wa Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima majira ya saa 4:00 usiku jana alisema mazishi ya gavana huyo wa zamani wa BoT yanatarajiwa kufanyika Ijumaa hii huko huko Marekani.

Mmoja wa wanasiasa aliye karibu na familia ya Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana alithibitisha pia kupokea taarifa za kifo cha Ballali kutoka kwa mkewe, Anna Muganda.

Ndugu mmoja wa Ballali alipoulizwa na Tanzania Daima sababu za kushindwa kutangazwa kwa taarifa za kifo hicho mapema alisema walilazimika kufanya hivyo ili wapate fursa ya kuwasiliana na serikali kwanza na kisha ndugu, jamaa na marafiki wa familia yao kabla ya habari hizo kusambazwa.

Kifo hicho cha Ballali ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Jakaya Kikwete Januari mwaka huu zimekuja siku chache tu baada ya serikali kupitia Ofisi ya Rais Ikulu kutangaza kwamba ilikuwa haimtafuti gavana huyo wa zamani wa BoT.

Baadhi ya jamaa za Ballali waliozungumza na Tanzania Daima walisema kulikuwa na wasiwasi kwamba kifo cha gavana huyo wa zamani wa BoT kikawa kikawa si cha kawaida.

“Kuna wasiwasi kwamba huenda alilishwa sumu wakati akiwa nchini mwaka jana na hili limekuwa likizungumzwa sana ndani ya familia,” alisema mmoja wa jamaa za karibu wa Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana.

Taarifa za kuwapo kwa wasiwasi wa Ballali kulishwa sumu zilipata kusikika mwaka jana na wakati fulani ilielezwa kwamba alipelekwa Marekani kwa matibabu kutokana na sababu hizo.

Tamko hilo la serikali lilitolewa mbele ya waandishi wa habari na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salvatory Rweyemamu.

Rweyemamu alisema kuwa serikali ina mkono mrefu na iwapo itafikia hatua ya kumtafuta gavana huyo wa zamani wa BoT ili aje atoe maelezo yake kuhusu wizi wa zaidi ya shilingi bilioni 133 uliogundulika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) haitashindwa kamwe kumfikia alipo.

Alisema kutokuwepo nchini kwa Ballai, au kutojulikana alipo, si jambo linaloisumbua serikali kwa sasa kwa sababu hivi sasa yeye ni raia wa kawaida, hivyo anao uhuru wa kuishi popote anapopenda.

“Serikali haimtafuti Ballali (kwa sasa), lakini ikiamua kufanya hivyo haitashindwa. Kwanza ni private citizen (raia huru) siyo mwajiriwa wa serikali tena,” alisema Rweyemamu na kuongeza kuwa, mkono wa serikali ni mrefu hautashindwa kumpata Ballali iwapo itamhitaji.

Akifafanua zaidi, alisema baada ya kutenguliwa kwa uteuzi wake, serikali iliunda timu ya kuwachunguza watuhumiwa wa EPA, kuhakikisha fedha zilizoibwa zinarudi na kuwachukulia hatua waliohusika, akiwemo Ballali.

Alisema: “Ninachofahamu ni kwamba, timu iliyopewa kazi kuhusu ubadhirifu wa EPA inaendelea na kazi yake na tunaona jinsi fedha zinavyorudishwa.”

Mkurugenzi huyo pia alikiri kwamba serikali haifahamu hospitali aliyokuwa akitibiwa Ballali, licha ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo, kukaririwa akisema alimtafuta Ballali bila mafanikio alipokuwa jijini Washington, Marekani.

“Kwa kweli sifahamu hasa Ballali alikuwa akitibiwa katika hospitali gani, lakini najua alikuwa nchini Marekani katika Jimbo la Boston, ila hospitali kwa kweli siijui.

“Lakini huyu ni mtu huru hivyo anaweza kuishi popote… huyu ana nyumba yake nchini Marekani… yupo huko anaishi na familia yake,” alisisitiza Rweymamu katika ufafanuzi wake.

Wiki iliyopita, ikiwa ni siku chache tu baada ya taarifa hiyo ya Ikulu, vyombo kadhaa vya habari viliandika habari zilizokuwa zikieleza kuwa makachero kutoka hapa nchini, walikuwa wamekwenda nchini Marekani katika miji ya Boston na Washington kufuatilia nyendo na maisha ya gavana huyo wa zamani.

Kwa mujibu wa habari hizo, ambazo zilikariri taarifa za ndani kutoka serikalini, makachero hao walikuwa wamekwenda huko ili kujua mahali anakoishi ili wakati wa kumhitaji utakapofika iwe rahisi kumpata.

Ballali aliondoka nchini, Agosti mwaka jana kwenda Marekani kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kwa matibabu, na tangu wakati huo taarifa zake zilikuwa ni zenye utata mkubwa.

Mara ya mwisho kwa Ballali kuonekana hadharani ilikuwa ni Julai 12 mwaka jana alipozungumza na wanahabari na akasema alikuwa hatarajii kujiuzulu wadhifa wake kutokana na kukabiliwa na tuhuma za ubadhirifu.

Katika mkutano huo, Ballali alisema madai ya ubadhilifu yanayotolewa dhidi yake ni uzushi na uongo mtupu.

Huku akionekana kujiamini alisema; “Niko Comfortable, moyo wangu mweupe, ari yangu ya kazi iko juu kwani tuhuma hizo ni uongo na uzushi mtupu na siwezi kujiuzulu kwa tuhuma zisizo na ushahidi.

“Tuhuma zote dhidi yangu ni za uongo mtupu. Kwanza sijui zimetoka wapi, nani mtunzi na kwanini amefanya hivyo. Hilo tunawaachia wanaofanya uchunguzi na naamini siku moja atajulikana na ukweli utajulikana, lakini mimi siwezi kujiuzulu kwa mambo ya uzushi,” alisisitiza.

Kashfa ya BoT kupitia mtandao wa Internet, uliibuliwa mara ya kwanza Bungeni na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa (CHADEMA).

Akichangia maoni ya kambi ya upinzani wakati wa mjadala wa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Fedha, Dk. Slaa alisema kambi ya upinzani imefarijika baada ya Waziri wa Fedha kukiri kufahamu taarifa aliyoitoa Bungeni kuhusu ubadhirifu mkubwa ndani ya BOT unaomgusa Ballali, pamoja na wafanya biashara wengine wakubwa akiwemo Mbunge wa Kwela, Dk. Chrisant Mzindakaya (CCM), kupitia kampuni anayoimiliki.

Dk. Slaa alisema Dk. Mzindakaya alichukua mkopo kwa shughuli za kampuni yake ya SAAFI wa sh 6.217 bilioni, uliogawanyika kama ifuatavyo.

Alisema aliomba ‘Overdraft facility ya 450 millioni zitakazolipwa kwa miaka 5; mkopo wa shs 2.8 bilioni zitakazolipwa katika miaka mitano; na Dola za Marekani 2.528. Jumla yote ni Bilioni 6.217.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, fedha zote zilikopwa Benki ya Standard Charter na Benki Kuu ilitoa (Guarantee) mdhamana wa asilimia 100. Mwaka huu wa 2007 Benki kuu kutokana na Mdhamana huo tayari imelipa kiasi cha sh 8.1 Billion kwa niaba ya Mzindakaya na fedha hizo pamoja na riba zinakisiwa kufikia 9.7 billioni hadi sasa (Hati ref. CIBD-14662 ya tarehe 24 May, 2007, na mkopo kutolewa 2005. Kutokana na tuhuma hizo, Meghji wakati akifanya majumuisho ya hoja yake, alisema Serikali imeagiza kuanza kufanyika kwa uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika akaunti ya madeni ya biashara ya nje zinazoikabili Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Alikiri serikali kupata taarifa za kuwapo kwa vitendo vya rushwa na nyingine za matumizi mabaya ya fedha katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Waziri Meghji alisema, tayari alikuwa ameshamwagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali, kuanza uchunguzi kuhusu tuhuma hizo. Meghji alisema, serikali ilikuwa ikitarajia kukamilisha kazi hiyo na taarifa kamili ya uchunguzi huo kutangazwa ifikapo mwishoni mwa mwaka huu. Mbali ya BoT kutuhumiwa kutumia fedha nyingi kuliko inavyostahili katika ujenzi wa majengo yake mapya ya ‘minara miwili pacha’ (Twin Towers), kiasi cha Dola za Marekani milioni 30.8 sawa na shilingi bilioni 40 kinatuhumiwa kufujwa katika akaunti ya madeni ya biashara ya nje. Taarifa zinaonyesha kuwa, wakopeshaji wa kimataifa kutoka nchi 12 waliingia mkataba wa kusimamia akaunti hiyo na kampuni ya Kitanzania ijulikanayo kwa jina la Kagoda Agriculture Ltd kati ya Septemba na Novermba mwaka jana. Uchunguzi wa awali wa wakaguzi wa nje wa mahesabu ya akaunti hiyo unaonyesha kuwapo kwa mazingira yenye utata mkubwa unaozingira makubaliano kati ya wakopeshaji na kampuni hiyo iliyolipwa dola milioni 30.8. Akichangia hotuba ya Waziri Mkuu, Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe (CHADEMA) alihoji kwa nini Serikali ilikalia kimya suala la kashfa ya BoT mara baada ya habari za kashfa kutangazwa kupitia mtandao wa internet tangu Novemba 2006 na kuonya kuwa hali hiyo inaathali kubwa kiuchumi iwapo kashfa kama hizi zinaachwa bila ya ufuatiliaji wa serikali. Taarifa za awali za uchunguzi huo zinaonyesha kuwa, BoT ilifikia hatua ya kuipa kampuni hiyo fedha zote hizo ikidai kuingia mkataba na wakopeshaji hao katika mazingira ambayo nyaraka zilizopatikana zinaonyesha kuwa na hitilafu nyingi. Miongoni mwa hitilafu zilizobainishwa katika uchunguzi wa awali ni, kukosekana kwa karatasi rasmi zenye majina ya makampuni hayo ya kimataifa.
Mwisho

Monday, May 19, 2008

Karume Kichwangumu

Rais wa Zanzibar, Amani Karume, amesema hawezi hivi sasa kuwateua mawaziri katika baraza lake kutoka chama cha upinzani kwa sababu katiba hairuhusu.
Akizungumza na waandishi wa habari Ikulu, alisema kuwa katiba iliyopo na mfumo wa utawalauliopo hautoi nafasi kwa yeye kuwateua mawaziri kutoka upinzani.
Alisema kuwa katika uchaguzi wa mwaka 2005, Pemba alipata kura 20,000 na waliwachagua wanaCCM wawili kuwa wawakilishi na tayari wameshaingizwa katika baraza ,a mawaziri na kuhoji hao wanaowataka wapemba waingizwe kwenye baraza watatokea wapi?
Aidha, aliwashangaa CUF kwa kukataa sualalakura ya maoni, akisema kuwa ushirikishwaji wa wananchi ni jambo muhimu ambalo linapiganiwa na kila mtu.
Aliwataka waandishiw a habari aliokuwa akizungumza nao kuwaelimisha CUF kuwa hali ya mambo haipo kama wao wanavyofikiri na kuwa madai yao ya kushirikishwa katika serikali hayana msingi kwa sababu hata sasa wanashirikishwa katika serikali kupitia baraza la wawakilishi.
Akifafanua kuhusu kura ya maoni, alisema kuwa si lazima Tume ya Uchaguzi Zanzibar isimamie kura hiyo na pia haitaubdwa tume maalum ya kuisimamia lakini akahakikisha kuwa kila Mzanzibari atashiriki kupiga kura.
Aidha, rais Karume amesema kuwa milango ya Ofisi yake ipo wazi kwa mtu yeyote mwenye shida kwenda.
Hata hivyo, alisema kuwa iwapo Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, anataka kuonana naye kama vilealivyomuomba Rais Jakaya Kikwete awakukutanishe, anapaswa kanza kumtambua yeye kuwa ni rais.

Sunday, May 18, 2008

CCM, CUF watwangana

Wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wale wa Chama cha Wananchi (CUF) katika jiji la Tanga wametwangana mangumi baada ya kutokea kutoelewana baina yao katika mkutano wa kisiasa.
watu kadhaa wmejeruhiwa katika mapigano hayo, yaliyowalazimisha polisi kurusha risasi hewani ili kuwatawanya watu, yalitokea katika Barabara ya 20, wakati wafuasi wa CUF walipoandaa mkutano wa hadhara katika eneo ambalo lipo karibu na opfisi za CCM katika mtaa huo.
Taarifa zinasema kuwa CUF walipewa kibali na Polisi kufanya mkutano huo ambao ulikuwa uhutubiwe na mmoja wa viongozi wa juu wa chama hicho, said Miraji.
Mara baada ya kupata taarifa kuwa CUF watafanya mkutano katika eneo hilo, CCM nayo ilijiandaa kukabiliana na hali hiyo. Waliweka maspika makubwa katika eneo la ofisi zao na kuanza kutangaza masuala yanayohusu chama chao.
Baada ya wafuasi wa CUF kukusanyika kwa ajili ya mkutano huo, kijana mmoja mfuasi wa chama hicho, alitakiwa kupanda jukwaani ili kutoa hotuba, kabla Miraji hajakaribishwa rasmi kumwaga sera za chama hicho.
Baada ya kuona hivyo, CCM nao walimchukua baba wa kijana aliyekuwa katika jukwaa la CUF, na kumtaka aeleze masuala kuhusu CCM. lakini inaelekea katika maelezo yao, walianza kushambuliana jambo lililoamsha hasira za wanachama waliokuwa wakisikiliza hotuba hizo za baba na mwana kutoka majukwaa tofauti yaliyo jirani.

Friday, May 16, 2008

Serikali Kudhibiti Bei ya Mafuta

Kuendlea kupanda kwa bei ya mafuta kumeilazimisha serikali kutekeleza kilio cha muda mrefu cha wananchi, walioiyaka kuhakikisha inaweka mfumo utakaosaidia kudhibiti bei ya mafuta. Kwa muda mrefu serikali imekwua ikikataa kufanya hivyo, kwa madai kwua inaogopa kuonekana kuwa inaingilia biashara iliyo katika mfumo wa soko huria.
Lakini sasa serikali imeshtuka kwua nkuna uwezekano na yenyewe 'inaliwa' katika soko la mafuta. hivyo, Wizara ya Nishati na Madini iliamua kuchukua uamuzi wa kuwakutanisha wadau wote katika sekta ndogo ya mafuta ili kupanga mikakati ya kudhibiti bei ya bidhaa hizo.
Kilichoamriwa na kutangazwa na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, ni mpango utakaohakikisha kuwa kunakuwa na utaratibu wa kupanga bei ya mafuta.
Ngeleja amesema kuwa chini ya utaratibu huo,wafanyabiashara wote wanaoagiza mafuta kutoka nje ya nchi,wanatakiwa kupeleka taarifa zao zote kwa Malmaka ya Udhibiti wa Nsiahti na Maji (EWURA).
Alisema kwua EWURA ikishapokea taarifa hizo, zitakazohusisha gharama za ununuzi wa mafuta, usafirishaji, upakuaji na kuhifadhi, itakuwa katika nafasi ya kukadiria bei inayofaa ya mafuta itakayotumika kwa wauzaji wote.
Ngeleja alisema kwua utaratibu huo uemshakubaliwa rasmi na atakayekuwa anakiuka atakuwa anatenda kosa hivyo kustahili kuchukuliwa hatua.

Zanzibar Yatetemesha Muungano

Kile kilio cha muda mrefu cha Zanzibar kutaka nayo ipewe mgawo kutokana na mapato yanayotokana na gesi asilia na mafuta kimefanikiwa. Kufanikiwa kwa kilio hichi kumedhihirishwa kupita kikao cha kamati ya muungano,ambacho baada ya mabadiliko sasa kinashirikisha mawaziri wote kutoka pande zote mbili za Muungano.
Kikao kilichofanyika Ahamisi kilifikia makubaliano kuwa Zanzibar iwe inapata mgawo huo. Inaelekea uamuzi huo ulifikiwa siku nyingi kwani tayari serikali ilishatafuta mshauri mwelekezi atakayelichunguza suala hilo na kuipendekeza njia muafaka ya kugawana mapato yatokanayo na rasilimali hizo.
Waziri wa nchi (Muungano), Muhamed Seif Khatib, amesema kwua tayari mshauri huyo ameshaianza kazi hiyo na anatarajiwa kuwasilisha ripoti yake mwezi Agosti mwaka huu.
Kwa muda mrefu Zanzibar imekuwa ikidai mgawo wa mapato hayo kwa kuwarasilimali hizo zimaeanishwa katika Katiba ya Muungano kama mali za Muungano. Hata hivyo, rasilimali nyingine za ardhini, kama vile madini, hazihusiki katika mgawo huo kwa sabbu hazijaanishwa kwenye katiba kama ilivyo kwa gesi na mafuta.
Aidha, kikaohicho, ambacho kipo chini ya uenyekiti wa Makamu wa Rais, kimeafiki kuoanishwa kwa sheria za kodi baina ya Bara na Zanzibar, baada ya kubainika kuwa wafanyabiashara kutoka Zanzibar wamekuwa wakitozwa kodi mara mbili wanapoingiza bidhaa zao Bara kutokea Zanzibar.
Hata hivyo, imebainika kuwa baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) wamekuwa wakitumia mwanya huo kuwakandamiza wafanyabiashara hao na ndio maana imeazimiwa kuwa sheria za kodi zioanishwe ili iwe inatumika sheria moja tu.
Jambo jingine litakaaloangaliwa katika kuoanisha sheria ni suala la usajiri wa magari, ili kuwaondolea usumbufu watu wa Zanzibar ambao hulazimika kulipia usajiri wa magari yao upya wanapoyaleta Bara, hata kama yalishasajirliwa Zanzibar.

Karamagi Apigwa Chini TICTS

Ni kama vile anaandamwa na mabalaa. Huu ni mwaka wa taabu kwa Nazir Karamagi, waziri wa zamani wa Nishati na Madini aliyelazimika kujiuzulu kutokana na kashfa ya Richmond. Hivi sasa Karamagi ameondolewa kuwa Mwenyekiti katika bodi ya Kampuni ya Kupakia na Kupakua makontena Bandarini (TICTS) ambako anamiliki asilimia 30 ya hisa.
Mabosi wa kampuni hiyo walitangaza kuwa Karamagi anaondolewa katika nafasi hiyo kama njia ya kurekebisha mahusiano mabaya yaliyopo baina ya kampuni hiyo na serikali.
Habari kutoka TICTS zinaeleza kuwa Karamagi ataendelea kubakia na hisa zake 30 lakini taarifa ambazo hazijathibitishwa zinaeleza kuwa mipango ipo mbioni kumnunua Karamagi ili kumuondoa kabisa katika kampuni hiyo.
Maelewano mabaya baina ya kampuni hiyo na serikali yalianza baada ya watu akuanza kuhoji jinsi serikali ya awamu ya tatu ilivyorefusha mkataba wa kampuni hiyo. awali, mkataba huo ulikuwa wa mkaoa 10 lakini uliongezwa kabla haujaisha na kuufanya uwe wa miaka 25.
Inaaminika kuwa Karamagi ndiye aliyewashawisho viongozi wa awamu ya tatu kurefusha mkataba huo, na tangu hapo wananchi wengi wamekuwa wakimchukulia Karamagi kama mnyonyaji kwa kuiingiza nchi katika mkataba huo ambao hautoi nafasi rahisi kwa mtu mwingine kujiingiza kwenye biashara hiyo.
Balaa la kuondolewa uenyekiti wa bodi ya TICTS kwa Karamagi, limekuja wakati bado anasubiri hatima ya 'kesi' aliyojizushia Bungeni baada ya ksuema kuwa uamuzi wa kurefusha mkataba wa TICTS ulifanywa na baraza la mawaziri.
Kwa kuwa Karamagi hakuwa mjumbe wa baraza hilo wakati mkataba unarefushwa, Bunge lilimtaka awasilishe ushahidiw a kauli aliyoitoa lakini siku chache baada alishindwa kufanya hivyo na kujitetea kuwa nyaraka za Baraza la Mawaziri ni siri hivyo ahawezi kuziwasilisha.
Spika alikataa utetezi huo na kumpa muda zaidi Karamagi ahakikishe anawasilisha utetezi wake. Imesharipotia kuwa tayari Karamagi ameshawasilisha utetezi wake na sasa anasubiri 'hukumu' yake.

Dk. Slaa Kidedea

Mbunge wa Karatu, Dk. Wilibrod Slaa (Chadema) ameshinda kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Akitoa hukumu ya kesi hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, jaji Robert Makaramba alizitupilia mbali hoja zote zilizotolewa na walalamikaji hao akisema kuwa hazina msingi.
Katika kesi hiyo, walalamika walidai mahakamani hapo kuwa msimamizi wa uchaguzi huoalikiuka taratibu kadhaa ambazo zilisababisha mgombea wao, Patrick Tsere, ashindwe.
Aidha, walalamika walidai kuwa kulikuwa na kura za mgombea waozilizoibwa na iwapo angepatiwa angeweaa kuibuka mshindi.
Katika dai jingine, waliieleza mahakama kuwa Msimamizi wa uchaguzi huo hakutangaza matokeo kwa sauti kubwa, jambo lililowafanya watilie shaka matokeo yaliyotangazwa. Pia walisema kuwa msimamizi huyo alitangaza matokeo ya jumla kabla vituo vingine havijawasilisha matokeo rasmi. Walidai pia kuwa msimamizi alitumia fomu tofauti kutangaza matokeo hayo.
lakini katika uamuzi wake, Jaji Makaramba alisema kuwa hoja hizo hazina msingi kwa sababu hazionyeshi ni jinsi gani zimemuathiri mgombea aliyeshindwa.
Alisema pia kuwa suala la kuibiwa kura, lilitokea pia hata kwa Dk. Slaa na aiwapo na yeye angepewa kura alizopunjwa, kama ilivyojionyesha kwenye vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo, bado angebakia kuwa mshindi hata kama mgombea wa CCM angepewa kura anazodai 3000.
Hata hivyo, Jajialikataa ombi la wakili wa utetezi, Tundu Lissu, kuomba walalamikaji na mawakili wao wafunguliwe mashitaka ya kuidanganya mahakama kwa kuleta vielelezo vya uongo mahakamani kama ilivyothibitika wakati wa kusikiliza kesi hiyo.
Jaji alisema kuwa suala la kuthibitisha nyaraka za kughushi lipo chini ya Jeshi la Polisi hivyo ni vema wakaachwa walishughulikie suala hilo na iwapo itaonekana kuwa watu hao wametenda kosa fulani, wachukuliwe hatua zinazostahili.

Wednesday, May 14, 2008

CUF wafichua siri ya mazungumzo

CHAMA cha Wananchi (CUF), kimerusha makombora mazito ya lawama dhidi ya mahasimu wao, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikiibua shutuma mpya ambazo hazikupata kuwekwa hadharani kabla.
Katika hatua inayoonyesha kuendelea kujikita kwa hali ya uhasama wa kisiasa kati ya vyama hivyo viwili, CUF imefikia hatua ya kuwahusisha viongozi wakuu wa CCM hususan wale wa Zanzibar kuwa na uhusiano wa moja kwa moja wa kikazi na kinasaba na chama cha kisultani cha Hizbu.
Kauli hizo nzito za CUF zilitolewa jana Buguruni, jijini Dar es Salaam mbele ya wana habari na viongozi wa juu watatu wa chama hicho, Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa ameongozana na Katibu Mwenza wa Kamati ya Pamoja (na CCM) ya Mazungumzo ya Muafaka, Ismael Jussa Ladhu na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho (Zanzibar), Juma Haji Duni.
Katika mkutano huo wa jana, viongozi hao wa CUF walisambaza miniti za vikao vyao vya siri na CCM ambazo zinaonyesha kuwa mazungumzo ya kutafuta ufumbuzi wa kisiasa Zanzibar kati ya vyama hivyo viwili yalikamilika, tofauti na ilivyoelezwa juzi na viongozi wa juu watatu wa CCM walioongozwa na Katibu Mkuu, Yussuf Makamba.
Akizungumza kwa kujiamini, Jussa, mmoja wa viongozi wenye ushawishi ndani ya CUF, aliwataja Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi na mke wa Rais wa Zanzibar, Shadya Karume, kuwa wana CCM wawili wenye uhusiano ama wa kikazi au kinasaba na chama hicho cha kisultani cha Hizbu.
Jussa ambaye alikuwa akikanusha madai ya kada mkongwe wa CCM aliyepata kuwa msoshalisti kiitikadi, Kingunge Ngombale-Mwiru, aliyeihusisha CUF na U-Hizbu, alisema chama hicho tawala ndicho ambacho kina historia ya kuwa na uhusiano na chama hicho cha kisultani.
Alisema inapofika mahali mtu mzima kama Kingunge akasema uzushi, ni dhahiri chama hicho (CCM) kimefikia mahala pagumu na kimepoteza dira na mwelekeo.
“CCM ndiyo ina sifa zote za mahusiano na Hizbu, na si CUF. Na kwa msingi huo, kama kuna hoja pia ya kurudisha Waarabu, hilo linapaswa kuhofiwa kutoka CCM na si kutoka CUF.
“CUF kiliasisiwa mwaka 1992, na viongozi wake wanne wakuu kutoka Zanzibar ni Seif Sharif Hamad, Ali Haji Pandu, Shaaban Khamis Mloo na Machano Khamis Ali. Wote ni wana-ASP wasio na chembe ya shaka.
“Lakini mawaziri wa Zanzibar wa hivi sasa, yupo ambaye anajulikana kuwa alikuwa mwanachama wa Hizbu. Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Mansour Yusuf Himid, ambaye ni ndugu wa mama mmoja na Shadya Karume, mke wa Amani Karume, wote wawili ni wajukuu wa Sheikh Mohammed Salim Jinja, ambaye alikuwa mwasisi wa Hizbu na ambaye wenyewe Hizbu wakimwita ‘‘Founding Father of Zanzibar Nationalism,” alisema Jussa.
Pia alisema yupo waziri mmoja katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar ambaye amekuwa akiandika makala katika magazeti kuipinda CUF, alipata kuwa mwanachama wa Umoja wa Vijana wa Hizbu uliokuwa ukijulikana kama Youth Own Union (YOU).
Ingawa hakumtaja kwa jina, waziri anayetoka Zanzibar ambaye amekuwa akiandika makala kuiponda CUF kupitia magazetini ni Muhammad Seif Khatib, ambaye sasa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano.
Khatibu kabla ya kuingia serikalini alipata kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (zamani UVT) kwa muda mrefu, miaka ya 1980.
Mbali na hao, alisema viongozi wastaafu, kama Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi na Spika mstaafu wa Baraza la Wawakilishi, Mzee Ali Khamis Abdallah, baada ya Uhuru wa Desemba 1963 (miezi kadhaa kabla ya mapinduzi ya Januari 12, 1964) waliteuliwa na serikali ya Hizbu kuwa makatibu wa kwanza (First Secretaries) wa Ofisi za Kibalozi za Zanzibar huko Indonesia na Misri.
“Ni bahati mbaya sana kwamba lugha zinazochochea ubaguzi na kujidai kuwakataa ma-Hizbu zilizotolewa katika Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM hazikukemewa hata na Mwenyekiti wa CCM mwenyewe.
“Ulitumiwa Uhizbu kukataa ufumbuzi wa kudumu wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar wakati hao waliokuwa wakiwakataa ma-Hizbu ndio ma-Hizbu wenyewe,” alisema Jussa katika kauli inayoweza kuamsha mtazamo mpya wa siasa za Zanzibar siku zijazo.
Kutokana na hayo, Jussa, aliwataka wana CCM kutambua kuwa, uzushi na upotoshaji hauwezi kukisaidia chama hicho tawala ambacho alisema sasa kimeanza kupoteza kwa kasi, uhalali wa kisiasa kama chama chenye dira na mwelekeo nchini.
Alisema CCM inapaswa ijirudi, ikiwa ni pamoja na kujisahihisha kama inataka ikubalike kuwa ni chama makini mbele ya macho ya Watanzania na jumuiya ya kimataifa.
“Kujidanganya kwamba wataendelea kufanya mchezo wa kitoto wa mazungumzo yasiyokwisha na baadaye kufikia miafaka ambayo hawana nia ya kuitekeleza sasa, hakuwasaidii tena, maana Watanzania wameamka.
Zanzibar kuna tatizo kubwa la kisiasa ambalo linahitaji kupatiwa ufumbuzi wa kweli, makini, wa dhati na wa haki.
“Ni lazima pia tuseme tumesikitishwa sana na kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kukaa kimya wakati chama chake kikichezea shere suala zito linalohusu mustakbali wa taifa kama hili linalohusu mpasuko wa kisiasa Zanzibar,” alisema Jussa.
Huku akitumia msemo usemao: ‘Sadaka huanzia nyumbani’, Jussa alisema Watanzania wanahitaji kumuona Kikwete akiifanyia kazi Zanzibar, kwa mfano ule ule wa anavyojishughulisha na masuala ya Kenya, Comoro, Zimbabwe na hivi karibuni mgogoro wa DRC Kongo na Uganda.
Kuhusu mazungumzo yao ya muafaka, huku akisoma miniti zote za vikao vyao na CCM, Jussa alisema, wamefikia hatua hiyo ili kuweka kumbukumbu sahihi za mwenendo mzima wa mazungumzo baada ya kufedheheshwa na upotoshaji wa makusudi wa CCM.
Akitumia nakala za kumbukumbu za vikao hivyo zilizokuwa katika buku hilo lililopewa jina la ‘Ukweli unaofichwa na CCM kuhusu mazungumzo ya muafaka’, Jussa alisema kwa makusudi CCM wameamua kuficha ukweli wa mazungumzo hayo, na kuihusisha na tuhuma nzito CUF na viongozi wake, akiwemo Katibu Mkuu, Seif Sharif Hamad.
Kuhusu kukamilika kwa mazungumzo hayo, Jussa alisema Kamati ya Mazungumzo ya CCM inawapotosha wananchi na jumuiya ya kimataifa kwamba mazungumzo hayakukamilika.
Alisema katika kikao cha mazungumzo kilichowashirikisha makatibu wakuu wa CUF na CCM cha Januari 21 mwaka huu, pamoja na mambo mengine, wajumbe wa pande zote mbili walikubaliana mwishoni mwa mwezi huo, lazima wawe wamepeleka taarifa ya mwisho ya mazungumzo hayo na kupatiwa maamuzi.
“Ujumbe wa CUF ulishauriwa kwa sasa usitishe hatua ya kufikisha taarifa ya mazungumzo katika vikao vyake, ili kusubiri mazungumzo yakamilike na baadaye vyama vyote viwili viwasilishe taarifa hiyo katika kipindi kimoja,” alisema Jussa akinukuu kumbukumbu za kikao hicho.
Alisema kutokana na hali hiyo, walikubaliana taarifa za mazungumzo ziwasilishwe kwa pamoja katika vikao vyake vya juu baada ya mazungumzo kukamilika.
Alisema CUF na CCM kuwasilisha taarifa ya mazungumzo katika vikao vyao vya Baraza Kuu la Uongozi la Taifa na Halmashauri Kuu ya Taifa Machi mwaka huu, ni ushahidi kuwa mazungumzo yalishakamilika.
Katibu huyo mwenza alisema walikubaliana kwamba mazungumzo hayo yakikwama, itakuwa fedheha kwa nchi na viongozi kutokana na matumaini yaliyojengwa kwa wananchi na jumuiya ya kimataifa.
“Tulikubaliana kwa kuwa mazungumzo yamechukua muda mrefu, hatua zichukuliwe kuyakamilisha ili ikifika Machi 2008 yawe yamemalizika.
“Mazungumzo hayo yalikamilishwa katika kikao cha 20 cha Februari 24 – 29 mwaka huu, ambapo ajenda namba tano ilijadiliwa. Ni bahati mbaya kwamba kwa sababu hakujafanyika tena vikao vya mazungumzo kutokana na ubabaishaji uliofanywa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM huko Butiama, hakujakuwa na kumbukumbu za kikao hicho zilizopitishwa rasmi,” alisema.
Alisema kama kuna ajenda iliyobaki ambayo haijajadiliwa, hiyo itakuwa agenda ya sita iliyozushwa na CCM inayohusu kura ya maoni.
Kuhusiana na kuwepo kwa rasimu ya makubaliano, alisema kamati ya mazungumzo ya CCM iliwapotosha wananchi kwamba hakukuwa na rasimu ya makubaliano iliyokubaliwa na CUF na CCM katika mazungumzo hayo.
Alisema rasimu ya makubaliano ipo na ilipitishwa kwa pamoja na Kamati ya Makatibu Wakuu wa CUF na CCM katika kikao cha mazungumzo cha 18 cha Januari 3-4 mwaka huu.
Jussa, alisema katika kikao hicho, kwanza walikubaliana kupokea rasimu ya makubaliano yaliyofikiwa na baadaye kujadili njia za kujengeana imani.
Alisema Kaimu Katibu wa kamati kutoka upande wa CCM, Dk. Masumbuko Lamwai, kwa niaba ya mwenzake kutoka CUF, aliwasilisha rasimu waliyoitayarisha.
Alisema rasimu hiyo ilikuwa na kichwa cha habari kisemacho: ‘Rasimu ya Makubaliano kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) katika kuupatia Ufumbuzi wa Kudumu Mpasuko wa Kisiasa Zanzibar’.
Aidha, alisema CCM walipotosha kwamba Katibu Mkuu wa CUF aliwapotosha wananchi kwamba katika serikali shirikishi kutakuwepo nafasi ya Waziri Kiongozi ambaye atatoka katika chama kitakachopata ushindi wa pili na kwamba jambo hilo halijakuwepo kabisa katika makubaliano.
Pia alisema CCM ilipotosha kuwa hakuna makubaliano kuwa serikali ya pamoja itaanza baada ya kutiwa saini makubaliano.
“Wajumbe wa CCM wamepotosha kwa makusudi suala hili. Wangetaka kuwa wakweli wangesema kwamba nafasi ya Waziri Kiongozi ilikubaliwa ifutwe katika muundo wa serikali shirikishi ambayo ilikubaliwa itaanza mwaka 2010.
“Hata hivyo, katika mazungumzo, ilikubaliwa kuwa CUF ishirikishwe katika Serikali ya Zanzibar katika kipindi hiki (baada ya kutiwa saini makubaliano ya mwafaka), ambapo serikali itaendelea kuwa na muundo wake kama ulivyo sasa.
“Hata hivyo, katika kipindi hiki cha kuelekea 2010, kuwe na njia za kujengeana imani ambazo katika hatua za kisiasa zitajumuisha na Rais wa Zanzibar aliyepo madarakani kuteua mawaziri kadhaa kutoka CUF, ili waingie serikalini,” alisema.
Alisema suala la CUF kuingizwa serikalini kabla ya 2010 yalikuwa ni makubaliano ya Kamati ya Makatibu Wakuu na kwamba mapendekezo ya CUF yalihusu kiwango cha ushirikishwaji na yaliwasilishwa kwa barua kwa Katibu Mkuu wa CCM Januari 22, mwaka huu.
Akifafanua, alieleza katika mapendekezo hayo CUF ilitaka Rais wa Zanzibar na Waziri Kiongozi watoke upande tofauti kati ya CCM na CUF, ili kujenga kuaminiana kwa kweli na kuendesha serikali kwa mashirikiano ya pamoja.
Pia mawaziri wagawiwe kwa idadi, wanane watoke CCM na saba CUF.
Chama hicho kilipendekeza manaibu waziri wanne watoke CCM na watatu CUF kwa utaratibu kwamba waziri na naibu waziri wa wizara watatoka vyama tofauti.
“Pande zetu mbili zilikubaliana kuwa iwapo mapendekezo ya CUF yataonekana yamekwenda mbali, viongozi wa CCM watarudi kwa wenzao wa CUF kuyazungumza kabla ya kuyafikisha kwa viongozi wa dola.
“Pamoja na barua hiyo, hakuna barua au mawasiliano yoyote mengine yaliyowasilishwa kwa CUF yaliyoashiria kutokubalika au kutaka marekebisho katika suala hilo mpaka kikao cha mwisho,” alisema Jussa.
Kuhusu hoja ya kura ya maoni, alisema CUF imeikataa hoja hiyo kwa kuwa haijawahi kuwa miongoni mwa ajenda zilizokubaliwa katika mazungumzo ya kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
Alisema iwapo CCM ingekuwa na nia ya kuwasilisha ajenda hiyo, ingeiwasilisha wakati wa mazungumzo, lakini imefanya hivyo baada ya mazungumzo kwa lengo la ‘kuipiku CUF kisiasa’.
“Mgogoro wa kisiasa Zanzibar kimsingi ni mgogoro uliotokana na kuendeshwa vibaya na kuvurugika kwa chaguzi za mwaka 1995, 2000 na 2005. Katika hali hiyo, uchaguzi kwa njia ya kura ya maoni hauwezi kuwa ufumbuzi wa mgogoro wa uchaguzi bila ya kwanza taasisi zote zinazohusika na masuala ya uchaguzi kufanyiwa marekebisho.
“CCM na CUF wote wanakubaliana kupitia rasimu ya makubaliano kuwa taasisi zote zinazohusika na uendeshaji na usimamizi wa uchaguzi, zikiwemo Tume ya Uchaguzi, Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, vyombo vya ulinzi na usalama na vyombo vya habari vya serikali zina kasoro kubwa ambazo zinahitaji kurekebishwa. Vipi unaweza ukafanya kura ya maoni iliyo huru na ya haki katika hali kama hiyo?” alihoji katibu mwenza huyo.
Hata hivyo, alisema maamuzi makubwa na mazito zaidi nchini yamefanywa bila ya kupigiwa kura ya maoni na kutoa mifano ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964, kufutwa kwa mfumo wa vyama vingi, Azimio la Arusha, kuunganishwa kwa TANU na ASP, kupitishwa kwa Katiba ya kudumu ya Muungano na marekebisho yake yote, kupitishwa kwa Katiba ya Zanzibar ya 1979 na 1984, na muafaka wa kwanza wa 1999 na muafaka wa pili wa 2001.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa CUF ambaye amekuwa mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho mara tatu, Maalim Seif, alisema anaamini Kikwete anaweza kuingilia kati suala hilo na kulimaliza, kwani hajapata kuyumba katika kauli zake.
“Sijui huko Butiama walimroga? Ninavyomjua ana uwezo wa kulisimamia na kulimaliza...bado anayo nafasi na sisi tutampa ushirikiano katika hilo, ” alisema.
Hata hivyo, alisema kamwe chama hicho hakipokei amri za CCM kurejea katika mazungumzo, kwani hali hiyo haiwezekani kamwe.
Alisema kurudi kwenye mazungumzo hayo ni kupoteza muda na kuwahadaa Watanzania.
Maalim, alisema hivi sasa chama hicho kimeanza jitihada za kuzunguka nchi nzima kuwashawishi kunusuru mazungumzo hayo.
“Hivi sasa Profesa Lipumba ameanza ziara za kuzungumza na viongozi wa dini, watu mashuhuri na asasi za kijamii kuhusu suala hilo. Pia tunashirikisha mabalozi mbalimbali katika suala hilo, ” alisema.
Mbali ya hayo CUF walimtaka Rais Kikwete achukue hatua za haraka kuitisha mkutano wa pamoja utakaoshirikisha wadau wakuu wa masuala hayo kwa Zanzibar na kujadili mapendekezo yaliyotolewa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na kisha kuhitimisha makubaliano hayo kati ya vyama hivyo.
Walisema endapo hayo hayatafanyika, CUF itatoa wito kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti, za uhakika na za haraka kuingilia kati suala hilo, ili kuhakikisha makubaliano yaliyofikiwa yanatiwa saini.
“Baada ya Tanzania yenyewe kushindwa katika utatuzi wa mgogoro wake huu wa muda mrefu, sasa ni wakati muafaka kwa jumuiya ya kimataifa kuingilia kati kwa kuhakikisha makubaliano ya dhati yanafikiwa yatakayotoa ufumbuzi wa kweli na wa haki wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
“CUF inatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuepuka fedheha iliyoipata katika nchi nyingine za Kiafrika, ambazo iliziachia hadi hali ikachafuka na ndipo ikaingilia kati. Hali ya Zanzibar ni mbaya. Ilitulia kwa sababu ya matumaini ya Wazanzibari na Watanzania kwamba mazungumzo ya CCM na CUF yataleta suluhisho la utulivu na umoja.
“Makubaliano yaliyofikiwa yanapokosa uongozi wa Rais Kikwete katika kuyakamilisha, yanahitaji kuona jumuiya ya kimataifa inaingilia kati, kwa hatua za wazi na madhubuti kuinusuru Zanzibar na Tanzania isitumbukie kule nchi nyingine za Kiafrika zilikotumbukia, ” alisema.

Hofu Pemba

SIKU moja baada ya maofisa usalama kuingia majumbani na kuwakamata wananchi waliopeleka barua Umoja wa Mataifa kutaka kuundwa kwa serikali shirikishi katika Kisiwa cha Pemba, baadhi ya watu wameingia mafichoni, wakihofia kukamatwa.
Wananchi hao ambao wameingia mafichoni kwa hofu ni miongoni mwa watu 12 waliokwenda Ofisi za UNDP jijini Dar es Salaam, wakitaka umoja huo usaidie utekelezaji wa mchakato wa kuundwa kwa serikali hiyo.
Polisi jana ilithibitisha kuwakamata watu kadhaa na ikasema wanashikiliwa kwa ajili ya mahojiano kuhusu hatua yao ya kwenda UNDP kuomba Pemba ijitenge kutoka Zanzibar.
Watu hao 12 waliwawakilisha wenzao zaidi ya 10,000 walioweka saini zao katika tamko hilo ambalo sasa linachukuliwa kuwa ni lenye dhamira ya kujitenga.
Licha ya Kamishna wa Polisi Zanzibar, Khamis Mohammed Simba, kukiri kukamatwa kwa wananchi hao, hakutaka kutoa maelezo, zaidi ya kuwataka waandishi kuwa na subira akisema chungu bado kiko jikoni kinatokota na kikiiva watapewa taarifa sahihi badala ya kukurupuka.
Kamishna Simba alisema, hakuna haja ya kufanya papara juu ya suala hilo, kwani bado linashughulikiwa na iwapo litakamilika umma utapewa taarifa zote kupitia vyombo vya habari.
Alisema Jeshi la Polisi nchini lina jukumu la kulinda uhuru na mipaka ya nchi yake na jaribio lolote la kutaka kumega nchi, lazima lishughulikiwe ipasavyo na vyombo vya ulinzi, ili kusitokee madhara.
Hata hivyo, akizungumza kwa njia ya simu ya kiganjani, mmoja wa watu walioshiriki kuandaa waraka uliopelekwa UNDP, alisema wamelazimika kuingia mafichoni wakihofia usalama wao, kutokana na taarifa za kutafutwa na vyombo vya usalama.
“Wenzetu wameshatiwa mbaroni na sisi tunatafutwa… bado tutaendelea kuishi huku (mafichoni) kwanza hadi hapo tutakapopewa taarifa za usalama wetu,” alisema Hamad Ali Mussa.
Alisema bado wataendelea kudai haki licha ya baadhi ya wananchi wenzao kukamatwa, kwani kwa muda mrefu wamekuwa wakionewa na kudhulumiwa katika nchi yao kama wakimbizi, wakati wanastahiki kuheshimiwa na kupewa haki zote za kiutu, ikiwemo huduma za kijamii.
Hamad alisisitiza kuwa, huo si mwisho, kwani azma yao ni kujipanga upya na kuwafikisha mahakamani wale wote walioshiriki kuwaua raia wasio na hatia tangu mwaka 1964 baada ya mapinduzi na mauaji ya mwaka 2001 yaliyofanyika chini ya utawala wa Rais Amani Karume.
“Huu ni mwanzo tu. Tutachukua hatua nyingine zaidi, tulikuwa tumejipanga kuchukua hatua za kisheria tuwafikishwe mahakamani wale wote walioua tokea mwaka 1964 hadi 2001 kwa sababu tumechoka kudhalilishwa na kuonewa katika nchi yetu,” alisema Hamad.
Alibainisha kuwa, awali walikuwa na matumaini makubwa baada ya kusikia kauli ya Rais Jakaya Kikwete kusononeshwa na hali ya kisiasa Zanzibar, na ahadi yake ya kuumaliza mgogoro huo, pamoja na kuundwa kwa kamati ya mazungumzo ya mwafaka, lakini baada ya Halmashauri Kuu ya CCM kutaka kuitishwe kura ya maoni, ndipo walipovunjika moyo na kuamua kuandika waraka huo.
Alipotakiwa kueleza viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) wamewasaidiaje katika suala hilo wakati huu ambapo wenzake hawajulikani walipo, Hamad alisema chama hicho hakihusiki na suala hilo kwa kuwa wao wameamua kufanya hivyo bila ya kutaka ushauri wa chama. “Hili si la CUF, ni la sisi Wapemba na tumepeleka ombi tutambuliwe kama raia wenye haki katika nchi yao… sisi sio wageni, lakini haya madhila na manyanyaso yametutosha sasa na ndio tumeamua kujitolea,” alisema.
“Nisamehe bibi simu yangu itakatika sasa hivi kwa kukosa chaji nimeshawasiliana na watu wengi kama wewe, kwa hivyo ikikatika nakuomba samahani, lakini kwa ufupi sisi tutaendelea kudai haki zetu, watatutafuta wakitupata watupeleke mahakamani…tukitoka tutadai tena,” alisema na muda mfupi baadaye ikakatika.
Akizungumza kwa njia ya simu, mtu mwingine ambaye hakutaka kutajwa jina lake, ambaye naye yupo mafichoni huko, alisema kukamatwa kwa wenzake si jambo la ajabu kwani wapo wananchi kadhaa waliowahi kukamatwa bila ya sababu yoyote huko Pemba na kushitakiwa kwa kesi za kubambikiziwa, lakini hatimaye waliachiwa.
Mtu huyo alitoa wito kwa serikali zote mbili kuacha kujidanganya kuwa kuwakamata au kuwatisha wananchi hao ndio suluhisho la matatizo ya kisiwani Pemba, kwani tatizo kubwa linatokana na mfumo wa serikali pamoja na muundo wa ubaguzi dhidi ya Wapemba.
Akizungumzia kwamba kauli zao hizo zinaweza kuhusishwa na uhaini, alisema kuliwahi kutokea kundi la wabunge Tanzania Bara waliojiita G55 na kudai serikali ya Tanganyika, lakini hawakuhesabiwa kuwa ni wahaini, na kueleza kushangazwa na wao kupakaziwa kuwa ni wahaini.
Mzee huyo alisema kilichowasukuma na kulalamika kudai kuundwa kwa serikali shirikishi huko Pemba ni uonevu na dhuluma dhidi yao wanaofanyiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambapo hakuna uwiano wa kiuchumi na hata kukoseshwa nyadhifa muhimu serikalini.
Akitoa mfano alisema hivi sasa kati ya mawaziri 15 ni mmoja tu anayetoka Pemba.
“Kuwepo uwiano basi… na sisi tupewe nafasi za mawaziri kwani ni kweli hakuna Mpemba anayeweza kuwa waziri? Hakuna Mpemba anayeweza kuwa naibu waziri? Nafasi za makatibu wakuu na watendaji wakuu wa serikali wote kutoka Unguja! Huu uonevu mpaka lini tutaendelea nao? Ifike pahali tuseme enough is enough (inatosha) jamani,” alisema mtu huyo ambaye alisema alipata kufukuzwa kazi wakati wa utawala wa Dk. Salmin Amour Juma.
Akizungumza kwa simu jana, Katibu wa Kamati ya Kutetea Haki za Waislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda naye alieleza kushangazwa na hatua ya serikali kuwakamata wananchi hao wa Pemba bila ya sababu za msingi.
Ponda alisema hoja za Wapemba hao ziko wazi, na akahoji ni kwa nini wabunge wa kundi la G 55 nao hawakukamatwa kwa uhaini, wakati walipodai ndani ya Bunge haja ya kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika.
Ingawa polisi hawajaeleza idadi ya watu waliokamatwa, habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kuwa waliokamatwa ni watu saba.
Habari kutoka ndani ya Jeshi la Polisi Zanzibar zinaeleza kuwa watu hao walikamatwa na maofisa wa usalama kutoka Bara na kupakiwa katika ndege ya jeshi na hivi sasa wanahifadhiwa katika vituo kadhaa vya polisi kisiwani Unguja.
Taarifa hizo zinapasha kuwa vituo ambamo watu hao wanahifadhiwa ni Mwembe Madema, Mazizini na Ng’ambo.
Miongoni mwa watu waliokamatwa ni kiongozi wa wazee wa Pemba, Ahmed Marshed Khamis, Maryam Hamad Bakar (Wete), Jiran Alli Hamad (Micheweni), Gharib Omar Gharib (Wete), Mohammed Mussa (Mkoani), Salim Abeid (Mkoani) na Hidaya Khamis Haji (Mkoani).

Monday, May 12, 2008

Kamata Kamata Pemba

ZAIDI ya watu 12 kutoka kisiwani Pemba wametiwa mbaroni na Jeshi la Polisi kuhusiana na tukio la kupelekwa kwa barua katika ofisi za Umoja wa Mataifa (UN) wakidai kujitenga kwa kisiwa hicho kutoka Zanzibar.

Watu wao walikamatwa kwa nyakati tofauti kuanzia usiku wa kuamkia Jumatatu, na familia zao zilithibitisha kukamatwa kwao kuanzia majira ya saa 5: 30 usiku wakiwa wamelala majumbani mwao.

Baadhi ya watu waliokamatwa wametambuliwa kwua ni ni Salim Mohammed Abeid, mkazi wa Mtambile, Mohammed Mussa Ali, mkazi wa Kiwani, Hidaya Khamis Haji wa Mkoani, Ahmed Marshed, Khamis Machomane na Mariam Hamad Bakar, wote wakaazi wa Kichangani Wawi, mkoa wa Kusini Pemba, Gharib Omar Ali, mkaazi wa Wete na Jirani Ali Ahmed wa Micheweni Kaskazini Pemba .

Sharifa Mussa, mke wa kiongozi wa kundi la watu 12 ambao walikwenda katika ofisi za UN wakiwakisha watu 10,000 waliotia saini barua hiyo, alithibitisha kukamatwa kwa mumewe, Ahmed Marshed Khamis, nyumbani kwake Mkanjuni mkoa wa Kusini Pemba.

Akielezea tukio hilo, Sharifa alisema mume wake alichukuliwa usiku na watu watano ambao hawakuwa na sare za polisi, ambao waligonga mlango wao wa nje na wao kulazimika kuamka haraka na kutoka nje kuangalia kinachoendelea.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Ameir Khatib, hakutaka kuzunguzia chochote kuhusiana na kukamatwa kwa watu hao, ingawa alikiri na kuwataka waandishi wawasiliane na Makao Makuu ya Polisi Unguja.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamishna wa Polisi Zanzibar, Khamis Mohamed Simba, alisema hana taarifa zaidi na kuahidi kutoa taarifa baadaye.

Taarifa zaidi kutoka Kisiwani Pemba zinaeleza kuwa hofu imetanga katika kisiwa hicho, kutokana na kukamatwa kwa watu hao ambao wengine hadi sasa hawajulikani wamepelekwa wapi.

Zainab Omar Hamad, ambaye ni Mtoto wa Fatma Abdallah Hamad, ambaye ni miongoni mwa watu 12 waliowasilisha waraka wa barua katika ofisi za UN jijini Dar es Salaam, alisema alifuatwa na askari majira ya saa 6 usiku akitakiwa kueleza alipo mama yake huyo.

Fatma Abdallah Hamad, Katibu wa watu waliokwenda kuwasilisha waraka huo, ambaye alieleza kuwa lengo lao ni kuomba msaada wa UN kuwasaidia kuunda serikali shirikishi kutokana na wakazi wa kisiwa cha Pemba kunyanyaswa na serikali hivi sasa.

Imeelezwa kuwa baada ya kuwakamata watu hao, polisi pia walizipekuwa nyumba wanamoishi, kwa maelezo kuwa walikuwa wakitafuta nyaraka nyingine, lakini hawakufanikiwa kupata chochote na kuondoka.

Wananchi wa Pemba wapatao 10,000 kwa mara ya kwanza waliwasilisha mapendekezo yao katika ofisi ya umoja huo, wakiongwa na aliyekuwa Mbunge wa Jimboi la Ole (CUF) Hamad Ali Mussa.

Wanafamilia wa watu hao walisema kwamba baada ya watu hao kukamatwa walijaribu kuwatafuta asubuhi katika vituo vya Polisi vya Pemba bila ya mafanikio na walielezwa kuwa walisafirishwa nje ya kisiwa cha Pemba kwa ndege.

Hata hivyo, walisema hadi Jumatatu mchana walikuwa hawafahamu jamaa zao iwapo wamesafirishwa kupelekwa kisiwani Unguja au Tanzania Bara.

Walieleza kwamba baada ya kuzunguuka katika vituo mbali mbali vya Polisi kisiwani Pemba walipata taarifa kutoka kwa baadhi ya askari kuwa watu hao wamesafirishwa usiku huo kwa ndege ya Jeshi kuelekea Bara.

Akilizungumzia tukio hilo, Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binaadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salum Bimani, alisema kwamba wamepata malalamiko kutoka kwa wanachama wa CUF Pemba kuwa usiku wa kuamkia jana, Polisi walifanya operesheni majumbani na kukamata baadhi ya watu.

Wiki iliyopita, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Muungano, Mohammed Seif Khatib, alikaririwa akisema kitendo cha wananchi hao kutaka Pemba ijitenge ni uhaini.

Alisema kwamba kitendo hicho hakina tofauti na kile kilichofanywa na muasi wa Anjouan, Kanali Mohammed Bacar.

Sunday, May 11, 2008

Mabadiliko Baraza la Mawaziri

Rais Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri katika zoezi la kuziba nafasi iliyobaki wazi baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge;

Ifuatayo ni taarifa ya mabadiliko hayo iliyotolewa na Ikulu:


TAARIFA YA SERIKALI KWA VYOMBO VYA HABARI


YAH: MABADILIKO MADOGO YA BARAZA
LA MAWAZIRI


Kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Mheshimiwa Andrew Chenge hivi karibuni, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri kama ifuatavyo:

MAWAZIRI:

1.1 Wizara ya Miundombinu:

Mheshimiwa Dk. Shukuru J. Kawambwa ameteuliwa kuwa Waziri mpya wa Miundombinu. Mheshimiwa Kawambwa anatokea Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia

1.2 Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia:

Profesa Peter M. Msolla anakuwa Waziri

1.3 Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI

Mhe. Celina O. Kombani ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI. Mheshimiwa Celina Kombani alikuwa ni Naibu Waziri wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI.


1.4 Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika

Mhe. Stephen M. Wassira - ameteuliwa kuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika. Mheshimiwa Wassira anatokea Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.


NAIBU MAWAZIRI

1.5 Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI

Mhe. Aggrey Mwandri, Mbunge wa SIHA.

1.6 Miundombinu

Mheshimiwa Ezekia Chibulunje (anahama kutoka Wizara ya Kazi)

1.7 Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana

Mhe. Dr. Milton M. Mahanga (anahamia kutoka Miundombinu)

Friday, May 9, 2008

Ajali tena Morogoro

AJALI nyingine mbaya imetokea leo mkoani Morogoro na watu 12 wamepoteza maisha yao. Ajali hiyo, iliyotokea katika kipindi cha wiki moja tangu itokee ajali nyingine iliyosababisha vifo vya watu 18, nayo ililihusisha basi pamoja na malori mawili.

Ajali hiyo ilitokea huko gairo majira ya saa 4 asubuhi wakati basi hilo la kampuni ya Al-Hushoom likielekea Dodoma kutokea Morogoro.

Malori yaliyohusika yote yalikuwa yakitokea Dodoma kuelekea Morogoro. Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Thobias Andengenye alisema kuwa ajali ilitokea wakati lori moja lilipokuwa linalipita loji jingine na ghafla likakutana na basi hilo.

Katika harakati za kulikwepa basi, dereva wa lori alilivaa trela la lori jingine ambalo lilikatika na kuligonga basi.

Waliofariki wanajumuisha wanaume wanane na wanawake wanne. Hadi hivi sasa marehemu waliotambuliwa ni pamoja na watawa wawili wa shirika la Carmelite la Kanisa Katoliki Kihonda, ambao ni Renatha Joseph na Anitha Bay, dereva wa basi Thomas Magosha, Khalid Mahai na Rehema Mzuwanda, mkazi wa Manispaa ya Morogoro.

Watu 32 walijeruhiwa na isipokuwa mmoja ambaye amelekwa Morogoro, wengine wamelazwa katika hospitali ya misheni ya Berega, iliyopo Gairo wilayani Kilosa na mmoja. Charles Kalekwa (39) ndiye aliyekimbizwa hospitali ya Mkoa kwa matibabu zaidi.

Hii ni ajali ya pili ndani ya wiki moja katika barabara hiyohiyo baada ya siku chache zilizopita watu wanane kufariki dunia baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka wilayani kahama kuelekea Dar es Salaam kukwaruzana na lori. Watu 16 walijeruhiwa.

Thursday, May 8, 2008

Serikali haina shida na Ballali

SERIKALI imesema haimtafuti aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daudi Ballali, ambaye mapema mwaka huu alifutwa kazi na Rais Jakaya Kikwete kutokana na kubainika kwa wizi wa mamilioni ya shilingi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salvatory Rweymamu, amesema kuwa serikali haina shida yoyote na Ballali kwa hivi sasa.

Alisema kutokuwepo nchini kwa Ballali, au kutojulikana alipo, si jambo linaloisumbua serikali kwa sasa kwa sababu hivi sasa Ballali ni raia wa kawaida, hivyo anao uhuru wa kuishi popote anapopenda.

Hata hivyo, alisema kuwa serikali ina mkono wa serikali, hivyo haitashindwa kumpata itakapomuhitaji wakati wowote.

Akifafanua zaidi, alisema baada ya kutenguliwa kwa uteuzi wake, serikali iliunda timu ya kuwachunguza watuhumiwa wa EPA, kuhakikisha fedha zilizoibwa zinarudi na kuwachukulia hatua waliohusika, akiwemo Ballali.

Mkurugenzi huyo pia alikiri kwamba serikali haifahamu hospitali aliyokuwa akitibiwa Ballali, licha ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mustafa Mukulo, kukaririwa akisema alimtafuta Ballali bila mafanikio alipokuwa jijini Washington, Marekani.

Mwanzoni mwa mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete alitengua uteuzi wa aliyekuwa Gavana wa BoT, baada ya taarifa ya uchunguzi wa hesabu uliofanywa na Kampuni ya Ukaguzi ya Ernst & Young na kubaini ubadhirifu wa zaidi ya sh bilioni 133.

Taarifa hiyo ilibaini kuwapo kwa kampuni hewa 22 zilizolipwa mamilioni ya fedha kutoka kwenye akaunti hiyo kati ya mwaka 2005 na 2006.

Hata hivyo, ilibainika kwamba, baadhi ya kampuni hizo zilidanganya kuhusu usajili na wamiliki wake huku nyingine zikimilikiwa na vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wengine wakitumia nyaraka za kughushi kuiba mabilioni hayo.

Mbali na udanganyifu huo, fedha za EPA zinadaiwa kusaidia kampeni za CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

BoT yaichunguza TPB

SIKU chache baada ya kuibuka kwa tuhuma za ubadhirifu ndani ya Benki ya Posta (TPB), Benki Kuu (BoT) imekiri kutuma maofisa wake kufanya uchunguzi ndani ya benki hiyo.

Ingawa alikuwa mgumu kukubali moja kwa moja kuwa BoT inaichunguza TPB, Gavana wa BoT, Profesa Beno Ndullu alithibitishia kuwa BoT imewatuma maofisa hao kufanya uchunguzi.

Akionekana kutaka kukwepa kulizungumzia suala hilo moja kwa moja, Ndullua alisema ni kawaida ya BoT kufanya ukaguzi wa mra kwa mara katika mabenki yote.

Hata hivyo, alipoulizwa inakuwaje wakati benki inakabiliwa na tuhuma kama ilivyo kwa TPB, Ndullu alisema kuwa katika mazingira hayo, ni lazima uchunguzi wa BoT uwe wa kina zaidi na usisubiri muda maalum.

Benki hiyop inachunguzwa kwa ufisadi wa mamilioni ya shilingi, udanganyifu wa baadhi ya watendaji wake na rushwa.

Tuhuma hizo zilichapishwa kwa mara ya kwanza katika mtandao wa Jambo Forusm, na kuwashtua viongozi wakuu wa benki hiyo, na Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo ambao waliunda kamati ya kuchunguza mtu aliyevujisha siri.

Habazi zilizopatikana zinadai kuwa moja kati ufisadi unaotajwa unamuhusisha Alphonce Kihwele, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo na tuhuma za kughushi barua ya bodi ya Benki ya Posta, ili kuongezewa mkataba wakati bodi inadai haikuwahi kukaa kikao kupendekeza aongezewe muda.

Mbali na tuhuma hizo, pia imeelezwa kuwa ufisadi mwingine uliofanyika unamhusisha kigogo mwingine anayedaiwa kuwalazimisha watengeneza mahesabu katika idara ya fedha kuhakikisha wanatoa hesabu zinazoonesha benki inapata faida kinyume na ukweli, hata hivyo inadaiwa kuwa Benki kuu ya Tanzania (BOT) imeweza kumbana baada ya kugundua hitilafu iliyofanywa.

Aidha, tuhuma nyingine ni zile zinazodai kuwa Mtendaji huyo ameandaa timu yake ya mtandao inayowahusisha baadhi ya wafanyakazi ndani ya benki hiyo, ili kuweza kufanikisha ufisadi huo.

Pamoja na mambo mengine, inadaiwa kuwa timu hiyo ndiyo iliyoiingiza Benki hiyo katika mikataba mibovu ikiwemo ule wa uwekaji na uendeshaji wa mashine za kutolea fedha (ATMs) ambazo zinadaiwa kuigharimu benki hiyo mamilioni ya fedha.