ALIPOLIHUTUBIA Bunge wakati analizindua Desemba 30, 2005, rais Jakaya Kikwete alitoa kauli iliyowahakikishia watu wengi kuwa sit u amedhamiria, bali pia atafanya kila lililo katika uwezo wake (kama rais) kumaliza mpasuko wa kisiasa unaokwamisha mambo mengi Zanzibar. Kauli aliyoitoa haikuonyesha mashaka yoyote kuhusu dhamira yake ya kukabiliana na suala hilo.
Kauli hiyo, ilionyesha kwa mara ya kwanza kuwa kiongozi mkuu wa nchyi ametambua matatizo yanayoikabili Zanzibar. Hili lilimpa sifa sana. Hata wakati mazungumzo hayo yaliposuasua, hili lilitumika kama sehemu ya ushawishi kwa Chama cha Wananchi (CUF) kisijitoe katika mazungumzo kama ambavyo kilikuwa kimetishia.
Kwa zaidi ya mwaka mmoja, watanzania walivumilia wakati mazungumzo hayo yakivuta miguu na hatimaye, mwezi uliopita, CUF ilipasua jibu kwa kueleza hadharani kile ambacho kilikubalika katika mazungumzo hayo yaliyokihusisha pia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Lakini kabla ya hapo, itakumbukwa kuwa masuala yaliyokuwa yakijadiliwa katika kamati ya mazungumzo yalikuwa yakivuja na kuufikia umma. Kwa mfano, ilipobainishwa kuwa moja kati ya masuala ambayo yanaelekea kuafikiwa ni kuundwa kwa serikali ya mseto, baadhi ya watu wasiopendelea mfumo huo wa utawala, walijitokeza na kueleza wazi wazi jinsi ambavyo hautokubalika hata kama kamati hiyo ya mazungumzo itaafiki hilo.
Na hivyo ndivyo ilivyotokea.
Lakini hakuna mtu ambaye aliuona mtego alioutega rais Kikwete katyika hotuba yake hiyo ya kihistoria. Katika sehemu ya hotuba hiyo, kwa kutaka kkujivua uwajibikaji katika suala hilo siku za usoni, Kikwete alisema: “Natambua kuwa uamuzi wa mwisho kuhusu hatma ya siasa na utawala Zanzibar ni wa Wazanzibari wenyewe.”
Maana ya kauli hii ni kuwa chochote kitakachoafikiwa katika yale atakayoayaanzisha kuhusiana na mazungumzo hayo, itapaswa kipate baraka za Wazanzibari wenyewe. Kauli hii ni kichaka ambacho CCM wanekitumia kujificha, hasa wale wahafidhina ambao hawapendi kuona CUF ikihusishwa serikalini.
Ilichofanya NEC ya CCM huko Butiama ni kwenda nje kabisa ya yale yaliyoafikiwa katika mazungumzo na kutafuta namna ya kuliingiza hilo la kura ya maoni. Kilichokuwa kinafahamika ni kuwa yaliyokubaliwa kwenye kamati ya mazungumzo ndiyo yafikishwe kwenye vyama husika ili yajadiliwe na kupata baraka. Inavyoelekea, kamati ya mazungumzo haikuweka kipengele chochote kinachohusisha kura ya maoni (ndio maana CUF wameng’aka).
Lakini hata kama itakubalika kuwa kura ya maoni kama ilivyopendekezwa na NEC ya CCM, kitakachotokea kinaweza kujulikana tangu sasa. Mgawanyo wa kura huko Zanzibar tangu 1995 unajulikana. Ni dhahiri kuwa kura hiyo itapigwa kwa kufuata itikadi ya vyama hivyo.
Wale wa CUF, kwa sababu chama chao kimekubali kuingia kwenye serikali ya mseto, wataliunga mkono suala la kuanzishwa kwa serikali hiyo. Kwa upande mwingine, wale wa CCM, ambao wameapa kutoishirikisha CUF kwenye serikali, watalipinga suala hilo.
Kutokana na mgawanyiko uliopo visiwani humo, matokeo ya kura hii hayatatofautiana sana na matokeo ya chaguzi kuu zilizopita. Tofauti ya kura utakuwa chache sana na hili litazusha mabishani upya huku CCM wakishangilia ushindi katika kura ya maoni na CUF ikibishia matokeo hayo kwa sababu wameibiwa kura.
Hapa tutakuwa tuinarudi tena kule kule tulikotoka. Kwa maana hiyo inabidi tujiandae na muafaka mwingine tena wa kupatanisha ugomvi utakaotokana na malumbaano ya kura za maoni. Hivi ndilo lengo letu?
Ilichokifanya CCM ni kutaka kuliingiza taifa katika aibu kubwa. Naamini kuwa kamati ya mazungumzo walijua fika kuwa upo uwezekano wa kupiga kura ya maoni kuhusiana na jambo lakini kwa kutambua ukweli wa hali halisi, waliamua kulikwepesha wakiamini kuwa walikuwa wanawakilisha maslahi ya watu wote. Kumbe huku nyuma kuna genge jingine ambalo lina malengo yake.
Haikuwa na maana kwa Kikwete kuanzisha mazungumzo haya akihusishsa akikundi kidogo cha watu, wakati akijua kuwa suala hilo linahitaji maamuzi ya Wazanzibari wote. Haikuwa na maana kwa Kikwete kuanzisha mazungumzo hayo wakati anafahamu kuwa kitakachokubaliwa kitageuzwa na chama chake kwa maslahi ya nani sijui.
Inavyoonekana, baada ya wawakilishi wa CCM na CUF kukubaliana jambo hili katika mazungumzo yao, CUF katika umoja wao wameamua kulikubali suala hilo wakati wale wa CCM wameamua kulikataa. Je, katika hali kama hiyo suluhisho ni kwenda kwenye kura ya maoni? Na ni nani atatoa uhakikisho leo kuwa kura ya maoni itakuwa ya huru na haki na kuwa matokeo yake yataheshimiwa?
Ieleweke kuwa kinachojadiliwa hapa ni mustakabali wa Zanzibar yote na Tanzania kwa ujumla. Ifahamike kuwa katika mfumo wa utawala ambao tumeamua kuufuata, hakuna maana kuvihusisha vyama viwili tu katika mazungumzo haya hata kama vyama hivyo ndivyo vyenye ushawishi mkubwa visiwani hum oleo hii.
Haipendezi na wala haitosaidia kutengeneza muafaka wa CCM na CUF wakati nchi sit u inafuataa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, bali pia kuna vyamka lukuki ambavyo vinaendesha siasa na vimeshaonyesha upinzani wa kweli katika masuala kadhaa.
Hata kama serikali ya mseto itakubalka Zanzibar, tumepata kujiuliza, iwapo tutafikia muafaka baina ya CUF na CCM leo hii, hivi itakuwaje wakati ambapo NCCR-Mageuzi itafanikiwa kupata nguvu ya kiaisasa Zabnzibar ka kushika nafasi ya pili katika matokeo ya kura? Nayo itahusika na mfumo wa kugawana madaraka au mfumo huu ni kwa ajili ya bCCM na CUF peke yao?
Kama na NCCR au chama kingine chochote kitakuwa kinahusika kutekeleza maamuzi haya, kwa nini nao hawakuhusishwa katika mazungumzo haya aambayo yamezaa mtafaruku mwingine badala ya muafaka?
CCM wanapozungumzia kura ya maoni hivi sasa wanafahamu kuwa suala hilo linahusu pia matumizi ya fedha? Zipo? Au ni namna nyingine ya kukwamisha maafikiano? Kwamba kura ya maoni haitofanyika mapema kwa sababu hakuna fedha na serikali zote mbili zipo katika juhudi ya kutafuta fedha ili kufanikisha suala hilo. Kuna aina fulani ya mchezo unafanyika hapa lakini umeshagunduliwa.
Nani atasimamia kura hii ya maoni? Chombo pekee kinachoweza kusimamia kura hii ni Tume ya Uchaguzi, ambayo inaweza kupewa jukumu hili. Lakini ni tume hii hii ambayo imekuwa ikilalamikiwa mara zote kuwa haitendi haki. Hivi sasa nani ataamini matokeo ya kura ya maoni iwapo mmojawapo wa wahusika atalalamika kuwa haki haikutendeka?
Kuna makosa ambayo kama nchi tumekuwa tukiyafanya kwa muda mrefu sana. Pamoja na kuwa suala hili linaweza lisionekane kuwa na uhusiano wa moja kwa moja, lakini hali ya Zanzibar na uhuru wake kama nchi nalo lina mchango wake humu.
Kwa muda mrefu, Zanzibar inajichukulia na kujiheshimu kama nchi (si taifa kama ilivyoamriwa na Mahakama). Lakini pamoja na mahakama kueleza kuwa hili si taifa, lakini yanayofanyika, jinsi ambavyio Zanzibar imeonekana katika harakati zake za kujiongezea mamlaka na madaraka, inaonekana ni jinsi gani ambavyo inapenda kuwa taifa kamili.
Kosa hapa ni kuwa wakati Zanzibar ikiwa na mwelekeo huo, inaonekana kuwa maamuzi makubwa mengi kuhusiana na nchio hiyo hufanywa aidha na Bara au kuathiriwa sana na Bara. Kwa Wazanzibari wengi, hasa wale wenye msimamo mkali, hili ni tusi.
Katika hili la mpasuko wa kisiasa ilipaswa ieleweke mapema iwapo ni suala lililopo katika malaka ya Zanzibar au la. Kikwete alipaswa kulijua hili kabla hajatoa kauli yake iliyoonyesha dhamira yake ya kulitafutia suala hilo ufumbuzi.
Inaelekea kuwa hata hakupata ushauri wa Wazanzibari kuhusiana na hili kama ambavyo wamemuonyesha juzi huko Butiama kwa kukataa mapendekezo ya kamati aliyoiunda. Kama angekuwa ameshauriana na kukubaliana na Wanzazibari kabla ya kuchukua hatua, ni dhahiri kuwa tusingefikia hali hii.
CCM wasipoanglia wanaweza kuwa wanafanya kosa la kuipa CUF nafasi ya kuendeleza mapambano ya kisiasa bila ya wao wenyewe kujua kuwa wanakipa faida chama hicho. Kwa kuwa kinaonekana kushindwa uchaguzi kila mara, CUF kinapata nafasi ya kuwa chama cha upinzani na kazi yake kubwa kuwa ni kuikosoa serikali iliyopo madarakani. Hili unaweza kulifanya kwa ufanisi iwapo utakuwa na hoja za msingi.
Mchezo unaofanywa na CCM kuhusiana na muafaka unakipa CUF hoja ambazo kwa kutumia uzoefu wake wa upinzani, kinaweza kuisumbua sana CCM hata kama kipo nje ya serikali. Inawezekana CCM wakaona kuwa harakati za CUF ambayo iko nje ya serikali kama keleleza mlango. Huo ni uamuazi wao.
Lakini kuna hatari nyingine kubwa zaidi ambayo inaweza kutokea ndani ya CCM yenyewe. Kwa muda mrefu sana kumekuwa na malalamiko kutoka kwa CUF kuwa wanaonewa, wanadhulumiwa na kunyanyaswa visiwani Zanzibar. Lakini habari kutoka kwenye kikao cha NWEC cha CCM cha Butiama, zinaeleza kuwa hata wana CCM, hasa wale walioko Pemba, nao wameanza kulalamika.
WanaCCM hao wa Pemba wanasema kuwa kutokana na mgawanyo wa kisiasa uliopo, wanafanya kazi kaatika mazingira magumu kisiwani humo, hasa kutokana na CUF kujiimarisha na kuwa hiyo ni ngome yake.
Kwao hawa, serikali ya mseto ilikuwa ni namna fulani ya kuwapunguzia ugumu wa kazi na maumivu wanayoyapata kukitumikia chama chao. Pale ambapo wenzao wa Unguja wameshindwa kusikiliza kilio chao, machozi yao yanaweza yasipotee hivi hivi. Lakini nani anayejua kuwa wanaweza kusikilizwa na kupozwa kwa namna nyingine?
Iwapo hali itaachwa iendelee kuwa hivi, ni dhahiri kwua itafika wakati, kutokana na kuimarika kwa harakati za CUF kutokana na kupatia hoja za msingi kisiasa, hali ya wanaCCM hawa wa Pemba ikawa mbaya zaidi kiasi cha kufikia kubadili msimamo wao.
Wazungu wana msemo kuwa iwapo huwezi kupambana nao basi jiunge nao. Itafika siku ambayo wanaCCM hawa kisiwani pemba wataona dhahiri kuwa hawawezi tena kuhimili vishindo na mikiki ya CUF, hivyo busara pekee watakayobakiwa nayo ni kujiunga nao.
Wednesday, April 2, 2008
Tuesday, April 1, 2008
Tabata Dampo wakataa fidia ya Serikali
Wakazi kadhaa wa eneo la Tabata Dampo katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam, ambao nyumba zao libomolewa hivi karibuni, wamekataa kupokea fidia ya sh milioni 20 kila mmoja, walizoahidiwa na serikali.
Wakazi hao wamesema hawawezi kupokea fedha hizo kwa sababu ni kidogo ukilinganisha na hali halisi inayowakabili hivi sasa baada ya kubomolewa nyumba zao.
Aidha, wakazi hao wamekataa viwanja vya bure walivyopewa na serikali kwa madai kuwa eneo la Buyuni, wakisema kuwa eneo hilo halina huduma zozote za kijamii na hakuna miundombinu kwa sasa.
Tamko la kutaka kuwalipa fuidia wananchi hao lilitolewa na waziri wa Sertikali za Mitaa, Stephen Wassira kama hatua ambazo serikali imezichukua baada ya kukabidhiwa ripoti ya timu iliyochunguza sakata hilo.
Wassira alisema fedha hizo zinalipwa kutokana na uvunjwaji wa haki za binadamu waliofanyiwa wakazi hao kwa kuvunjiwa nyumba zao kinyama.
Timu ya watu wanne ilifanyakazi yake kwa siku 16 na kubaini ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu uliofanywa na watendaji wa Manispaa ya Ilala katika kusimamia zoezi hilo, na kusababisha kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi, Mhandisi na Mwanasheria.
Timu ilibaini kuwa ubomoaji huo haukuzingatia uamuzi wa Baraza la Ardhi ulioisisitiza Halmashauri ya Ilala kuangalia taratibu zilizopo za kuwaondoa wavamizi katika eneo husika.
Aidha, timu hiyo pia iligundua kuwa taratibu za uendeshaji wa Halmashauri hazikuzingatiwa kwa kuwa ilipaswa dhamira ya kubomoa makazi hayo, ilitelewe katika vikao vya menejimenti na baraza la madiwani.
Wassira alisema, timu hiyo ilibaini mambo yaliyojitokeza wakati wa zoezi hilo ambayo ni kunyanyasika na kuteseka kisaikolojia kwa wakazi hao na familia zao na kubainisha kuwa leseni za makazi zilitolewa kimakosa.
Kwa mujibu wa kanuni na sheria kama ilivyoelezwa na Wassira, notisi ya kuondoka katika maeneo hayo ilitakiwa kutolewa siku 30 kabla ya ubomoaji huo kwa vile hilo ni eneo la makazi.
Baraza la ardhi, Februari 27 mwaka huu lilitoa hukumu yenye kueleza kuwa kiwanja namba 52 eneo la viwanda Tabata dampo ni mali ya Kampuni ya Allied Cargo na baada ya siku mbili watendaji wa Manispaa ya Ilala ilibomoa makazi ya watu hao kinyume cha sheria na taratibu.
“Hilo ni kosa, serikali wajibu wetu ni kulinda haki za raia hasa kuishi salama…nataka tuelewane vizuri. Ninachosema hapa ni kwamba tunashughulikia ukiukwaji wa sheria uliofanywa na watendaji wetu.
“Katika hili, kanuni za ubomoaji zimekiukwa na tunachokitoa hapa siyo malipo ya makazi yao, hapana hii ni pole kwa yaliyowakuta. Na mimi kama Waziri wa TAMISEMI, nawashauri kuhamia buyuni kwenye viwanja vya bure.
“We are concerned with human right (tunafuata haki za binadamu) kutokana na makosa ya maofisa wetu wachache, hii watalipwa wenye nyumba tuu,” alisisitiza Wassira.
Alisema, serikali imejifunza kutokana na ukiukwaji huu hivyo imeziagiza mamlaka zote za halmashauri nchini zinazoshughulikia mipango miji kuwawajibisha watendaji wote wanaokiuka sheria, taratibu na kanuni za kuwahamisha wananchi.
Wassira pia, alisema iwapo kuna baadhi ya watendaji wa Manispaa hiyo wanaotuhumiwa kwa ruhwa au uzembe, mamlaka husika ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) itawashighulikia.
Wakazi hao wamesema hawawezi kupokea fedha hizo kwa sababu ni kidogo ukilinganisha na hali halisi inayowakabili hivi sasa baada ya kubomolewa nyumba zao.
Aidha, wakazi hao wamekataa viwanja vya bure walivyopewa na serikali kwa madai kuwa eneo la Buyuni, wakisema kuwa eneo hilo halina huduma zozote za kijamii na hakuna miundombinu kwa sasa.
Tamko la kutaka kuwalipa fuidia wananchi hao lilitolewa na waziri wa Sertikali za Mitaa, Stephen Wassira kama hatua ambazo serikali imezichukua baada ya kukabidhiwa ripoti ya timu iliyochunguza sakata hilo.
Wassira alisema fedha hizo zinalipwa kutokana na uvunjwaji wa haki za binadamu waliofanyiwa wakazi hao kwa kuvunjiwa nyumba zao kinyama.
Timu ya watu wanne ilifanyakazi yake kwa siku 16 na kubaini ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu uliofanywa na watendaji wa Manispaa ya Ilala katika kusimamia zoezi hilo, na kusababisha kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi, Mhandisi na Mwanasheria.
Timu ilibaini kuwa ubomoaji huo haukuzingatia uamuzi wa Baraza la Ardhi ulioisisitiza Halmashauri ya Ilala kuangalia taratibu zilizopo za kuwaondoa wavamizi katika eneo husika.
Aidha, timu hiyo pia iligundua kuwa taratibu za uendeshaji wa Halmashauri hazikuzingatiwa kwa kuwa ilipaswa dhamira ya kubomoa makazi hayo, ilitelewe katika vikao vya menejimenti na baraza la madiwani.
Wassira alisema, timu hiyo ilibaini mambo yaliyojitokeza wakati wa zoezi hilo ambayo ni kunyanyasika na kuteseka kisaikolojia kwa wakazi hao na familia zao na kubainisha kuwa leseni za makazi zilitolewa kimakosa.
Kwa mujibu wa kanuni na sheria kama ilivyoelezwa na Wassira, notisi ya kuondoka katika maeneo hayo ilitakiwa kutolewa siku 30 kabla ya ubomoaji huo kwa vile hilo ni eneo la makazi.
Baraza la ardhi, Februari 27 mwaka huu lilitoa hukumu yenye kueleza kuwa kiwanja namba 52 eneo la viwanda Tabata dampo ni mali ya Kampuni ya Allied Cargo na baada ya siku mbili watendaji wa Manispaa ya Ilala ilibomoa makazi ya watu hao kinyume cha sheria na taratibu.
“Hilo ni kosa, serikali wajibu wetu ni kulinda haki za raia hasa kuishi salama…nataka tuelewane vizuri. Ninachosema hapa ni kwamba tunashughulikia ukiukwaji wa sheria uliofanywa na watendaji wetu.
“Katika hili, kanuni za ubomoaji zimekiukwa na tunachokitoa hapa siyo malipo ya makazi yao, hapana hii ni pole kwa yaliyowakuta. Na mimi kama Waziri wa TAMISEMI, nawashauri kuhamia buyuni kwenye viwanja vya bure.
“We are concerned with human right (tunafuata haki za binadamu) kutokana na makosa ya maofisa wetu wachache, hii watalipwa wenye nyumba tuu,” alisisitiza Wassira.
Alisema, serikali imejifunza kutokana na ukiukwaji huu hivyo imeziagiza mamlaka zote za halmashauri nchini zinazoshughulikia mipango miji kuwawajibisha watendaji wote wanaokiuka sheria, taratibu na kanuni za kuwahamisha wananchi.
Wassira pia, alisema iwapo kuna baadhi ya watendaji wa Manispaa hiyo wanaotuhumiwa kwa ruhwa au uzembe, mamlaka husika ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) itawashighulikia.
TAMKO RASMI LA CUF KUHUSU MAZUNGUMZO YA MUAFAKA
TAMKO LA CHAMA CHA WANANCHI (CUF) KUFUATIA TAMKO LA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM KUHUSIANA NA MAZUNGUMZO YA KUTAFUTA UFUMBUZI WA KUDUMU WA MPASUKO WA KISIASA ZANZIBAR
Tarehe 17 Machi, 2008, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama Cha Wananchi (CUF) lilifanya kikao chake mjini Zanzibar ambapo lilipokea na kuridhia makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Siku hiyo hiyo, CUF iliwatangazia wanachama wake na Watanzania kwa jumla matokeo ya kikao hicho cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Demokrasia, mjini Zanzibar.
Hiyo ilikuwa ni hatua kubwa na muhimu kutekelezwa na upande wa CUF baada ya vyama vyetu viwili kukubaliana kuwa viwasilishe makubaliano hayo kwa vikao vya juu vya maamuzi vya vyama vyetu ili kuyaridhia kabla ya kutiwa saini. Baada ya CUF kutekeleza wajibu wake, yalikuwa matarajio na imani yetu kwamba na upande wa CCM nao ungefanya wajibu wake.
Kwa mshangao na masikitiko makubwa, jana tumepokea Tamko la Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuhusiana na mazungumzo ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar ambalo kimsingi limeyakataa makubaliano yaliyofikiwa na Kamati zetu mbili.
CCM imeamua kufanya usanii wa kisiasa kwa kutumia lugha ya mzunguko, ya ubabaishaji na ya upotoshaji kwa lengo la ama kuendelea kurefusha muda hadi mwaka 2010 au kuyakataa makubaliano ambayo wajumbe wake wameshiriki kuyaandaa katika miezi 14 ya mazungumzo kati ya vyama vyetu viwili.
Hali hiyo iko wazi kwa sababu mbili kuu zifuatazo:
CCM imetamka ‘kuyakubali kimsingi’ mapendekezo yaliyowasilishwa na Kamati ya chama hicho inayoshiriki mazungumzo lakini wakati huo huo inazungumzia marekebisho ambayo inataka yafanywe na hivyo kuiagiza Kamati yake kukutana na wajumbe wa CUF ili kuyajadili marekebisho hayo.
Kwanza, CCM haikutaja ni maeneo gani inataka yafanyiwe marekebisho. Pili, hoja hii inashangaza kwa sababu wajumbe wa Kamati ya Mazungumzo kutoka upande wa CCM walikuwa wakiwaarifu wajumbe wa Kamati kutoka upande wa CUF kwamba wao walikuwa wakiwasilisha taarifa kwa kila hatua inayofikiwa katika vikao vya chama vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa na pia kwa viongozi wao wa juu, Rais Jakaya Kikwete na Mheshimiwa Amani Karume, na kupata maelekezo na miongozo inayohitajika. Hata taarifa ya karibuni kabisa ya CCM iliyokuwa ikikanusha taarifa za vyombo vya habari kwamba Mheshimiwa Amani Karume si kikwazo cha kufikiwa makubaliano ya muafaka iliweka mkazo na msisitizo kwamba katika kila hatua, viongozi hao wameshauriwa ipasavyo. Hatua hii ya mwisho ilikusudiwa kubariki makubaliano hayo yaliyokuwa yakifikiwa hatua kwa hatua na siyo kufungua mjadala mpya kupitia duru mpya ya mazungumzo.
CCM imekuja na hoja mpya kwamba iwapo mapendekezo haya yatakubaliwa, yatakuwa yanaleta mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala katika Zanzibar na hivyo yanapaswa kuridhiwa na wananchi wenyewe kwa njia ya kura ya maoni.
CCM kuleta hoja hii ni kulifanyia mzaha jambo kubwa linalohitaji umakini wa hali ya juu kwani linagusa mustakbali wa taifa letu. Muda wote wa mazungumzo ambayo yamechukua miezi 14 na yakiwa yamehusisha vikao 21, wajumbe wa Kamati ya CCM wanaoshiriki mazungumzo hawakuleta hoja hii ya kura ya maoni. Kinachosikitisha zaidi ni kuwa tofauti na ilivyoelezwa, pendekezo la kutaka kura ya maoni halikuwa limeibuliwa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM bali lilikuwemo katika Taarifa ya Kamati ya CCM inayoshiriki mazungumzo likiwa ni pendekezo walilotaka liridhiwe na Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa. Hivyo, ni wazi liliandaliwa mapema kutokana na kile Kamati hiyo ya CCM ilichokiita “kuipiku CUF katika ubunifu wa kujenga”. Kitendo cha Kamati ya CCM kuwasilisha kitu kipya nje ya makubaliano yaliyofikiwa ni upotoshaji mkubwa wenye lengo la kulifanyia usanii wa kisiasa suala kubwa kama hili linalogusa maslahi ya taifa na watu wake moja kwa moja. Na iwapo pendekezo hilo lina nia njema ya kuwashirikisha wananchi, kwa nini wajumbe wa Kamati ya CCM wasiliwasilishe katika vikao vya mazungumzo na badala yake wakaamua kuliingiza kama mtego wa kisiasa wenye lengo la “kuipiku CUF”?
Hoja nyengine ni kwamba kura ya maoni hiyo itaendeshwa na chombo kipi na kwa utaratibu upi hasa ikitiliwa maanani tayari CCM na CUF wamekubaliana kuwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na Daftari la Kudumu la Wapiga Kura vina matatizo ya msingi ambayo yanahitaji kurekebishwa? Ni vipi basi Tume hiyo chini ya Daftari bovu liliopo itaweza kuendesha kura ya maoni ambayo itakuwa huru na ya haki?
Sisi tunaona suala hilo ni mbinu chafu tu yenye lengo la kuendelea kupoteza muda ili makubaliano yaliyofikiwa yasiweze kutiwa saini na utekelezaji kuanza. Kwa lugha yao CCM waliyoandika katika waraka wao ni njia ya “kuipiku CUF” na kamwe haikusudiwi kupata maoni ya wananchi.
Kwa msingi huo CUF haikubaliani na hoja hizo zote mbili.
Ni lazima tukiri kuwa tumeshtushwa sana na kiwango hiki cha CCM kulifanyia usanii wa kisiasa suala kubwa kama hili. Lakini pia tumepata faraja kuwa Watanzania sasa wameweza kujua ni nani kati ya CCM na CUF asiyeitakia mema nchi hii. Wamejua ni nani kati ya CCM na CUF asiyetaka amani na utulivu katika nchi hii. Wamejua ni nani kati ya CCM na CUF asiyetaka siasa za maelewano na mashirikiano katika nchi hii.
Sasa ni wazi kwamba CCM iliingia katika mazungumzo haya ikiwa haina dhamira ya kweli na ya dhati ya kuupatia ufumbuzi wa kweli mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Inaonekana lengo pekee la CCM katika mazungumzo haya lilikuwa ni kuwahadaa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kwa kujidanganya kwamba wangeweza kuidhibiti kisiasa CUF kupitia utaratibu wa kuwapa matumaini ya uongo (strategic engagement) na kuyarefusha mazungumzo hayo kadiri inavyowezekana hadi kipindi kinachokaribia uchaguzi mkuu ujao pasina kuchukua hatua zozote za maana zenye kulenga kutoa ufumbuzi wa kweli wa mpasuko uliopo. CCM imeonesha wazi wazi kuwa haiitakii mema Tanzania yetu na wala haitaki kuona umoja wa kitaifa na utulivu wa kudumu vinapatikana Zanzibar ambayo ni sehemu moja ya Jamhuri ya Muungano.
Kwa upande mwengine, Watanzania wote na jumuiya ya kimataifa ni mashahidi kuwa CUF imefanya kila liliomo katika uwezo wake kuinusuru hali tete ya kisiasa Zanzibar isichafuke. CUF imechukua kila juhudi kuona mazungumzo haya yanafanikiwa. Imetoa kila ushirikiano unaohitajika kwa CCM na hata kuachia madai yake makuu (kutoa ‘concessions’) ili kuyanusuru mazungumzo hayo na kuyafanikisha.
CUF imeonesha ustahamilivu, ustaarabu na uelewa mkubwa katika mazungumzo haya. Tumeweza kukubaliana na CCM kwa kila hatua tuliyoombwa tuwe na subira ili kupisha mambo kadhaa ya kisiasa yapite. Mara nyengine, hata bila ya kutuomba, sisi wenyewe tumeonyesha uelewa na kuwapa nafasi pale yalipoibuka matukio ya kisiasa ambayo hayakutarajiwa na ambayo tulihisi yanahitaji tuwape muda wenzetu. CCM haionekani kujali au kuthamini juhudi hizo na imeamua kuzipiga teke.
Kama tulivyowahi kusema, hatukufanya hivyo kwa sababu CUF ni dhaifu kisiasa kama ambavyo CCM wangependa kujidanganya. Tulifanya yote hayo kwa sababu tunaongozwa na dhamira njema ya kuhakikisha nchi yetu inabaki katika hali ya amani na utulivu huku tukiamini kwa dhati kwamba mazungumzo ndiyo njia pekee ya kistaarabu ya kumaliza tofauti au migogoro ya kisiasa na kijamii. Lakini ni lazima tusisitize kuwa mazungumzo yenye lengo hilo ni lazima yawe mazungumzo makini yanayoongozwa na utashi wa kweli wa kisiasa uliojengeka juu ya nia njema na kuheshimiana baina ya pande zinazohusika. Hilo limekosekana kwa upande wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Kufuatia misukosuko iliyoyakumba mazungumzo haya mwaka jana, Rais Kikwete, alitoa taarifa kwa umma tarehe 14 Agosti, 2007 akiuomba upande wa CUF ukubali kuendelea na mazungumzo na akiwahakikishia Watanzania kuwa angechukua hatua kuona yanakamilishwa na yanafanikishwa. Wakati akiwahutubia Mabalozi wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa nchini katika sherehe za kuukaribisha mwaka mpya, mapema mwaka huu, Rais Kikwete aliwaeleza kwamba mazungumzo yamefikia ukingoni na kwamba karibu suala la mpasuko wa kisiasa Zanzibar litakuwa historia. Kauli hiyo ilipokewa kwa matumaini makubwa na wananchi ambao wamekuwa wakifuatilia kwa makini kila hatua ya mazungumzo yetu. Ni bahati mbaya kwamba Rais Kikwete ameyaangusha matumaini hayo ya Watanzania kama ambavyo ameyaangusha matumaini yao katika masuala mengine yote aliyowaahidi wakati anaomba kura na anaingia madarakani.
CUF imevunjwa moyo sana na Mheshimiwa Jakaya Kikwete akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM. Imani tuliyokuwa nayo kwake kama kiongozi wa nchi na ambayo tulibaki nayo hadi CCM inaelekea katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa imetetereka sana. Kitendo cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM chini ya Uenyekiti wake kukataa kupitisha makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF na badala yake kuja na hoja mpya za ajabu ajabu zenye lengo la “kuipiku CUF” kisiasa kunamwonyesha Rais Kikwete ama hakuwa mkweli na mwaminifu tokea mwanzoni na kwamba alikuwa akifanya usanii wa kisiasa wakati alipotangaza kuwa anasononeshwa sana na mpasuko wa kisiasa Zanzibar au ni kiongozi dhaifu asiye na udhibiti wa chama anachokiongoza. Yote mawili hayampi sifa za kiongozi ambaye nchi inamhitaji inapopita katika vipindi vigumu.
Kama tulivyofanya mwaka jana, ni vyema tumkumbushe tena Mheshimiwa Jakaya Kikwete kauli yake mwenyewe aliyoitoa wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tarehe 16 Septemba, 2003 wakati anafungua Mkutano wa Kumi na Moja wa Hali ya Siasa Tanzania ambao ulihusu ‘Udhibiti na Utatuzi wa Migogoro’, pale aliposema:
“…[N]aelewa kuwa utaratibu wa kung’amua dalili za migogoro hauwezi kuwa na manufaa kama haukuambatana na vitendo vya haraka. Taarifa za dalili za uendelezaji wa migogoro zinapopatikana zitakuwa hazina manufaa katika uzuiaji wa migogoro hiyo kama zitashughulikiwa kwa njia ya mlolongo wa uamuzi wa kirasimu ambao unaweza kuchelewesha utekelezaji hadi migogoro inapotokea. Kwa hiyo ni wazi kuwa upatikanaji wa taarifa za dalili za migogoro unakuwa wa maana katika uzuiaji wa migogoro kama mara zipatikanapo, zinatafsiriwa kwa vitendo. Mtiririko wa hoja hapa unapaswa kuwa “dalili za mwanzo kujumlisha na vitendo halisi ni sawa sawa na uzuiaji wa migogoro.” Ili haya yatokee unahitaji kuharakisha au kurekebisha utaratibu wa utoaji wa maamuzi ili dalili za mwanzo ziweze kutafsirika kwa vitendo haraka iwezekanavyo.”
Maamuzi ya Chama chake kupitia kikao alichokiongoza yeye mwenyewe akiwa Mwenyekiti wake hayaonyeshi kuwa anayazingatia haya aliyowaasa wenzake mwaka 2003 maana maamuzi ya Halmshauri Kuu ya Taifa yanawakilisha hasa “mlolongo wa maamuzi ya kirasimu” ambayo kama alivyosema hayawezi kuwa msingi wa utatuzi wa mgogoro. Inasikitisha zaidi kwa Rais Kikwete kuwatangazia Watanzania na ulimwengu kuwa amefanikiwa kuwakutanisha Rais Mwai Kibaki na Mheshimiwa Raila Odinga wa Kenya na kufanikisha kufikiwa kwa makubaliano kati ya ODM na PNU nchini humo lakini anashindwa kulifanikisha hilo nchini mwake ndani ya chama anachokiongoza mwenyewe na kati ya CCM na CUF. Rais Kikwete anaona fakhari kuwa Tanzania imeongoza Jeshi la Umoja wa Afrika (AU) katika operesheni ya kijeshi iliyopewa jina la “Operesheni Demokrasia” kisiwani Anjouan, nchini Comoro lakini ameshindwa kuongoza operesheni ya kisiasa ya kusimamisha demokrasia visiwani Zanzibar.
Rais anapaswa ajue kuwa heshima ya ofisi yake na uadilifu wake binafsi ameutia doa kubwa kutokana na kushindwa kusimamia kwa vitendo ahadi yake aliyoitoa kwa Watanzania kupitia hotuba yake ya Desemba 30, 2005 Bungeni na pia ahadi aliyoitoa na kuirejea mara kadhaa kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa katika ziara zake za nje ya nchi kila mara pale alipoulizwa kuhusiana na mgogoro wa muda mrefu wa kisiasa Zanzibar.
MSIMAMO WETU:
Chama Cha Wananchi (CUF) hakiko tayari kushirikiana na CCM kuwafanyia Watanzania usanii wa kisiasa. Huu sio utaratibu wa CUF katika uendeshaji wa siasa. Kwa CUF, siasa si proaganda zilizopitwa na wakati bali ni utumishi wa dhati na uliotukuka kwa umma uliowaamini viongozi wake. Kwa msingi huo, CUF haitakubali kurejea katika mazungumzo kwa utaratibu inaoutaka CCM.
CUF kinakitaka CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya vyama vyetu viwili na endapo kweli Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho “ imeyakubali kimsingi” makubaliano yaliyofikishwa kwake kama ilivyosema taarifa yake, basi kikubali kutia saini makubaliano hayo na utekelezaji wa yaliyokubaliwa uanze mara moja.
Kinyume na hayo, CUF inatoa wito kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti, za uhakika na za haraka kuingilia kati suala hili ili kuhakikisha makubaliano yaliyofikiwa yanatiwa saini. Baada ya Tanzania yenyewe kushindwa katika utatuzi wa mgogoro wake huu wa muda mrefu, sasa ni wakati muafaka kwa Jumuiya ya Kimataifa kuingilia kati kwa kuchagua Mpatanishi wa Kimataifa anayeheshimika kuja kuyasimamia hadi kuyafikisha ukingoni kwa kuhakikisha makubaliano ya dhati yanafikiwa yatakayotoa ufumbuzi wa kweli na wa haki wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
CUF inatoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuepuka fedheha iliyoipata katika nchi nyengine za Kiafrika ambazo iliziachia hadi hali ikachafuka na ndipo ikaingilia kati. Hali ya Zanzibar ni mbaya. Ilitulia kwa sababu ya matumaini ya Wazanzibari na Watanzania kwamba mazungumzo ya CCM na CUF yataleta suluhisho la utulivu na umoja. Makubaliano yaliyofikiwa yanapokosa uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuyakamilisha, yanahitaji kuona jumuiya ya kimataifa inaingilia kati kwa hatua za wazi na madhubuti kuinusuru Zanzibar na Tanzania isitumbukie kule nchi nyengine za Kiafrika zilipotumbukia.
Wakati tunawashukuru kwa dhati viongozi wa vyama vyengine vya siasa, viongozi wa dini, taasisi na jumuiya za kijamii, mabalozi wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania na vyombo vya habari hususan magazeti huru kwa mchango wao mkubwa walioutoa na ambao ulisaidia kuyafikisha mazungumzo hadi hatua ya kukamilishwa, CUF tunatoa wito tena kwao kuendelea kutoa ushirikiano wao na kutimiza wajibu wao kuona mgogoro huu unamalizwa kwa njia za amani na za haki.
CUF inawataka wanachama na wapenzi wake pamoja na Wazanzibari na Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki na siku zote upande wa amani, ukweli na haki utashinda.
Kwa jinsi inavyoyachezea masuala mazito yanayohusu maslahi ya taifa kama ilivyodhihirika kwa mambo yote makubwa yaliyojitokeza hivi karibuni, ni wazi kuwa CCM imepoteza uhalali wa kuongoza nchi na wakati sasa umefika wa Watanzania kuchagua chama makini kitakachoipa Tanzania uongozi makini unaohitajika.
HAKI SAWA KWA WOTE
SEIF SHARIF HAMAD
KATIBU MKUU – CUF
Dar es Salaam
01 Aprili, 2008
Tarehe 17 Machi, 2008, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama Cha Wananchi (CUF) lilifanya kikao chake mjini Zanzibar ambapo lilipokea na kuridhia makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Siku hiyo hiyo, CUF iliwatangazia wanachama wake na Watanzania kwa jumla matokeo ya kikao hicho cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Demokrasia, mjini Zanzibar.
Hiyo ilikuwa ni hatua kubwa na muhimu kutekelezwa na upande wa CUF baada ya vyama vyetu viwili kukubaliana kuwa viwasilishe makubaliano hayo kwa vikao vya juu vya maamuzi vya vyama vyetu ili kuyaridhia kabla ya kutiwa saini. Baada ya CUF kutekeleza wajibu wake, yalikuwa matarajio na imani yetu kwamba na upande wa CCM nao ungefanya wajibu wake.
Kwa mshangao na masikitiko makubwa, jana tumepokea Tamko la Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuhusiana na mazungumzo ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar ambalo kimsingi limeyakataa makubaliano yaliyofikiwa na Kamati zetu mbili.
CCM imeamua kufanya usanii wa kisiasa kwa kutumia lugha ya mzunguko, ya ubabaishaji na ya upotoshaji kwa lengo la ama kuendelea kurefusha muda hadi mwaka 2010 au kuyakataa makubaliano ambayo wajumbe wake wameshiriki kuyaandaa katika miezi 14 ya mazungumzo kati ya vyama vyetu viwili.
Hali hiyo iko wazi kwa sababu mbili kuu zifuatazo:
CCM imetamka ‘kuyakubali kimsingi’ mapendekezo yaliyowasilishwa na Kamati ya chama hicho inayoshiriki mazungumzo lakini wakati huo huo inazungumzia marekebisho ambayo inataka yafanywe na hivyo kuiagiza Kamati yake kukutana na wajumbe wa CUF ili kuyajadili marekebisho hayo.
Kwanza, CCM haikutaja ni maeneo gani inataka yafanyiwe marekebisho. Pili, hoja hii inashangaza kwa sababu wajumbe wa Kamati ya Mazungumzo kutoka upande wa CCM walikuwa wakiwaarifu wajumbe wa Kamati kutoka upande wa CUF kwamba wao walikuwa wakiwasilisha taarifa kwa kila hatua inayofikiwa katika vikao vya chama vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa na pia kwa viongozi wao wa juu, Rais Jakaya Kikwete na Mheshimiwa Amani Karume, na kupata maelekezo na miongozo inayohitajika. Hata taarifa ya karibuni kabisa ya CCM iliyokuwa ikikanusha taarifa za vyombo vya habari kwamba Mheshimiwa Amani Karume si kikwazo cha kufikiwa makubaliano ya muafaka iliweka mkazo na msisitizo kwamba katika kila hatua, viongozi hao wameshauriwa ipasavyo. Hatua hii ya mwisho ilikusudiwa kubariki makubaliano hayo yaliyokuwa yakifikiwa hatua kwa hatua na siyo kufungua mjadala mpya kupitia duru mpya ya mazungumzo.
CCM imekuja na hoja mpya kwamba iwapo mapendekezo haya yatakubaliwa, yatakuwa yanaleta mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala katika Zanzibar na hivyo yanapaswa kuridhiwa na wananchi wenyewe kwa njia ya kura ya maoni.
CCM kuleta hoja hii ni kulifanyia mzaha jambo kubwa linalohitaji umakini wa hali ya juu kwani linagusa mustakbali wa taifa letu. Muda wote wa mazungumzo ambayo yamechukua miezi 14 na yakiwa yamehusisha vikao 21, wajumbe wa Kamati ya CCM wanaoshiriki mazungumzo hawakuleta hoja hii ya kura ya maoni. Kinachosikitisha zaidi ni kuwa tofauti na ilivyoelezwa, pendekezo la kutaka kura ya maoni halikuwa limeibuliwa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM bali lilikuwemo katika Taarifa ya Kamati ya CCM inayoshiriki mazungumzo likiwa ni pendekezo walilotaka liridhiwe na Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa. Hivyo, ni wazi liliandaliwa mapema kutokana na kile Kamati hiyo ya CCM ilichokiita “kuipiku CUF katika ubunifu wa kujenga”. Kitendo cha Kamati ya CCM kuwasilisha kitu kipya nje ya makubaliano yaliyofikiwa ni upotoshaji mkubwa wenye lengo la kulifanyia usanii wa kisiasa suala kubwa kama hili linalogusa maslahi ya taifa na watu wake moja kwa moja. Na iwapo pendekezo hilo lina nia njema ya kuwashirikisha wananchi, kwa nini wajumbe wa Kamati ya CCM wasiliwasilishe katika vikao vya mazungumzo na badala yake wakaamua kuliingiza kama mtego wa kisiasa wenye lengo la “kuipiku CUF”?
Hoja nyengine ni kwamba kura ya maoni hiyo itaendeshwa na chombo kipi na kwa utaratibu upi hasa ikitiliwa maanani tayari CCM na CUF wamekubaliana kuwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na Daftari la Kudumu la Wapiga Kura vina matatizo ya msingi ambayo yanahitaji kurekebishwa? Ni vipi basi Tume hiyo chini ya Daftari bovu liliopo itaweza kuendesha kura ya maoni ambayo itakuwa huru na ya haki?
Sisi tunaona suala hilo ni mbinu chafu tu yenye lengo la kuendelea kupoteza muda ili makubaliano yaliyofikiwa yasiweze kutiwa saini na utekelezaji kuanza. Kwa lugha yao CCM waliyoandika katika waraka wao ni njia ya “kuipiku CUF” na kamwe haikusudiwi kupata maoni ya wananchi.
Kwa msingi huo CUF haikubaliani na hoja hizo zote mbili.
Ni lazima tukiri kuwa tumeshtushwa sana na kiwango hiki cha CCM kulifanyia usanii wa kisiasa suala kubwa kama hili. Lakini pia tumepata faraja kuwa Watanzania sasa wameweza kujua ni nani kati ya CCM na CUF asiyeitakia mema nchi hii. Wamejua ni nani kati ya CCM na CUF asiyetaka amani na utulivu katika nchi hii. Wamejua ni nani kati ya CCM na CUF asiyetaka siasa za maelewano na mashirikiano katika nchi hii.
Sasa ni wazi kwamba CCM iliingia katika mazungumzo haya ikiwa haina dhamira ya kweli na ya dhati ya kuupatia ufumbuzi wa kweli mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Inaonekana lengo pekee la CCM katika mazungumzo haya lilikuwa ni kuwahadaa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kwa kujidanganya kwamba wangeweza kuidhibiti kisiasa CUF kupitia utaratibu wa kuwapa matumaini ya uongo (strategic engagement) na kuyarefusha mazungumzo hayo kadiri inavyowezekana hadi kipindi kinachokaribia uchaguzi mkuu ujao pasina kuchukua hatua zozote za maana zenye kulenga kutoa ufumbuzi wa kweli wa mpasuko uliopo. CCM imeonesha wazi wazi kuwa haiitakii mema Tanzania yetu na wala haitaki kuona umoja wa kitaifa na utulivu wa kudumu vinapatikana Zanzibar ambayo ni sehemu moja ya Jamhuri ya Muungano.
Kwa upande mwengine, Watanzania wote na jumuiya ya kimataifa ni mashahidi kuwa CUF imefanya kila liliomo katika uwezo wake kuinusuru hali tete ya kisiasa Zanzibar isichafuke. CUF imechukua kila juhudi kuona mazungumzo haya yanafanikiwa. Imetoa kila ushirikiano unaohitajika kwa CCM na hata kuachia madai yake makuu (kutoa ‘concessions’) ili kuyanusuru mazungumzo hayo na kuyafanikisha.
CUF imeonesha ustahamilivu, ustaarabu na uelewa mkubwa katika mazungumzo haya. Tumeweza kukubaliana na CCM kwa kila hatua tuliyoombwa tuwe na subira ili kupisha mambo kadhaa ya kisiasa yapite. Mara nyengine, hata bila ya kutuomba, sisi wenyewe tumeonyesha uelewa na kuwapa nafasi pale yalipoibuka matukio ya kisiasa ambayo hayakutarajiwa na ambayo tulihisi yanahitaji tuwape muda wenzetu. CCM haionekani kujali au kuthamini juhudi hizo na imeamua kuzipiga teke.
Kama tulivyowahi kusema, hatukufanya hivyo kwa sababu CUF ni dhaifu kisiasa kama ambavyo CCM wangependa kujidanganya. Tulifanya yote hayo kwa sababu tunaongozwa na dhamira njema ya kuhakikisha nchi yetu inabaki katika hali ya amani na utulivu huku tukiamini kwa dhati kwamba mazungumzo ndiyo njia pekee ya kistaarabu ya kumaliza tofauti au migogoro ya kisiasa na kijamii. Lakini ni lazima tusisitize kuwa mazungumzo yenye lengo hilo ni lazima yawe mazungumzo makini yanayoongozwa na utashi wa kweli wa kisiasa uliojengeka juu ya nia njema na kuheshimiana baina ya pande zinazohusika. Hilo limekosekana kwa upande wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Kufuatia misukosuko iliyoyakumba mazungumzo haya mwaka jana, Rais Kikwete, alitoa taarifa kwa umma tarehe 14 Agosti, 2007 akiuomba upande wa CUF ukubali kuendelea na mazungumzo na akiwahakikishia Watanzania kuwa angechukua hatua kuona yanakamilishwa na yanafanikishwa. Wakati akiwahutubia Mabalozi wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa nchini katika sherehe za kuukaribisha mwaka mpya, mapema mwaka huu, Rais Kikwete aliwaeleza kwamba mazungumzo yamefikia ukingoni na kwamba karibu suala la mpasuko wa kisiasa Zanzibar litakuwa historia. Kauli hiyo ilipokewa kwa matumaini makubwa na wananchi ambao wamekuwa wakifuatilia kwa makini kila hatua ya mazungumzo yetu. Ni bahati mbaya kwamba Rais Kikwete ameyaangusha matumaini hayo ya Watanzania kama ambavyo ameyaangusha matumaini yao katika masuala mengine yote aliyowaahidi wakati anaomba kura na anaingia madarakani.
CUF imevunjwa moyo sana na Mheshimiwa Jakaya Kikwete akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM. Imani tuliyokuwa nayo kwake kama kiongozi wa nchi na ambayo tulibaki nayo hadi CCM inaelekea katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa imetetereka sana. Kitendo cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM chini ya Uenyekiti wake kukataa kupitisha makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF na badala yake kuja na hoja mpya za ajabu ajabu zenye lengo la “kuipiku CUF” kisiasa kunamwonyesha Rais Kikwete ama hakuwa mkweli na mwaminifu tokea mwanzoni na kwamba alikuwa akifanya usanii wa kisiasa wakati alipotangaza kuwa anasononeshwa sana na mpasuko wa kisiasa Zanzibar au ni kiongozi dhaifu asiye na udhibiti wa chama anachokiongoza. Yote mawili hayampi sifa za kiongozi ambaye nchi inamhitaji inapopita katika vipindi vigumu.
Kama tulivyofanya mwaka jana, ni vyema tumkumbushe tena Mheshimiwa Jakaya Kikwete kauli yake mwenyewe aliyoitoa wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tarehe 16 Septemba, 2003 wakati anafungua Mkutano wa Kumi na Moja wa Hali ya Siasa Tanzania ambao ulihusu ‘Udhibiti na Utatuzi wa Migogoro’, pale aliposema:
“…[N]aelewa kuwa utaratibu wa kung’amua dalili za migogoro hauwezi kuwa na manufaa kama haukuambatana na vitendo vya haraka. Taarifa za dalili za uendelezaji wa migogoro zinapopatikana zitakuwa hazina manufaa katika uzuiaji wa migogoro hiyo kama zitashughulikiwa kwa njia ya mlolongo wa uamuzi wa kirasimu ambao unaweza kuchelewesha utekelezaji hadi migogoro inapotokea. Kwa hiyo ni wazi kuwa upatikanaji wa taarifa za dalili za migogoro unakuwa wa maana katika uzuiaji wa migogoro kama mara zipatikanapo, zinatafsiriwa kwa vitendo. Mtiririko wa hoja hapa unapaswa kuwa “dalili za mwanzo kujumlisha na vitendo halisi ni sawa sawa na uzuiaji wa migogoro.” Ili haya yatokee unahitaji kuharakisha au kurekebisha utaratibu wa utoaji wa maamuzi ili dalili za mwanzo ziweze kutafsirika kwa vitendo haraka iwezekanavyo.”
Maamuzi ya Chama chake kupitia kikao alichokiongoza yeye mwenyewe akiwa Mwenyekiti wake hayaonyeshi kuwa anayazingatia haya aliyowaasa wenzake mwaka 2003 maana maamuzi ya Halmshauri Kuu ya Taifa yanawakilisha hasa “mlolongo wa maamuzi ya kirasimu” ambayo kama alivyosema hayawezi kuwa msingi wa utatuzi wa mgogoro. Inasikitisha zaidi kwa Rais Kikwete kuwatangazia Watanzania na ulimwengu kuwa amefanikiwa kuwakutanisha Rais Mwai Kibaki na Mheshimiwa Raila Odinga wa Kenya na kufanikisha kufikiwa kwa makubaliano kati ya ODM na PNU nchini humo lakini anashindwa kulifanikisha hilo nchini mwake ndani ya chama anachokiongoza mwenyewe na kati ya CCM na CUF. Rais Kikwete anaona fakhari kuwa Tanzania imeongoza Jeshi la Umoja wa Afrika (AU) katika operesheni ya kijeshi iliyopewa jina la “Operesheni Demokrasia” kisiwani Anjouan, nchini Comoro lakini ameshindwa kuongoza operesheni ya kisiasa ya kusimamisha demokrasia visiwani Zanzibar.
Rais anapaswa ajue kuwa heshima ya ofisi yake na uadilifu wake binafsi ameutia doa kubwa kutokana na kushindwa kusimamia kwa vitendo ahadi yake aliyoitoa kwa Watanzania kupitia hotuba yake ya Desemba 30, 2005 Bungeni na pia ahadi aliyoitoa na kuirejea mara kadhaa kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa katika ziara zake za nje ya nchi kila mara pale alipoulizwa kuhusiana na mgogoro wa muda mrefu wa kisiasa Zanzibar.
MSIMAMO WETU:
Chama Cha Wananchi (CUF) hakiko tayari kushirikiana na CCM kuwafanyia Watanzania usanii wa kisiasa. Huu sio utaratibu wa CUF katika uendeshaji wa siasa. Kwa CUF, siasa si proaganda zilizopitwa na wakati bali ni utumishi wa dhati na uliotukuka kwa umma uliowaamini viongozi wake. Kwa msingi huo, CUF haitakubali kurejea katika mazungumzo kwa utaratibu inaoutaka CCM.
CUF kinakitaka CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya vyama vyetu viwili na endapo kweli Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho “ imeyakubali kimsingi” makubaliano yaliyofikishwa kwake kama ilivyosema taarifa yake, basi kikubali kutia saini makubaliano hayo na utekelezaji wa yaliyokubaliwa uanze mara moja.
Kinyume na hayo, CUF inatoa wito kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti, za uhakika na za haraka kuingilia kati suala hili ili kuhakikisha makubaliano yaliyofikiwa yanatiwa saini. Baada ya Tanzania yenyewe kushindwa katika utatuzi wa mgogoro wake huu wa muda mrefu, sasa ni wakati muafaka kwa Jumuiya ya Kimataifa kuingilia kati kwa kuchagua Mpatanishi wa Kimataifa anayeheshimika kuja kuyasimamia hadi kuyafikisha ukingoni kwa kuhakikisha makubaliano ya dhati yanafikiwa yatakayotoa ufumbuzi wa kweli na wa haki wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
CUF inatoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuepuka fedheha iliyoipata katika nchi nyengine za Kiafrika ambazo iliziachia hadi hali ikachafuka na ndipo ikaingilia kati. Hali ya Zanzibar ni mbaya. Ilitulia kwa sababu ya matumaini ya Wazanzibari na Watanzania kwamba mazungumzo ya CCM na CUF yataleta suluhisho la utulivu na umoja. Makubaliano yaliyofikiwa yanapokosa uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuyakamilisha, yanahitaji kuona jumuiya ya kimataifa inaingilia kati kwa hatua za wazi na madhubuti kuinusuru Zanzibar na Tanzania isitumbukie kule nchi nyengine za Kiafrika zilipotumbukia.
Wakati tunawashukuru kwa dhati viongozi wa vyama vyengine vya siasa, viongozi wa dini, taasisi na jumuiya za kijamii, mabalozi wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania na vyombo vya habari hususan magazeti huru kwa mchango wao mkubwa walioutoa na ambao ulisaidia kuyafikisha mazungumzo hadi hatua ya kukamilishwa, CUF tunatoa wito tena kwao kuendelea kutoa ushirikiano wao na kutimiza wajibu wao kuona mgogoro huu unamalizwa kwa njia za amani na za haki.
CUF inawataka wanachama na wapenzi wake pamoja na Wazanzibari na Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki na siku zote upande wa amani, ukweli na haki utashinda.
Kwa jinsi inavyoyachezea masuala mazito yanayohusu maslahi ya taifa kama ilivyodhihirika kwa mambo yote makubwa yaliyojitokeza hivi karibuni, ni wazi kuwa CCM imepoteza uhalali wa kuongoza nchi na wakati sasa umefika wa Watanzania kuchagua chama makini kitakachoipa Tanzania uongozi makini unaohitajika.
HAKI SAWA KWA WOTE
SEIF SHARIF HAMAD
KATIBU MKUU – CUF
Dar es Salaam
01 Aprili, 2008
BREAKING NEWS: CUF yakataa kura ya maoni
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema kuwa hakitashiriki kuwafanyia wananchi usanii kama ambavyo ilivyopendekezwa na CCM. Katika kikao chake cha NEC hivi karibuni, CCM iliamua kuwa suala la kuundwa kwa serikali ya mseto huko Zanzibar.
Aidha, chama hichio kimesema kuwa imani yake kwa rais Jakaya Kikwete kuhusiana na suala la majadiliano ya kusaka muafaka wa Zanzibar imekwisha. Sasa chama hicho kimeamua kismingi kutoshiriki tena katika mchakato wa harakati hizo zilizoanzishwa na Kikwete na kuitaka jumuiya ya kimtaifa kingilia kati ili kuvinusuru visiwa hivyo kuingia katika machafuko.
Msimamo huo wa CUF umetangazwa hivi punde na katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad. Katika tamko la chama hicho, Hamad amesema kuwa CUF haikubaliani na hoja zilizotolewa na CCM za kutaka kuendeshwa kwa kura ya maoni.
CUF haikubaliani na hoja hiyo kwa sababu: “Sisi tunaona suala hilo ni mbinu chafu tu yenye lengo la kuendelea kupoteza muda ili makubaliano yaliyofikiwa yasiweze kutiwa saini na utekelezaji kuanza.”
CUF inasema kuwa kilichofanywa na CCM ni ghiliba na usanii mkubwa lakini kinafurahi kuwa hatua hiyo ya CCM imesaidia kuwaonyesha wananchi kuwa CCM haina dhamira na kulimaliza suala hilo kubwa.
(more coming later)
Aidha, chama hichio kimesema kuwa imani yake kwa rais Jakaya Kikwete kuhusiana na suala la majadiliano ya kusaka muafaka wa Zanzibar imekwisha. Sasa chama hicho kimeamua kismingi kutoshiriki tena katika mchakato wa harakati hizo zilizoanzishwa na Kikwete na kuitaka jumuiya ya kimtaifa kingilia kati ili kuvinusuru visiwa hivyo kuingia katika machafuko.
Msimamo huo wa CUF umetangazwa hivi punde na katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad. Katika tamko la chama hicho, Hamad amesema kuwa CUF haikubaliani na hoja zilizotolewa na CCM za kutaka kuendeshwa kwa kura ya maoni.
CUF haikubaliani na hoja hiyo kwa sababu: “Sisi tunaona suala hilo ni mbinu chafu tu yenye lengo la kuendelea kupoteza muda ili makubaliano yaliyofikiwa yasiweze kutiwa saini na utekelezaji kuanza.”
CUF inasema kuwa kilichofanywa na CCM ni ghiliba na usanii mkubwa lakini kinafurahi kuwa hatua hiyo ya CCM imesaidia kuwaonyesha wananchi kuwa CCM haina dhamira na kulimaliza suala hilo kubwa.
(more coming later)
Monday, March 31, 2008
Mashaka Yaanza Zanzibar
Kile kilichokuwa kikihofiwa siku zote, sasa kinaweza kutokea. Hali ya mambo kisiwani Zanzibar imeanza kuwa ya wasi wasi kutokana na maamuzi yaliyofikiwa katika kikao cha NEC ya CCM huko Butiama.
Kinachoonekana kikuweka rehani kisiwa hicho ni kukengeuka kwa CCM na kuamua kupindisha kilichokubaliwa katika kamati ya Mazungumzo na kutaka ifanyike kura ya maoni kuhusu kuanzishwa kwa serikali ya Mseto visiwani humo.
Katika kile kinachoashiria kuwa hali ya mambo imeanza kuwa mbaya, wajumbe wa Baraza la wawakilishi wa CUF, waliacha kuendelea na vikao vya baraza na kwenda katika makao makuu ya chama chao ambajko ulifanyika mkutano.
Habari kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa wajumbe hao wametakiwa na wanachama wao kususia vikao vyote vya baraza la wawakilishi.
Aidha, kuna taarifa pia kuwa wanaCUF wamewataka wabunge wao kutohudhuria vikao vya Bunge, linalotarajia kuanza kukutana mjini Dodoma wiki ijayo.
Wajumbe hao wa CUF walitoka Barazani wakiongozwa na Mnadhimu wa kambi ya upinzani, Soud Yussuf Mgeni, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika.
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma na Haki za Binaadamu wa CUF, Salum Bimani alisema kwamba kikao hicho kiliitishwa baada ya viongozi wa chama na wajumbe wa Baraza hilo kupewa ujumbe wa simu kutoka kwa wanachama kuwataka wasusie mara moja vikao vya Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Tayari watu kadhaa wameshaanza kuonyesha wasi wasi wao kutokana na maamuzi yaliyofikiwa na CCM , ambayo yabnaonekana kurudisha nyuma hatua iliyokubaliwa na Kamatio ya Mazungumzo ambayo iliwashirikisha wajumbe kutoka CCM na CUF.
Katika mazungumzo hayop, ilikubaliwa kuwa iundwe serikali ya mseto Zanzibar, ambapo chaka kitakachoshinda uchagzui kitatoa rais na kile kinachofuatia kitatoa waziri Kiongozi.
Lakini suala hili limekuwa likipingwa miaka yote ya wahafidhina walio ndani ya CCM Zanzibat na wamejiapiza kuwa kamwe hawatoiruhusu CUF katika serikali yao.
Biomani alisema kuwa CUF kimepokea maamuzi ya NEC lakini kitatoa maamuzi yake Jumanne kupitia mkutano na waandishi wa habari, ambao utahutubiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad.
Wakati huo huo, uamuzi wa NEC ya CCM kuwa suala hilo liamuriwe kupitia kura ya maobni, limezua mjadala visiwani hapa, huku baadhi ya watu wakipinga wazo hilo.
Katibu wa TADEA, Juma Ali Khatib, alisema suala la kuitisha kura ya maoni juu ya serikali ya pamoja visiwani humu si muafaka kwa sasa kwa sababu muda uliobakia ni mdogo.
Alieleza kwamba Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ilipaswa kulitambua hilo mapema, kwa vile linagusa katiba na sheria za uchaguzi.
Naye Mkurugenzi wa Habari wa NCCR-Mageuzi, Ali Omar, alisema kwamba wakati muafaka umefika kwa Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa ameshindwa kutatua mpasuko wa kisiasa wa Zanzibar.
Alisema kwamba kwa kuzingatia kuwa suala la serikali ya mseto linahusu maslahi ya taifa halikupaswa kurejeshwa kwa wananchi kwa vile hatua hiyo ni sawa na kupoteza muda.
“NCCR-Mageuzi tunavyoona Rais Kikwete ameshindwa kutekeleza ahadi yake ya kumaliza mpasuko wa kisiasa kama alivyoahdi katika Bunge,” alisema kiongozi huyo.
mwisho
Kinachoonekana kikuweka rehani kisiwa hicho ni kukengeuka kwa CCM na kuamua kupindisha kilichokubaliwa katika kamati ya Mazungumzo na kutaka ifanyike kura ya maoni kuhusu kuanzishwa kwa serikali ya Mseto visiwani humo.
Katika kile kinachoashiria kuwa hali ya mambo imeanza kuwa mbaya, wajumbe wa Baraza la wawakilishi wa CUF, waliacha kuendelea na vikao vya baraza na kwenda katika makao makuu ya chama chao ambajko ulifanyika mkutano.
Habari kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa wajumbe hao wametakiwa na wanachama wao kususia vikao vyote vya baraza la wawakilishi.
Aidha, kuna taarifa pia kuwa wanaCUF wamewataka wabunge wao kutohudhuria vikao vya Bunge, linalotarajia kuanza kukutana mjini Dodoma wiki ijayo.
Wajumbe hao wa CUF walitoka Barazani wakiongozwa na Mnadhimu wa kambi ya upinzani, Soud Yussuf Mgeni, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika.
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma na Haki za Binaadamu wa CUF, Salum Bimani alisema kwamba kikao hicho kiliitishwa baada ya viongozi wa chama na wajumbe wa Baraza hilo kupewa ujumbe wa simu kutoka kwa wanachama kuwataka wasusie mara moja vikao vya Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Tayari watu kadhaa wameshaanza kuonyesha wasi wasi wao kutokana na maamuzi yaliyofikiwa na CCM , ambayo yabnaonekana kurudisha nyuma hatua iliyokubaliwa na Kamatio ya Mazungumzo ambayo iliwashirikisha wajumbe kutoka CCM na CUF.
Katika mazungumzo hayop, ilikubaliwa kuwa iundwe serikali ya mseto Zanzibar, ambapo chaka kitakachoshinda uchagzui kitatoa rais na kile kinachofuatia kitatoa waziri Kiongozi.
Lakini suala hili limekuwa likipingwa miaka yote ya wahafidhina walio ndani ya CCM Zanzibat na wamejiapiza kuwa kamwe hawatoiruhusu CUF katika serikali yao.
Biomani alisema kuwa CUF kimepokea maamuzi ya NEC lakini kitatoa maamuzi yake Jumanne kupitia mkutano na waandishi wa habari, ambao utahutubiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad.
Wakati huo huo, uamuzi wa NEC ya CCM kuwa suala hilo liamuriwe kupitia kura ya maobni, limezua mjadala visiwani hapa, huku baadhi ya watu wakipinga wazo hilo.
Katibu wa TADEA, Juma Ali Khatib, alisema suala la kuitisha kura ya maoni juu ya serikali ya pamoja visiwani humu si muafaka kwa sasa kwa sababu muda uliobakia ni mdogo.
Alieleza kwamba Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ilipaswa kulitambua hilo mapema, kwa vile linagusa katiba na sheria za uchaguzi.
Naye Mkurugenzi wa Habari wa NCCR-Mageuzi, Ali Omar, alisema kwamba wakati muafaka umefika kwa Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa ameshindwa kutatua mpasuko wa kisiasa wa Zanzibar.
Alisema kwamba kwa kuzingatia kuwa suala la serikali ya mseto linahusu maslahi ya taifa halikupaswa kurejeshwa kwa wananchi kwa vile hatua hiyo ni sawa na kupoteza muda.
“NCCR-Mageuzi tunavyoona Rais Kikwete ameshindwa kutekeleza ahadi yake ya kumaliza mpasuko wa kisiasa kama alivyoahdi katika Bunge,” alisema kiongozi huyo.
mwisho
Wednesday, March 19, 2008
Timu ya Pinda Yakamilisha Kazi
Timu iliyoteuliwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kupitia kwa kina mapendekezo yaliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wa Richmond, imemaliza kazi yake na kukabidhi ripoti.
Pinda amesema kuwa hivi sasa, serikali inaipitia ripoti hiyo kabla ya kutoa maamuzi kutokana na mapendekezo ya Timu hiyo.
Katika ripoti yake, Kamati teule ya Bunge iliyokuwa na wajumbe watano chini ya uenyekiti wa Dk. Harison Mwakyembe, ilipendekeza watumishi kadhaa wa umma, walio katika ngazi za juu serikalini, wachukuliwe hatua kutokana na uzembe uliosababisha taifa kupata hasara kupitia mkatana huow a Richmond.
Mtumishi mmojawapo mkubwa wa umma ambaye kamati hiyo imependekeza awajibishwe ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, John Mwanyika, kutokana na kile kilichoelezwa na kamati kuwa ni kushindwa kwa ofisi anayoiongoza kuishauri vema serikali katika suala hilo.
Pia, pamoja na kushauri hatua zichukuliwe dhidi ya Mkurugenzi wa Takukuru, kamati hiyo inapendekeza pia taasisi hiyo imulikwe baada ya kutoa taarifa iliyoonyesha kuwa kimsingi hakukuwa na tatizo lolote la ufisadi katika mkataba wa Richmond.
Tayari aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wawili, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, walishajiuzulu nyadhfa zao baada ya kuwasilishwa kwa ripoti hiyo Bungeni.
Kukamilika kwa ripoti hiyo kunafanya idadi ya ripoti kuhusiana na sakata la Richmond kufikia tatu baada ya timu nyingine iliyohusisha wanasheria wa Bunge kuipitia mikataba baina ya Tanesco na makamopuni binafsi ya kzualisha umeme, ukiwemo wa Richmond.
Wataalam hao wa washeria walibaini kwua mikataba na makampuni matano baina ya sita ilikuwa inafanana kwa kiasi kikubwa na kuleta wasi wasi wa umahiri wa watu walioandika au kuidhinisha mikataba hiyo.
Pinda amesema kuwa hivi sasa, serikali inaipitia ripoti hiyo kabla ya kutoa maamuzi kutokana na mapendekezo ya Timu hiyo.
Katika ripoti yake, Kamati teule ya Bunge iliyokuwa na wajumbe watano chini ya uenyekiti wa Dk. Harison Mwakyembe, ilipendekeza watumishi kadhaa wa umma, walio katika ngazi za juu serikalini, wachukuliwe hatua kutokana na uzembe uliosababisha taifa kupata hasara kupitia mkatana huow a Richmond.
Mtumishi mmojawapo mkubwa wa umma ambaye kamati hiyo imependekeza awajibishwe ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, John Mwanyika, kutokana na kile kilichoelezwa na kamati kuwa ni kushindwa kwa ofisi anayoiongoza kuishauri vema serikali katika suala hilo.
Pia, pamoja na kushauri hatua zichukuliwe dhidi ya Mkurugenzi wa Takukuru, kamati hiyo inapendekeza pia taasisi hiyo imulikwe baada ya kutoa taarifa iliyoonyesha kuwa kimsingi hakukuwa na tatizo lolote la ufisadi katika mkataba wa Richmond.
Tayari aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wawili, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, walishajiuzulu nyadhfa zao baada ya kuwasilishwa kwa ripoti hiyo Bungeni.
Kukamilika kwa ripoti hiyo kunafanya idadi ya ripoti kuhusiana na sakata la Richmond kufikia tatu baada ya timu nyingine iliyohusisha wanasheria wa Bunge kuipitia mikataba baina ya Tanesco na makamopuni binafsi ya kzualisha umeme, ukiwemo wa Richmond.
Wataalam hao wa washeria walibaini kwua mikataba na makampuni matano baina ya sita ilikuwa inafanana kwa kiasi kikubwa na kuleta wasi wasi wa umahiri wa watu walioandika au kuidhinisha mikataba hiyo.
Friday, March 14, 2008
BOT sasa yaiogopa EPA!
Baada ya moto uliowaka sasa inaonekana kuwa akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) ni moto kweli kweli na Benki Kuu imeonyesha dhamira ya kutaka kujitoe kuendesha akaunti hiyo.
Gavana wa BoT, Benno Ndulu amesema leo kuwa tayari BoT imeshawasiliana na mtaalamu, ambaye ni kampuni moja kutoka nchini kutoka nchini Ufaransa, ili aje kufanya tathmini itakayosaidia kuamua iwapo akaunti hiyo iendelee kubaki BoT au la.
Lakini Ndulu amesema kuwa kimsingi, EPA si sehemu ya shughuli za BoT na ndio maana wanataka kuiondoa akaunti hiyo chini yao.
Gavana Ndulu amesema kuwa kampuni hiyo itatakiwa kukamilisha kazi yake kabla ya katikati ya mwaka huu ili uamuzi wa wapi akaunti hiyo iwekwe ufanywe. Inaonekana kuwa lengo lake ni kuhakikisha kuwa unapoanza mwaka mpya wa fedha mwezi Julai, shughuli za akaunti hiyo zikabidhiwe kwa taasisi inayostahili kuiendesha.
Awali, kabla ya kuhamishiwa BoT, akaunto hiyo ilikuwa ikiendeshwa na NBC.
Baada ya kuhamishiwa BoT, wajanja wachache, kwa kutumia nyaraka za kughushi na ulaghai, walichota kisi cha sh bilioni 133 kutoka katika akaunti hiyo.
Wizi huo ulibainishwa na wanasiasa, hasa wa upinzani walipozungumza bungeni, ingawa viongozi wa serikali walijipanga kukanusha.
Hata hivyo, mbinyo wa wapinzani uliendelea hadi serikali kulazimika kuialika kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu wa Ernst & Young ambayo mwishoni mwa mwaka jana ilithibitisha kuwa kweli wajanja wamejichotea mabilioni kutoka katika akaunti hiyo.
Gavana wa BoT, Benno Ndulu amesema leo kuwa tayari BoT imeshawasiliana na mtaalamu, ambaye ni kampuni moja kutoka nchini kutoka nchini Ufaransa, ili aje kufanya tathmini itakayosaidia kuamua iwapo akaunti hiyo iendelee kubaki BoT au la.
Lakini Ndulu amesema kuwa kimsingi, EPA si sehemu ya shughuli za BoT na ndio maana wanataka kuiondoa akaunti hiyo chini yao.
Gavana Ndulu amesema kuwa kampuni hiyo itatakiwa kukamilisha kazi yake kabla ya katikati ya mwaka huu ili uamuzi wa wapi akaunti hiyo iwekwe ufanywe. Inaonekana kuwa lengo lake ni kuhakikisha kuwa unapoanza mwaka mpya wa fedha mwezi Julai, shughuli za akaunti hiyo zikabidhiwe kwa taasisi inayostahili kuiendesha.
Awali, kabla ya kuhamishiwa BoT, akaunto hiyo ilikuwa ikiendeshwa na NBC.
Baada ya kuhamishiwa BoT, wajanja wachache, kwa kutumia nyaraka za kughushi na ulaghai, walichota kisi cha sh bilioni 133 kutoka katika akaunti hiyo.
Wizi huo ulibainishwa na wanasiasa, hasa wa upinzani walipozungumza bungeni, ingawa viongozi wa serikali walijipanga kukanusha.
Hata hivyo, mbinyo wa wapinzani uliendelea hadi serikali kulazimika kuialika kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu wa Ernst & Young ambayo mwishoni mwa mwaka jana ilithibitisha kuwa kweli wajanja wamejichotea mabilioni kutoka katika akaunti hiyo.
Thursday, March 13, 2008
BREAKING NEWS: Mwekezaji TRL asalimu amri
Mwekezaji katika Kampuni ya Reli nchini (TRL) amesalimu amri na kukubali kutekeleza madai ya watumishi ambao jana walianza mgomo kushinikiza waongezewe mishahara.
Habari zinaeleza kuwa mwekezaji huyo (Shirika la Rites na India na Serikali ya Tanzania) amekubali kuwaongezea mishahara ya kima cha chini wafanyakazi hao kutoka kima wanacholipwa hivi sasa cha sh 86,000 hadi sh 160,000 kwa mwezi.
Aidha, mwekezaji huyo ameahidi kuwa ifikapo Agosti mwaka huu, ataongeza kima hicho cha chini na kufikia sh 200,000. watumishi hao waligoma wakitaka nyongeza ya mishahara wakidai kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakiahidiwa nyongeza hiyo lakini hawajaipata.
Msimamo huo uliomaliza rasmi mgomo, ulifikiwa leo katika kikao baina ya wafanyakazi hao, mwekezaji pamoja na serikali kupitia Wizara ya Miundombinu.
Hali ilianza kuwa mbaya katyika reli hiyo kwani mgomo huo ulisitisha shughuli zote za safari za treni. Moja ya treni ambayo iliondoka juzi dare s Salaam ikielekea mikoa ya Dodoma, tabora, Kigoma na Mwanza, ilikwama ilipofika mjini Dodoma, baada ya watumishi waliokuwa wakiiendesha kugoma kuendelea na safari.
Hali hiyo ilisababisha mtafaruku mkubwa baada ya baadhi ya wabiria kuandamana hadi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambaye alipojadiliana na wafanyakazi hao, alishindwa kuwashawishi waendelee na safari baada ya wenzao wa tabora kueleza kuwa hawapo tayari kuipokea treni hiyo.
Jambo hilo liliwafnay abiria waliokuwa na hasira kuanza kurusha mawe wakiwalenga watumishi wa treni hiyo waliokuwa katika injini na kuwalazimisha askari walioitwa kulinda usalama kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya.
Habari zinaeleza kuwa mwekezaji huyo (Shirika la Rites na India na Serikali ya Tanzania) amekubali kuwaongezea mishahara ya kima cha chini wafanyakazi hao kutoka kima wanacholipwa hivi sasa cha sh 86,000 hadi sh 160,000 kwa mwezi.
Aidha, mwekezaji huyo ameahidi kuwa ifikapo Agosti mwaka huu, ataongeza kima hicho cha chini na kufikia sh 200,000. watumishi hao waligoma wakitaka nyongeza ya mishahara wakidai kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakiahidiwa nyongeza hiyo lakini hawajaipata.
Msimamo huo uliomaliza rasmi mgomo, ulifikiwa leo katika kikao baina ya wafanyakazi hao, mwekezaji pamoja na serikali kupitia Wizara ya Miundombinu.
Hali ilianza kuwa mbaya katyika reli hiyo kwani mgomo huo ulisitisha shughuli zote za safari za treni. Moja ya treni ambayo iliondoka juzi dare s Salaam ikielekea mikoa ya Dodoma, tabora, Kigoma na Mwanza, ilikwama ilipofika mjini Dodoma, baada ya watumishi waliokuwa wakiiendesha kugoma kuendelea na safari.
Hali hiyo ilisababisha mtafaruku mkubwa baada ya baadhi ya wabiria kuandamana hadi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambaye alipojadiliana na wafanyakazi hao, alishindwa kuwashawishi waendelee na safari baada ya wenzao wa tabora kueleza kuwa hawapo tayari kuipokea treni hiyo.
Jambo hilo liliwafnay abiria waliokuwa na hasira kuanza kurusha mawe wakiwalenga watumishi wa treni hiyo waliokuwa katika injini na kuwalazimisha askari walioitwa kulinda usalama kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya.
Monday, March 10, 2008
BREAKING NEWS: TRL kwafukuta
Jitihada za kuwazuia wafanyakazi wa Kampuni ya reli nchini kufanya mgomo zimegonga mwamba. Muda mfupi uliopita, wafanyakazi wa kampuni hiyo ambayo ilikodishwa na serikali mwaka huu, wametoa notisi ya saa 48 kwa mwajiri wao, awaongezee mshahara.
Iwapo mwajiri atashindwa kutekeleza ombi hilo, wafanyakazi hao wamejiandaa kufanya mgomo nchi nzima na madhara ya mgomo huo yanaweza kuhatarisha hali ya uchumi wa nchi na kusababisha mvugano katika jamii.
Hii ni kwa sababu Reli hiyo ndiyo tegemeo la usafiri kwa mikoa mingi ya bara hivyo iwapo itashindwa kufanya kazi kutokana na mgomo huo, kuna uwezekano mkubwa bidhaa nyingi zikakosekana katika mikoa kadhaa.
Sakata la wafanyakazi hao lilianza mara tu baada ya mkodishaji, kampuni ya rites ya India, alipoingia kuanza kazi mwanzoni mwa mwaka huu.
Baada ya kuja kwa mkodishaji huyo anayemiliki sehemu kubwa ya hisa za kampuni hiyo, wafanyakazi walitaka kulipwa mafao yaao ya miaka iliyopita na kuanza mkataba upya na mwajiri huyo.
Lakini madai hayo yalitawaliwa na mizengwe na kabla halijapatiwa ufumbuzi unaoeleweka, wafanyakazi walikuja na dai jingine wakitaka nyonmgeza ya mishahara.
Dai hilo la pili ndilo lililozaa notisi iliyotolewa jana na iwapo haitatekelezwa hadi Jumatano, wafanyakazi hao wamesema kuwa watagoma.
Iwapo mwajiri atashindwa kutekeleza ombi hilo, wafanyakazi hao wamejiandaa kufanya mgomo nchi nzima na madhara ya mgomo huo yanaweza kuhatarisha hali ya uchumi wa nchi na kusababisha mvugano katika jamii.
Hii ni kwa sababu Reli hiyo ndiyo tegemeo la usafiri kwa mikoa mingi ya bara hivyo iwapo itashindwa kufanya kazi kutokana na mgomo huo, kuna uwezekano mkubwa bidhaa nyingi zikakosekana katika mikoa kadhaa.
Sakata la wafanyakazi hao lilianza mara tu baada ya mkodishaji, kampuni ya rites ya India, alipoingia kuanza kazi mwanzoni mwa mwaka huu.
Baada ya kuja kwa mkodishaji huyo anayemiliki sehemu kubwa ya hisa za kampuni hiyo, wafanyakazi walitaka kulipwa mafao yaao ya miaka iliyopita na kuanza mkataba upya na mwajiri huyo.
Lakini madai hayo yalitawaliwa na mizengwe na kabla halijapatiwa ufumbuzi unaoeleweka, wafanyakazi walikuja na dai jingine wakitaka nyonmgeza ya mishahara.
Dai hilo la pili ndilo lililozaa notisi iliyotolewa jana na iwapo haitatekelezwa hadi Jumatano, wafanyakazi hao wamesema kuwa watagoma.
Sunday, March 9, 2008
Mwanyika azusha maswali mapya kashfa ya EPA
Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Kiongozi wa Timu iliyoteuliwa na Rais Kikwete kuchunguza wizi wa mabilioni ya EPA, Johnsom Mwanyika ametoa taarifa ambayo inaibua maswali mengi bila kujibu maswali yaliyoibuliwa awali.
Katika taarifa hiyo, ambayo kimsingi haina kipya, Mwanyika amewataka watanzania na wanahabari kuwa na uvumilivu wakati Timu yake ikiendelea na kazi ya uchunguzi.
Kwa kudhihirisha kuwa hataki kutoa taarifa mpya, Mwanyika amejificha chini ya kivuli cha kuogopa kuharibu wa upelelezi unaoendelea.
Anasema: “Timu inaona ni vyema kutotoa taarifa ambazo zitaathiri kazi ya uchunguzi inayoendelea. Tunapenda kuusihi Umma na Wanahabari kuwa na subira wakati kazi hii inaendelea.”
Aidha, alishindwa kutaja majina ya watuhumiwa ambao tayari wamerejesha sh bil 50 walizoiba. Mwanyika anasema hawezi kuwataja kwa sababu wao ni makampuni na utu wao unatambuliwa kisheria tu.
Taarifa kamili ya Mwanyika hi hii hapa:
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TIMU YA RAIS YA UCHUNGUZI WA FEDHA ZA EPA
TAARIFA KWA UMMA
Kama mnavyofahamu tarehe 08 Januari, 2008 Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete aliunda Timu inayojumuisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili, pamoja na mambo mengine, kuchunguza na kuchukua hatua za kisheria kwa makampuni na watuhumiwa wa upotevu wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Mheshimiwa Rais alituagiza kuwa tuwe tumekamilisha kazi hiyo katika kipindi cha miezi sita.
Taarifa hii ya tatu inatolewa kufafanua na kutoa taarifa ya namna kazi inavyoendelea kama alivyoagiza Mheshimiwa Rais takriban miezi miwili iliyopita.
Timu inapenda kuufahamisha umma kuwa pamoja na majukumu mengi iliyopewa, kwa sasa Timu imejikita katika kufanya uchunguzi wa kitaalam na wa kina. Kwa msingi huo, pamoja na fedha zinazorudishwa, ni vyema Umma na Wanahabari wakafahamu kuwa kazi ya uchunguzi haijafika mwisho na kwa sasa Timu inaona ni vyema kutotoa taarifa ambazo zitaathiri kazi ya uchunguzi inayoendelea. Tunapenda kuusihi Umma na Wanahabari kuwa na subira wakati kazi hii inaendelea.
Hata hivyo, Timu inapenda kuuhakikishia Umma na Vyombo vya Habari kuwa kazi hii ya uchunguzi inaendelea vizuri na Timu inapata ushirikiano mzuri kutoka kwa makampuni na wamiliki wanaohusika na upotevu wa fedha za EPA.
Vilevile tunapenda kuukumbusha Umma na Wanahabari kuwa Timu imepewa miezi sita ya kufanya kazi na hatimaye kuwasilisha Taarifa kwa Mheshimiwa Rais. Huu ni mwezi wa pili tangu Timu ianze kazi yake. Kwa msingi huo, Timu inawasihi Umma na Wanahabari kuwa na subira kwani Wahenga walisema SUBIRA YAVUTA HERI. Tunawahakakishia kuwa kazi inaendelea vizuri na heri yaja kwani tulichonacho hadi sasa katika uchunguzi si haba.
Vilevile Timu inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu maswali na malalamiko ya kutokamatwa kwa waliohusika. Tunapenda kuueleza umma kwamba uchunguzi wetu hadi hivi sasa unaonyesha kwamba wahusika wakuu ni makampuni. Kisheria, makampuni hayo ni mtu yaani ‘Legal Person’. Hata hivyo, makampuni hayo ni tofauti na mtu wa kawaida. Kampuni katika maana hii, inajitegemea yenyewe.
Kwa msingi huo, ikiwa kampuni imefanya kosa, kuna utaratibu wa kufuata kisheria. Kazi inayofanyika hivi sasa, ni uchunguzi wa kina kuhusu maafisa wa makampuni hayo ili kufahamu ni kitu gani kilichosababisha hali hiyo kutokea. Uchunguzi huu unaendelea na ndiyo utakaotuwezesha kujua hatua za kisheria zitakazochukuliwa.
Timu inapenda kuutarifu Umma na Wanahabari kuwa itaendelea kutoa taarifa ambazo inaamini hazitaathiri uchunguzi unaoendelea mara kwa mara.
Imetolewa na Johnson P.M Mwanyika,
Mwenyekiti wa Timu
9 Machi, 2008
Katika taarifa hiyo, ambayo kimsingi haina kipya, Mwanyika amewataka watanzania na wanahabari kuwa na uvumilivu wakati Timu yake ikiendelea na kazi ya uchunguzi.
Kwa kudhihirisha kuwa hataki kutoa taarifa mpya, Mwanyika amejificha chini ya kivuli cha kuogopa kuharibu wa upelelezi unaoendelea.
Anasema: “Timu inaona ni vyema kutotoa taarifa ambazo zitaathiri kazi ya uchunguzi inayoendelea. Tunapenda kuusihi Umma na Wanahabari kuwa na subira wakati kazi hii inaendelea.”
Aidha, alishindwa kutaja majina ya watuhumiwa ambao tayari wamerejesha sh bil 50 walizoiba. Mwanyika anasema hawezi kuwataja kwa sababu wao ni makampuni na utu wao unatambuliwa kisheria tu.
Taarifa kamili ya Mwanyika hi hii hapa:
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TIMU YA RAIS YA UCHUNGUZI WA FEDHA ZA EPA
TAARIFA KWA UMMA
Kama mnavyofahamu tarehe 08 Januari, 2008 Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete aliunda Timu inayojumuisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili, pamoja na mambo mengine, kuchunguza na kuchukua hatua za kisheria kwa makampuni na watuhumiwa wa upotevu wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Mheshimiwa Rais alituagiza kuwa tuwe tumekamilisha kazi hiyo katika kipindi cha miezi sita.
Taarifa hii ya tatu inatolewa kufafanua na kutoa taarifa ya namna kazi inavyoendelea kama alivyoagiza Mheshimiwa Rais takriban miezi miwili iliyopita.
Timu inapenda kuufahamisha umma kuwa pamoja na majukumu mengi iliyopewa, kwa sasa Timu imejikita katika kufanya uchunguzi wa kitaalam na wa kina. Kwa msingi huo, pamoja na fedha zinazorudishwa, ni vyema Umma na Wanahabari wakafahamu kuwa kazi ya uchunguzi haijafika mwisho na kwa sasa Timu inaona ni vyema kutotoa taarifa ambazo zitaathiri kazi ya uchunguzi inayoendelea. Tunapenda kuusihi Umma na Wanahabari kuwa na subira wakati kazi hii inaendelea.
Hata hivyo, Timu inapenda kuuhakikishia Umma na Vyombo vya Habari kuwa kazi hii ya uchunguzi inaendelea vizuri na Timu inapata ushirikiano mzuri kutoka kwa makampuni na wamiliki wanaohusika na upotevu wa fedha za EPA.
Vilevile tunapenda kuukumbusha Umma na Wanahabari kuwa Timu imepewa miezi sita ya kufanya kazi na hatimaye kuwasilisha Taarifa kwa Mheshimiwa Rais. Huu ni mwezi wa pili tangu Timu ianze kazi yake. Kwa msingi huo, Timu inawasihi Umma na Wanahabari kuwa na subira kwani Wahenga walisema SUBIRA YAVUTA HERI. Tunawahakakishia kuwa kazi inaendelea vizuri na heri yaja kwani tulichonacho hadi sasa katika uchunguzi si haba.
Vilevile Timu inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu maswali na malalamiko ya kutokamatwa kwa waliohusika. Tunapenda kuueleza umma kwamba uchunguzi wetu hadi hivi sasa unaonyesha kwamba wahusika wakuu ni makampuni. Kisheria, makampuni hayo ni mtu yaani ‘Legal Person’. Hata hivyo, makampuni hayo ni tofauti na mtu wa kawaida. Kampuni katika maana hii, inajitegemea yenyewe.
Kwa msingi huo, ikiwa kampuni imefanya kosa, kuna utaratibu wa kufuata kisheria. Kazi inayofanyika hivi sasa, ni uchunguzi wa kina kuhusu maafisa wa makampuni hayo ili kufahamu ni kitu gani kilichosababisha hali hiyo kutokea. Uchunguzi huu unaendelea na ndiyo utakaotuwezesha kujua hatua za kisheria zitakazochukuliwa.
Timu inapenda kuutarifu Umma na Wanahabari kuwa itaendelea kutoa taarifa ambazo inaamini hazitaathiri uchunguzi unaoendelea mara kwa mara.
Imetolewa na Johnson P.M Mwanyika,
Mwenyekiti wa Timu
9 Machi, 2008
Tuesday, March 4, 2008
Butiama Kuitikisa CCM
HALI ya kisiasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) si shwari na taarifa za hivi karibuni zinaonyesha kuwa, makundi ya kisiasa ndani ya chama hicho yameshaanza kujipanga kwa ajili ya kushtakiana ndani ya vikao vikubwa viwili vitakavyoitishwa baadaye mwezi huu.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kwamba, wajumbe wanaounda makundi hayo ambayo yamechipua kutokana na Kashfa ya Richmond wameshaanza kufanya mashauriano ya namna ya kukabiliana wakati wa vikao vya Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.
Maandalizi ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kinatarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu huko Butiama ambako ndiko nyumbani na mahali alikozikwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya makundi hayo mawili, moja likiwa ni lile lililofanikisha kuanguka kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na jingine linalojaribu kumsafisha yeye na wenzake wengine kadhaa tayari yanaonyesha mwelekeo wa kujipanga, tayari kukabiliana na mwenendo huo wa mambo.
Mmoja wa makada maarufu wa chama hicho anayetoka katika kundi linaloshangilia kuanguka kwa Lowassa, Nazir Karamagi na kusakamwa kwa mfanyabiashara Rostam Aziz anasemakuwa tayari walikuwa wameshajipanga kwa ajili ya kukamilisha kazi hiyo.
Mwana CCM huyo ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho, alisema tayari wameshaanza kufuatilia kile walichokiita nyendo za Lowassa na wana CCM wenzake wengine wanaomuunga mkono ili kuweza kupata msingi imara wa kujenga hoja zao dhidi ya kundi hilo.
Kada huyo machachari wa CCM alisema miongoni mwa hadidu za rejea ambazo watazitumia kummaliza Lowassa, Rostam, Karamagi na wanasiasa wenzao wa kundi hilo ni kauli walizozitoa nje ya Bunge dhidi ya ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.
Kwa mujibu wa kada huyo, watu kadhaa wenye msimamo kama wake tayari wameshaanza kukusanya vielelezo na kujenga hoja ambazo wanaamini wakizitumia zitasaidia kuzima jitihada zozote zinazoonekana kuanza za Lowassa na wana CCM wenzake kujisafisha.
Mbali ya Lowassa, kundi hilo linataka pia chama hicho kitoe karipio kali dhidi ya Rostam na Karamagi kutokana na kile wanachokieleza kuwa ni kukitia doa chama na serikali kwa sababu tu ya kuweka kwao mbele maslahi ya kibiashara kuliko ya umma.
Habari zaidi kutoka ndani ya kundi hilo la kwanza zinaeleza kwamba, iwapo mkakati wao huo utakwama ndani ya chama, basi hatua itakayofuata itakuwa ni kuupeleka bungeni ambako wataitumia Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuwachukulia hatua Lowassa na wenzake kadhaa wanaodaiwa kutoa kauli ambazo zinaonyesha dharau kwa Bunge.
Wakati kundi hilo la kwanza likijipanga kwa ajili ya kupigilia msumari wa mwisho katika kile wanachokiona kuwa ni ‘jeneza la kisiasa’ la akina Lowassa, Rostam na Karamagi upande wa pili nao unaonekana kujipanga kwa ajili ya kulikabili kundi hilo la kwanza.
Habari zinaonyesha kuwa, nalo limeanza kukusanya vielelezo kadhaa ambavyo wanataka kuvitumia kwa lengo la kukishawishi chama chao kuwa Kashfa ya Richmond ilikuwa na lengo la kuwadhalilisha, kuwaumiza na kuwamaliza kisiasa.
“We will definitely hit back (Ni wazi kwamba tutajibu mapigo). Hatuwezi tukakaa kimya wakati tukijua waziwazi kwamba watu hawa wameazimia kutuumiza kwa malengo ya kisiasa.
“Hii si haki hata kidogo, mtu unazushiwa uongo wa wazi halafu watu wanakuwa washangiliaji. Ni jambo baya kwamba taasisi za kisheria zimefanya ‘mob justice’ (zinachukua sheria mikononi).
“Hili hatuwezi kukubali liendelee. You wait and see,” alisema mmoja wa wanasiasa hao waliotajwa katika sakata la Richmond ambalo lilisababisha Lowassa ajiuzulu uwaziri mkuu huku Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha wakijiuzulu nyadhifa zao za uwaziri.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kwamba, wajumbe wanaounda makundi hayo ambayo yamechipua kutokana na Kashfa ya Richmond wameshaanza kufanya mashauriano ya namna ya kukabiliana wakati wa vikao vya Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.
Maandalizi ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kinatarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu huko Butiama ambako ndiko nyumbani na mahali alikozikwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya makundi hayo mawili, moja likiwa ni lile lililofanikisha kuanguka kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na jingine linalojaribu kumsafisha yeye na wenzake wengine kadhaa tayari yanaonyesha mwelekeo wa kujipanga, tayari kukabiliana na mwenendo huo wa mambo.
Mmoja wa makada maarufu wa chama hicho anayetoka katika kundi linaloshangilia kuanguka kwa Lowassa, Nazir Karamagi na kusakamwa kwa mfanyabiashara Rostam Aziz anasemakuwa tayari walikuwa wameshajipanga kwa ajili ya kukamilisha kazi hiyo.
Mwana CCM huyo ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho, alisema tayari wameshaanza kufuatilia kile walichokiita nyendo za Lowassa na wana CCM wenzake wengine wanaomuunga mkono ili kuweza kupata msingi imara wa kujenga hoja zao dhidi ya kundi hilo.
Kada huyo machachari wa CCM alisema miongoni mwa hadidu za rejea ambazo watazitumia kummaliza Lowassa, Rostam, Karamagi na wanasiasa wenzao wa kundi hilo ni kauli walizozitoa nje ya Bunge dhidi ya ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.
Kwa mujibu wa kada huyo, watu kadhaa wenye msimamo kama wake tayari wameshaanza kukusanya vielelezo na kujenga hoja ambazo wanaamini wakizitumia zitasaidia kuzima jitihada zozote zinazoonekana kuanza za Lowassa na wana CCM wenzake kujisafisha.
Mbali ya Lowassa, kundi hilo linataka pia chama hicho kitoe karipio kali dhidi ya Rostam na Karamagi kutokana na kile wanachokieleza kuwa ni kukitia doa chama na serikali kwa sababu tu ya kuweka kwao mbele maslahi ya kibiashara kuliko ya umma.
Habari zaidi kutoka ndani ya kundi hilo la kwanza zinaeleza kwamba, iwapo mkakati wao huo utakwama ndani ya chama, basi hatua itakayofuata itakuwa ni kuupeleka bungeni ambako wataitumia Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuwachukulia hatua Lowassa na wenzake kadhaa wanaodaiwa kutoa kauli ambazo zinaonyesha dharau kwa Bunge.
Wakati kundi hilo la kwanza likijipanga kwa ajili ya kupigilia msumari wa mwisho katika kile wanachokiona kuwa ni ‘jeneza la kisiasa’ la akina Lowassa, Rostam na Karamagi upande wa pili nao unaonekana kujipanga kwa ajili ya kulikabili kundi hilo la kwanza.
Habari zinaonyesha kuwa, nalo limeanza kukusanya vielelezo kadhaa ambavyo wanataka kuvitumia kwa lengo la kukishawishi chama chao kuwa Kashfa ya Richmond ilikuwa na lengo la kuwadhalilisha, kuwaumiza na kuwamaliza kisiasa.
“We will definitely hit back (Ni wazi kwamba tutajibu mapigo). Hatuwezi tukakaa kimya wakati tukijua waziwazi kwamba watu hawa wameazimia kutuumiza kwa malengo ya kisiasa.
“Hii si haki hata kidogo, mtu unazushiwa uongo wa wazi halafu watu wanakuwa washangiliaji. Ni jambo baya kwamba taasisi za kisheria zimefanya ‘mob justice’ (zinachukua sheria mikononi).
“Hili hatuwezi kukubali liendelee. You wait and see,” alisema mmoja wa wanasiasa hao waliotajwa katika sakata la Richmond ambalo lilisababisha Lowassa ajiuzulu uwaziri mkuu huku Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha wakijiuzulu nyadhifa zao za uwaziri.
Monday, March 3, 2008
BREAKING NEWS: JENGO LA USHIRIKA LAUNGUA
Sehemu ya jengo maarufu la ushirika, zilimo ofisi mbalimbali imeungua kwa moto usiku wa kuamkia leo. Habari zinapasha kuwa ingawa haijathibitishwa na mamlaka husika, chanzo cha moto huo kinaweza kuwa umeme.
Mashuhuda wanapasha kuwa usiku umeme ulikatika katika jengo hilo na uliporejea baadaye, waliona cheche za moto kana kwamba kuna mtu alikuwa anachomelea vyuma . baada ya muda kidogo waliona moshi mzito ukifuka sehemu hiyo na moto mkubwa kuzuka.
Takriban ofisi 15 zimeungua na mojawapo ni ofisi ya Prince bagenda, ambaye alikuwa katika harakati za kuanzisha gazeti jipya lililotarajiwa kuwa mitaani kwa mara ya kwanza Ijumaa ijayo (bado haijaelezwa kuwa mipango ya kulitoa Ijumaa imefuitwa).
Akizungumza eneo la tukio, Bagenda alisema kuwa vitu vilivyokuwa katika ofisi yake vina thamani ya zaidi y ash milioni 250. vuti hivyo vinajumuisha na kompyuta na vifaa vingine vinavyohusiana na uandaaji wa gazeti.
Aidha, alisema kuwa ndani ya ofisi hiyo ndimo ilimokuwa inaendeshwa mipango ya kuanzisha TV na radio.
Wamiliki wa ofisi zilizoungua wamesema kuwa watatoa taarifa hapo baadaye.
Waziri wa Mambo ya ndani, Lawarence Masha, alifika eneo la tukio leo asubuhi lakini hakutaka kuzungumza chochote bkwa maelezo kuwa hajapatiwa taarifa za kutosha kuhusiana na ajali hiyo.
Mashuhuda wanapasha kuwa usiku umeme ulikatika katika jengo hilo na uliporejea baadaye, waliona cheche za moto kana kwamba kuna mtu alikuwa anachomelea vyuma . baada ya muda kidogo waliona moshi mzito ukifuka sehemu hiyo na moto mkubwa kuzuka.
Takriban ofisi 15 zimeungua na mojawapo ni ofisi ya Prince bagenda, ambaye alikuwa katika harakati za kuanzisha gazeti jipya lililotarajiwa kuwa mitaani kwa mara ya kwanza Ijumaa ijayo (bado haijaelezwa kuwa mipango ya kulitoa Ijumaa imefuitwa).
Akizungumza eneo la tukio, Bagenda alisema kuwa vitu vilivyokuwa katika ofisi yake vina thamani ya zaidi y ash milioni 250. vuti hivyo vinajumuisha na kompyuta na vifaa vingine vinavyohusiana na uandaaji wa gazeti.
Aidha, alisema kuwa ndani ya ofisi hiyo ndimo ilimokuwa inaendeshwa mipango ya kuanzisha TV na radio.
Wamiliki wa ofisi zilizoungua wamesema kuwa watatoa taarifa hapo baadaye.
Waziri wa Mambo ya ndani, Lawarence Masha, alifika eneo la tukio leo asubuhi lakini hakutaka kuzungumza chochote bkwa maelezo kuwa hajapatiwa taarifa za kutosha kuhusiana na ajali hiyo.
Thursday, February 14, 2008
JESHI KATIKA KASHFA
Hospitali ya Jeshi la Lugalo Jijini Dar es Salaam imeingia katika kashfa ya kuwageuza watanzania kuwa nguruwe wa majaribio kwa kuruhusu kufanyika kwa utafiti kwa kutumia dawa iliyopigwa marufuku.
Kashfa hiyo imebainishwa Bunbgeni jana kufuatia swali lililoulizwa na Mbunge machachari wa Karatu, Dk. Wilnrod Slaa na Naibu waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda kukiri kutokea kwa jambo hilo.
Dk. Aisha Kigoda alisema kuwa licha ya taasisi ya serikali, Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupiga marufuku kufanyika kwa utafiti huo, Jeshi, huku likionyesha kiburi, liliiruhusu kampuni moja ya Afrika Kusini, sit u kuleta dawa hizo ziitwazo virodene PO 58 kuzifanyia utafiti kwa kuwatumia watanzania, bali pia kampuni hioyo ilianza kuziuza dawa hizo kiholela mitaani.
Taarifa zilizotolewa na Dk. Slaa akilinukuu gazeti la Washington Post la Marekani, zinaonyesha kuwa watanzania 64 wamefanyiwa majaribio ya dawa hiyo ya ukimwi iliyotengenezwa Afrika Kusini lakini meshapigwa marufuku nchini humo.
Dk. Slaa aliitaka serikali kueleza ni chombo gani cha sheria kilitoa kibali cha watanzania kufanyiwa majaribio ya dawa ambayo imeshapigwa marufuku.
Dk. Slaa alisema kuwa pamoja na Hospitali ya Lugalo, kuna taarifa kuwa majaribio hayo yalifanywa pia katika zahanati binafsi inayomilikiwa na Mkuu wa Jshi la Polisi mstaafu ambaye hakumtaja jina.
Kwa kawaifda, vyombo vya serikali vinavyohusika na utoaji wa vibali vya utafiti wa kisayansi ni Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) pamoja na COSTECH.
Hata hivyo, hakuna hata moja ya taasisi nilizozitaja iliyowahi kutoa kibali kwa ajili ya utafiti huo na kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kuwa ombi la kibali cha kufanya utafiti liliwasilishwa NIMR Julai 2000.
Baada ya NIMR kufanya tathimini ya utafiti huo, ililikataa ombi hilo kwa kuwa andiko kuhusu utafiti wa dawa hiyo lilikuwa na upungufu mkubwa kisayansi na kimaadili.
Lakini katika hali ya kushangaza, hata baada ya kukataliwa kwa ombi la kufanya utafiti, wanasayansi hao waliingiza dawa bila kibali cha serikali na kuanza kufanya utafiti katika hospitali ya Lugalo.
Alipopewa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, Dk. Slaa alimtaka Naibu waziri huyo kueleza hatua zilizochukuliwa kwa watanzania ambao walishirikiana na watafiti hao kutoka nje kufanya uhalifu huo.
Dk. Slaa alisema anazo taarifa kuwa ombi la utafiti lilipokataliwa na NIMR, viongozi wa Jeshi walisema wazi wazi kuwa Wizara ya asfya haihusiki kutoa vibali vya utafiti.
Dk. Kigoda hakulijibu swali hilo ipasavyo kwani hakueleza viongozi wa jeshi walioshiriki kuwaleta watafiti hao walichukuliwa hatua gani.
Badala yake, alilieleza Bunge kuwa Wizara ilikaa na Jeshi la kukubaliana kuwa utafiti huo usiendelee na kuwa iwapo wanataka utafiti huo unedelee basi wafuate sheria na taratibu zilizopo.
Kashfa hiyo imebainishwa Bunbgeni jana kufuatia swali lililoulizwa na Mbunge machachari wa Karatu, Dk. Wilnrod Slaa na Naibu waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda kukiri kutokea kwa jambo hilo.
Dk. Aisha Kigoda alisema kuwa licha ya taasisi ya serikali, Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupiga marufuku kufanyika kwa utafiti huo, Jeshi, huku likionyesha kiburi, liliiruhusu kampuni moja ya Afrika Kusini, sit u kuleta dawa hizo ziitwazo virodene PO 58 kuzifanyia utafiti kwa kuwatumia watanzania, bali pia kampuni hioyo ilianza kuziuza dawa hizo kiholela mitaani.
Taarifa zilizotolewa na Dk. Slaa akilinukuu gazeti la Washington Post la Marekani, zinaonyesha kuwa watanzania 64 wamefanyiwa majaribio ya dawa hiyo ya ukimwi iliyotengenezwa Afrika Kusini lakini meshapigwa marufuku nchini humo.
Dk. Slaa aliitaka serikali kueleza ni chombo gani cha sheria kilitoa kibali cha watanzania kufanyiwa majaribio ya dawa ambayo imeshapigwa marufuku.
Dk. Slaa alisema kuwa pamoja na Hospitali ya Lugalo, kuna taarifa kuwa majaribio hayo yalifanywa pia katika zahanati binafsi inayomilikiwa na Mkuu wa Jshi la Polisi mstaafu ambaye hakumtaja jina.
Kwa kawaifda, vyombo vya serikali vinavyohusika na utoaji wa vibali vya utafiti wa kisayansi ni Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) pamoja na COSTECH.
Hata hivyo, hakuna hata moja ya taasisi nilizozitaja iliyowahi kutoa kibali kwa ajili ya utafiti huo na kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kuwa ombi la kibali cha kufanya utafiti liliwasilishwa NIMR Julai 2000.
Baada ya NIMR kufanya tathimini ya utafiti huo, ililikataa ombi hilo kwa kuwa andiko kuhusu utafiti wa dawa hiyo lilikuwa na upungufu mkubwa kisayansi na kimaadili.
Lakini katika hali ya kushangaza, hata baada ya kukataliwa kwa ombi la kufanya utafiti, wanasayansi hao waliingiza dawa bila kibali cha serikali na kuanza kufanya utafiti katika hospitali ya Lugalo.
Alipopewa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, Dk. Slaa alimtaka Naibu waziri huyo kueleza hatua zilizochukuliwa kwa watanzania ambao walishirikiana na watafiti hao kutoka nje kufanya uhalifu huo.
Dk. Slaa alisema anazo taarifa kuwa ombi la utafiti lilipokataliwa na NIMR, viongozi wa Jeshi walisema wazi wazi kuwa Wizara ya asfya haihusiki kutoa vibali vya utafiti.
Dk. Kigoda hakulijibu swali hilo ipasavyo kwani hakueleza viongozi wa jeshi walioshiriki kuwaleta watafiti hao walichukuliwa hatua gani.
Badala yake, alilieleza Bunge kuwa Wizara ilikaa na Jeshi la kukubaliana kuwa utafiti huo usiendelee na kuwa iwapo wanataka utafiti huo unedelee basi wafuate sheria na taratibu zilizopo.
Thursday, February 7, 2008
BREAKING NEWS: Lowassa Aomba Kujiuzulu
Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ameandika barua kjwa Rais Jakaya Kikwete akiomba kujiuzulu wadhifa huo.
Lowassa alitangaza hayo Bungeni leo wakati alipotakiwa kuchangia ripoti ya Kamati nTeule ya Bunge kuhusu kampuni ya Richmond.
Lowassa amesema kuwa ameamua kujiuzulu ili kuonyesha uwajibikaji ingawa hakubaliani na jinsi kamati hiyo ilivyomhukumu bila kumhoji.
Alisema kuwa baada ya kuisoma taarifa ya kamati hiyo amebaini kuwa kinachotakiwa ni Uwaziri Mkuu, hivyo kwa manufaa ya serikali, chama chake na nchi, ameamua kuuachia wadhifa huo.
Huku akiongea kwa masikitiko makubwa, Lowassa alisema kuwa imemshangaza kuwa wakati ripoti hiyo inamtuhumu yeye, hakuhojiwa wakati yeye alikuwa tayari kutoa maelezo yake. Alisema ahata aliponong'onezwa suala hilo na Spika, samwel Sitta, alimletea ushahidi wa maandishi.
Habari kutoka Ikulu zinaeleza kuwa tayari barua hiyo imeshapokelewa na maamuzi yatakapofanywa yatatangazwa.
Mwandishi wa Habari wa rais, Premmy Kibanga aliiambia tovuti hii kuwa suala hilo litatangazwa hadharani ingawa hakusema lini maamuzi hayo yatafanywa na kutangazwa
Lowassa alitangaza hayo Bungeni leo wakati alipotakiwa kuchangia ripoti ya Kamati nTeule ya Bunge kuhusu kampuni ya Richmond.
Lowassa amesema kuwa ameamua kujiuzulu ili kuonyesha uwajibikaji ingawa hakubaliani na jinsi kamati hiyo ilivyomhukumu bila kumhoji.
Alisema kuwa baada ya kuisoma taarifa ya kamati hiyo amebaini kuwa kinachotakiwa ni Uwaziri Mkuu, hivyo kwa manufaa ya serikali, chama chake na nchi, ameamua kuuachia wadhifa huo.
Huku akiongea kwa masikitiko makubwa, Lowassa alisema kuwa imemshangaza kuwa wakati ripoti hiyo inamtuhumu yeye, hakuhojiwa wakati yeye alikuwa tayari kutoa maelezo yake. Alisema ahata aliponong'onezwa suala hilo na Spika, samwel Sitta, alimletea ushahidi wa maandishi.
Habari kutoka Ikulu zinaeleza kuwa tayari barua hiyo imeshapokelewa na maamuzi yatakapofanywa yatatangazwa.
Mwandishi wa Habari wa rais, Premmy Kibanga aliiambia tovuti hii kuwa suala hilo litatangazwa hadharani ingawa hakusema lini maamuzi hayo yatafanywa na kutangazwa
Wednesday, February 6, 2008
BREAKING NEWS: Lowassa ananuka Richmond
Kamati teule ya Bunge, iliyopewa kazi ya kuangalia mkataba wa uzalishaji umeme wa dharura kati ya kampuni ya Richmond Development ya Marekani na serikali, imemkuta waziri Mkuu, Edward Lowassa, akiwa mchafu kimaadili na kumshauri kujiuzulu.
Kwa maneno yake, kamati hiyo inahitimisha: “Kamati teule haikufurahishwa hata kidogo na taarifa zinazomgusa moja kwa mowa moja Mhe waziri Mkuu katika kuipendelea Richmond Development Company LLC. Hata hivyo, Kamati teule imetimiza wajibu wake kwa uwazi na ukweli kama ilivyoagizwa na Bunge letu tukufu.
“Kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi aliyonayo Mhe. Waziri Mkuu katika uendeshaji wa shughuli za serikali na uongozi wan chi kwa ujumla, ni wajibu wake yeye mwenyewe kupima uzito wa matokeo ya uchunguzi huu na wajibu wake kikatiba ndani na nje ya Bunge.
“Vile vile ni wajibu wa Bunge ambalo linathibitisha uteuzi wake kwa mujibu wa Ibara ya 51 inayothibitisha uteuzi wake, kuangalia ikiwa matokeo ya uchunguzi huu hayajaathiri hadhi na uzito wake ndani ya Bunge.”
Kwa maneno mengine, Kamati hiyo iliyokuwa inaongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe (Kyela-CCM) ilikuwa inamtaka waziri Mkuu kujiuzulu kutokana na kuhusika kwake na kashfa hiyo.
Aidha, iwapo Lowassa angeshindwa kuchukua uamuzi wa kumwajibisha kwa kumpigia kura ya kutokwua na imani naye.
Kwa ujumla, Kamati hiyo imebaini kuwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha, na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wanahusishwa moja kwa moja na kuipatia kampuni hiyo kazi ya kuzalisha umeme wa dharura wakati ikiwa haina sifa.
Aidha, wengine wanaotajwa katika ripoti hiyo na kushauri wawajibishwe kutokana na ushiriki wao katika sakata hilo ni waziri wa sasa wa Nishati na Madini, nazir Karamagi, katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Ather Mwakapugi pamoja na Kamishna wa Madini, Bashir Mrindoko.
Wengine ni Mwanassheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye kwa mujibuw a ripoti hiyo ameonekana kutojua alichokuwa anakifanya wakati baadhi ya viongozi wakiwa wanatekjeleza njama za kupindisha sheria na taratibu ili kuhakikisha kuwa Richmond inapatiwa kazi hiyo.
Uchunguzi wa Kamati pia ulibaini kuhusika kwa aliyekuwa waziri katika serikali ya awamu ya tatu, Daniel Yona, jinsi ambavyio naye alishiriki katika kuhakikisha kuwa Richmond inapata kazi hiyo.
Inaelezwa katika ripoti hiyo kuwa Dk. Msabaha aliamua kukiuka maagizo ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na mchakato wa kuipata kampuni itakayozalisha umeme wa dharura, na kuilazimisha Tanesco kupindisha taratibu na kuikumbatia Richmond ingawa ilidhihirika wazi kuwa haikuwa na sifa ya kupata kazi hiyo.
Hata hivyo, Msabaha anakaririwa na ripoti hiyo akisema kuwa katika suala hilo, yeye amefanywa kuwa kondoo wa kafara tu.
Mtiririko wa ripoti hiyo unaonyesha kuwepo kwa maelekezo na maagizo kutoka kwa Lowassa, kwenda kwa Dk. Msabaha kuhakikisha kuwa Richmond inapatiwa kazi hiyo kwa njia yoyote ile.
Pia ripoti hiyo imeonyesha jinsi Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Nchini (Takukuru), kwa jinsi ambavyo ilitumia mamlaka yake kuficha ukweli wa mambo na kuisafisha Richmond pamoja na viongozi wasio waadilifu walioileta kampuni hiyo.
Kwa msingi huo, Kamati hiyo imependekeza kuwa uongozi wa Takukuru ufanyiwe mabadiliko makubwa ili kulinda hadhi ya taasisi hiyo muhimu katika mapamvbano dhidi ya rushwa.
Kwa maneno yake, kamati hiyo inahitimisha: “Kamati teule haikufurahishwa hata kidogo na taarifa zinazomgusa moja kwa mowa moja Mhe waziri Mkuu katika kuipendelea Richmond Development Company LLC. Hata hivyo, Kamati teule imetimiza wajibu wake kwa uwazi na ukweli kama ilivyoagizwa na Bunge letu tukufu.
“Kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi aliyonayo Mhe. Waziri Mkuu katika uendeshaji wa shughuli za serikali na uongozi wan chi kwa ujumla, ni wajibu wake yeye mwenyewe kupima uzito wa matokeo ya uchunguzi huu na wajibu wake kikatiba ndani na nje ya Bunge.
“Vile vile ni wajibu wa Bunge ambalo linathibitisha uteuzi wake kwa mujibu wa Ibara ya 51 inayothibitisha uteuzi wake, kuangalia ikiwa matokeo ya uchunguzi huu hayajaathiri hadhi na uzito wake ndani ya Bunge.”
Kwa maneno mengine, Kamati hiyo iliyokuwa inaongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe (Kyela-CCM) ilikuwa inamtaka waziri Mkuu kujiuzulu kutokana na kuhusika kwake na kashfa hiyo.
Aidha, iwapo Lowassa angeshindwa kuchukua uamuzi wa kumwajibisha kwa kumpigia kura ya kutokwua na imani naye.
Kwa ujumla, Kamati hiyo imebaini kuwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha, na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wanahusishwa moja kwa moja na kuipatia kampuni hiyo kazi ya kuzalisha umeme wa dharura wakati ikiwa haina sifa.
Aidha, wengine wanaotajwa katika ripoti hiyo na kushauri wawajibishwe kutokana na ushiriki wao katika sakata hilo ni waziri wa sasa wa Nishati na Madini, nazir Karamagi, katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Ather Mwakapugi pamoja na Kamishna wa Madini, Bashir Mrindoko.
Wengine ni Mwanassheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye kwa mujibuw a ripoti hiyo ameonekana kutojua alichokuwa anakifanya wakati baadhi ya viongozi wakiwa wanatekjeleza njama za kupindisha sheria na taratibu ili kuhakikisha kuwa Richmond inapatiwa kazi hiyo.
Uchunguzi wa Kamati pia ulibaini kuhusika kwa aliyekuwa waziri katika serikali ya awamu ya tatu, Daniel Yona, jinsi ambavyio naye alishiriki katika kuhakikisha kuwa Richmond inapata kazi hiyo.
Inaelezwa katika ripoti hiyo kuwa Dk. Msabaha aliamua kukiuka maagizo ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na mchakato wa kuipata kampuni itakayozalisha umeme wa dharura, na kuilazimisha Tanesco kupindisha taratibu na kuikumbatia Richmond ingawa ilidhihirika wazi kuwa haikuwa na sifa ya kupata kazi hiyo.
Hata hivyo, Msabaha anakaririwa na ripoti hiyo akisema kuwa katika suala hilo, yeye amefanywa kuwa kondoo wa kafara tu.
Mtiririko wa ripoti hiyo unaonyesha kuwepo kwa maelekezo na maagizo kutoka kwa Lowassa, kwenda kwa Dk. Msabaha kuhakikisha kuwa Richmond inapatiwa kazi hiyo kwa njia yoyote ile.
Pia ripoti hiyo imeonyesha jinsi Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Nchini (Takukuru), kwa jinsi ambavyo ilitumia mamlaka yake kuficha ukweli wa mambo na kuisafisha Richmond pamoja na viongozi wasio waadilifu walioileta kampuni hiyo.
Kwa msingi huo, Kamati hiyo imependekeza kuwa uongozi wa Takukuru ufanyiwe mabadiliko makubwa ili kulinda hadhi ya taasisi hiyo muhimu katika mapamvbano dhidi ya rushwa.
Friday, February 1, 2008
Masuala Nyeti Yapigwa Danadana Bungeni
KIU ya watanzania kufahamu hatma ya hoja nyeti zinazosubiri maamuzi ya Bunge itabidi kusubiri kwa wiki moja zaidi.
Hii ni kutokana na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kutangaza kuwa masuala hayo nyeti, hayatajadiliwa Bungeni wiki hii hadi atakaporejea kutoka Marekani.
Spika Sitta alitangaza kuwa atakuwa na ziara ya wiki moja nchini Marekani alikoalikwa na Baraza la Wawakilishi na kutoa maelekezo kuwa katika muda ambao hatokuwepo, masuala nyeti yaliyo Bungeni yatapaswa kusubiri.
Alisema kuwa anatarajia kuondoka Jumatatu na kurejea Alhamisi hivyo Naibu Spika, Anne Makinda, atakaimu nafasi yake lakini kati ya majukumu yake hayatahusisha kushughulikia masuala hayo nyeti.
Sitta aliyataja masuala hayo kuwa ni pamoja na suala la ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoangalia mchakato wakuipata kampuni ya Richmond Development (RDC) ya Marekani, iliyopewa kandarasi ya kuzalisha umeme za dharura wakati taifa lilipokabiliwa na upungufu wa nishati hiyo mwaka juzi.
Pia aliitaja hoja nyingine nzito kuwa ni lile linalohusiana na sakata la kashfa ya akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) ya Benki Kuu (BoT).
“Sikutaka Naibu Spika akurupuke na kuvamia masuala haya nyeti, itabidi yasubiri mpaka pale nitakaporejea… tunayo wiki nzima ya kuyaangalia haya,” alisema.
Hata hivyo, dalili za kupigwa danadana kwa suala la EPA zilianza kuonekana mapema Bungeni jana wakati wa kipindi cha maswali na majibu, pale ambapo masuali kuhusiana na suala hilo yalipozuiliwa na Spika, kwa maelezo kuwa suala hilo bado linajadiliwa.
Wakati fulani, Spika alizima swali la nyongeza lililoulizwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed (Wawi-CUF), ambaye baada ya Naibu Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo kubainisha kuwa suala la EPA linafanyiwa kazi kutokana na maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
Aliposimama kuuliza swali la nyongeza, Hamad Rashid alikumbusha kwua kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, taasisi hiyo ambayo ni moja ya mihimili ya utawala, haizuiliwi kujadili suala ambalo linachunguzwa na taasisi nyingine, ukiacha masuala ambayo yapo mahakamani.
Lakini Spika badala ya kumwita Mkulo kujibu suala hilo, alisimama na kutoa maelezo kuwa alishatoa maelezo awali kuwa majadiliano kuhusu suala hilo yanaendelea na atalitaarifu Bunge hatma ya majadiliano hayo.
Baada ya jitihada za Hamad Rashid kugonga mwamba, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema) alisimama kwa lengo la kuuliza swali la nyongeza, na kwa kudhani kuwa anakusudiakuuliza swali kuhusiana na suala hilo, Spika alimzuia akisema kuwa maelezo aliyoyatoa yameizima hoja hiyo kuendelea kuhojiwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa mapema wiki hii, Spika aliliambia Bunge kuwa ndani ya wiki huii angetoa taarifa kuhusiana na matokeo ya mashauriano kati ya ofisi yake na serikali kuhusiana na suala la kuwasilishwa Bungeni kwa ripoti kamili iliyoandaliwa na kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu ya Ernst & Young kuhusiana na EPA.
Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili nje ya Bunge baada ya kipindi cha maswali na najibu, Zitto alisema kuwa lengo lake la kusimama halikuwa kuulizia masuala ya EPA.
“Inaonekana mzimu wa EPA umevawaa serikalini, kila kitu wao wanaona kama EPA… mimi sikutaka kuulizia kuhusu EPA, hoja yangu ilikuwa ni kuwa Naibu Waziri hakujibu swali lililoulizwa.
“Swali liliuliza kuhusu Debt Conversion Scheme, hizi ni fedha ilizoliwa na wafanyabishara waliouziwa madeni, hilo ndilo lililoulizwa lakini waziri alikwepa kulijibu hilo,” alisema Zitto.
Hii ni kutokana na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kutangaza kuwa masuala hayo nyeti, hayatajadiliwa Bungeni wiki hii hadi atakaporejea kutoka Marekani.
Spika Sitta alitangaza kuwa atakuwa na ziara ya wiki moja nchini Marekani alikoalikwa na Baraza la Wawakilishi na kutoa maelekezo kuwa katika muda ambao hatokuwepo, masuala nyeti yaliyo Bungeni yatapaswa kusubiri.
Alisema kuwa anatarajia kuondoka Jumatatu na kurejea Alhamisi hivyo Naibu Spika, Anne Makinda, atakaimu nafasi yake lakini kati ya majukumu yake hayatahusisha kushughulikia masuala hayo nyeti.
Sitta aliyataja masuala hayo kuwa ni pamoja na suala la ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoangalia mchakato wakuipata kampuni ya Richmond Development (RDC) ya Marekani, iliyopewa kandarasi ya kuzalisha umeme za dharura wakati taifa lilipokabiliwa na upungufu wa nishati hiyo mwaka juzi.
Pia aliitaja hoja nyingine nzito kuwa ni lile linalohusiana na sakata la kashfa ya akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) ya Benki Kuu (BoT).
“Sikutaka Naibu Spika akurupuke na kuvamia masuala haya nyeti, itabidi yasubiri mpaka pale nitakaporejea… tunayo wiki nzima ya kuyaangalia haya,” alisema.
Hata hivyo, dalili za kupigwa danadana kwa suala la EPA zilianza kuonekana mapema Bungeni jana wakati wa kipindi cha maswali na majibu, pale ambapo masuali kuhusiana na suala hilo yalipozuiliwa na Spika, kwa maelezo kuwa suala hilo bado linajadiliwa.
Wakati fulani, Spika alizima swali la nyongeza lililoulizwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed (Wawi-CUF), ambaye baada ya Naibu Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo kubainisha kuwa suala la EPA linafanyiwa kazi kutokana na maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
Aliposimama kuuliza swali la nyongeza, Hamad Rashid alikumbusha kwua kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, taasisi hiyo ambayo ni moja ya mihimili ya utawala, haizuiliwi kujadili suala ambalo linachunguzwa na taasisi nyingine, ukiacha masuala ambayo yapo mahakamani.
Lakini Spika badala ya kumwita Mkulo kujibu suala hilo, alisimama na kutoa maelezo kuwa alishatoa maelezo awali kuwa majadiliano kuhusu suala hilo yanaendelea na atalitaarifu Bunge hatma ya majadiliano hayo.
Baada ya jitihada za Hamad Rashid kugonga mwamba, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema) alisimama kwa lengo la kuuliza swali la nyongeza, na kwa kudhani kuwa anakusudiakuuliza swali kuhusiana na suala hilo, Spika alimzuia akisema kuwa maelezo aliyoyatoa yameizima hoja hiyo kuendelea kuhojiwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa mapema wiki hii, Spika aliliambia Bunge kuwa ndani ya wiki huii angetoa taarifa kuhusiana na matokeo ya mashauriano kati ya ofisi yake na serikali kuhusiana na suala la kuwasilishwa Bungeni kwa ripoti kamili iliyoandaliwa na kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu ya Ernst & Young kuhusiana na EPA.
Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili nje ya Bunge baada ya kipindi cha maswali na najibu, Zitto alisema kuwa lengo lake la kusimama halikuwa kuulizia masuala ya EPA.
“Inaonekana mzimu wa EPA umevawaa serikalini, kila kitu wao wanaona kama EPA… mimi sikutaka kuulizia kuhusu EPA, hoja yangu ilikuwa ni kuwa Naibu Waziri hakujibu swali lililoulizwa.
“Swali liliuliza kuhusu Debt Conversion Scheme, hizi ni fedha ilizoliwa na wafanyabishara waliouziwa madeni, hilo ndilo lililoulizwa lakini waziri alikwepa kulijibu hilo,” alisema Zitto.
Tuesday, January 29, 2008
Wabunge Wadai Ripoti Kamili ya Ernst & Young
SASA inaelekea mambo yataanza kunoga. Wabunge wameshaanza kuidai ripoti kamili iliyoandikwa na kampuni ya Ernst & Young kuhusiana na ubadhirifu uliobainika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), iliyopo Benki Kuu (BoT).
Wabunge walitoa msimamo wao huo jana, mara baada ya Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, kumaliza kuwasilisha bungeni kauli ya serikali ambayo ilikuwa ni taarifa kuhusu ripoto ya ukaguzi wa EPA.
Wabunge waliona huo ni mwanzo wa ubabaishaji kwani alichokiwasilisha Meghji ilikuwa ni muhtasari wa kilichomo katika ripoti ya Ernst & Young, na hatua ambazo rais Jakaya Kikwete na Wizara yake imezichukua baada ya kukabidhiwa ripoti hiyo.
Taarifa hiyo ya Meghji, haina tofauti sana na taarifa ambayo ilitolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, ikielezea kilichobainika katika ukaguzi uliofanywa na Ernst & Young na hatua ambazo rais Kikwete alizichukua.
Baada ya kumaliza kusoma kauli hiyo, Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo (UDP) na Christopher ole Sendeka (Simanjiro-CCM), walisimama wakitaka mwongozi wa Spika kuhusiana na suala hilo.
Alipopewa nafasi ya kusema, Cheyo alieleza kuwa taarifa iliyoeasilishwa na Meghji ni nzuri, lakini akabainisha kuwa ni finyu mno ukilinganisha ya ripoti ya Ernst & Young.
Aidha, Cheyo alihoji iwapo ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) itawasilishwa Bungeni na kutaka tipoti hiyo, pamoja na taarifa ya Meghji, vyote vijadiliwe na wabunge kwa kina
Kwa upande wake, Sendeka aliposimama, alibainisha kuwa kilichowasilishwa na Waziri Meghji ni muhtasari tu.
Huku akimwelekea Spika, ole Sendeka alisema: “Naomba kama itakubalika uielekeze serikali ilete taarifa kamili ya mkaguzi (Ernst & Young) na bunge lipate fursa ya kuijadili kwa kina.”
Kwa kuoinyesha kuwa wanaunga mkono yanayowasilishwa na wenzao, wabunge wengi walikuwa wakishangilia kwa kupiga makofi wakati wabunge hao wawili walipokuwa wakiwasilisha hoja zao.
Akijibu maombi hayo, Spika Samuel Sitta alikubaliana na hoja za wabunge hao na kusema kuwa yote waliyaomba yamo katika mchakato wa mashauriano baina ya ofisi ya Spika na serikali.
Aliwakumbusha watoa hoja na wabunge wengine kwua tangu awali, alishakubaliana na hoja iliyowasilishwa na Lucy Mayenga (Viti Maalum-CCM), akitaka ripoti ya hesabu za BoT za mwaka 2005/06 iwasilishwe bungeni na kujadiliwa na wabunge wote.
“Hoja hii bado ni hai na taarifa iliyotolewa leo si kipingamizi. Naamini kuwa katika wakati huu wa uwazi na ukweli serikali imeeshasikia hoja zenu na itazitafakari ipasavyo na bila shaka tutafikia mahali pazuri,” alisema Spika Sitta.
Katika taarifa aliyoiwasilisha jana Bungeni, pamoja na kubainisha yaliyogunduliwa na Ernst & Young katika ukaguzi wa EPA na hatua zilizochukuliwa na rais, meghji alisema kuwa wizara yake nayo imechukua hatua kadhaa.
Alisema kuwa baada ya kupata ripoti hiyo, Wizara ya fedha imeiagiza Mamlaka ya Mapato cnhini (TRA), kufanya uchunguzi wa kina kubaini mienendo ya ulipaji kodi wa makampuni yote yaliyohiska katia kashfa ya EPA.
Aidha, Meghji alisema kuwa iwapo itabainika kuwaepo kwa ukwepaji wa kodi, TRA imetakiwa kuchukua hatua za kisheria.
Pia wizara yake imeielekeza BoT kufanya uhcunguzi wa kina na kuwasilisha taarifa serikalini kuhusu hatua zilizochukuliwa kwa mabenkiya biashara yaliyohusika na kupokea fedha kutoka makampuni yaliyotajwa kuhusika katika kashfa ya EPA, iwapo sheria, taratibu na kanuni kuhusu udhibioti wa fedha haramu zilizingatiwa.
Aidha, akifafanua hatua ya rais Kikwete kuwaagiza Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG), Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) kuchunguza zaidi suala hilo, unalenga kupata ushahidi wa kisheria utakaowezesha kufunguliwa kwa mashtaka dhidi ya watu na kampuni zote zilizohusika katika kashfa ya EPA.
Wabunge walitoa msimamo wao huo jana, mara baada ya Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, kumaliza kuwasilisha bungeni kauli ya serikali ambayo ilikuwa ni taarifa kuhusu ripoto ya ukaguzi wa EPA.
Wabunge waliona huo ni mwanzo wa ubabaishaji kwani alichokiwasilisha Meghji ilikuwa ni muhtasari wa kilichomo katika ripoti ya Ernst & Young, na hatua ambazo rais Jakaya Kikwete na Wizara yake imezichukua baada ya kukabidhiwa ripoti hiyo.
Taarifa hiyo ya Meghji, haina tofauti sana na taarifa ambayo ilitolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, ikielezea kilichobainika katika ukaguzi uliofanywa na Ernst & Young na hatua ambazo rais Kikwete alizichukua.
Baada ya kumaliza kusoma kauli hiyo, Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo (UDP) na Christopher ole Sendeka (Simanjiro-CCM), walisimama wakitaka mwongozi wa Spika kuhusiana na suala hilo.
Alipopewa nafasi ya kusema, Cheyo alieleza kuwa taarifa iliyoeasilishwa na Meghji ni nzuri, lakini akabainisha kuwa ni finyu mno ukilinganisha ya ripoti ya Ernst & Young.
Aidha, Cheyo alihoji iwapo ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) itawasilishwa Bungeni na kutaka tipoti hiyo, pamoja na taarifa ya Meghji, vyote vijadiliwe na wabunge kwa kina
Kwa upande wake, Sendeka aliposimama, alibainisha kuwa kilichowasilishwa na Waziri Meghji ni muhtasari tu.
Huku akimwelekea Spika, ole Sendeka alisema: “Naomba kama itakubalika uielekeze serikali ilete taarifa kamili ya mkaguzi (Ernst & Young) na bunge lipate fursa ya kuijadili kwa kina.”
Kwa kuoinyesha kuwa wanaunga mkono yanayowasilishwa na wenzao, wabunge wengi walikuwa wakishangilia kwa kupiga makofi wakati wabunge hao wawili walipokuwa wakiwasilisha hoja zao.
Akijibu maombi hayo, Spika Samuel Sitta alikubaliana na hoja za wabunge hao na kusema kuwa yote waliyaomba yamo katika mchakato wa mashauriano baina ya ofisi ya Spika na serikali.
Aliwakumbusha watoa hoja na wabunge wengine kwua tangu awali, alishakubaliana na hoja iliyowasilishwa na Lucy Mayenga (Viti Maalum-CCM), akitaka ripoti ya hesabu za BoT za mwaka 2005/06 iwasilishwe bungeni na kujadiliwa na wabunge wote.
“Hoja hii bado ni hai na taarifa iliyotolewa leo si kipingamizi. Naamini kuwa katika wakati huu wa uwazi na ukweli serikali imeeshasikia hoja zenu na itazitafakari ipasavyo na bila shaka tutafikia mahali pazuri,” alisema Spika Sitta.
Katika taarifa aliyoiwasilisha jana Bungeni, pamoja na kubainisha yaliyogunduliwa na Ernst & Young katika ukaguzi wa EPA na hatua zilizochukuliwa na rais, meghji alisema kuwa wizara yake nayo imechukua hatua kadhaa.
Alisema kuwa baada ya kupata ripoti hiyo, Wizara ya fedha imeiagiza Mamlaka ya Mapato cnhini (TRA), kufanya uchunguzi wa kina kubaini mienendo ya ulipaji kodi wa makampuni yote yaliyohiska katia kashfa ya EPA.
Aidha, Meghji alisema kuwa iwapo itabainika kuwaepo kwa ukwepaji wa kodi, TRA imetakiwa kuchukua hatua za kisheria.
Pia wizara yake imeielekeza BoT kufanya uhcunguzi wa kina na kuwasilisha taarifa serikalini kuhusu hatua zilizochukuliwa kwa mabenkiya biashara yaliyohusika na kupokea fedha kutoka makampuni yaliyotajwa kuhusika katika kashfa ya EPA, iwapo sheria, taratibu na kanuni kuhusu udhibioti wa fedha haramu zilizingatiwa.
Aidha, akifafanua hatua ya rais Kikwete kuwaagiza Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG), Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) kuchunguza zaidi suala hilo, unalenga kupata ushahidi wa kisheria utakaowezesha kufunguliwa kwa mashtaka dhidi ya watu na kampuni zote zilizohusika katika kashfa ya EPA.
Thursday, January 17, 2008
Mgonja Anangoja Nini Hazina?
HATUA ya Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wa Daudi Ballali kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) inadhihirisha kuwa kulikuwa na makosa makubwa katika taasisi hiyo nyeti. Ukubwa wa makosa hayo unaweza kuonekana kupitia hatua hiyo ya rais ambayo kwa namna yoyote ile ni hatua kubwa mno.
Hatua yake ya kuagiza vyombo kadhaa kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua watu wengine waliohusika na kashfa hiyo, inadhihirisha pia kuwa Ballali si mhusika pekee katika sakata hili. Wapo wengine wengi tu ambao baadhi yao ni rahisi kuwatambua kutokana na nafasi zao.
Mtu asiyeweza kukwepa kunukia tuhuma hizi moja kwa moja ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha. Kwa mujibu wa wadhifa huo, mtu huyo ndiye anayehusika kuidhinisha malipo ambayo serikali inayafanya. Kwa Kiingereza yeye anaitwa ‘Paymaster General.’
Kashfa iliyomng’oa Ballali inahusiana na malipo. Ni malipo ya Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) iliyopo BoT. Kwa sababu malipo haya yalifanywa na serikali ni dhahiri kuwa ‘Paymaster General’ aliidhinisha yafanyike.
Malipo yaliyotiliwa shaka na kuchunguzwa ni yale yaliyofanyika kipindi cha 2005/2006 wakati huo Gray Mgonja akiwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha pamoja na Peniel Lyimo. Lyimo alikwishaondolewa wizarani hapo lakini Mgonja bado anaendelea na wadhifa wake huo hadi hivi sasa.
Iwapo tunataka kupata maelezo ya kina kuhusiana na malipo haya, Mgonja na Lyimo wanaweza kutusaidia sana. Watatusaidia kwa sababu wao au mmoja wao - kulingana na mgawanyo wa kazi zao - ndio walioidhinisha malipo haya.
Kwa kawaida ‘paymaster general’ anaidhinisha malipo baada ya kujiridhisha kuwa malipo hayo ni halali na yanatolewa kwa kufuata taratibu zote za kiserikali zilizopo. Itashangaza sana iwapo ‘paymaster general’ akaamua kutoa tu fedha na kuzilipa bila kufuata taratibu hizo.
Kwa maana hiyo, Mgonja na Lyimo wanayo nafasi nzuri ya kutueleza Watanzania nini hasa kilifanyika katika malipo haya. Wala wasikwepe hili kwa namna yoyote ile kwa sababu wao ndio walihusika kuidhinisha malipo hayo.
Watueleze ilikuwaje wakakubali kuidhinisha malipo ya mabilioni haya ya fedha za wavuja jasho na kututia hasara kiasi hicho? Umakini wao uko wapi katika kuidhinisha malipo ya fedha zetu? Iwapo waliweza kuidhinisha malipo haya yenye kutia shaka, watashindwaje kuidhinisha malipo mengine mengi tu tusokuwa na habari nayo?
Uchunguzi uliofanywa unahusu mwaka 2005/2006 lakini akaunti ya EPA imefanya kazi kwa miaka mingi na Mgonja na Lyimo (pamoja na wengine) wamekuwapo wizarani wakiidhinisha malipo kupitia akaunti hii kwa miaka hiyo yote.
Inashangaza kuwa Mgonja bado anaendelea kuwapo madarakani hadi hivi sasa, wakati kasoro kubwa kama hii imeshajitokeza na Rais ameshawaonyesha Watanzania kuwa kuna kasoro kubwa kiasi cha yeye kutengua uteuzi wa gavana.
Kuna uwezekano kuwa gavana alihusika na wizi uliogunduliwa lakini pia kuna uwezekano kuwa hakuhusika. Kama alihusika hiyo ni sababu tosha ya Rais kusikiliza na kutekeleza maombi ya watu wanaotaka Ballali arudi nchini kuja kukabili mashtaka kuhusiana na kadhfa hiyo ya EPA.
Lakini kama hakuhusika, alipaswa kuwajibika kwa sababu yeye kama kiongozi wa taasisi nyeti, alipaswa kubaini ujanja huo uliofanywa na watu wengine na kuuzuia.
Ndiyo maana tulimwamini kuwa gGavana wa BoT. Hata kama hakuhusika, kutokea kwa wizi huu kunamaanisha kuwa Ballali hakuifanya kazi yake ipasavyo. Na ndiyo maana Rais hakuona kigugumizi na kuchukua hatua ya kutengua uteuzi wake mara moja.
Sasa ndugu yetu Mgonja, wewe ndiye uliyeidhinisha malipo ya mabilioni hayo yote; hivi hauoni tu kuwa nawe unahusika kwa karibu mno na kashfa hii? Au unataka hadi Rais atengue uteuzi wako pia? Hata kama hukuhusika, kwa nini usiwe mstaarabu na kuamua kuachia ngazi ili ule uchunguzi aliosema rais ufanyike uje ukusafishe?
Mgonja anatakiwa kutambua kuwa watu wanaomwangalia na kumpima katika hili, wanarejea tuhuma nyingine alizowahi kutupiwa huko nyuma naye akashindwa kuzitolea majibu ya kuridhisha.
Watu bado wanakumbuka kuwa jina lako lilikuwamo kwenye orodha ya viongozi waliotuhumiwa kwa ufisadi. Wewe mwenyewe ulikaririwa kuwa utashitaki kwa sababu umepakaziwa. Lakini hadi leo haijajulikana kesi yako imekwama wapi!
Hilo lina tafsiri kubwa sana machoni pa Watanzania na sasa inapobainika kuwa ulikuwapo katika Wizara ya Fedha kama ‘paymaster general’ wakati malipo ya EPA yanafanyika mwaka 2005/2006, Watanzania wamepata kitu kingine cha kukupima.
Hata kama ulitumiwa kuidhinisha malipo hayo bila ya wewe mwenyewe kujua, unatakiwa kuwajibika kwa sababu utakuwa ulishindwa kufanya kazi yako vema na kubaini kuwa malipo hayo yalikuwa na mushkeli.
Ningependa kukushauri kuwa uwe muungwana na ujiondoe haraka iwezekanavyo kwa sababu hata ufanye nini, utaendelea kunukia marashi ya EPA. Hilo hauwezi kulikwepa.
Hatua yake ya kuagiza vyombo kadhaa kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua watu wengine waliohusika na kashfa hiyo, inadhihirisha pia kuwa Ballali si mhusika pekee katika sakata hili. Wapo wengine wengi tu ambao baadhi yao ni rahisi kuwatambua kutokana na nafasi zao.
Mtu asiyeweza kukwepa kunukia tuhuma hizi moja kwa moja ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha. Kwa mujibu wa wadhifa huo, mtu huyo ndiye anayehusika kuidhinisha malipo ambayo serikali inayafanya. Kwa Kiingereza yeye anaitwa ‘Paymaster General.’
Kashfa iliyomng’oa Ballali inahusiana na malipo. Ni malipo ya Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) iliyopo BoT. Kwa sababu malipo haya yalifanywa na serikali ni dhahiri kuwa ‘Paymaster General’ aliidhinisha yafanyike.
Malipo yaliyotiliwa shaka na kuchunguzwa ni yale yaliyofanyika kipindi cha 2005/2006 wakati huo Gray Mgonja akiwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha pamoja na Peniel Lyimo. Lyimo alikwishaondolewa wizarani hapo lakini Mgonja bado anaendelea na wadhifa wake huo hadi hivi sasa.
Iwapo tunataka kupata maelezo ya kina kuhusiana na malipo haya, Mgonja na Lyimo wanaweza kutusaidia sana. Watatusaidia kwa sababu wao au mmoja wao - kulingana na mgawanyo wa kazi zao - ndio walioidhinisha malipo haya.
Kwa kawaida ‘paymaster general’ anaidhinisha malipo baada ya kujiridhisha kuwa malipo hayo ni halali na yanatolewa kwa kufuata taratibu zote za kiserikali zilizopo. Itashangaza sana iwapo ‘paymaster general’ akaamua kutoa tu fedha na kuzilipa bila kufuata taratibu hizo.
Kwa maana hiyo, Mgonja na Lyimo wanayo nafasi nzuri ya kutueleza Watanzania nini hasa kilifanyika katika malipo haya. Wala wasikwepe hili kwa namna yoyote ile kwa sababu wao ndio walihusika kuidhinisha malipo hayo.
Watueleze ilikuwaje wakakubali kuidhinisha malipo ya mabilioni haya ya fedha za wavuja jasho na kututia hasara kiasi hicho? Umakini wao uko wapi katika kuidhinisha malipo ya fedha zetu? Iwapo waliweza kuidhinisha malipo haya yenye kutia shaka, watashindwaje kuidhinisha malipo mengine mengi tu tusokuwa na habari nayo?
Uchunguzi uliofanywa unahusu mwaka 2005/2006 lakini akaunti ya EPA imefanya kazi kwa miaka mingi na Mgonja na Lyimo (pamoja na wengine) wamekuwapo wizarani wakiidhinisha malipo kupitia akaunti hii kwa miaka hiyo yote.
Inashangaza kuwa Mgonja bado anaendelea kuwapo madarakani hadi hivi sasa, wakati kasoro kubwa kama hii imeshajitokeza na Rais ameshawaonyesha Watanzania kuwa kuna kasoro kubwa kiasi cha yeye kutengua uteuzi wa gavana.
Kuna uwezekano kuwa gavana alihusika na wizi uliogunduliwa lakini pia kuna uwezekano kuwa hakuhusika. Kama alihusika hiyo ni sababu tosha ya Rais kusikiliza na kutekeleza maombi ya watu wanaotaka Ballali arudi nchini kuja kukabili mashtaka kuhusiana na kadhfa hiyo ya EPA.
Lakini kama hakuhusika, alipaswa kuwajibika kwa sababu yeye kama kiongozi wa taasisi nyeti, alipaswa kubaini ujanja huo uliofanywa na watu wengine na kuuzuia.
Ndiyo maana tulimwamini kuwa gGavana wa BoT. Hata kama hakuhusika, kutokea kwa wizi huu kunamaanisha kuwa Ballali hakuifanya kazi yake ipasavyo. Na ndiyo maana Rais hakuona kigugumizi na kuchukua hatua ya kutengua uteuzi wake mara moja.
Sasa ndugu yetu Mgonja, wewe ndiye uliyeidhinisha malipo ya mabilioni hayo yote; hivi hauoni tu kuwa nawe unahusika kwa karibu mno na kashfa hii? Au unataka hadi Rais atengue uteuzi wako pia? Hata kama hukuhusika, kwa nini usiwe mstaarabu na kuamua kuachia ngazi ili ule uchunguzi aliosema rais ufanyike uje ukusafishe?
Mgonja anatakiwa kutambua kuwa watu wanaomwangalia na kumpima katika hili, wanarejea tuhuma nyingine alizowahi kutupiwa huko nyuma naye akashindwa kuzitolea majibu ya kuridhisha.
Watu bado wanakumbuka kuwa jina lako lilikuwamo kwenye orodha ya viongozi waliotuhumiwa kwa ufisadi. Wewe mwenyewe ulikaririwa kuwa utashitaki kwa sababu umepakaziwa. Lakini hadi leo haijajulikana kesi yako imekwama wapi!
Hilo lina tafsiri kubwa sana machoni pa Watanzania na sasa inapobainika kuwa ulikuwapo katika Wizara ya Fedha kama ‘paymaster general’ wakati malipo ya EPA yanafanyika mwaka 2005/2006, Watanzania wamepata kitu kingine cha kukupima.
Hata kama ulitumiwa kuidhinisha malipo hayo bila ya wewe mwenyewe kujua, unatakiwa kuwajibika kwa sababu utakuwa ulishindwa kufanya kazi yako vema na kubaini kuwa malipo hayo yalikuwa na mushkeli.
Ningependa kukushauri kuwa uwe muungwana na ujiondoe haraka iwezekanavyo kwa sababu hata ufanye nini, utaendelea kunukia marashi ya EPA. Hilo hauwezi kulikwepa.
Wednesday, January 16, 2008
BREAKING NEWS- Balali anyang'anywa Visa na Marekani
Habari za uhakika nilizozipata hivi punde zinaeleza kuwa aliyekuwa Gavana wa BoT, Daudi ballali, amenyang'anywa visa na serikali ya Marekani.
taarifa hizo zinaeleza kuwa Marekani imefikia uamuzi huo baada ya kuthibitishiwa na serikali ya Tanzania kuwa Ballali si mwakilishi tena wa serikali.
Marekani tayari imeshaitaarifu serikali ya Tanzania kuwa inabatilisha viza ya Balali kwa sababu haiwakilishi tena Tanzania.
Kwa mujibu wa vyanzo vyangu, Balali alipewa viza hiyo kutokana na wadhifa wake kama Gavana, akiiwakilisha Tanzania katika nchi mbalibali ikiwamo Marekani.
Lakini kwa sababu ajira yake imekoma, Marekani imeona kuwa hana sifa za kuwa na visa hiyo ambayo inaitwa kwa kimombo non-immigrant visa.
taarifa hizo zinaeleza kuwa Marekani imefikia uamuzi huo baada ya kuthibitishiwa na serikali ya Tanzania kuwa Ballali si mwakilishi tena wa serikali.
Marekani tayari imeshaitaarifu serikali ya Tanzania kuwa inabatilisha viza ya Balali kwa sababu haiwakilishi tena Tanzania.
Kwa mujibu wa vyanzo vyangu, Balali alipewa viza hiyo kutokana na wadhifa wake kama Gavana, akiiwakilisha Tanzania katika nchi mbalibali ikiwamo Marekani.
Lakini kwa sababu ajira yake imekoma, Marekani imeona kuwa hana sifa za kuwa na visa hiyo ambayo inaitwa kwa kimombo non-immigrant visa.
Dk. Willbrod Slaa; Muasisi wa hoja ya Ufisadi iliyomng'oa Ballali
KATI ya watu waliotakiwa wawe na furaha baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangaza kutengua uteuzi wa aliyekuwa gavana wa Benki Kuu (BoT), Dk. Daudi Ballali, ni Dk. Wilbrod Slaa, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Mbunge wa Karatu.Lakini hali si hivyo kwa Dk Slaa. Kilichofanywa na Rais Kikwete hakijamridhisha kiasi cha kutosha. Anaamini kuwa sehemu iliyoshughulikiwa ni ndogo sana.
Kwamba Rais ametangaza uamuzi aliochukua kutokana na sababu alizozitoa, lakini kilichoelezwa ni sehemu ndogo sana ya tatizo kubwa lililopo.
“Tumeikubali taarifa, tunafurahi kuwa baadhi ya hatua zimewekwa hadharani, lakini serikali haijawa wazi kwa kiwango yenyewe ilichoahidi.
“Tuliambiwa kuwa ripoti ya uchunguzi uliofanywa na kampuni ya Ernst & Young itawekwa hadharani yote. Lakini walichofanya ni kutoa taarifa iliyotokana na sehemu ya ripoti, hilo silo walilotuahidi,” hivyo ndivyo anavyoeleza Dk. Slaa kuhusu kutoridhishwa na uwazi wa serikali kuhusu ripoti ya uchunguzi wa Ernst & Young.
Kingine kinachomfanya Dk. Slaa asifurahie sana hatua ya Rais Kikwete ni kuwa hata hicho kilichoelezwa katika taarifa, hakijibu sehemu kubwa ya matatizo yeye na wapinzani wenzake waliyojaribu kuyaonyesha.
Kipimo chake katika hili ni majina ya kampuni zilizotajwa kuhusika na kashfa ya akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA). Wakati akitangaza kwa waandishi wa habari taarifa ya serikali na hatua Rais Jakaya alizozichukua baada ya kukasirishwa na kuhuzunishwa ripoti hiyo, Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, aliyataja makampuni 22 kuwa yalihusika na malipo yenye kutia shaka ya EPA.
Lakini Dk. Slaa anasema kuwa hiki ni kiinimacho kwa sababu kampuni zilizotajwa zinahusisha watu wadogo sana na sehemu ndogo sana ya ubadhirifu ambao yeye ana taarifa nao.
“There is no way (haiwezekani), deep green isionekane humu, uchunguzi uliofanywa EPA unahusisha 2005/06. Mimi ninazo taarifa kuhusiana na nini kampuni hii imefanya, nina hadi cheque number (namba za hundi) zilizotumika kulipa mabilioni katika kampuni hii.
“Lakini inavyoonekana wao walichokitoa (katika taarifa ya Luhanjo) ni kile walichotaka kukitoa, kile ambacho kilistahili kutolewa kimefichwa “wamewataja watu wadogo sana,” anasema.
Katika sakata hili la ubadhirifu BoT na kashfa ya mafisadi, historia itaendelea kumuonyesha Dk. Slaa kama muasisi wa hoja hizo. Ingawa kabla yake kulikuwa na taarifa zilizosambaa chini chini kuhusiana na tuhuma za ufisadi na ubadhirifu, lakini yeye ndiye aliyeibua mambo hayo hadharani.
Aliposimama bungeni na kueleza mambo hayo, wapo waliomdhihaki wakidhani kuwa ulikuwa ni mchezo wa kisiasa uliozoeleka wa wapinzani kuwarushia makombora watu walio upande wa pili.
Lakini Dk. Slaa hakukatishwa tamaa na kejeli, dharau na masimango mengine yaliyotoka hata kwa viongozi wakuu serikalini (wako hata waliosema kelele za mlango hazimnyimi mwenye nyumba usingizi). Dk Slaa aliamua kusimama kidete akitetea hoja yake, akitumia taarifa alizozikusanya kutoka katika mtandao wa intaneti na vyanzo vingine.
“Ndiyo, nilitumia taarifa za kwenye intaneti kwa sababu nilijua kuwa zinaruhusiwa kisheria wakati (viongozi wa serikali) walipoleta sheria ya kutaka vyanzo vya intaneti vitumike kama ushahidi mimi nilipinga bungeni, lakini kutokana na wingi wao (wabunge wa CCM) waliipitisha, na nikaamua kuitumia hiyo hiyo,” anasema.
Utata kuhusu ushahidi wa Dk. Slaa uliotoka katika intaneti ulipingwa hata na Spika, Samuel Sitta, ambaye katika hatua fulani alionekana kuwa na shaka na ushahidi huo.
Lakini hii ni kama ilimchochea Dk. Slaa na kueleza nia yake ya kuandaa hoja binafsi, akilitaka Bunge liunde kamati teule kuchunguza tuhuma alizokuwa nazo.
Lakini Dk. Slaa hakufanikiwa kuiwasilisha hoja hiyo bungeni. Anaeleza sababu za kushindwa kuwasilisha hoja hiyo kuwa alipata taarifa mapema kuwa hoja hiyo ingezimwa.
“Sikutishwa na mtu. Nilipata taarifa kuwa hoja itazimwa, kulikuwa na tarifa zilizonifikia kuwa kiongozi mmoja serikalini alikuwa ametahadharishwa kuwa asije akaiacha hoja hii ikatua bungeni kwa sababu serikali haikuwa na majibu wakati ule.
“Walijiandaa kuikwamisha kwa namna yoyote na mimi nikaona kuwa iwapo nitaiwasilisha haitatendewa haki. Nikatafuta mahali muafaka pa kuipeleka na matokeo yake yameshaonekana,” anaeleza kwa kujiamini.
Maelezo haya ya Dk. Slaa yanamaanisha kuwa uamuzi wake pamoja na viongozi wenzake wa kambi ya upinzani kuichukua hoja hiyo na kuipeleka kwa wananchi, wakiifanya ajenda yao kuu katika mikutano ya hadhara iliyofanyika mikoa kadhaa nchini, ndiyo mahali muafaka alikoipeleka hoja hiyo.
Walianzia katika viwanja vya Mwembeyanga, Dar es Salaam, ambako Dk. Slaa alifanya kile ambacho watu wengi waliamini kuwa hakiwezi kufanywa na mwanasiasa wa Tanzania.
Siku hiyo, Dk. Slaa aliweka hadharani majina ya viongozi kadhaa wa serikali na chama, si tu akiwatuhumu kwa ufisadi, bali akiorodhesha tuhuma za kila mmoja wao.
Huko nyuma wanasiasa wa upinzani wamewahi kutaja majina mawili matatu ya watu wanaowatuhumu kwa ubadhirifu wa mali za umma lakini hoja hizo hazikupata mashiko.
Hii ya Dk. Slaa ilikuwa ni tofauti. Jitihada za watuhumiwa kutaka kujisafisha zilibakiwa kuwa matishio ambayo hayakumteteresha Dk. Slaa na wenzake.
Lakini Dk. Slaa alipata wapi ujasiri wote huu? Au ni namna nyingine ya kujitafutia umaarufu?
“Ndugu yangu, ukiyavulia nguo maji ya baridi huna budi kuyaoga. Mimi nilishayavulia nguo maji haya na hivyo nililazimika kuyaoga. Katika hili ninatimiza wajibu wangu kama mwakilishi wa wananchi, wala sitafuti jingine lolote, niliwaomba wananchi niwatumikie, wakanichagua na sasa natimiza ahadi ya kuwatumikia,” anasema.
Anaeleza zaidi kuwa ujasiri mwingine aliupata kutokana na kuwa na taarifa za uhakika kuhusu kile alichokisema.
Kwamba alikuwa na uhakika na taarifa alizokuwa nazo kwa sababu zilizotokana na taarifa za serikali yenyewe pamoja na vyanzo vingine. Dk. Slaa ni miongoni mwa wabunge na wanasiasa wenye tabia ya kusoma sana.
Yeye mwenyewe anaeleza kuwa hutumia muda wake mwingi kuperuzi habari mbalimbali kwenye intanet na ana muda maalumu wa kupitia rekodi za serikali na tafiti mbalimbali kuhusu masuala anayoyafuatilia.
Akisisitiza kuhusu usahihi wa taarifa alizo nazo kuhusu watu na makampuni anayoyatuhumu kwa ufisadi, anasema katika kutafuta taarifa za kampuni anazozituhumu, alifika ofisi za wakala wa kuandikisha kampuni (Brela) alikopata ushahidi wa yale aliyokuwa akiyafuatilia.
“Nilijifunza kufanya hivi baada ya sisi (wapinzani) kudharauliwa sana bungeni na kukejeliwa kuwa hatujui kufanya ‘research’ (utafiti) na sisi tukakiri kuwa kweli bado ni wachanga sana na tunajifunza, lakini katika uchanga wetu haya ndiyo tuliyoweza kuyafanya na bado tunaendelea,” anasema.
Anaeleza kuwa jambo lililomtia matumaini kuendelea na mapambano ya kuwataja hadharani watu waliojihusisha na ufisadi ni kilichotokea baada ya kutaja majina yao, ambapo walijitokeza Watanzania anaowaeleza kuwa wenye uchungu na nchi yao na ari ya kulitetea taifa lao, na kumpelekea taarifa nyingine nyingi za jinsi fedha za umma zinavyotafunwa na wachache.
“Hili ni kundi la Watanzania ambao wameanza kutuamini (wapinzani) kuwa tumedhamiria kupambana na maovu na ufisadi katika jamii,” anaongeza kuwa kati ya hao waliowasiliana naye ni watumishi kutoka serikalini, baadhi yao kutoka idara nyeti za serikali.
“Hawa si kwamba wametoa siri za serikali, kwa mujibu wa sheria namba 3 ya mwaka 1988 kifungu cha 10. Walichofanya ni kutoa taarifa za wizi na si siri za serikali, hivyo sheria hiyo haiwezi kutumika kuwabana.
“Ndiyo maana baada ya kupitia shida zote hizi na nyingine nyingi, sijaridhika na kilichotokea na kumweka nje Dk. Ballali. Wapo wengine wengi ambao nina ushahidi nao kuwa walihusika katika sakata hili, nao washughulikwe na kuwekwa pembeni.
“Hii si siasa, tunapigania maslahi ya nchi na ndiyo maana hata walipovamiwa wahariri wa ‘MwanaHalisi’ kila mtu alilaani, kwa sababu ule ulikuwa ni uvamizi dhidi ya demokrasia. Na ufisadi nao hivyo hivyo, hauna rangi ya chama cha siasa, unaumiza Watanzania wote na kuneemesha wachache.
“Tutaendelea kudai ripoti ya ukaguzi wa Ernst & Young iwekwe hadharani yote ili wananchi wajionee wenyewe kilichomo na hapo ndipo watakapogundua maana halisi ya kilichoonekana kuwa ni kelele za wapinzani.
“Sisi tunaonekana kama tunapiga kelele (kama zile za mlango zisizoweza kumkosesha mwenye nyumba usingizi, sasa ana hiyari mwenye nyumba kutengeneza mlango au auache mlango uendelee kumpigia kelele)…tunakejeliwa sana, lakini nataka niwahakikishieni Watanzania kuwa tuna uhakika na tunachokisema, sisi si wendawazimu hadi tuwe tunaropoka mambo ambayo hatuna uhakika nayo,” anasisitiza Dk. Slaa.
Huku akionyesha wazi kuwa na shauku ya ripoti hiyo kuwekwa hadharani ili Watanzania wote wafahamu kilichomo, anasema serikali inapaswa kuiweka hadharani kama ilivyowaahidi wabunge wakati ilipotoa maelezo kuhusu uchunguzi huo.
Lakini pia Dk. Slaa anawakumbusha watawala kuwa wao si waamuzi wa mwisho wa mambo yanayohusu maslahi ya taifa, walichokabidhiwa ni dhamana ya kuwaonyesha watanzania kule wanakotakiwa kwenda na si kuwafanyia maamuzi yote.
Hata hivyo, katika mazingira ya kawaida, Dk. Slaa anaweza kuwa anahatarisha maisha yake kwa sababu anapingana na watu wenye uwezo wa kufanya chochote kutokana na uwezo mkubwa wa kifedha waliojikusanyia.
Ingawa yeye mwenyewe anaonekana kutotishika na ukweli huo, watu wengi sasa wanaonekana kufuatilia zaidi mwenendo wa maisha yake, hasa wananchi wa chini ambao amekuwa akiwaita mawakili wa kesi yake.
“Ndiyo maana nimeamua sasa kuwa kila ninachokifahamu kuhusiana na ufisadi nakieleza hadharani, hivi ninapozungumza na wewe nimetoka kuhutubia mkutano wa hadhara na tangu juzi nafanya mikutano hiyo katika jimbo langu.
“Natumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi yote ninayoyafahamu kuhusiana na ubadhirifu na ufisadi ili kama likinitokea lolote, wawe na taarifa zote na wataamua wenyewe cha kufanya,” anasema.
Dk. Slaa alifanya mahojiano haya kwa njia ya simu akiwa jimboni kwake Karatu, baada ya kutolewa kwa taarifa za Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wa Ballali kuwa gavana.
Rais alifikia uamuazi huo baada ya ripoti ya uchunguzi uliofanywa na kampuni ya ukaguzi wa hesabu ya Ernst & Young kubaini kasoro kubwa katika akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) katika mwaka wa fedha 2005/06.
Katika maamuzi hayo, baada ya kutengua uteuzi wa Dk. Ballali, Rais Kikwete alimteua aliyekuwa Naibu Gavana, Profesa Benno Ndulu, kuchukua nafasi hiyo.
Aidha, Rais alimpa miezi sita Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwa kushirikiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) kuendesha uchunguzi dhidi ya wale wote waliohusika na upotevu wa fedha kupitia akaunti hiyo na kuwachukulia hatua.
Hatua zitakazochukuliwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa fedha zote zilizoibwa kupitia EPA zinarejeshwa.
Pia aliitaka bodi ya BoT kufanya vikao na kuwashughulikia wafanyakazi walio chini ya mamlaka yake walioshiriki katika kashfa hiyo ya EPA.
Ili kuhakikisha kuwa EPA haiendelei kuwa mrija wa mapato kwa wajanja wachache, Rais Kikwete alisitisha ulipaji wa madeni kwa kutumia akaunti hiyo mpaka hapo utaratibu mzuri utakapoandaliwa.
Tuesday, January 15, 2008
Ballali Ana Siri Nzito Moyoni
WASIWASI na woga umeanza kuwatesa baadhi ya viongozi serikalini, na wafanyabiashara wakubwa wanaotajwa kuhusika katika kashfa ya upotevu wa mabilioni ya shilingi dhidi ya siri nzito aliyonayo moyoni, aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Dk. Daudi Ballali.
Inaaminika kuwa kokote aliko, Dk. Ballali, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Jakaya Kikwete mapema wiki hii, anayo siri nzito moyoni mwake, na iwapo atapata nafasi ya kuiweka hadharani, mwenendo wa kashfa hizo unaweza kubadilika na kuharibu kabisa upepo wa kisiasa, utawala na biashara hapa nchini.
Aidha, siri hiyo inaelezwa kuwa ni nzito kiasi kwamba inaweza pia kuwaharibia watu wengi na hata kuchafua kabisa rekodi zao licha ya sifa nzuri walizonazo sasa.
Dk. Ballali ameamua kutumia siri hiyo kama turufu ya kujilinda na kujihakikishia usalama wake dhidi ya tuhuma zinazomkabili.
Ballali analinda siri hiyo kwa hali na mali ili kuhakikisha inamsaidia kabla haijavuja na kwamba ameamua kwenda hatua kadhaa mbele akitumia siri hiyo kama kinga dhidi yake na mtego dhidi ya maadui zake.
Watu walio karibu naye walieleza kuwa, baada ya kuona hali ya mambo imeanza kugeuka, Dk. Ballali aliamua kumtafuta wakili na kuandika maelezo ya kina kuhusu kile anachokifahamu katika sakata zima la akaunti ya madeni ya nje (EPA).
Kwamba katika maelezo hayo, Dk. Ballali ametoa sehemu ya siri hiyo, huku akitaja majina ya kampuni na watu ambao kwa namna moja au nyingine walihusika katika mipango ya sakata zima la upotevu wa fedha za EPA.
Aidha, taarifa hiyo ya Ballali iliyohifadhiwa kwa wakili huyo ambaye hajatajwa, ina maelezo ya kina pia kuhusu watu ambao kwa namna moja au nyingine walikuwa na mkono wao katika maamuzi kuhusu EPA, lakini ushiriki wao huo unaweza usionekane katika uchunguzi wa kawaida.
Baada ya kutoa maelezo hayo, Dk. Ballali ambaye mpaka sasa hali ya afya yake inaendelea kuwa kitendawili, inadaiwa kuwa alitoa maelekezo kwa wakili huyo na watu wengine wa karibu yake, kuhusu wanachopaswa kufanya iwapo atafikwa na jambo lolote ambalo aidha yeye mwenyewe au mtu mwingine wa karibu yake atalitilia shaka.
Dk. Ballali ameelezwa kufanya hivyo kama jitihada zake za makusudi za kuhakikisha kuwa hafanywi kuwa mbuzi wa kafara katika mchezo ambao ulihusisha wachezaji wengi.
Kwamba lengo lake kubwa la kufanya hivyo, ni kutaka kuhakikisha kuwa, baadhi ya watu waliohusika katika mchezo huo hawamtumii yeye kwa aidha kujisafisha kwa namna yoyote ya kujivua madhambi waliyokuwa nayo katika kashfa hiyo na kumvika yeye.
Kasoro zilizobainika katika akaunti ya malipo ya madeni ya nje ndani ya BoT, zilihusisha watu wengi, akiwemo Ballali na wengine anaowafahamu moja kwa moja na wale ambao hawafahamu.
Lakini, baada ya Kampuni ya Ernst & Young kukamilisha ripoti yake na Rais Kikwete kutoa maamuzi, inaonekama kuwa Ballali ndiye alikuwa mchezaji mkuu katika mchezo huo ambao kuibuliwa kwake kumelitikisa taifa na mataifa ya nje.
Hata katika akili ya kawaida, inaonyesha kuwa Dk. Ballali hakuwa peke yake katika suala hili, bali wapo wengine wengi, hususan vigogo kuliko Ballali.
Hayo yanatokea wakati haijawekwa wazi Dk. Ballali yupo katika hali gani au yupo wapi hasa.
Kinachoshangaza, wakati kulazwa kwa gavana huyo wa zamani wa BoT hakukustahili kuwa siri, hakuna aliyekuwa tayari kutoa taarifa za kina tangu alipoondoka nchini kwenda Marekani kutibiwa, takriban miezi minne sasa.
Awali ilidaiwa kuwa, amekwenda Marekani kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake lakini alipokuwa huko ikatolewa taarifa kuwa anaumwa na amelazwa. Baadaye kidogo zikaja taarifa kuwa amefanyiwa upasuaji mubwa.
Tangu uteuzi wake ulipotenguliwa, watu wengi wamekuwa wakitaka Dk. Ballali arejeshwe Tanzania na kushitakiwa sambamba na watu wengine watakaobainika kuhusika na kashfa ya EPA.
Dhamira hiyo ya wengi hailengi kuona tu kuwa kiongozi huyo anashtakiwa, bali wanaamini kuwa, akiwa nchini, anaweza kutoa maelezo mengi na ya kina kuhusu EPA na masuala mengine yaliyomo katika kashfa zinazoelekezwa BoT.
Dk. Willibrod Slaa, ambaye ni muasisi wa tuhuma za ubadhirifu BoT, ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa Dk. Ballali ana mengi ya kueleza kuhusu ubadhirifu huo.
Dk. Slaa alisema kuwa, yaliyoelezwa na serikali baada ya kupokea ripoti ya uchunguzi wa EPA uliofanywa na Ernst & Young, ni sehemu ndogo tu ya ubadhirifu mkubwa ambao umefanywa na baadhi ya watu waliopo madarakani na wafanyabiashara.
Dk. Slaa alikwemda mbali zaidi kwa kusema kuwa yeye binafsi anafahamu ubadhirifu uliofanywa kupitia kampuni nyingine kama vile Deep Green, Meremeta na Tangold na iwapo serikali itaendelea kuwa na kigugumizi cha kusema kuhusu hayo, itafika siku ataamua kuyaweka hadharani.
Inaaminika kuwa kokote aliko, Dk. Ballali, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Jakaya Kikwete mapema wiki hii, anayo siri nzito moyoni mwake, na iwapo atapata nafasi ya kuiweka hadharani, mwenendo wa kashfa hizo unaweza kubadilika na kuharibu kabisa upepo wa kisiasa, utawala na biashara hapa nchini.
Aidha, siri hiyo inaelezwa kuwa ni nzito kiasi kwamba inaweza pia kuwaharibia watu wengi na hata kuchafua kabisa rekodi zao licha ya sifa nzuri walizonazo sasa.
Dk. Ballali ameamua kutumia siri hiyo kama turufu ya kujilinda na kujihakikishia usalama wake dhidi ya tuhuma zinazomkabili.
Ballali analinda siri hiyo kwa hali na mali ili kuhakikisha inamsaidia kabla haijavuja na kwamba ameamua kwenda hatua kadhaa mbele akitumia siri hiyo kama kinga dhidi yake na mtego dhidi ya maadui zake.
Watu walio karibu naye walieleza kuwa, baada ya kuona hali ya mambo imeanza kugeuka, Dk. Ballali aliamua kumtafuta wakili na kuandika maelezo ya kina kuhusu kile anachokifahamu katika sakata zima la akaunti ya madeni ya nje (EPA).
Kwamba katika maelezo hayo, Dk. Ballali ametoa sehemu ya siri hiyo, huku akitaja majina ya kampuni na watu ambao kwa namna moja au nyingine walihusika katika mipango ya sakata zima la upotevu wa fedha za EPA.
Aidha, taarifa hiyo ya Ballali iliyohifadhiwa kwa wakili huyo ambaye hajatajwa, ina maelezo ya kina pia kuhusu watu ambao kwa namna moja au nyingine walikuwa na mkono wao katika maamuzi kuhusu EPA, lakini ushiriki wao huo unaweza usionekane katika uchunguzi wa kawaida.
Baada ya kutoa maelezo hayo, Dk. Ballali ambaye mpaka sasa hali ya afya yake inaendelea kuwa kitendawili, inadaiwa kuwa alitoa maelekezo kwa wakili huyo na watu wengine wa karibu yake, kuhusu wanachopaswa kufanya iwapo atafikwa na jambo lolote ambalo aidha yeye mwenyewe au mtu mwingine wa karibu yake atalitilia shaka.
Dk. Ballali ameelezwa kufanya hivyo kama jitihada zake za makusudi za kuhakikisha kuwa hafanywi kuwa mbuzi wa kafara katika mchezo ambao ulihusisha wachezaji wengi.
Kwamba lengo lake kubwa la kufanya hivyo, ni kutaka kuhakikisha kuwa, baadhi ya watu waliohusika katika mchezo huo hawamtumii yeye kwa aidha kujisafisha kwa namna yoyote ya kujivua madhambi waliyokuwa nayo katika kashfa hiyo na kumvika yeye.
Kasoro zilizobainika katika akaunti ya malipo ya madeni ya nje ndani ya BoT, zilihusisha watu wengi, akiwemo Ballali na wengine anaowafahamu moja kwa moja na wale ambao hawafahamu.
Lakini, baada ya Kampuni ya Ernst & Young kukamilisha ripoti yake na Rais Kikwete kutoa maamuzi, inaonekama kuwa Ballali ndiye alikuwa mchezaji mkuu katika mchezo huo ambao kuibuliwa kwake kumelitikisa taifa na mataifa ya nje.
Hata katika akili ya kawaida, inaonyesha kuwa Dk. Ballali hakuwa peke yake katika suala hili, bali wapo wengine wengi, hususan vigogo kuliko Ballali.
Hayo yanatokea wakati haijawekwa wazi Dk. Ballali yupo katika hali gani au yupo wapi hasa.
Kinachoshangaza, wakati kulazwa kwa gavana huyo wa zamani wa BoT hakukustahili kuwa siri, hakuna aliyekuwa tayari kutoa taarifa za kina tangu alipoondoka nchini kwenda Marekani kutibiwa, takriban miezi minne sasa.
Awali ilidaiwa kuwa, amekwenda Marekani kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake lakini alipokuwa huko ikatolewa taarifa kuwa anaumwa na amelazwa. Baadaye kidogo zikaja taarifa kuwa amefanyiwa upasuaji mubwa.
Tangu uteuzi wake ulipotenguliwa, watu wengi wamekuwa wakitaka Dk. Ballali arejeshwe Tanzania na kushitakiwa sambamba na watu wengine watakaobainika kuhusika na kashfa ya EPA.
Dhamira hiyo ya wengi hailengi kuona tu kuwa kiongozi huyo anashtakiwa, bali wanaamini kuwa, akiwa nchini, anaweza kutoa maelezo mengi na ya kina kuhusu EPA na masuala mengine yaliyomo katika kashfa zinazoelekezwa BoT.
Dk. Willibrod Slaa, ambaye ni muasisi wa tuhuma za ubadhirifu BoT, ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa Dk. Ballali ana mengi ya kueleza kuhusu ubadhirifu huo.
Dk. Slaa alisema kuwa, yaliyoelezwa na serikali baada ya kupokea ripoti ya uchunguzi wa EPA uliofanywa na Ernst & Young, ni sehemu ndogo tu ya ubadhirifu mkubwa ambao umefanywa na baadhi ya watu waliopo madarakani na wafanyabiashara.
Dk. Slaa alikwemda mbali zaidi kwa kusema kuwa yeye binafsi anafahamu ubadhirifu uliofanywa kupitia kampuni nyingine kama vile Deep Green, Meremeta na Tangold na iwapo serikali itaendelea kuwa na kigugumizi cha kusema kuhusu hayo, itafika siku ataamua kuyaweka hadharani.
Friday, January 11, 2008
Kenya Kuchemka Upya
Mambio yanazidi kuwa mabaya huko Kenya. Baada ya kushindwa kwa juhudi za kidiplomasia kumaliza mgogoro uliokuwepo, sasa chama cha ODM kimeamua kurudi kwa wananchi. Hivi punde kimetoa tangazo kikiwataka wafuasi wake wajiandae kwa maadamano makubwa nchi nzima kupinga ushindi wa Kibaki. Hakuna anayejua ni nini kitatokea, hasa ukizingatia uzoefu wa maandamano ya kwanza ambapo mamia ya watu waliuawa na mali kuharibiwa.
Hali hii inatishia sana usalama hata wa Tanzania kwa sababu upo uwezekano kuwa madhara yake yakawa makubwa, hasa baada ya kuonyeshwa kuwa Tanzania inapoteza mapato mengi kutokana na vurugu nchini Kenya.
Hali hii inatishia sana usalama hata wa Tanzania kwa sababu upo uwezekano kuwa madhara yake yakawa makubwa, hasa baada ya kuonyeshwa kuwa Tanzania inapoteza mapato mengi kutokana na vurugu nchini Kenya.
Wednesday, January 9, 2008
BREAKING NEWS: JK AMTIMUA BALALI
Sasa Kikwete anaweza kuwa ameamua kukifanya kile ambacho watanzania wengi walitaka akifanye tangu alipoingia madarakani. Habari zinazosambaa sasa hivi ni kuwa amemfukuza kazi Gavana wa benki Kuu na kuagiza watu wote ambao wametuhumiwa katika ripoti ya uchunguzi wa benki Kuu washughulikiwe.
Kama hatua hii haitakuwa na maana ya kuwatoa mbuzi wa kafara (ili kundi kubwa lipone) sasa tutarajie kupanda kwa chati ya rais Kikwete.
lakini ametoa mtihani kwa Mwanasheria mkuu kwa sababu iwapo watalaamu waliochunguza wamebaini ubadhirifu kiasi cha rais kufikia uamuzi wa kumfukuza mtu, itashangaza sana wao watakaposhindwa kuja na kesi ya kumfunga mtu kifungo kirefu
Kama hatua hii haitakuwa na maana ya kuwatoa mbuzi wa kafara (ili kundi kubwa lipone) sasa tutarajie kupanda kwa chati ya rais Kikwete.
lakini ametoa mtihani kwa Mwanasheria mkuu kwa sababu iwapo watalaamu waliochunguza wamebaini ubadhirifu kiasi cha rais kufikia uamuzi wa kumfukuza mtu, itashangaza sana wao watakaposhindwa kuja na kesi ya kumfunga mtu kifungo kirefu
Tuesday, January 8, 2008
POLISI WANATUZUGA?
Akizungumzia tukio la kushambuliwa kwa wahariri wawili wa Mwana halisi, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya dar es Salaam, Kamishna Alfred Tibaigana amesema kuwa watu wawili wamekamatwa. Mmoja wa watu hawa ni mzee wa miaka inayokarinia 70! Mwingine amekamatwa kwa sababu amekutwa na kofia yenye damu! Sijui Polisi wana ushahidi uliowashawishi wawakate watu hawa lakini kama ushahidi wenyewe ndio huu ambao Tibaigana anausema, nina wasiwasi sana kwamba Polisi wanatuzuga.
Itashangaza sana iwapo mzee wa miaka hiyo awe ndiye aliyepambana kijasiri na kufanikiwa kuchomoka na kukimbia.
Na huyu mwenye kofia yenye damu, hivi kama akiwa ni mchinja mbuzi wa kule Vingunguti, polisi wanataka kutushawishi vipi?
Sasa hivi ndio Tibaigana anashituka na kuunda timu ya watu saba, inayioongozwa na yeye mwenyewe kulishughulikia tatizo hili. Sijui kama anafahamu kuwa anachokifanya ni kutibu tatizo ambalo tayari limeshatokea.
Alikuwa na nafasi ya kuzuia jambo hilo lisitokee. Mmoja kati ya walioshambuliwa, saed Kubenea, mara kadhaa ametoa taarifa polisi kuwa alikuwa si tu akipokea ujumbe wa vitisho, bali kulikuwa na majaribia ya kumdhuru.
Tibaigana na watu wake labda walidhani kuwa Kubenea anatafuta umaarufu au vipi? Wakadharau na kumuacha hivihivi mpaka alipopatwa na makubwa. Tunashukuru Mungu kuwa ameanza kuona tena na tunaamini kuwa huko India alikopelekwa, atapatiwa matibabu yatakayomrudishia afya yake kama awali.
lakini hili linafaa kuwa funzo kwa polisi kuwa mtu anapotoa taarifa za kutishiwa maisha yake, ifahamike kuwa maisha yake yapo hatarini. Na kwa kuwa ni kazi ya polisi kulinda raia na mali zake, wanawajibika kuyalinda maisha ya mtu huyo kwa gharama yoyote ile kwa sababu yeye ndiye anayelipa kodi inayowalipa wao mshahara kwa kazi ya kumlinda.
Itashangaza sana iwapo mzee wa miaka hiyo awe ndiye aliyepambana kijasiri na kufanikiwa kuchomoka na kukimbia.
Na huyu mwenye kofia yenye damu, hivi kama akiwa ni mchinja mbuzi wa kule Vingunguti, polisi wanataka kutushawishi vipi?
Sasa hivi ndio Tibaigana anashituka na kuunda timu ya watu saba, inayioongozwa na yeye mwenyewe kulishughulikia tatizo hili. Sijui kama anafahamu kuwa anachokifanya ni kutibu tatizo ambalo tayari limeshatokea.
Alikuwa na nafasi ya kuzuia jambo hilo lisitokee. Mmoja kati ya walioshambuliwa, saed Kubenea, mara kadhaa ametoa taarifa polisi kuwa alikuwa si tu akipokea ujumbe wa vitisho, bali kulikuwa na majaribia ya kumdhuru.
Tibaigana na watu wake labda walidhani kuwa Kubenea anatafuta umaarufu au vipi? Wakadharau na kumuacha hivihivi mpaka alipopatwa na makubwa. Tunashukuru Mungu kuwa ameanza kuona tena na tunaamini kuwa huko India alikopelekwa, atapatiwa matibabu yatakayomrudishia afya yake kama awali.
lakini hili linafaa kuwa funzo kwa polisi kuwa mtu anapotoa taarifa za kutishiwa maisha yake, ifahamike kuwa maisha yake yapo hatarini. Na kwa kuwa ni kazi ya polisi kulinda raia na mali zake, wanawajibika kuyalinda maisha ya mtu huyo kwa gharama yoyote ile kwa sababu yeye ndiye anayelipa kodi inayowalipa wao mshahara kwa kazi ya kumlinda.
Sunday, January 6, 2008
BREAKING NEWS: WAHARIRI WASHAMBULIWA
Katika kile kinachoweza kuelezewa kuwa ni hujuma mbaya kabisa nchini, wahariri wawili wa gazeti la Mwana Halisi, wameshambuliwa siku ya Jumamosi kati ya saa 3 na saa 4 usiku.
Mhariri Mkuu wa gazeti hilo, Saed Kubenea ndiye aliyeathirika zaidi baada ya kumwagiwa tindikali usoni na taarifa zilizopatikana hivi punde kutoka Hosptali ya taifa Muhimbili alikolazwa, zinaelezwa kuwa amepoteza uwezo wake wa kuona.
Watu hao watatu, ambao mmoja alikuwa na panga, mwingine rungu na mwingine chupa iliyokuwa na rtindikali, waliwavamia wahariri hao ofisini kwao wakati walipokuwa wakiendelea na kazi ya kuandaa gazeti.
Walianza kugonga mlango baada ya kushindwa kuufungua na Kubenea alidhani kuwa ni wageni wa kawaida hivyio aliondoka kwenda kuwafungulia huku akiwataka wagomge polepole lakini alipofungua na kuona zana zao, alirudi ndani kwa kasi akiandamwa na yule mwenye chupa ya tindikali.
Wakati Kubenea akivamiwa na watu hao na kumwagiwa tindikali, Mhariri wa Habari wa gazeti hilo linalotoka mara moja kila wiki, Ndimara Tegambwage, alivamiwa na wale wawili na mmoja akaanza kumshambulia kwa panga.
Katika purukushani hiyo walimjeruhi Tegambwage, ambaye pia huandikia safu ya SITAKI katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili.
Inaweza kuwa ni ajali ya kawaida lakini mazingira yake yanatia shaka kubwa sana. Tangu lianzishwe, Mwana Halisi limejidhihirisha katika jamii kama gazeti ambalo lipo mstari wa mbele kufumua na kuandika maovu yanayofanywa na viongozi kadhaa.
Gazeti hilo limejijengea sifa ya kutomung'unya maneno pale linapokuwa na habari fulani. Habari zake huandikwa kwa kutaja kila kitu pamoja na majina halisi ya wahusika. lakini kutokana na ujasiri huo, Mwana Halisi, wahariri na waandishi wake wamejijengea uadui na kundi fulani la watu na vitisho kwao viligeuka kuwa suala la kawaida.
Kubenea na Tegambwage labda hawakuwa na habari kuwa waliokuwa wakiwatishia walikuwa wanaandaa nini mkapa maswahibu haya yalipowakuta.
Wakati tunawaombea Kubenea na Tegambwage, ni wakati wa kuangalia waaandishi wanafanya nini ili kujilinda dhidi ya njama na hujuma kama hizi.
Mhariri Mkuu wa gazeti hilo, Saed Kubenea ndiye aliyeathirika zaidi baada ya kumwagiwa tindikali usoni na taarifa zilizopatikana hivi punde kutoka Hosptali ya taifa Muhimbili alikolazwa, zinaelezwa kuwa amepoteza uwezo wake wa kuona.
Watu hao watatu, ambao mmoja alikuwa na panga, mwingine rungu na mwingine chupa iliyokuwa na rtindikali, waliwavamia wahariri hao ofisini kwao wakati walipokuwa wakiendelea na kazi ya kuandaa gazeti.
Walianza kugonga mlango baada ya kushindwa kuufungua na Kubenea alidhani kuwa ni wageni wa kawaida hivyio aliondoka kwenda kuwafungulia huku akiwataka wagomge polepole lakini alipofungua na kuona zana zao, alirudi ndani kwa kasi akiandamwa na yule mwenye chupa ya tindikali.
Wakati Kubenea akivamiwa na watu hao na kumwagiwa tindikali, Mhariri wa Habari wa gazeti hilo linalotoka mara moja kila wiki, Ndimara Tegambwage, alivamiwa na wale wawili na mmoja akaanza kumshambulia kwa panga.
Katika purukushani hiyo walimjeruhi Tegambwage, ambaye pia huandikia safu ya SITAKI katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili.
Inaweza kuwa ni ajali ya kawaida lakini mazingira yake yanatia shaka kubwa sana. Tangu lianzishwe, Mwana Halisi limejidhihirisha katika jamii kama gazeti ambalo lipo mstari wa mbele kufumua na kuandika maovu yanayofanywa na viongozi kadhaa.
Gazeti hilo limejijengea sifa ya kutomung'unya maneno pale linapokuwa na habari fulani. Habari zake huandikwa kwa kutaja kila kitu pamoja na majina halisi ya wahusika. lakini kutokana na ujasiri huo, Mwana Halisi, wahariri na waandishi wake wamejijengea uadui na kundi fulani la watu na vitisho kwao viligeuka kuwa suala la kawaida.
Kubenea na Tegambwage labda hawakuwa na habari kuwa waliokuwa wakiwatishia walikuwa wanaandaa nini mkapa maswahibu haya yalipowakuta.
Wakati tunawaombea Kubenea na Tegambwage, ni wakati wa kuangalia waaandishi wanafanya nini ili kujilinda dhidi ya njama na hujuma kama hizi.
Bei ya mafuta kukwaza uchumi 2008
SASA watanzania wanapaswa kujiandaa na hali ngumu itakayotokana na kushindwa kukua kwa uchumi kwa kasi ambayo ilitarajiwa kuleta nafuu katika maisha.
Kudumaa kwa hali ya uchumi kutatokana na kuongezeka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia, jambo ambalo mara kadhaa Rais Jakaya Kikwete amekuwa akilielezea kama moja ya sababu kubwa zinazoikwamisha serikali yake kutekeleza kwa kasi ahadi ya kumletea kila mtanzania maisha bora.
Kwamba kupanda kwa bei ya mafuta ni kidonda kwa uchumi wa nchi inathibitishwa na ukweli kuwa bajeti ya serikali ya mwaka 2007/08, iliyopitishwa mwezi Agosti mwaka jana, haikufikiria wala kuweka tahadhari ya kukua kwa bei ya mafuta kama moja ya matatizo ambayo yanaweza kusababisha matatizo katika utekelezaji wa bajeti.
Licha ya kutoweka tahadhari hiyo katika bajeti, pia mipango ya nchi kuhusiana na uchumi, tangu kuanza kwa mageuzi ya kiuchumi, haijawahi kufikiria bei ya mafuta kama kigezo muhimu katika upangaji wa mipango hiyo.
Licha ya kuwa suala la bei ya mafuta linafahamika kwa wataalamu wanaoandaa mipango ya uchumi wa nchi, hakuna sehemu katika mipango hiyo panapoonyesha jinsi nchi ilivyojiandaa kukabili kikwazo hicho.
Suala la bei ya mafuta limekuwa likitajwa tu kama tatizo linaloikwamisha serikali ambayo viongozi wake wengi, akiwamo rais Kikwete, wanaishia kusema kuwa serikali haina lolote la kufanya kuhusiana na bei hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya utafiti wa uchumi ya ESRF, Dk. Lunogelo Bohela, ameniambia kuwa upangaji wa mipango kama vile MKUKUTA, MKURABITA na mingineyo, haukuzingatia bei ya mafuta kama moja ya vikwazo vinavyoweza kukwamisha utekelezaji wake.
Katika mahojiano nami, Dk. Bohela alibainisha kuwa huo ni upungufu mkubwa katika masuala ya uchumi, kwani athari za bei ya mafuta kwa uchumi wa nchi kama Tanzania, ambayo inategemea nishani hiyo katika uzalishaji, ni kubwa sana na ilipaswa kutiliwa maanani.
“Hadi hivi sasa bado tunategemea mafuta kama nishati ya msingi ya uzalishaji, tunatumia umeme kwa kiasi fulani lakini hata huo umeme nao sehemu yake unazalishwa kwa mafuta, hivyo tutake tusitake bado mafuta yataendelea kuwa ndio msingi wa uchumi wetu,” alisema.
Dk. Bohela alisema kuwa ilitarajiwa kuwa gesi asilia ingesaidia kupunguza utegemezi wa mafuta lakini haijafanya hivyo kwa sababu hivi sasa bado uwekezaji katika eneo hilo haujafikia kiwango kikubwa.
Akielezea matarajio yake kuhusiana na kufikiwa kwa malengo ya kukua kwa uchumi yaliyowekwa, baada ya bei ya mafuta kufikia rekodi ya dola za Marekani 100 kwa pipa na kutoonyesha dalili za kupungua, Dk. Bohela alisema kuwa itakuwa vigumu sana kwa Tanzania kufikia malengo hayo mwaka huu.
“Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita bei ya mafuta imeongezeka maradufu… inavyoonekana ni kuwa bei haiwezi kupungua, itandelea kupanda tu na hii itatuathiri sana.
“Sana sana, iwapo tutajitahidi kuchukua tahadhari kuzuia athari za kupanda kwa bei mafuta, tunachoweza kufanya ni kuhakikisha kasi ya kukua kwa uchumi ina-stabilise (inabaki kama ilivyo), yaani ibakie ileile ya mwaka uliotangulia, lakini sina matarajio makubwa sana kuwa tutaweza kuongeza kasi ya kukua kwa uchumi katika hali hii,” alisema.
Dk. Bohela, ambaye ni mtaalamu wa uchumi katika nyanja ya kilimo, alisema kuwa kungekuwa na nafuu kubwa iwapo nchi ingekuwa inategemea malighafi nyingi kutoka nchini.
Alisema kuwa iwapo viwanda vinavyozalisha bidhaa nchini vingekuwa vinatumia malighafi nyingi za ndani, hiyo ingepunguza gharama za uzalishaji na kufanya bei ya bidhaa zinazozalishwa kuwa ya chini na kuleta unafuu kwa walaji.
“Hii gharama ya uzalishaji ndiyo kimsingi inayosababisha kupanda kwa mfumko wa bei za bidhaa… tuna bahati mbaya kwamba tunategemea nishati ya mafuta kutoka nje na pia malighafi kutoka nje,” alisema.
Akifafanua madhara ya kupanda kwa bei ya mafuta, alisema kuwa licha ya kuongeza gharama za uzalishaji, lakini kupanda kwa bei ya nishati hiyo kutaongeza pia gharama za usafiri na usafirishaji.
Akitoa ushauri, Dk. Bokela alisema serikali inaweza kuanzisha mazungumzo na moja ya nchi marafiki zinazozalisha mafuta na kukubaliana bei maalum ya upendeleo ambayo Tanzania itakuwa ikuziwa.
“Hii imeshawahi kufanyika huko nyuma na nadhani inaweza kufanyika hivi sasa kwa sababu tutaumia sana iwapo tutaendelea kutegemea mafuta kupitia soko la dunia,” alisema.
Mara kadhaa, rais Kikwete ameelezea kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia kama moja ya sababu zinazoikwamisha serikali kutekeleza mipango yake ipasavyo.
Katika hotuba zake, Kikwete husema kuwa bei ya mafuta katika soko la dunia imeiweka serikali kwenye hali mbaya kwa sababu haina uwezo wa kufanya lolote kuhusiana na udhibiti wa bei hiyo.
Kudumaa kwa hali ya uchumi kutatokana na kuongezeka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia, jambo ambalo mara kadhaa Rais Jakaya Kikwete amekuwa akilielezea kama moja ya sababu kubwa zinazoikwamisha serikali yake kutekeleza kwa kasi ahadi ya kumletea kila mtanzania maisha bora.
Kwamba kupanda kwa bei ya mafuta ni kidonda kwa uchumi wa nchi inathibitishwa na ukweli kuwa bajeti ya serikali ya mwaka 2007/08, iliyopitishwa mwezi Agosti mwaka jana, haikufikiria wala kuweka tahadhari ya kukua kwa bei ya mafuta kama moja ya matatizo ambayo yanaweza kusababisha matatizo katika utekelezaji wa bajeti.
Licha ya kutoweka tahadhari hiyo katika bajeti, pia mipango ya nchi kuhusiana na uchumi, tangu kuanza kwa mageuzi ya kiuchumi, haijawahi kufikiria bei ya mafuta kama kigezo muhimu katika upangaji wa mipango hiyo.
Licha ya kuwa suala la bei ya mafuta linafahamika kwa wataalamu wanaoandaa mipango ya uchumi wa nchi, hakuna sehemu katika mipango hiyo panapoonyesha jinsi nchi ilivyojiandaa kukabili kikwazo hicho.
Suala la bei ya mafuta limekuwa likitajwa tu kama tatizo linaloikwamisha serikali ambayo viongozi wake wengi, akiwamo rais Kikwete, wanaishia kusema kuwa serikali haina lolote la kufanya kuhusiana na bei hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya utafiti wa uchumi ya ESRF, Dk. Lunogelo Bohela, ameniambia kuwa upangaji wa mipango kama vile MKUKUTA, MKURABITA na mingineyo, haukuzingatia bei ya mafuta kama moja ya vikwazo vinavyoweza kukwamisha utekelezaji wake.
Katika mahojiano nami, Dk. Bohela alibainisha kuwa huo ni upungufu mkubwa katika masuala ya uchumi, kwani athari za bei ya mafuta kwa uchumi wa nchi kama Tanzania, ambayo inategemea nishani hiyo katika uzalishaji, ni kubwa sana na ilipaswa kutiliwa maanani.
“Hadi hivi sasa bado tunategemea mafuta kama nishati ya msingi ya uzalishaji, tunatumia umeme kwa kiasi fulani lakini hata huo umeme nao sehemu yake unazalishwa kwa mafuta, hivyo tutake tusitake bado mafuta yataendelea kuwa ndio msingi wa uchumi wetu,” alisema.
Dk. Bohela alisema kuwa ilitarajiwa kuwa gesi asilia ingesaidia kupunguza utegemezi wa mafuta lakini haijafanya hivyo kwa sababu hivi sasa bado uwekezaji katika eneo hilo haujafikia kiwango kikubwa.
Akielezea matarajio yake kuhusiana na kufikiwa kwa malengo ya kukua kwa uchumi yaliyowekwa, baada ya bei ya mafuta kufikia rekodi ya dola za Marekani 100 kwa pipa na kutoonyesha dalili za kupungua, Dk. Bohela alisema kuwa itakuwa vigumu sana kwa Tanzania kufikia malengo hayo mwaka huu.
“Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita bei ya mafuta imeongezeka maradufu… inavyoonekana ni kuwa bei haiwezi kupungua, itandelea kupanda tu na hii itatuathiri sana.
“Sana sana, iwapo tutajitahidi kuchukua tahadhari kuzuia athari za kupanda kwa bei mafuta, tunachoweza kufanya ni kuhakikisha kasi ya kukua kwa uchumi ina-stabilise (inabaki kama ilivyo), yaani ibakie ileile ya mwaka uliotangulia, lakini sina matarajio makubwa sana kuwa tutaweza kuongeza kasi ya kukua kwa uchumi katika hali hii,” alisema.
Dk. Bohela, ambaye ni mtaalamu wa uchumi katika nyanja ya kilimo, alisema kuwa kungekuwa na nafuu kubwa iwapo nchi ingekuwa inategemea malighafi nyingi kutoka nchini.
Alisema kuwa iwapo viwanda vinavyozalisha bidhaa nchini vingekuwa vinatumia malighafi nyingi za ndani, hiyo ingepunguza gharama za uzalishaji na kufanya bei ya bidhaa zinazozalishwa kuwa ya chini na kuleta unafuu kwa walaji.
“Hii gharama ya uzalishaji ndiyo kimsingi inayosababisha kupanda kwa mfumko wa bei za bidhaa… tuna bahati mbaya kwamba tunategemea nishati ya mafuta kutoka nje na pia malighafi kutoka nje,” alisema.
Akifafanua madhara ya kupanda kwa bei ya mafuta, alisema kuwa licha ya kuongeza gharama za uzalishaji, lakini kupanda kwa bei ya nishati hiyo kutaongeza pia gharama za usafiri na usafirishaji.
Akitoa ushauri, Dk. Bokela alisema serikali inaweza kuanzisha mazungumzo na moja ya nchi marafiki zinazozalisha mafuta na kukubaliana bei maalum ya upendeleo ambayo Tanzania itakuwa ikuziwa.
“Hii imeshawahi kufanyika huko nyuma na nadhani inaweza kufanyika hivi sasa kwa sababu tutaumia sana iwapo tutaendelea kutegemea mafuta kupitia soko la dunia,” alisema.
Mara kadhaa, rais Kikwete ameelezea kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia kama moja ya sababu zinazoikwamisha serikali kutekeleza mipango yake ipasavyo.
Katika hotuba zake, Kikwete husema kuwa bei ya mafuta katika soko la dunia imeiweka serikali kwenye hali mbaya kwa sababu haina uwezo wa kufanya lolote kuhusiana na udhibiti wa bei hiyo.
Wednesday, January 2, 2008
Uchaguzi Kenya na Mustakabali wa EAC
Uchaguzi Kenya na mustakabali wa EAC
Wakati wa ukusanyaji wa maoni kuhusu haja ya kuharakisha uundwaji wa Shirikisho la Afrika Mashariki, asilimia 75 ya watanzania walipinga wakisema hakukuwa na haja ya kuharakisha uundwaji wa shirikisho. Katika hao waliopinga, wapo waliohusisha hali ya amani na utulivu katika nchi za Kenya na Uganda na kueleza wasi wasi wao kuwa huenda ikaathiri shirikisho hilo.
Walitilia wasiwasi hali na mifumo ya kisiasa na kueleza kuwa haiendani na hali na mifumo ya kisiasa inayofuatwa na Tanzania. Baadhi ya viongozi waliwabeza wananchi hawa, wakisema kuwa hiyo ni hofu tu.
Walihakikisha kuwa hali ya kisiasa katika nchi hizo si sababu ya kuhofu. Lakini viongozi na wananchi wa Kenya wameamua kuonyesha kwa vitendo kuwa hofu hiyo iliyoonyeshwa na watanzania wengi na kuopuuzwa na badhi ya viongozi ni hofu halisi ambayo inapaswa kzuingatiwa kwa makini.
‘Sarakasi’ zilizofanywa katika uchaguzi mkuu wa Kenya hadi hivi sasa zimesababisha vifo vya zaidi ya watu 160. na hakuna anayejua kuwa idadi hiyo ni halisi au la kwa sababu hali ya mawasiliano imekuwa ngumu kiasi kwamba kuna uwezekano wapo wengi waliokufa lakini hawajatambuliwa.
Katika hatua iliyofikiwa nchini humo kutokana na uchaguzi mkuu, ni rahisi kumlaumu kila mtu. Lakini kwa ujumla, viongozi wa serikali na upinzani, wanasiasa na wananchi, wanapaswa kubeba lawama kutokana na machafuko yaliyotokea.
Wanachopigania ni matokeo ya uchaguzi. Wakati rais Kibaki, serikali yake pamoja na chama chake cha PNU wanatangaza kuwa wameshinda kihalali (sijui kama wanaamini hivyo), wapinzani, wakiongozwa na raila odinga wa ODM, wanadai kwa nguvu kuwa wameporwa ushindi wao.
Mabishano haya ndiyo yaliingiza wananchi mitaani, hasa baada ya kuapishwa kwa Kibaki, dakika chache tu baada ya kutangazwa kwa matokeo katika mazingira ya kutatanisha.
Polisi, waliotakiwa kulinda usalama, waliwapiga watu risasi katika kile kinachoelezwa kutuliza ghasia. Habari zilizopo zinaonyesha kuwa polisi hawakushambuliwa na silaha za moto na watu waliokuwa wanafanya fujo. Ni sehemu moja, Kisumu, ambako inaelezwa kuwa polisi waliwapuiga risasi wananchi wlaiowarushia mawe.
Inashangaza kuwa wakati wana zana nyingi za kutuliza ghasia bila kulazimika kupiga risasi za moto, polisi wanawesza kujibu mashambulizi ya mawe kwa risasi za moto!
Kwa upande mwingine, Odinga anafahamu kuwa ana wafuasi wengi nchini humo. Huu ni mtaji wa kisiasa ambao ameamua kuutumia kufikia malengo yake, kuwa kiongozi wa Kenya. Inatia moyo kuwa anahubiri amani, akiwataka wafuasi wake kuacha kufanya fujo na kuwa watulivu.
Lakini wakati huo huo, anawahimiza kushiriki katika maandamano ya amani kushinikiza Kibaki aachie ngazi. Odinga ameshawajaza wafuasi wake ujumbe kuwa kura zai zimeibwa, na anajua wazi kuwa katika mazingira ya siasa za mgawanyika kama zilizopo Kenya, haiwezekani kwa wafuasi wake kuwa wartulivu huku wakifahamu fika kuwa kura zao zimehujumiwa.
Hawawezi kuwa watulivu hasa bada ya msimamo na tabia zinazoonyeshwa na Kibaki, chama chake na serikali yake. Jinsi anavyong’ang’ania madaraka wakati ushahidi uliopo unaonyesha kuwa ushindi wake ni wa kupikwa.
Wafuasi wa Odinga hawawezi kutulia sasa wakati baadhi ya Tume ya Uchaguzi (ECK) wameanza kutoa maelezo yanayozidi kuthibitisha kuwa matokeo yaliyotangazwa yalikuwa na mushkeli.
Wajumbe wanne wa tume hiyo waliwaambia waandishi wa habari kuwa kuna umuhimu wa kuunda chombo kingine huru kuchunguza kile kilichotokea kwa sababu inavyoonekana kuna kasoro nyingi katika ujumlishaji wa matokeo.
Hata kama mwenyekiti wa ECK, Samuel Kivuitu atajitokeza kukanusha taarifa hizo, bado haitaondoa ukweli kuwa wajumbe hao wameongezea tu kwenye kasoro ambazo zilishaelezwa awali na waangalizi wa uchaguzi huo kutoka nje na ndani ya Kenya.
Serikali imeaanza jitihada za kutuliza hali ya mambo. Lakini inachokifanya hakiwezi kufanikiwa kwa sababu mazingira yanaonyesha wazi wazi kuwa ushindi wa Kibaki una kila aina ya dosari, si halali.
Katika mazingira hayo, Odinga, ambaye amekuwa akiipigania nafasi hiyo kwa miaka mingi, hawezi kukubaliana na ameshaonyesh hilo. Inafahamika kuwa mazungumzo ndio njia bora zaidi ya kumakliza tofauti baina ya watu wanaopingana. Kutokana na vurugu hizo, Odinga aliombwa kukutana na Kibaki ili kuzungumza na kumaliza tofauti zilizojitokeza.
Sharti kubwa alilolitoa ni kuwa Kibaki ajiuzulu kwanza na ndipo atakapokaana naye mza moja na kujadili. Anasema kua kukaa na Kibaki wakati akiwa bado anashikilia wadhifa wake wa urais, ni sawa na kukubali kuwa ameshinda kihalali wakati yeye (Odinga) anaamini kuwa Kibaki hakuingia madarakani kihalali.
Haya yanakumbushia yaliyowahi kutokea Zanzibar katika chaguzi. Mara zaote, Chama cha Wananchi (CUF) kimekuwa kikitoa madai baada ya uchaguzi kuwa kimeporwa ushindi. Jitihada zilifanywa kila mara kuwaleta CUF kaatika meza ya mazungumzo pamoja na mshindi. Lakini mara zote, CUF wamekataa kwa kusema kuwa kukaa meza moja na mtu huyo, ni sawa na kukubali ushindi wake.
Kilichotokea katika mabishano hayo bado ni kidonda ambachio kinaiumiza Tanzania hadi hivi leo. Katika uchaguizi wa mwisho, rais Abeid Aman karume aliapishwa saa chache tu baada ya matokeo kutangazwa kama ambavyo Kibaki ameapishwa dakika chache tu baada ya kutangazwa kwa matokeo.
Kama ilivyowahi kutokea kwa Zanzibar, mtiririko wa matukio katika uchaguzi unafanana na wa Kenya. Kila chama kilianza kujitangazia matokeo yake mapema huku tume ya uchaguzi nayo ikitoa matokeo yake. Inapofika wakati fulani karibu na mwisho, kama ambavyo CUF na CCM waliandika kwa tume ya uchgauzi kulalamikia matokeo, ODM na PNU nao walilalamika kwa tume kuwa wananyongwa.
Polsii na vikosi vya usalama vilitumika kuhalalisha matokeo ya uchaguzi zanizbra kama ambavyo sasa polisi na vikosi vya usalama vinavyotumika kuhalalisha ushindi wa Kibaki Kenya.
Lakinimkuna tofauti kubwa. Wananchi wa Kenya inaonekana wana mwamko mkubwa. Inaweza kuwa mwamko huo umejengwa kutokana na ukabila wao na watu wa kabila fulani wanaamua kulinda maslahi ya mgombea wa kabuila lao. Lakini kinachoonekana ni mwamko wao wa kutokubali kuibiwa.
Hali hii ni tofauti na watanzania ambao ishindi wa chama cha siasa hauna maana sana kwao kiasi cha kuwa tayari kupoteza maisha wakiutetea.
Na hiki ndicho walichokuwa wakikielezea watu waliokuwa wakipinga uharakishwaji wa uundwaji wa shirikisho la Afrika Mashariki, ingawa hakukieleweka wakati ule.
Watanzania wanauogopa mwamko huo wa wakenya wa kuwa tayari kupoteza maisha kwa ajili ya ushindi wa kiaisa. Wanaogopa kwa sababu hawajaiona mipaka ya mtu huyo aliye tayari kufa kwa ajili ya siasa. Wanajiuliza mpaka hivi sasa, kama yupo tayari kufa kwa ajili ya siasa, ambayo haina uhusiano wa moja kwa moja na kuleta sahani ya ugali mezani kwake, atafanya nini katika suala linalohusiana moja kwa moja na maisha yake, kwa mfano ajira.
Wakati wakenya wameonyesha kwa vitendo kuwa hofu ya watanzania kuhisna na siasa za Kenya ni halisi, inakuja changamoto nhingine. Pamoja na yanayotokea Kenya, bado dhamira ya kuunda Shirikisho la Afrika mashariki itaendelea.
Lakini, matukio haya yamethibitisha hofu ya watanzania na nidhahiri kuwa yatakuwa ni rejea pale ambapo watanzani watatakiwa kufikiri tena kuhusiana uundwaji wa shirikisho.
Wakati tunafikiri jinsi ya kuisadia Kenya kumaliza changamoto za uchaguzi wake mkuu, inapaswa tufikirie pia athari ya yaliyotokea katika dhamira yetu ya kuunda shirikisho la Afrika Mashariki. Tutafanya makosa makubwa iwapo tutaamua kufunika kombe ili mwanaharamu apite.
Huyo mwanaharamu hatopita, na kama akipita hatokwenda mbali, na atarudi kuja kutuandama. Hivyo ni uamuzi wetu iwapo tumshughulikie sasa hivi au tuendelee kuahirisha tatizo.
Wakati wa ukusanyaji wa maoni kuhusu haja ya kuharakisha uundwaji wa Shirikisho la Afrika Mashariki, asilimia 75 ya watanzania walipinga wakisema hakukuwa na haja ya kuharakisha uundwaji wa shirikisho. Katika hao waliopinga, wapo waliohusisha hali ya amani na utulivu katika nchi za Kenya na Uganda na kueleza wasi wasi wao kuwa huenda ikaathiri shirikisho hilo.
Walitilia wasiwasi hali na mifumo ya kisiasa na kueleza kuwa haiendani na hali na mifumo ya kisiasa inayofuatwa na Tanzania. Baadhi ya viongozi waliwabeza wananchi hawa, wakisema kuwa hiyo ni hofu tu.
Walihakikisha kuwa hali ya kisiasa katika nchi hizo si sababu ya kuhofu. Lakini viongozi na wananchi wa Kenya wameamua kuonyesha kwa vitendo kuwa hofu hiyo iliyoonyeshwa na watanzania wengi na kuopuuzwa na badhi ya viongozi ni hofu halisi ambayo inapaswa kzuingatiwa kwa makini.
‘Sarakasi’ zilizofanywa katika uchaguzi mkuu wa Kenya hadi hivi sasa zimesababisha vifo vya zaidi ya watu 160. na hakuna anayejua kuwa idadi hiyo ni halisi au la kwa sababu hali ya mawasiliano imekuwa ngumu kiasi kwamba kuna uwezekano wapo wengi waliokufa lakini hawajatambuliwa.
Katika hatua iliyofikiwa nchini humo kutokana na uchaguzi mkuu, ni rahisi kumlaumu kila mtu. Lakini kwa ujumla, viongozi wa serikali na upinzani, wanasiasa na wananchi, wanapaswa kubeba lawama kutokana na machafuko yaliyotokea.
Wanachopigania ni matokeo ya uchaguzi. Wakati rais Kibaki, serikali yake pamoja na chama chake cha PNU wanatangaza kuwa wameshinda kihalali (sijui kama wanaamini hivyo), wapinzani, wakiongozwa na raila odinga wa ODM, wanadai kwa nguvu kuwa wameporwa ushindi wao.
Mabishano haya ndiyo yaliingiza wananchi mitaani, hasa baada ya kuapishwa kwa Kibaki, dakika chache tu baada ya kutangazwa kwa matokeo katika mazingira ya kutatanisha.
Polisi, waliotakiwa kulinda usalama, waliwapiga watu risasi katika kile kinachoelezwa kutuliza ghasia. Habari zilizopo zinaonyesha kuwa polisi hawakushambuliwa na silaha za moto na watu waliokuwa wanafanya fujo. Ni sehemu moja, Kisumu, ambako inaelezwa kuwa polisi waliwapuiga risasi wananchi wlaiowarushia mawe.
Inashangaza kuwa wakati wana zana nyingi za kutuliza ghasia bila kulazimika kupiga risasi za moto, polisi wanawesza kujibu mashambulizi ya mawe kwa risasi za moto!
Kwa upande mwingine, Odinga anafahamu kuwa ana wafuasi wengi nchini humo. Huu ni mtaji wa kisiasa ambao ameamua kuutumia kufikia malengo yake, kuwa kiongozi wa Kenya. Inatia moyo kuwa anahubiri amani, akiwataka wafuasi wake kuacha kufanya fujo na kuwa watulivu.
Lakini wakati huo huo, anawahimiza kushiriki katika maandamano ya amani kushinikiza Kibaki aachie ngazi. Odinga ameshawajaza wafuasi wake ujumbe kuwa kura zai zimeibwa, na anajua wazi kuwa katika mazingira ya siasa za mgawanyika kama zilizopo Kenya, haiwezekani kwa wafuasi wake kuwa wartulivu huku wakifahamu fika kuwa kura zao zimehujumiwa.
Hawawezi kuwa watulivu hasa bada ya msimamo na tabia zinazoonyeshwa na Kibaki, chama chake na serikali yake. Jinsi anavyong’ang’ania madaraka wakati ushahidi uliopo unaonyesha kuwa ushindi wake ni wa kupikwa.
Wafuasi wa Odinga hawawezi kutulia sasa wakati baadhi ya Tume ya Uchaguzi (ECK) wameanza kutoa maelezo yanayozidi kuthibitisha kuwa matokeo yaliyotangazwa yalikuwa na mushkeli.
Wajumbe wanne wa tume hiyo waliwaambia waandishi wa habari kuwa kuna umuhimu wa kuunda chombo kingine huru kuchunguza kile kilichotokea kwa sababu inavyoonekana kuna kasoro nyingi katika ujumlishaji wa matokeo.
Hata kama mwenyekiti wa ECK, Samuel Kivuitu atajitokeza kukanusha taarifa hizo, bado haitaondoa ukweli kuwa wajumbe hao wameongezea tu kwenye kasoro ambazo zilishaelezwa awali na waangalizi wa uchaguzi huo kutoka nje na ndani ya Kenya.
Serikali imeaanza jitihada za kutuliza hali ya mambo. Lakini inachokifanya hakiwezi kufanikiwa kwa sababu mazingira yanaonyesha wazi wazi kuwa ushindi wa Kibaki una kila aina ya dosari, si halali.
Katika mazingira hayo, Odinga, ambaye amekuwa akiipigania nafasi hiyo kwa miaka mingi, hawezi kukubaliana na ameshaonyesh hilo. Inafahamika kuwa mazungumzo ndio njia bora zaidi ya kumakliza tofauti baina ya watu wanaopingana. Kutokana na vurugu hizo, Odinga aliombwa kukutana na Kibaki ili kuzungumza na kumaliza tofauti zilizojitokeza.
Sharti kubwa alilolitoa ni kuwa Kibaki ajiuzulu kwanza na ndipo atakapokaana naye mza moja na kujadili. Anasema kua kukaa na Kibaki wakati akiwa bado anashikilia wadhifa wake wa urais, ni sawa na kukubali kuwa ameshinda kihalali wakati yeye (Odinga) anaamini kuwa Kibaki hakuingia madarakani kihalali.
Haya yanakumbushia yaliyowahi kutokea Zanzibar katika chaguzi. Mara zaote, Chama cha Wananchi (CUF) kimekuwa kikitoa madai baada ya uchaguzi kuwa kimeporwa ushindi. Jitihada zilifanywa kila mara kuwaleta CUF kaatika meza ya mazungumzo pamoja na mshindi. Lakini mara zote, CUF wamekataa kwa kusema kuwa kukaa meza moja na mtu huyo, ni sawa na kukubali ushindi wake.
Kilichotokea katika mabishano hayo bado ni kidonda ambachio kinaiumiza Tanzania hadi hivi leo. Katika uchaguizi wa mwisho, rais Abeid Aman karume aliapishwa saa chache tu baada ya matokeo kutangazwa kama ambavyo Kibaki ameapishwa dakika chache tu baada ya kutangazwa kwa matokeo.
Kama ilivyowahi kutokea kwa Zanzibar, mtiririko wa matukio katika uchaguzi unafanana na wa Kenya. Kila chama kilianza kujitangazia matokeo yake mapema huku tume ya uchaguzi nayo ikitoa matokeo yake. Inapofika wakati fulani karibu na mwisho, kama ambavyo CUF na CCM waliandika kwa tume ya uchgauzi kulalamikia matokeo, ODM na PNU nao walilalamika kwa tume kuwa wananyongwa.
Polsii na vikosi vya usalama vilitumika kuhalalisha matokeo ya uchaguzi zanizbra kama ambavyo sasa polisi na vikosi vya usalama vinavyotumika kuhalalisha ushindi wa Kibaki Kenya.
Lakinimkuna tofauti kubwa. Wananchi wa Kenya inaonekana wana mwamko mkubwa. Inaweza kuwa mwamko huo umejengwa kutokana na ukabila wao na watu wa kabila fulani wanaamua kulinda maslahi ya mgombea wa kabuila lao. Lakini kinachoonekana ni mwamko wao wa kutokubali kuibiwa.
Hali hii ni tofauti na watanzania ambao ishindi wa chama cha siasa hauna maana sana kwao kiasi cha kuwa tayari kupoteza maisha wakiutetea.
Na hiki ndicho walichokuwa wakikielezea watu waliokuwa wakipinga uharakishwaji wa uundwaji wa shirikisho la Afrika Mashariki, ingawa hakukieleweka wakati ule.
Watanzania wanauogopa mwamko huo wa wakenya wa kuwa tayari kupoteza maisha kwa ajili ya ushindi wa kiaisa. Wanaogopa kwa sababu hawajaiona mipaka ya mtu huyo aliye tayari kufa kwa ajili ya siasa. Wanajiuliza mpaka hivi sasa, kama yupo tayari kufa kwa ajili ya siasa, ambayo haina uhusiano wa moja kwa moja na kuleta sahani ya ugali mezani kwake, atafanya nini katika suala linalohusiana moja kwa moja na maisha yake, kwa mfano ajira.
Wakati wakenya wameonyesha kwa vitendo kuwa hofu ya watanzania kuhisna na siasa za Kenya ni halisi, inakuja changamoto nhingine. Pamoja na yanayotokea Kenya, bado dhamira ya kuunda Shirikisho la Afrika mashariki itaendelea.
Lakini, matukio haya yamethibitisha hofu ya watanzania na nidhahiri kuwa yatakuwa ni rejea pale ambapo watanzani watatakiwa kufikiri tena kuhusiana uundwaji wa shirikisho.
Wakati tunafikiri jinsi ya kuisadia Kenya kumaliza changamoto za uchaguzi wake mkuu, inapaswa tufikirie pia athari ya yaliyotokea katika dhamira yetu ya kuunda shirikisho la Afrika Mashariki. Tutafanya makosa makubwa iwapo tutaamua kufunika kombe ili mwanaharamu apite.
Huyo mwanaharamu hatopita, na kama akipita hatokwenda mbali, na atarudi kuja kutuandama. Hivyo ni uamuzi wetu iwapo tumshughulikie sasa hivi au tuendelee kuahirisha tatizo.
Subscribe to:
Posts (Atom)