THE CIVIC UNITED FRONT
HOTUBA YA MWENYEKITI WA TAIFA WA CHAMA CHA WANANCHI (CUF), MHE. PROF. IBRAHIM LIPUMBA, KATIKA MKUTANO NA WAZEE, WANAWAKE NA VIJANA VIONGOZI WA CHAMA WA MKOA WA DAR ES SALAAM, KUTOA UFAFANUZI KUHUSIANA NA MAZUNGUMZO YA KUTAFUTA UFUMBUZI WA KUDUMU WA MPASUKO WA KISIASA ZANZIBAR
UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE, DAR ES SALAAM
TAREHE 06 APRILI, 2008
UTANGULIZI
Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia kuwa wazima na kuweza kukutana leo hii. Naamini ataendelea kutupa baraka na mwongozo wake ili tuweze kuutekeleza wajibu wetu kama viongozi ambao ni watumishi wa Watanzania kuweza kuwapa uongozi thabiti wenye hekima na busara na utakaoiepusha nchi yetu na shari ambayo watawala waliopo madarakani hivi sasa wanaonekana kuiandaa. Nawashukuru nyinyi pia Wazee, viongozi wa Chama chetu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kina mama na vijana kwa kufika kwa wingi kuja kutusikiliza licha ya taarifa ya muda mfupi ya kufanyika kwa mkutano huu. Najua mmeacha shughuli zenu muhimu kuja kunisikiliza na kwa hilo, nasema Ahsanteni sana.
Watanzania wenzangu, sina haja ya kuwaficha, nimelazimika kuja kuzungumza nanyi ili kutumia fursa hii kuweka kumbukumbu sahihi kuhusiana na mchakato mzima wa mazungumzo kati ya Chama Cha Wananchi (CUF) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) yenye lengo la kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar na hasa hii hali ya mtafaruku iliyopo sasa ambayo tumefikishwa na CCM. Nimeamua kufanya hivi baada ya kumsikiliza Mwenyekiti mwenzangu wa upande wa pili ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, akitoa maelezo kuhusiana na mazungumzo hayo katika ukumbi huu huu wa Diamond Jubilee tarehe 2 Aprili, mwaka huu wa 2008 lakini kwa bahati mbaya maelezo hayo yakiwa yamejaa upotoshaji na ubabaishaji wa hali ya juu. Rais anatumia usanii wa kisiasa kukanusha kwamba yeye na chama chake hawafanyi usanii wa kisiasa. Nchi inapoongozwa na watu wa aina hii, Watanzania tuna kila haki na sababu ya kujiuliza iwapo kweli tuko salama hivi sasa na huko mbele tunakokwenda.
Wakati wa ufunguzi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu za chama cha CUF mjini Tabora Septemba 2005 niliwatahadharisha Watanzania kuwa Mheshimiwa Kikwete ni Mtu wa mzaha mzaha, hana kauli thabiti hafai kuwa Rais na tukimchagua matokeo yake itakuwa rushwa na ufisadi itaongezeka kwa kasi, mpya na nguvu mpya. Uchambuzi wa kina wa rushwa nitaufanya katika mikutano ifuatayo leo nitachambua mazungumzo ya CCM na CUF. Hata hivyo la kuzingatia ni kuwa Mafisadi wamejikita na kujenga kambi ndani ya CCM. Hawataki demokrasia kwa sababu itawaumbua na kuwanyima nafasi ya kuendelea na ufisadi wao.
MCHAKATO WA MAZUNGUMZO
Watanzania wenzangu, mtakumbuka kuwa mara baada ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 30, 2005, ambao kwa mara ya tatu mfululizo uliendelea kutawaliwa na wizi wa kura uliofanywa na CCM na kumuweka madarakani kwa nguvu Mheshimiwa Amani Karume kinyume na matakwa ya Wazanzibari, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF lilikutana tarehe 5 Novemba, 2005 kutafakari hali mbaya ya kisiasa iliyokuwapo wakati huo ambayo ingeweza kuzaa maafa makubwa kwa nchi yetu. Wazanzibari walikuwa tayari kwa lolote baada ya kuchoshwa na wizi wa kura wa CCM katika chaguzi zote tatu, yaani 1995, 2000 na 2005. Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama chetu likaamua kutumia busara na kuepusha shari kwa kuwataka Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla watulie na kuwapa nafasi viongozi wao kutafuta ufumbuzi wa suala hilo kwa njia za amani.
Wengi waliomsikia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, wakati akilihutubia na kulizindua Bunge jipya tarehe 30 Desemba, 2005, pamoja na mambo mengine akilieleza Taifa nia yake ya kuutafutia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar walidhani hiyo ilikuwa ni hoja yake mwenyewe tu. Hamkuelewa kwamba maelezo hayo ya Rais hayakuja kwa sababu ya nia yake tu bali yalitokana na mawasiliano baina ya baadhi ya wasaidizi na washauri wake wa karibu na baadhi ya viongozi wa CUF ambayo yalianza mara baada ya uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 30, 2005 kumalizika na kabla hata ya yeye kushika madaraka ya Urais. Tukakubaliana kuwa tusubiri hadi baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa Muungano na tutachukua hatua za pamoja za kulipatia ufumbuzi tatizo hilo.
Rais alipotoa hotuba yake Bungeni, hata kama haikuwakilisha kisawa sawa mtazamo wa CUF kuhusiana na mgogoro wa kisiasa Zanzibar, tuliamua kumpa ushirikiano wetu katika kutimiza ile ahadi tuliyokubaliana. Siku moja tu baada ya hotuba yake, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alitoa taarifa kwa vyombo vya habari na akamuandikia barua rasmi Rais Kikwete tarehe 31 Desemba, 2005 akimhakikishia ushirikiano wetu. Kuanzia hapo mazungumzo yasiyo rasmi yakawa yanafanyika kati ya baadhi ya wasaidizi na washauri wa Rais aliowaamini na baadhi ya viongozi wa CUF tuliowapa ridhaa ya kuendeleza mawasiliano hayo. Ubalozi wa nchi moja iliyo rafiki mkubwa wa Tanzania nao ukajitolea kuratibu mawasiliano hayo ili kujenga maelewano mazuri.
Jambo moja ambalo nataka niliweke wazi na Watanzania wote walielewe ni kwamba tokea hatua hizo za mwanzo kabisa, ambazo hazikuwa zikitangazwa hadharani, tulikubaliana kuwa ufumbuzi tunaoutafuta utapatikana kwa CUF kusamehe madai yake ya kutaka Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar urudiwe na badala yake itapewa nafasi ya Waziri Kiongozi na idadi kadhaa ya mawaziri kama itakavyokubaliwa. Kwa maneno mengine, makubaliano hayo yalikuwa na sura kama ile iliyokuja kujitokeza baadaye katika suluhisho la mgogoro wa Uchaguzi Mkuu wa Kenya ambao Rais Kikwete amejisifia sana kuwa aliweza kuumaliza kwa masaa matano tu.
Kilichokuwa kikizungumzwa katika duru hizo za awali kilikuwa ni utaratibu upi utakuja kutumika kufanikisha malengo hayo. CUF ilimweleza wazi Rais kupitia wasaidizi wake kwamba haikuwa na imani kwamba Mheshimiwa Karume na wahafidhina wenzake wa CCM Zanzibar watakubaliana na ufumbuzi huu. Naye, kupitia wasaidizi hao hao, akatuhakikishia kuwa hilo ni la ndani ya CCM na tuwaachie wao. Tulipouliza lini utaratibu huu utaanza kazi rasmi tukaambiwa tusubiri miezi sita hadi Juni 2006 pale Rais Kikwete atakapokabidhiwa uenyekiti wa Chama chake kwani atakuwa na mamlaka kamili na muhimu yatakayomuwezesha kulifanikisha suala hili.
Juni 2006 ilifika na Rais Kikwete akawa Mwenyekiti wa CCM. Tukahimiza haja ya sasa kuyawekea utaratibu wa kuyatekeleza yale tuliyokuwa tumeelewana tokea Januari 2006, tukaambiwa tumpe nafasi zaidi ya miezi sita mingine ili aweze kuweka safu vyema na kuimarisha mamlaka yake katika Chama kusudi awe na nguvu za kupitisha maamuzi mazito kama hayo. CUF kwa maslahi ya Taifa, tukakubali kusubiri hadi Desemba 2006. Ilipofika Desemba 2006, badala ya kuwa na utaratibu wa kutuelekeza kule tulikokuwa tayari tumeshaelewana kuwa ndiyo suluhisho, tukapokea tamko la Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuwa imeagiza yafanyike mazungumzo kati ya CCM na CUF kwa lengo la kuanzisha siasa za maelewano Zanzibar. Pamoja na kuona hatua hiyo inaturejesha nyuma na ina lengo la kuchelewesha kufikia malengo tuliyokubaliana, CUF kwa nia njema ya kuwaamini wenzetu na hasa Rais Kikwete, tukatoa tamko kuridhia mazungumzo hayo.
Januari 17, 2007, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, akiambatana na Mhe. Hamad Rashid Mohamed na Mhe. Ismail Jussa, walikutana na Katibu Mkuu wa CCM, Mhe. Yusuf Makamba akiwa amefuatana na Mhe. Ali Ameir Mohamed na Mhe. Saleh Ramadhani Feruzi kukubaliana utaratibu wa kuendesha mazungumzo. Miongoni mwa mambo waliyokubaliana ilikuwa ni kubadilishana hadidu za rejea ambazo kila upande utaeleza matarajio yake katika mazungumzo hayo na baadaye hadidu hizo ndizo zitumike kutengeneza agenda za mazungumzo.
Katibu Mkuu wa CUF aliwasilisha hadidu za rejea zetu kwa Katibu Mkuu wa CCM kupitia barua ya tarehe 26 Januari, 2007 ambazo zilikuwa kama ifuatavyo:
Kurudiwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar:
(a) chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa; au
(b) chini ya usimamizi wa Serikali ya Mpito ya CCM na CUF
kutokana na Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 30, 2005 kutokuwa huru na wa haki ambako kulisababishwa na ama kutotekelezwa kikamilifu au kutotekelezwa kabisa kwa maeneo mengi ya Muafaka wa CCM na CUF wa 2001 na pia kutumika kwa nguvu kubwa na ya kupita kiasi ya Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Vikosi vya SMZ na makundi ya vijana wa CCM ya ’Janjaweed’ katika kuwatisha wananchi wasiweze kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa uhuru na uwazi.
Kutengwa, kubaguliwa, kunyanyaswa na kukandamizwa kwa wanachama na wafuasi wa CUF walioko Zanzibar na hasa Pemba ikiwemo kunyimwa haki zote za kiraia kutokana na itikadi zao za kisiasa na kufanywa hawana haki katika nchi yao, hali inayotishia hata umoja na usalama wa nchi kwa kukuza hisia za sehemu kubwa ya wakaazi wa Pemba kuanza kufikiria hawatakiwi katika Zanzibar na katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuendelea kuizuia na kuiwekea vikwazo CUF kufanya shughuli zake halali za kisiasa katika visiwa vya Zanzibar kama inavyopaswa kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Katiba ya Zanzibar na Sheria ya Vyama vya Siasa (Nam. 5/1992).
Askari wa Polisi na Vikosi vya SMZ pamoja na vijana wa ’Janjaweed’ waliohusika katika matukio ya uhalifu na uvunjwaji wa haki za binadamu dhidi ya raia wasio na hatia kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria na kushtakiwa kwa mujibu wa sheria za nchi.
Utaratibu wa Utekelezaji na Programu ya Utekelezaji wa makubaliano yatakayofikiwa katika mazungumzo haya.
Kwa upande wa Katibu Mkuu wa CCM, kama ilivyo kawaida yao, akakiuka makubaliano hayo ya mapema kabisa kwa kutowasilisha hadidu zao. Hiyo ilikuwa hatua ya awali ya CCM kutokuwa wakweli katika mazungumzo haya na kama itavyokuja kudhihirika huko mbele, mara zote kutoheshimu yale yaliyokwisha kubaliwa au kujitia hamnazo kwamba hakukuwa na makubaliano kama hayo.
Badala ya kuwasilisha hadidu za rejea, CCM wakawasilisha barua ya kutaka ziteuliwe timu za watu sita kutoka kila upande na mazungumzo yaanze na kwamba wao wangetoa hadidu za rejea na mapendekezo ya agenda zao katika kikao cha kwanza cha timu hizo.
Tarehe 1 Februari, 2007, kikao cha kwanza cha timu zetu kikafanyika mjini Dodoma bila ya CCM kuwasilisha hadidu za rejea zake kama walivyokuwa wameahidi na badala yake wakasema wametumia hadidu za rejea za CUF tulizowapelekea kuandaa mapendekezo ya agenda. Baada ya mvutano wa muda, hatimaye timu yetu ilikubali yaishe na kwa pamoja kukubaliana agenda tano za mazungumzo zifuatazo:
Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 30, 2005: Uhalali na Taathira zake.
Usawa na Haki katika Kuendesha Siasa.
Masuala ya Utawala wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Njia za Kuimarisha Mazingira ya Maelewano na Uendeshaji wa Uchaguzi Huru na wa Haki Zanzibar.
Utaratibu wa Utekelezaji na Programu ya Utekelezaji wa makubaliano yatakayofikiwa.
Hata baada ya hatua hiyo, katika kila walichokieleza ni kumridhisha Mhe. Amani Karume ili asiwe na kinyongo na mazungumzo hayo, CCM ikarudi tena kutuomba upande wa CUF tukubali kuliondoa neno “Uhalali“ katika agenda ya kwanza inayohusu uchaguzi mkuu na badala yake iwe “Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 30, 2005 na Taathira zake“. CUF kwa mara nyingine tena ikaonyesha uungwana kwa kukubali ombi hilo la CCM bila ya kipingamizi chochote. Uzuri wa haya ninayoyaeleza ni kwamba yote yamo katika Kumbukumbu za Vikao vya Kamati ya Mazungumzo ambazo zimetiwa saini na pande zote mbili.
Ni baada ya hatua hiyo, ndipo mjadala wa agenda moja baada ya nyingine ukaanza, na kila hatua makubaliano yakifikiwa. Kwa yale maeneo ambayo hayakuwa na makubaliano, ikakubaliwa kila upande ubaki na msimamo wake. Jumla ya vikao 21 vya mazungumzo vimefanyika katika kipindi cha miezi 14 tokea Januari 2007 hadi Februari 2008. Katika hatua zote hizo, kila upande ulikuwa ukitoa taarifa kwa viongozi wake wakuu na katika vikao vya maamuzi vya vyama vyetu ambavyo ni Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kwa upande wa CUF na Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa kwa upande wa CCM.
Watanzania wenzangu, mtakumbuka kwamba mwezi Agosti mwaka jana ulizuka mtafaruku mkubwa kuhusu mazungumzo hayo pale CUF ilipobaini kwamba CCM haikuwa na nia ya dhati ya kuyakamilisha na kutekeleza yale tuliyokubaliana tokea hatua za awali kabisa za mazungumzo yasiyo rasmi. Mimi kwa niaba ya CUF nikatoa tamko tarehe 7 Agosti, 2007 kuiomba jumuiya ya kimataifa iingilie kati ili kuyanusuru mazungumzo yetu na kuiepusha nchi yetu na shari. Nilichukua hatua hiyo baada ya kuona tarehe 15 Agosti, 2007 ambayo Makatibu Wakuu wa CCM na CUF walikubaliana kuwa mazungumzo yawe yamekamilika inakaribia na hakuna dalili zote za kufanya hivyo huku CCM ikijikurupusha huku na kule kwa visingizio kemkem. Mwenyekiti mwenza wa CCM katika kamati ya mazungumzo alikuwa anadai kuwa kinyume na na uchaguzi wa mwaka 2000 na matukio ya 2001, safari hii CUF haina hoja kwa sababu hakuna mtu aliyekufa kwenye uchaguzi wa 2005. Katika jitihada za kuyanusuru mazungumzo haya nikiambatana na Mhe. James Mbatia, Mwenyekiti wa Taifa wa NCCR-Mageuzi, niliwasiliana na viongozi wakuu wa dini akiwemo Muadhama Kadinali Polycap Pengo wa Kanisa Katoliki, Askofu Mstaafu Elinaza Sendoro wa Kanisa la Kilutheri Tanzania na Mufti Shaaban Simba wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) na kuwaomba wayaombee Mazungumzo ya CCM na CUF yanusurike na watumie nyadhifa zao kuhakikisha Rais Kikwete hayafanyii mzaha mazungumzo haya. Vile vile niliende Dodoma kuzungumza na aliyekuwa Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Bara, Mhe. John Samuel Malecela na aliyekuwa Waziri Mkuu Mhe. Edward Lowasa kuwaomba watumie nyadhifa zao kuyanusuru mazungumzo.
Rais Jakaya Kikwete hatimaye akatoa tamko tarehe 14 Agosti, 2007 akiinasihi CUF ikubali kuendelea na mazungumzo hata baada ya kupita tarehe 15 Agosti iliyokuwa imekubaliwa kuwa yawe yamekwisha na akaahidi binafsi atayasimamia kuona yanafanikiwa. CUF ikaheshimu kauli ya Rais na ikakubali kuendelea na mazungumzo kwa sharti kwamba hatua zichukuliwe kuyakamilisha. Imepita miezi mingine saba baada ya ahadi hiyo ya Rais kabla ya mazungumzo hayo kukamilishwa.
Timu ya CUF iliporudi katika mazungumzo, ujumbe wa CCM ukawaeleza wenzao kuwa kwa vile makubaliano yanayotarajiwa kufikiwa yanahusu mambo makubwa, ni vyema CUF ikaonyesha ustahmilivu hadi umalizike Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM hapo Novemba, 2007 ili kumruhusu Rais Kikwete kujipanga vyema na safu mpya za Chama kuweza kukabili maamuzi mazito kwa maslahi ya taifa. CUF ikawakubalia tena.
Watanzania wenzangu, ni vyema mkaelewa kuwa ustahmilivu na uungwana huo uliokuwa ukionyeshwa na CUF haukutokana na kwamba labda CUF ni dhaifu bali ni maumbile ya chama chetu, misingi yake ya ukweli na uaminifu na kujali kwake amani ya nchi yetu. Ni bahati mbaya sana kwamba CUF ilikuwa ikiyazingatia haya mbele ya CCM, chama ambacho kinaamini katika hadaa, udanganyifu, upotoshaji, ubabaishaji na usanii wa kisiasa.
Waswahili wanasema njia ya mwongo fupi. Hatimaye Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM ulimalizika na mazungumzo yakaendelea na yakahitimishwa katika kikao cha tarehe 25 – 29 Februari, 2008. Tukakubaliana kuwa sasa rasimu ya makubaliano yaliyohusu agenda zote zilizowasilishwa na kujadiliwa ifikishwe kwenye vikao vya juu vya vyama vyetu ili kuidhinishwa na kisha kupanga tarehe ya kutiwa saini makubaliano na utekelezaji kuanza.
Hii ilikuwa ni hatua ya mwisho ya utaratibu (formality) tu kwa sababu kila hatua ya mazungumzo na makubaliano, viongozi wakuu wa vyama vyetu na vikao vya juu vya vyama vyetu vilikuwa vinashirikishwa na kutoa miongozo yake. Yapo mambo mengi yakiwemo hata yale yanayohusu muundo wa Serikali Shirikishi ambayo yaliwahi kufikishwa mbele ya vikao na vikao hivyo vikaagiza marekebisho yafanywe na yakafanywa. Hatua ya mwisho ilikuwa ni kuyaweka pamoja tu katika rasimu ya makubaliano ili iidhinishwe, siyo kufungua upya mjadala wa mambo yaliyokuwa yameshakubaliwa.
aik
Watanzania na ulimwengu ni mashahidi kuwa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF lilikutana na kuridhia makubaliano hayo tarehe 17 Machi, 2008. Timu ya CUF katika mazungumzo na CCM iliwasilisha taarifa ya mazungumzo kwa kusoma rasimu ya makubaliano ya CCM na CUF iliyokubaliwa na kupitishwa katika vikao vya kamati ya mazungumzo. Siyo kama hakukuwa na wajumbe wa Baraza Kuu la CUF ambao hawakutaka marekebisho katika makubaliano yaliyowasilishwa au waliokuwa wakiyakataa kabisa kwa kutowaamini CCM kutokana na uzoefu wa Muafaka wa Kwanza wa 1999 na Muafaka wa Pili wa 2001. Walikuwepo, lakini wajumbe wa timu ya mazungumzo ya CUF chini ya Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad, na mimi nikiwa Mwenyekiti wa kikao, tulitumia busara na hekima zote kuwaeleza kwamba hatua ya sasa hairuhusu tena mabadiliko bali ni ya kuidhinisha tu kwa ajili ya kutiwa saini na utekezaji kuanza. Tulifanya hivyo kwa sababu misingi ya Chama chetu ni uungwana, ukweli, uaminifu na uadilifu.
Tulitarajia na CCM nayo kupitia vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama chao ingefanya hivyo. Kwa mshangao mkubwa, wetu na hata wa watu waadilifu na waaminifu wote wa hapa Tanzania na katika Jumuiya ya Kimataifa, tumeshuhudia CCM ikiyapiga teke makubaliano hayo. Huku wakitumia makada wao waliochoka wa propaganda zilizopitwa na wakati na mabingwa wa kisasa wa siasa za kisanii maarufu kama ’spin doctors’ wamekuja na hoja mpya ya kura ya maoni na pia wakisema wamefanya mabadiliko katika baadhi ya vifungu vya makubaliano.
Katika waraka walioupeleka Butiama, ambao CUF inao nakala yake, wanasema kwa kuibua hoja ambayo haikuwepo ya kura ya maoni, CCM itakuwa imeipiku CUF kisiasa.
“Liko wazo ambalo ujumbe wetu umelipata kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais Aman Abeid Karume linalohusu uzito wa makubaliano juu ya kuanzisha mustakabali mpya wa kisiasa kwa msingi wa Serikali shirikishi (power sharing arrangement) katika Zanzibar. Yeye alikuwa na fikra kwamba jambo kubwa na la kutia matumaini kama hili isingefaa maamuzi yake yakahitimishwa na viongozi katika Kamati Kuu na NEC tu. Kwa vile wadau wakuu katika hili ni wananchi wenyewe wa Zanzibar, ingekuwa bora kama suala hili likafikishwa kwao. Sisi (yaani Katibu Mkuu, ndugu Yusuf Makamba, Ndugu Ali Ameir Mohamed na Ndugu Kinguge Ngobale- Mwiru) tulivutiwa sana na pendekezo hili na tuliliunga mkono. … Kwa kukubali wazo hili CCM itakuwa imeipiku CUF katika ubunifu wa kujenga.”
Katika hali ya kawaida, waraka huu usingeweza kufikishwa mbele ya vikao bila ya Mwenyekiti wa vikao kuuona na hivyo ni wazi kuwa Rais Kikwete aliijua hoja hiyo ya kura ya maoni tokea mapema, kama si kuwa ameshiriki hata kuiandaa. Halafu eti wanataka Watanzania wawaamini kuwa hoja hiyo iliibuliwa na wajumbe wa vikao. Rais Jakaya Kikwete na CCM yake wanafanya usanii wa kisiasa katika masuala mazito yanayohusu mustakbali wa taifa letu na maisha ya wananchi wetu.
HOTUBA YA RAIS KIKWETE NA UTETEZI WAKE
Kufuatia usanii huo wa Butiama, CUF ilitoa tamko rasmi kupitia Katibu Mkuu wetu, Maalim Seif Sharif Hamad, kuzikataa hoja zote mbili za CCM, ile ya kutaka mabadiliko ya yaliyokwishakubaliwa na ile ya kura ya maoni. Katibu Mkuu wa CUF alishatoa hoja zetu za kwa nini hatuzikubali hoja hizo lakini naomba nizirejee kwa ufupi hapa:
Kuhusu hoja ya CCM kutaka marekebisho katika yaliyokubaliwa.
Kwanza, CCM haikutaja ni maeneo gani inataka yafanyiwe marekebisho. Pili, hoja hii inashangaza kwa sababu wajumbe wa Kamati ya Mazungumzo kutoka upande wa CCM walikuwa wakiwaarifu wajumbe wa Kamati kutoka upande wa CUF kwamba wao walikuwa wakiwasilisha taarifa kwa kila hatua inayofikiwa katika vikao vya chama vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa na pia kwa viongozi wao wa juu, Rais Jakaya Kikwete na Mheshimiwa Amani Karume, na kupata maelekezo na miongozo inayohitajika. Hatua hii ya mwisho ilikusudiwa kubariki makubaliano hayo yaliyokuwa yakifikiwa hatua kwa hatua na siyo kufungua mjadala mpya kupitia duru mpya ya mazungumzo.
Kuhusu hoja ya CCM makubaliano yanapaswa kuridhiwa na wananchi wenyewe kwa njia ya kura ya maoni.
Muda wote wa mazungumzo ambayo yamechukua miezi 14 na yakiwa yamehusisha vikao 21, wajumbe wa Kamati ya CCM wanaoshiriki mazungumzo hawakuleta hoja hii ya kura ya maoni. Kama nilivyoeleza, pendekezo la kutaka kura ya maoni halikuwa limeibuliwa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM bali lilikuwemo katika Taarifa ya Kamati ya CCM inayoshiriki mazungumzo likiwa ni pendekezo walilotaka liridhiwe na Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa. Kitendo hicho cha Kamati ya CCM kuwasilisha kitu kipya nje ya makubaliano yaliyofikiwa ni upotoshaji mkubwa wa yale yaliyokubaliwa. Iwapo pendekezo hilo lina nia njema ya kuwashirikisha wananchi, kwa nini wajumbe wa Kamati ya CCM wasiliwasilishe katika vikao vya mazungumzo na badala yake wakaamua kuliingiza kama mtego wa kisiasa wenye lengo la “kuipiku CUF”?
Kufuatia Tamko hilo la CUF, Rais Jakaya Kikwete alikuja katika ukumbi huu huu wa Diamond Jubilee na kutoa kile alichokiita ufafanuzi wa maamuzi ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuhusu Muafaka. Katika hotuba yake hiyo aliilaumu CUF kwa kile alichokiita ‘kukurupuka’ katika kutoa Tamko lake kabla ya kupata undani na msingi wa maamuzi hayo.
Inaonyesha Rais Kikwete alikuwa amesahau kauli aliyoitoa katika hotuba yake ya ufunguzi ya tarehe 28 Machi 2008 aliposema na ninanukuu
“kama ilivyo kawaida yetu, tutatoa taarifa kwa ukamilifu mwishoni mwa kikao kuhusu nini kimezungumzwa na nini kimeamuliwa.”
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Mhe. Pius Msekwa alisoma Tamko la Halmashauri Kuu ya Taifa kuhusu Mazungumzo ya Mwafaka baina ya CCM na CUF. Kwa kuzingatia kauli ya Mwenyekiti wa CCM katika hotuba yake ya ufunguzi hapakuwa na sababu ya kusubiri mawasiliano toka kwa Katibu Mkuu kwani ilikuwa wazi kuwa CCM hawataki kutekeleza yale tuliyokubaliana.
Katika hotuba yake ya tarehe 2 Aprili 2008 Rais Kikwete alisema kwamba amemuagiza Katibu Mkuu wa CCM kumuandikia barua Katibu Mkuu wa CUF kuyaeleza hayo kwa undani. Barua hiyo imeletwa kwetu juzi Alhamisi, tarehe 3 Aprili, 2008 ikiwa haina chochote kati ya yale yaliyoahidiwa na Rais. Kwa hakika, tamko lililosomwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Mhe. Pius Msekwa, lina maelezo yanayoeleweka kuliko barua iliyoletwa kwetu ambayo bahati nzuri si siri maana katika utaratibu mpya wa utendaji kazi wa CCM imeisambaza nakala yake kwa vyombo vya habari vyote.
Katika barua hiyo, ambayo nakala pia imeletwa kwangu, Mhe. Makamba anasema: “Sasa naomba nikuarifu rasmi kuwa Wajumbe wa Kamati ya Mazungumzo kwa upande wetu tuko tayari kukutana na Kamati yako ili kuwasilisha uamuzi na maelekezo ya Halmshauri Kuu ya Taifa kama tulivyokubaliana.“ Ndiyo kusema kuwa uamuzi na maelekezo hayo hayamo katika barua hiyo isipokuwa sasa yanatumiwa kuitega CUF kwamba ikubali kurudi katika vikao visivyokwisha na huko ndiko yatakakoelezwa. Ni wazi kuwa Rais Kikwete hakusema kweli aliposema maamuzi na maelekezo hayo yatawasilishwa katika barua ya Katibu Mkuu wa CCM kwa Katibu Mkuu wa CUF. Ni ule ule usanii wa kisiasa kwa mara nyingine tena.
Tumesikitishwa zaidi kupata taarifa kuwa katika mkutano ulioitishwa kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe, na Mabalozi wote wa nchi za kigeni wanaowakilisha nchi zao hapa nchini juzi Ijumaa, tarehe 4 Aprili, 2008, Waziri Membe aliamua kuwafungia ngulai mabalozi hao kwamba eti maelezo kamili ya maeneo CCM inayotaka marekebisho katika rasimu ya makubaliano pamoja na utaratibu mzima wa vipi kura ya maoni iliyopendekezwa utakuwa, umeelezwa kwa kina katika barua ya Mhe. Makamba kwa Maalim Seif. Serikali inapofikia hatua ya kuwadanganya hata mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, hatuwezi kutegemea kuwa wakweli kwa CUF na kwa Watanzania.
Rais Kikwete aliwaeleza mabalozi katika hotuba yake ya kuukaribisha mwaka mpya (Sherry Party) Januari 2006 na ninanukuu:
“I will offer the authority of my office to promote, assist and facilitate an inter-party, broad dialogue on the best way to reduce the polarisation of politics in Zanzibar.” Kwa tafsiri ya kiswahili isiyo rasmi
Nitatumia madaraka ya ofisi yangu kuendeleza, kusaidia na kuwezesha mazungumzo mapana baina ya vyama ili kupata njia bora ya kupunguza mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
Sherry Party ya Januari 2007 aliwaeleza mabalozi:
“We are serious about the multi-stake holder dialogue on Zanzibar. We are doing the final touches to the process. Please continue to be as supportive as you have been.” Ambayo tafsiri yake ni
Tuko makini kuhusu mazungumzo baina ya wadau Zanzibar. Tuko katika kumalizia mchakato huo. Tafadhalini endeleeni kutuunga mkono katika suala hili.
Na sherry party ya mwaka huu Rais kawaeleza mabalozi kuwa
“Muafaka talks between the Civic United Front (CUF) and the ruling party, Chama cha Mapinduzi (CCM), over the situation in Zanzibar, are nearing conclusion. Hopefully, this time around we will succeed in building a firm basis for relegating divisive politics in Zanzibar as a relic of the past. I want to thank you all for being supportive of the process and for understanding its complexities, and therefore the nature of its slow pace.” Tafsiri ya kauli ya Rais ni “Mazungumzo ya Muafaka kati ya the Civic United Front (CUF) na Chama tawala Chama cha Mapinduzi (CCM) kuhusu Zanzibar yanakaribia kuhitimishwa. Ni matumaini yangu safari hii tutafaulu kujenga msingi imara wa kumaliza mpasuko wa kisiasa na kuufanya historia ya zamani. Nataka kuwashukuru nyie nyote kwa kutuunga mkono katika mchakato huu na kwa uelewa wenu wa ugumu wa tatizo lenyewe na ndiyo maana limechukua muda mrefu.”
Kinachosikitisha Rais anashindwa kuheshimu wadhifa wake na kutoa kauli nzito kwa mabalozi na viongozi wa mataifa mengine kimzaha mzaha bila ya kuwa na nia thabiti ya kutekeleza. Anayachukua mambo mazito ya nchi kama vile alivyoahidi kuwa Real Madrid watakuja kucheza mechi ya kufungua uwanja mwaka 2007 bila kujua gharama za kuwaleta Real Madrid na uwanja utakamilika lini. Bila shaka Watanzania tutamvumilia Rais wetu na usanii wake katika mambo ya mpira. Kuendeleza usanii katika mambo mazito ya Muafaka na kuwahadaa mabalozi kunahatarisha amani ya nchi yetu na kulivunjia heshima taifa letu.
Katika hotuba yake ya tarehe 2 April 2008, Rais ameeleza kuwa
“Halmashauri Kuu iliona haja ya kufanya marekebisho fulani fulani katika baadhi ya mapendekezo hasa kuhusu mapendekezo ya muundo wa Serikali Shirikishi. Shabaha ya mapendekezo hayo ni kuboresha na kuimarisha mfumo huo unaopendekezwa. Marekebisho yanapendekezwa kwenye utaratibu wa uteuzi wa Wasaidizi Wakuu wawili wa Rais wa Zanzibar na Baraza la Mawaziri. Marekebisho mengine yanahusu pendekezo la kuwepo Baraza la Usuluhishi. “
Waheshimiwa wananchi pendekezo la Muundo wa Serikali Shirikishi lilitolewa na timu ya CCM katika kamati ya mazungumzo. Timu ya CCM ilieleza mapendekezo hayo yanatokana na mashauriano waliyoyafanya na Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete na Makamu wake Mhe. Aman Abeid Karume. Mapendekezo ya CUF ilikuwa kugawa nyadhifa za Rais na Waziri Kiongozi kati ya vyama vitakavyokuwa vimepata kura zilizokaribiana katika kura za Rais. CUF ikatoa concession, ikaachia pendekezo lake na kulikubali pendekezo la CCM. Pendekezo la kwanza la CCM ilikuwa pawepo na Makamu mmoja wa Rais. CUF ikaridhia. Baadaye wakabadilisha kuwepo makamu wawili wa Rais. CUF tukawakubalia. Rais anaeleza kuwa NEC inataka kulifanyia marekebisho pendekezo lililoletwa na ujumbe wa CCM baada ya kupokea ushauri wake na wa Makamu wake. Sisi tuwaeleweje CCM? Kama hii siyo mbinu na usanii wa kupoteza muda na kufanya mazungumzo yasiyokwisha ni kitu gani?
Katika kutapatapa na kujitetea, Rais Kikwete amesema kwamba eti yeye ni mwanademokrasia sana na hivyo aliamua kuruhusu mjadala wa wazi kuhusu suala hilo kusudi wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa watoe maoni yao kwa uwazi. Akajigamba kwamba huo ndiyo utaratibu wa CCM. Lakini akashindwa kutueleza Watanzania kuwa iwapo huo ndio utaratibu wake na wa CCM, kwa nini hakuruhusu mjadala wa wazi na wa kidemokrasia katika vikao hivyo hivyo kuhusu mafisadi wa Richmond na fedha za akaunti ya nje ya Benki Kuu ya Tanzania, ambao inadaiwa ni marafiki zake wa karibu kisiasa.
Katika hotuba yake hiyo, Rais Kikwete aliitaja mifano ya nchi kadhaa zilizotumia utaratibu wa kugawana madaraka kama njia ya kumaliza migogoro ya kisiasa kama vile Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Rwanda, Afrika Kusini na hata Kenya. Nilikuwa na hamu ya kumsikia akitutajia angalau mfano mmoja wa nchi iliyopiga kura ya maoni katika kuidhinisha makubaliano ya kumaliza mgogoro wa kisiasa kama ambavyo chama chake chini ya uongozi wake kimeamua kuhusu Zanzibar. Aliporudi kutoka Kenya, alijisifu sana kwamba ameweza kufanikisha kufikiwa makubaliano ya kugawana madaraka kati ya ODM na PNU, lakini hakutwambia kwa nini hakuwapa wazo la kura ya maoni ili wananchi wayaridhie makubaliano hayo.
Katika maamuzi mazito yaliyofanywa na CCM, TANU na ASP hakuna hata mara moja kura ya maoni ilitumiwa. Mwaka 1964, Tanganyika na Zanzibar ziliungana, hapakuwa na kura ya maoni. Mwaka 1965 mfumo wa vyama vingi vya siasa ulifutwa hapakuwa na kura ya maoni. Mwaka 1977 vyama vya TANU na ASP viliunganishwa, hapakuwa na kura ya maoni ya wanachama TANU na ASP. Kamati iliyounganisha vyama ikapewa kazi ya kuandika katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hapakuwa na kura ya maoni. Katiba ya Zanzibar ya kwanza ya 1979 na1984 haikupigiwa kura ya maoni. Waliodai kuwepo kura ya maoni kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika miaka ya mwishoni ya 1980 waliambiwa wamechafua hali ya hewa ya kisiasa na kuwekwa kizuizuni. Tuliporejea katika mfumo wa vyama vingi hapakuwa na kura ya maoni. Katika mabadiliko ya katiba ya 11 yaliondoa nafasi ya Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jambo ambalo ndiyo msingi wa mkataba wa kimataifa wa Muungano wa dola mbili wa 1964. Jambo hili linaloidhalilisha Zanzibar lilipingwa na Wazanzibari wakiwemo wana CCM, hapakuwa na kura ya maoni.
Katiba ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano haina kipengele chochote kinachoelezea kufanya maamuzi yeyote kwa kutumia kura ya maoni. Tanzania haina sheria ya kura ya maoni. Rais hakueleza kura ya maoni itakapopigwa itakuwa ya maamuzi ya mwisho au ni ya ushauri? Kama ni ya mamuzi ya mwisho, Katiba ya Zanzibar inaeleza kuwa Baraza la Wawakilishi ndilo lenye mamlaka ya kufanya marekebisho ya katiba. Au kwa kuwa CCM wamezoea kuvunja Katiba basi suala hili haliwapi shida? Kama ni ya ushauri kwa nini kupoteza gharama kubwa ya kura ya maoni kwa maamuzi ambayo siyo ya mwisho?
Kwa muda mrefu Watanzania wamekuwa wanadai kushiriki kuandika katiba mpya yenye misingi imara ya demokrasia, CCM wamekataa kata kata. Bila kuona haya sasa wanadai kupanua demokrasia kwa kuitisha kura ya maoni kuwa ndio njia yakutatua mgogoro wa kisiasa Zanzibar.
Katika ufunguzi wa Mkutano wa Butiama, Rais Kikwete alisema wamekutana Butiama kuiweka “hai kumbukumbu ya Mzee wetu hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.” Hata hivyo CCM imeendelea kudharau ushauri wa Mwalimu Nyerere alioutoa mwaka 1995 kuwa suluhisho la Zanzibar ni serikali ya umoja wa kitaifa. Rais Kikwete alimnukuu Rais wa zamani wa Marekani, John F. Kennedy, aliyesema: “mifano ya watu mashuhuri huzaa watu wa kiwango hicho”. Kuja hapa kutatupa ari ya kuishi na kutumikia taifa na watu wake kwa mfano wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Tulitegemea Rais ataiga alau mfano wa Mwalimu alivyokuwa akiendesha vikao vya CCM. Katika hotuba yake ya Aprili 2 inaonyesha wazi kuwa Uenyekiti wake ni dhaifu na hana dira wala msimamo. Mfano wa Uenyekiti wa Mwalimu Nyerere haujazaa Mwenyekiti wa CCM mwenye kiwango alau cha asilimia tano ya kiwango chake. Kwa Rais Kikwete kujikweza kuwa anafuata mikoba ya Mwalimu kama nukuu ya maneno ya JFK inavyolenga ni kuidhalilisha kumbu kumbu ya Baba wa Taifa.
Kwa ufupi, hotuba ya Rais Kikwete haikuwa na jipya ambalo lingetufanya CUF kufikiria upya msimamo wetu uliotolewa kupitia Katibu Mkuu wetu. Kama kuna jipya basi ni ule usanii wa Rais Kikwete wa kukanusha kufanya usanii kwa kisiasa kwa kurejea tena usanii wa kisiasa. Sasa ni rasmi kwamba Tanzania yetu inaongozwa na watu wanaosimamia usanii wa siasa na ufisadi wa uchumi. Watanzania tuna sababu na haki ya kutaka mabadiliko ili kuipatia nchi yetu uongozi makini unaohitajika kufanya maamuzi makini yanayohusu mustakbali wetu.
MUSTAKBALI WA MAKUBALIANO YETU:
Napenda nimalizie kwa kusema kuwa baada ya kumsikia Rais Jakaya Kikwete, na iwapo kweli anataka tumuamini tena kwamba dhamira yake katika kuumaliza mgogoro wa kisiasa Zanzibar iko pale pale, basi CUF iko tayari kumsaidia kwa kukubaliana na mojawapo ya njia hizi mbili:
CCM ikubali kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya vyama vyetu viwili na endapo kweli Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho “imeyakubali kimsingi” makubaliano yaliyofikishwa kwake kama ilivyosema taarifa yake, basi ikubali kutia saini makubaliano hayo na utekelezaji wa yaliyokubaliwa uanze mara moja.
Kama kuna haja ya kutafakari maeneo hayo machache ambayo CCM inataka marekebisho, basi kwanza Rais Kikwete atembee juu ya maneno yake kwa kumuagiza Katibu Mkuu ayawasilishe kwa CUF maeneo hayo yakiwa na maelezo ya kina. Baada ya hapo, kama alivyofanya Kenya kwa kuwaweka pamoja Rais Mwai Kibaki na Mheshimiwa Raila Odinga kuhitimisha makubaliano, basi atumie kipaji chake na uwezo wake huo kuwaweka pamoja wadau wakuu wa masuala haya ambao ni Mheshimiwa Amani Karume na Maalim Seif Sharif Hamad kuhitimisha makubaliano hayo. Kwa njia hii, hata ile hoja inayojaribiwa kujengwa sana katika siku za karibuni kwamba viongozi wa CCM Zanzibar ndiyo kikwazo kwa kuwa hawashirikishwi katika maamuzi yanayoihusu Zanzibar na kwamba ndiyo waliokwamisha ‘nia njema’ ya Rais Kikwete itakuwa imeondoka.
Pendekezo la kufanya kiini macho cha kura ya maoni yenye lengo la kuchelewesha utiaji saini na utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa HALIKUBALIKI KWA CUF.
Nawashukuru kwa kunisikiliza. Ahsanteni sana.
HAKI SAWA KWA WOTE
Dar es Salaam
06 Aprili, 2008
Monday, April 7, 2008
Sunday, April 6, 2008
Meli yazama bahari ya Hindi
MELI isiyofahamika iliyokuwa na abiria na wafanyakazi 14, imezama katika Bahari ya Hindi mwishoni mwa wiki.
Mbali na kuwa na abiria hao, meli hiyo ilikuwa na shehena ya magari matatu ya Idara ya Magereza na lita 90 za mafuta ya mitambo ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco).
Habari zilizopatikana jana zilieleza kuwa meli hiyo ilizama usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita katika Bahari ya Hindi wakati ikiwa njiani kutokea Dar es Salaam kuelekea Mafia.
Habari hizo zinaeleza kati ya abiria hao, mwili mmoja unaosadikiwa kuwa wa nahodha wa meli hiyo umepatikana huku abiria wanane kati ya hao wakipatikana wakia hai katika eneo la Makunduchi, Zanzibar na wengine watano hado hawajulikani walipo.
Miongoni mwa abiria ambao hawajulikani waliko, ni askari magereza ambaye alikuwa akisindikiza shehena ya magari matatu ambayo ni mali ya idara hiyo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, tayari ametuma salamu za rambirambi kwa ndugu na familia wa marehemu, abiria na wafanyakazi wa meli hiyo.
Aidha, Pinda ameagiza Polisi Wanamaji kwenda eneo la ajali kusaidia kuokoa watu ambao watakuwa bado wako hai na kama wameshakufa waopoe miili yao.
Mbali na kuwa na abiria hao, meli hiyo ilikuwa na shehena ya magari matatu ya Idara ya Magereza na lita 90 za mafuta ya mitambo ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco).
Habari zilizopatikana jana zilieleza kuwa meli hiyo ilizama usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita katika Bahari ya Hindi wakati ikiwa njiani kutokea Dar es Salaam kuelekea Mafia.
Habari hizo zinaeleza kati ya abiria hao, mwili mmoja unaosadikiwa kuwa wa nahodha wa meli hiyo umepatikana huku abiria wanane kati ya hao wakipatikana wakia hai katika eneo la Makunduchi, Zanzibar na wengine watano hado hawajulikani walipo.
Miongoni mwa abiria ambao hawajulikani waliko, ni askari magereza ambaye alikuwa akisindikiza shehena ya magari matatu ambayo ni mali ya idara hiyo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, tayari ametuma salamu za rambirambi kwa ndugu na familia wa marehemu, abiria na wafanyakazi wa meli hiyo.
Aidha, Pinda ameagiza Polisi Wanamaji kwenda eneo la ajali kusaidia kuokoa watu ambao watakuwa bado wako hai na kama wameshakufa waopoe miili yao.
CUF yatoa masharti kwa JK
Chama cha Wananchi (CUF) kimeto masharti kwa Rais Jakaya Kikwete ili kuyanusuru mazungumzo ya kusaka mwafaka huko Zanzibar.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, amemtaka Rais Kikwete kufanya kila analoweza kuhakikisha kuwa chama chake (CCM) kinasaini makubaliano yaliyofikiwa na kamati ya mazungumzo, kabla CCM haijatumbukiza suala la kura ya maoni.
Iwapo Kikwete atashindwa kulitekeleza hilo, Profesa Lipumba amemtaka atekeleze sharti la pili ambalo ni kuwakutanisha Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad, na Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, kujadili suala hilo.
Lipumba alisema kuwa Kikwete hawezi kushindwa kufanya hilo hasa ikizingatiwa kuwa hivi karibuni tu alifanikiwa kuwakutanisha mahasimu wakubwa huko Kenya, Rais Mwai Kibaki na Raila Odinga katika mgogoro wao wa matokeo ya uchaguzi.
CUF imetoa msimamo huo baada ya rais Kikwete kukiomba chama hicho kurejea katika meza ya mazungumzo, kupitia hotuba yake kwa taifa aliyoitoa wiki iliyopita.
Aidha, katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, amekiandikia chama hicho, kukifahamisha kilichojiri katika kikao cha CC na NEC ya CCM huko Butiama na kukitaka warudi waendelee na mazungumzo hayo.
Lakini CUF ilishatangaza kuwa hakipo tayari kushirikiana na CCM kufanya kile ilichokiita ‘usanii wa kisiasa’ kikimaanisha utekelezaji wa pendekezo ya upigwaji wa kura ya maoni kuhusiana na mfumo wa utawala huko Zanzibar.
Kwa upande mwingine CUF imetangaza maandamanao ya nchi nzima ili kuonyesha msimamo wake katika suala hilo.
Kwa mujibu wa Lipumba, maandamano hayo yatawahusisha pia viongozi wengine wa vyama vya upinzania na yamepangwa kuanza Jumamosi ijayo huko Zanzibar kabla hayajahamia kwenye mikoa mingine.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, amemtaka Rais Kikwete kufanya kila analoweza kuhakikisha kuwa chama chake (CCM) kinasaini makubaliano yaliyofikiwa na kamati ya mazungumzo, kabla CCM haijatumbukiza suala la kura ya maoni.
Iwapo Kikwete atashindwa kulitekeleza hilo, Profesa Lipumba amemtaka atekeleze sharti la pili ambalo ni kuwakutanisha Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad, na Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, kujadili suala hilo.
Lipumba alisema kuwa Kikwete hawezi kushindwa kufanya hilo hasa ikizingatiwa kuwa hivi karibuni tu alifanikiwa kuwakutanisha mahasimu wakubwa huko Kenya, Rais Mwai Kibaki na Raila Odinga katika mgogoro wao wa matokeo ya uchaguzi.
CUF imetoa msimamo huo baada ya rais Kikwete kukiomba chama hicho kurejea katika meza ya mazungumzo, kupitia hotuba yake kwa taifa aliyoitoa wiki iliyopita.
Aidha, katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, amekiandikia chama hicho, kukifahamisha kilichojiri katika kikao cha CC na NEC ya CCM huko Butiama na kukitaka warudi waendelee na mazungumzo hayo.
Lakini CUF ilishatangaza kuwa hakipo tayari kushirikiana na CCM kufanya kile ilichokiita ‘usanii wa kisiasa’ kikimaanisha utekelezaji wa pendekezo ya upigwaji wa kura ya maoni kuhusiana na mfumo wa utawala huko Zanzibar.
Kwa upande mwingine CUF imetangaza maandamanao ya nchi nzima ili kuonyesha msimamo wake katika suala hilo.
Kwa mujibu wa Lipumba, maandamano hayo yatawahusisha pia viongozi wengine wa vyama vya upinzania na yamepangwa kuanza Jumamosi ijayo huko Zanzibar kabla hayajahamia kwenye mikoa mingine.
PINDA AUSHTUKIA MKATABA WA TRL
Kuna uwezekano mkubwa kuwa mkataba baina ya Serikali na kampuni ya Rites ya India kuhusu ukodishaji wa lililokuwa Shirika la reli Tanzania (TRC) nao ni wa kinyonyaji kama ilivyo mikataba ya umeme.
Lakini Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ameshaushtukia mkataba huo na ameeleza wazi wazi suala hilo.
Kilichomshtua Pinda na kutofautiana kwa taarifa za wakati TRC inakaribia kumaliza kazi na zilizotolewa baada ya TRL kuanza kazi.
Mathalani, Pinda anasema kuwa wakati TRC inakaribia kumaliza kazi, kulikuwa na na injia zaidi ya 90, lakini mara baada ya TRL kuanza kazi, ilieleza kuwa kuna injini takriban 50 tu. Sasa inashangaza kuwa injini nyingine zimekwenda wapi?
Kwa upande wao, wafanyakazi wa TRL walishaonyesha wasi wasi huo tangu awali na sasa wanaitumia kauli ya Pinda kushinikiza mkataba huo upelekwe Bungeni ukajadiliwe kama ulivyojadiliwa mkataba wa Richmond.
Mwekezaji huo tayari ameshakodi injini saba ambazo kama ilivyo kwa mitambo ya kuzalisha umeme, zinalipiwa capacity charge. Capacity charge ya kila injini iliyokodiwa kutoka kwa kampuni ya Rites ni sh 600,000 kwa siku, ambazo zinalipwa hata kama injini hizo hazifanyi kazi.
Wakati huo huo, wafanyakaziw a TRL waliamua kurejea kazini jana baada ya Pinda kuwaeleza kuwa serikali imeamua kumkopesha mwekezaji huyo zaidi ya sh bil. 3 zitakazotumika kulipa viwangio vipya vya mishahara kuanzia mwezi Machi hadi Julai.
Pinda aliwaeleza wafanyakazi hao kwua mwekezaji atapaswa kurejesha fedha hizo kwa sababu ni mkopo na kuwa atumie kipindi huiki ambacho serikali imemwezesha kujipanga ili kuanzia Agosti alipe mishahara hiyo yeye mwenyewe bila matatizo.
Lakini Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ameshaushtukia mkataba huo na ameeleza wazi wazi suala hilo.
Kilichomshtua Pinda na kutofautiana kwa taarifa za wakati TRC inakaribia kumaliza kazi na zilizotolewa baada ya TRL kuanza kazi.
Mathalani, Pinda anasema kuwa wakati TRC inakaribia kumaliza kazi, kulikuwa na na injia zaidi ya 90, lakini mara baada ya TRL kuanza kazi, ilieleza kuwa kuna injini takriban 50 tu. Sasa inashangaza kuwa injini nyingine zimekwenda wapi?
Kwa upande wao, wafanyakazi wa TRL walishaonyesha wasi wasi huo tangu awali na sasa wanaitumia kauli ya Pinda kushinikiza mkataba huo upelekwe Bungeni ukajadiliwe kama ulivyojadiliwa mkataba wa Richmond.
Mwekezaji huo tayari ameshakodi injini saba ambazo kama ilivyo kwa mitambo ya kuzalisha umeme, zinalipiwa capacity charge. Capacity charge ya kila injini iliyokodiwa kutoka kwa kampuni ya Rites ni sh 600,000 kwa siku, ambazo zinalipwa hata kama injini hizo hazifanyi kazi.
Wakati huo huo, wafanyakaziw a TRL waliamua kurejea kazini jana baada ya Pinda kuwaeleza kuwa serikali imeamua kumkopesha mwekezaji huyo zaidi ya sh bil. 3 zitakazotumika kulipa viwangio vipya vya mishahara kuanzia mwezi Machi hadi Julai.
Pinda aliwaeleza wafanyakazi hao kwua mwekezaji atapaswa kurejesha fedha hizo kwa sababu ni mkopo na kuwa atumie kipindi huiki ambacho serikali imemwezesha kujipanga ili kuanzia Agosti alipe mishahara hiyo yeye mwenyewe bila matatizo.
Waziri Mkuu Pinda aingilia kati TRL
Ule mgogoro baina ya kampuni ya reli nchini (TRL) na wafanyakazi wake huenda ukachukua sura mpya leo wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda atakapokutana na wafanyakazi waliogoma asubuhi hii.
Uamuzi huo wa Pinda unaonekana ni juhudi za serikali kuokoa jahazi baada ya wafanyakazi hao kumgomea wazairi wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Pofesa Juma Kapuya.
Pinda anaingilia kati suala hilo wakati watu kadhaa wakiwa wameshateseka kutokana na kukosa usafiri wa kuwarejesha makwao bada ta wafanyakazi wa TRL kugoma.
Kutoka Dodoma, ilishaelezwa kuwa baadhi ya abiria waligeuka ombaomba baada ya kuishiwa na kushindwa kuwa na fedha kwa ajili ya usafiri mbadala wa kuwafikisha makao.
aWalipokutana na waziri huyo wiki iliyopita, wafanyakazi hao, licha ya kumzomea na kumuanikizia mabango yenye ujumbe mkali kwa serikali, walimueleza wazi wazi kuwa pasipo kulipwa mishahara mipya ambayo mwajiri mwenyewe aliahidi wiki kadhaa zilizopita, hawatorejea kazini.
Sehemu ya ujumbe katika mabango hayo ulikuwa ukiilaumu serikali kwa kumkumbatia mwekezaji huyo kutoka India huku ikishindwa kutetea haki za raia wake wanaonyonywa kwa kisingizio cha uwekezaji.
Walifikia hatua ya kumzomea kapuya baada ya waziri huyo kuonyesha wazi wazi kuwa serikali ipo pamoja na mwekezaji huyo, kiasi cha kufikia hatua ya kuanza kusikiliza sababu zuilizompfanya ashindwe kulipa mishahara ambayo aliiahidi siku chache tu zilizopita.
Leo wafanyakazi hao wanaingia katika siku ya nne ya mgomo wao, wakidai kulipwa viwango vipya vya mishahara ambayo mwajiri aliahisi katikati ya mwezi uliopita. Menejiment ya TRL ilikubali kulipa mishahara hiyo baada ya wafanyakazi hao kugoma kwa siku mbili wakidai nyongeza ya mishahara.
Makubaliano yaliyokuwa yamefikiwa ni mwajiri kuongeza mshahara kwa kima cha chini kutoka sh 87,000 za wakati huo hadi sh 200,000. zaidi ya hayo, mwajiri huyo aliahidi kuongeza kiwango hicho ifikapo Agosti mwaka huu.
Lakini kwa mashangao wa wafanyakazi hao, ilipofika mwisho wa mwezi wa tatu, mwajiri hakulipa viwango hivyo vya mishahara kama alivyokuwa ameahidi na jambo hilo liliwafanya wafanyakazi wampe mwajiri huyo notisi ya saa 48, ambayo ilishamalizika na wakafikia uamuzi wa kutangaza mgomo mwingine.
Kilichoshangaza zaidi, mwajiri huyo aliamua kukaa kimya aliposhindwa kulipa mishahara. Hata wafanyakazi walipomwendea na notisi, hakutoa sababu yoyote hadi aalipoitwa na waziri kapuya alipoeleza kwa mshangao kuwa anashindwa kulipa mishahara hiyo mipya kutokana na kutokuwa na uwezo wa kifedha.
Wafanyakazi wanahoji; kama mwekezaji hakuwa na uwezo wa kifedha, kwa nini alikubali na kuahidi kulipa mishahara hiyo?
Hivi sasa, ofisi ya Kapuya imeunda kamati inayojumuisha serikali, menejiment ya TRL na wafanyakazi, kukagua hesabu zilizotolewa na mwajiri huyo, ili kuthibitisha kuwa kweli hawezi kulipa mishahara hiyo.
Uamuzi huo wa Pinda unaonekana ni juhudi za serikali kuokoa jahazi baada ya wafanyakazi hao kumgomea wazairi wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Pofesa Juma Kapuya.
Pinda anaingilia kati suala hilo wakati watu kadhaa wakiwa wameshateseka kutokana na kukosa usafiri wa kuwarejesha makwao bada ta wafanyakazi wa TRL kugoma.
Kutoka Dodoma, ilishaelezwa kuwa baadhi ya abiria waligeuka ombaomba baada ya kuishiwa na kushindwa kuwa na fedha kwa ajili ya usafiri mbadala wa kuwafikisha makao.
aWalipokutana na waziri huyo wiki iliyopita, wafanyakazi hao, licha ya kumzomea na kumuanikizia mabango yenye ujumbe mkali kwa serikali, walimueleza wazi wazi kuwa pasipo kulipwa mishahara mipya ambayo mwajiri mwenyewe aliahidi wiki kadhaa zilizopita, hawatorejea kazini.
Sehemu ya ujumbe katika mabango hayo ulikuwa ukiilaumu serikali kwa kumkumbatia mwekezaji huyo kutoka India huku ikishindwa kutetea haki za raia wake wanaonyonywa kwa kisingizio cha uwekezaji.
Walifikia hatua ya kumzomea kapuya baada ya waziri huyo kuonyesha wazi wazi kuwa serikali ipo pamoja na mwekezaji huyo, kiasi cha kufikia hatua ya kuanza kusikiliza sababu zuilizompfanya ashindwe kulipa mishahara ambayo aliiahidi siku chache tu zilizopita.
Leo wafanyakazi hao wanaingia katika siku ya nne ya mgomo wao, wakidai kulipwa viwango vipya vya mishahara ambayo mwajiri aliahisi katikati ya mwezi uliopita. Menejiment ya TRL ilikubali kulipa mishahara hiyo baada ya wafanyakazi hao kugoma kwa siku mbili wakidai nyongeza ya mishahara.
Makubaliano yaliyokuwa yamefikiwa ni mwajiri kuongeza mshahara kwa kima cha chini kutoka sh 87,000 za wakati huo hadi sh 200,000. zaidi ya hayo, mwajiri huyo aliahidi kuongeza kiwango hicho ifikapo Agosti mwaka huu.
Lakini kwa mashangao wa wafanyakazi hao, ilipofika mwisho wa mwezi wa tatu, mwajiri hakulipa viwango hivyo vya mishahara kama alivyokuwa ameahidi na jambo hilo liliwafanya wafanyakazi wampe mwajiri huyo notisi ya saa 48, ambayo ilishamalizika na wakafikia uamuzi wa kutangaza mgomo mwingine.
Kilichoshangaza zaidi, mwajiri huyo aliamua kukaa kimya aliposhindwa kulipa mishahara. Hata wafanyakazi walipomwendea na notisi, hakutoa sababu yoyote hadi aalipoitwa na waziri kapuya alipoeleza kwa mshangao kuwa anashindwa kulipa mishahara hiyo mipya kutokana na kutokuwa na uwezo wa kifedha.
Wafanyakazi wanahoji; kama mwekezaji hakuwa na uwezo wa kifedha, kwa nini alikubali na kuahidi kulipa mishahara hiyo?
Hivi sasa, ofisi ya Kapuya imeunda kamati inayojumuisha serikali, menejiment ya TRL na wafanyakazi, kukagua hesabu zilizotolewa na mwajiri huyo, ili kuthibitisha kuwa kweli hawezi kulipa mishahara hiyo.
Thursday, April 3, 2008
Serikali yakubali kuibeba TRL
Serikali imesema kuwa ipo tayari kulipa sehemu ya mishahara ambayo mwajiri wa kampuni ya reli nchini (TRL) anapaswa kuwalipa waajiriwa wake.
Waziri wa kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Alhaj Juma Kapuya, amesema kuwa serikali itajitisha mzigo huo baada ya kuzipitia hesabu za mwekezaji huyo.
Ameyasema hayo baada ya mwekezaji huyo kubainisha kuwa hana uwezo wa kuwalipa watumishi wake mishahara wanayohitaji, licha ya yeye mwenyewe kukubali na kusaini makubaliano mapema mwezi uliopita kuwa atalipa kima cha chini cha sh 200,000 kuanzia mwezi machi na ifikapo Agosti ataongeza kiwango hicho.
Mwekezaji huo ameushangaza ulimwengu kwa kukubali kulipa kiasi hicho, lakini akashindwa kufanya hivyo bila kutoa sababu yoyote mpaka pale wafanyakazi walipogoma. Hata walipotoa tishio hilo la kugioma, mwajiri huyo hakueleza sababu ya kushindwa kulipa mishahara hiyo, zaidi ya kutabngaza kusitisha kwa safari za treni kwa muda usiojulikana.
Lakini inaelekea kuwa mwajiri huyo aliidokeza serikali kuwa haina uwezo wa kifedha kulipa mishahara hiyo na kumpelekea kapuya hesabu zao zinazoonyesha kuwa hawezi kulipa mishahara hiyo.
Hiyo inathibitishwa na kauli ya Kapuya kuwa serikali itazipitia hesabu hizo kwa kuwa zimeandaliwa na mwekezaji huyo peke yake.
Lakini kapuya ameshangaza zaidi pale alipoahidi kuwa serikali italipia sehemu ya mishahara hiyo iwapo itajiridhisha kuwa kweli mwekezaji huyo hawezi kuwalipa watumishi viwango vya mishahara ambavyo yeye mwenyewe alivikubali na kupanga muda wa kulipa!
Waziri wa kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Alhaj Juma Kapuya, amesema kuwa serikali itajitisha mzigo huo baada ya kuzipitia hesabu za mwekezaji huyo.
Ameyasema hayo baada ya mwekezaji huyo kubainisha kuwa hana uwezo wa kuwalipa watumishi wake mishahara wanayohitaji, licha ya yeye mwenyewe kukubali na kusaini makubaliano mapema mwezi uliopita kuwa atalipa kima cha chini cha sh 200,000 kuanzia mwezi machi na ifikapo Agosti ataongeza kiwango hicho.
Mwekezaji huo ameushangaza ulimwengu kwa kukubali kulipa kiasi hicho, lakini akashindwa kufanya hivyo bila kutoa sababu yoyote mpaka pale wafanyakazi walipogoma. Hata walipotoa tishio hilo la kugioma, mwajiri huyo hakueleza sababu ya kushindwa kulipa mishahara hiyo, zaidi ya kutabngaza kusitisha kwa safari za treni kwa muda usiojulikana.
Lakini inaelekea kuwa mwajiri huyo aliidokeza serikali kuwa haina uwezo wa kifedha kulipa mishahara hiyo na kumpelekea kapuya hesabu zao zinazoonyesha kuwa hawezi kulipa mishahara hiyo.
Hiyo inathibitishwa na kauli ya Kapuya kuwa serikali itazipitia hesabu hizo kwa kuwa zimeandaliwa na mwekezaji huyo peke yake.
Lakini kapuya ameshangaza zaidi pale alipoahidi kuwa serikali italipia sehemu ya mishahara hiyo iwapo itajiridhisha kuwa kweli mwekezaji huyo hawezi kuwalipa watumishi viwango vya mishahara ambavyo yeye mwenyewe alivikubali na kupanga muda wa kulipa!
HOTUBA YA JK MACHI 2008
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWENYE MKUTANO NA VIONGOZI NA WANACHAMA WA CCM NA JUMUIYA ZAKE, DIAMOND JUBELEE
02 APRILI, 2008
Ndugu Wana-CCM Wenzangu;
Viongozi na Wanachama Jumuiya za CCM;
Ndugu Wananchi;
Kama mjuavyo tumejiwekea utaratibu wa Rais kuzungumza na taifa kila mwisho wa mwezi. Lakini, kwa mwisho wa mwezi wa Machi nilishindwa kufanya hivyo kwa sababu ya kulazimika kwenda Mererani, Mkoani Manyara ambako kumetokea maafa makubwa kwa wachimbaji wa madini. Maafa hayo yalisababishwa na mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa zilizonyesha katika eneo hilo usiku wa tarehe 28 kuamkia tarehe 29. Nilikwenda kuwafariji wenye migodi, wachimbaji na familia zao kwa maafa yaliyowakuta. Pia nilikwenda kuona shughuli za uokoaji na uopoaji wa miili ya wale waliofariki.
Kwenye hotuba yangu ya mwezi Machi, nilikuwa nimepanga kuongea na Watanzania kuhusu mambo mawili. Mambo hayo ni Ushiriki wa Majeshi ya Tanzania kama sehemu ya Jeshi la Umoja wa Afrika nchini Comoro na tatizo la mauaji ya ndugu zetu Maalbino kwa imani za kishirikina. Awali nilikuwa na wazo kuwa maadam tarehe 31 Machi imeshapita basi niache na hotuba ipite. Lakini, baada ya kusikia kueleweka vibaya kwa uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM kuhusu Mazungumzo ya Muafaka baina ya CCM na CUF nikaona ipo haja ya kuzungumza. Niitumie fursa hii kuzungumzia yale mambo mawili niliyoyakusudia, na pia nizungumzie maafa ya Mererani na uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuhusu mazungumzo ya Muafaka baina ya CCM na CUF.
Tanzania Kupeleka Majeshi Comoro
Ndugu Wananchi;
Tanzania imepeleka wanajeshi wake 924 kuungana na wanajeshi wa Sudan, Senegal na Libya katika Jeshi la Umoja wa Afrika lililoundwa kuisaidia Serikali ya Jamhuri ya Shirikisho la Visiwa vya Comoro kurejesha mamlaka yake katika Kisiwa cha Nzuani. Jamhuri ya Shirikisho la Visiwa vya Comoro inaundwa na visiwa vitatu, yaani Ngazija (Grand Comoro), Nzuani (Anjouan) na Mwali (Moeli). Kwa mujibu wa mfumo wao wa utawala, kila kisiwa kina Serikali yake ya ndani inayoongozwa na Rais, na kuna Rais wa Shirikisho anayekaa na kufanyia kazi mjini Moroni, kwenye Makao Makuu ya Taifa la Comoro.
Urais wa Shirikisho unashikiliwa kwa mzunguko baina ya raia wa visiwa hivyo vitatu. Rais wa sasa ni Mheshimiwa Abdallah Sambi ambaye anatokea Kisiwa cha Nzuani. Uchaguzi ujao wa Urais unaenda kwa mtu wa kisiwa kingine.. Kipindi cha Urais wa Shirikisho na wa Visiwa vinavyounda Shirikisho ni miaka mitano.
Mwezi Aprili, 2002 uchaguzi wa Marais wa Visiwa vya Ngazija, Mwali na Anzuan ulifanyika. Kipindi cha miaka mitano cha Marais hao kiliisha rasmi tarehe 13 Aprili, 2007. Kwa mujibu wa utaratibu na Katiba ya Comoro uchaguzi wa Rais hufanyika ndani ya siku 90 baada ya kipindi cha uongozi cha Rais kumalizika. Katika kipindi hicho cha siku 90, Spika wa Bunge huwa Kiongozi wa muda. Kwa mujibu huo wa Katiba, tarehe 14 Aprili, 2007, Marais wa visiwa vya Ngazija na Mwali waliachia madaraka kwa Maspika wa Mabunge ya Visiwa vyao, lakini Bw. Mohamed Bakari, Rais wa Kisiwa cha Nzuan akakataa na kudai kuwa ataendelea kuwepo mpaka baada ya uchaguzi. Akamfukuza Spika ili kutengeneza mazingira ya kutokuwepo mtu anayestahili kuchukua nafasi yake. Rais wa Shirikisho alitumia mamlaka yake ya Kikatiba kuteua mtu mwingine badala ya Spika aliyeondolewa kibabe na Bwana Mohamed Bakari. Lakini naye huyo pia Bwana Bakari akamkataa.
Rais Abdallah Sambi aliamua kwenda Nzuani kumuona na kuzungumza na Bw. Mohamed Bakari na viongozi wengine ili kupata ufumbuzi wa mgogoro huo usiokuwa wa lazima. Bwana Mohamed Bakari akafunga kiwanja cha ndege cha Ouani, Nzuani na kuweka magogo uwanjani hapo hivyo ndege ya Rais wa Shirikisho ikashindwa kutua.
Aidha, Bwana Mohamed Bakari akaamuru kuteremshwa bendera za Shirikisho na kukamatwa kwa askari 30 wa Jeshi la Shirikisho. Mmoja wakamuua, watatu wakawajeruhi, na 26 wakawanyang’anya silaha na kuwafukuza kisiwani humo.
Baada ya hapo, Umoja wa Afrika ukaingilia kati na kufanya mazungumzo na Bwana Mohamed Bakari kumtaka aheshimu Katiba aondoke madarakani na kuruhusu taratibu stahiki zifanyike. Imefanyika mikutano tisa (9) ya namna hiyo; miwili Pretoria, mwili Cape Town, mitatu Addis Ababa na miwili Nzuani. Mikutano yote hiyo haikufanikiwa.
Ndugu Wananchi;
Bwana Mohamed Bakari alikaidi mara zote kuondoka na kufanya mambo kuwa magumu zaidi. Alikaidi uamuzi wa Rais wa Shirikisho ulioungwa mkono na Umoja wa Afrika na kutaka uchaguzi Nzuani usifanyike tarehe 10 Juni, 2007. Sababu ya agizo hilo ni kutaka uchaguzi huo ufanyike siku ambayo Serikali ya Shirikisho na Umoja wa Afrika utakuwepo kusimamia. Bwana Mohamed Bakari akakaidi na kuendelea kufanya uchaguzi huo chini ya usimamizi wake yeye mwenyewe. Kwa kutumia madaftari ya shule, akaendesha uchaguzi na kutangaza kuwa amepata ushindi wa asilimia 85. Mahakama ya Katiba ya Comoro ikakataa kuutambua uchaguzi huo, lakini yeye akaendelea kula kiapo na kuendelea kuwa Rais wa Nzuani kwa kipindi cha pili cha miaka mitano.
Umoja wa Afrika ukaendelea na juhudi za kumtaka aachie madaraka kuruhusu taratibu za Kikatiba zifuatwe na uchaguzi halali ufanyike. Kama nilivyosema hapo awali, mikutano tisa iliyofanywa (wa mwisho ulikuwa mwezi Februari, 2008) haikuzaa matunda.
Kwa sababu ya ukaidi wa dhahiri wa Bw. Mohamed Bakari, ndipo katika kikao kilichopita, Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika walikubali ombi la Rais Abdallah Sambi la kuunda Jeshi la Umoja wa Afrika kusaidia Jeshi la Comoro kurejesha mamlaka ya Serikali ya Shirikisho katika kisiwa cha Nzuani. Iliamuliwa kuwa, Baraza la Amani na Usalama la AU lishirikiane na Kamisheni ya Afrika kutafuta nchi zitakazotoa majeshi ya kufanya kazi hiyo. Kwa kushirikiana na Serikali ya Comoro ndipo zikaombwa nchi nne yaani Libya, Senegal, Sudan na Tanzania kuchangia wanajeshi kwenye Jeshi la UA.
Baada ya kupokea uamuzi huo wa Baraza la Amani na Usalama la UA, tulijadiliana na kufanya mashauriano na wahusika mbalimbali na hatimaye tukakubaliana kuwa tuyakubali maombi hayo. Tumefanya hivyo kwa kutambua wajibu wetu kwa UA na wajibu wetu kwa nchi jirani ya Comoro ambayo wetu wake na wetu wana mahusiano makubwa hata ya kinasaba. Lakini pia kwetu sisi kama Mwenyekiti wa AU tunao wajibu wa kuhakikisha maamuzi muhimu kama haya ya kuhakikisha kuwa nchi ya Comoro haimeguliwi tena kama ilivyofanywa huko nyuma.
Ndugu Wananchi;
Kama mnavyofahamu, operesheni maalum ya kumng’oa Bwana Mohamed Bakari na utawala wake ilianza rasmi alfajiri ya tarehe 24 Machi, 2008 na siku iliyofuata, yaani tarehe 25 Machi, 2008, majeshi ya Umoja wa Afrika yakiongozwa na Tanzania yaliweza kukamilisha zoezi hilo bila umwagaji wa damu au uharibifu wa mali. Hakuna mtu aliyeuawa wakati wa operesheni hiyo. Bwana Mohamed Bakari ametoroka na kiongozi wa muda Nzuani amepatikana kwa mujibu wa Katiba ya Comoro. Ameanza kazi ya kuliongoza taifa kwenye uchaguzi utakaofanyika mwezi Mei, 2008.
Majeshi yetu yataondoka kwa awamu mbili: Awamu ya kwanza yataondoka mwisho wa mwezi huu na ya pili mara baada ya uchaguzi. Umoja wa Afrika una dhamana ya kugharamia operesheni hii. Kiasi cha fedha kimetolewa na UA unaendelea kutoa. Pale ambapo tutalazimika kutumia fedha zetu tumeelewana kuwa UA utatufidia.
Kwanini Tanzania Imeshiriki
Ndugu Wananchi;
Operesheni hii imefanikiwa. Ni heshima kwa UA na ni heshima kwa nchi yetu kuwa sehemu ya mafanikio haya. Kwa niaba yenu napenda kuitumia nafasi hii kuwapongeza Wanajeshi wetu kwa kazi nzuri waliyoifanya. Imeliletea jeshi letu heshima kubwa na sifa kwa nchi yetu. Kabla ya operesheni ile kwanza kulikuwa na hofu kubwa hasa ya kutokea vifo na uharibifu wa mali. Mkuu wa Majeshi yetu Jenerali Davis Mwamunyange alinihakikishia kuwa wameiandaa kisayansi kuepuka hayo yote. Na kweli ndivyo ilivyotokea. Nawashukuru na kumpongeza Mkuu wa Majeshi na Maofisa Wakuu Wanadhimu Makao Makuu ya Jeshi katika operesheni hii huko Comoro kwa kazi nzuri iliyotukuka. Nawapa pole kwa magumu yote waliyokabiliana nayo. Nawapa pole kwa msiba uliowapata wa kumpoteza mwenzao mmoja aliyezama majini pale Kisiwani Mwali siku moja kabla ya majeshi yetu kuondoka kuelekea Nzuani. Ajali haina kinga.. Kila mtu ana siku yake na namna yake ya kuondoka. Tuzidi kumuombea marehemu wetu huyo kwa Mwenyezi Mungu aipokee roho yake na kuiweka mahala pema peponi, Amin.
Tatizo la Mauaji Yanayotokana na Imani za Kishirikina
Ndugu Wananchi;
Jambo la pili ninalotaka kuliongelea ni kuhusu mauaji ya ndugu zetu wa jamii ya albino yanayofanyika hapa nchini. Niseme mapema tu kwamba jambo hili ni la aibu kubwa kwa jamii yetu. Ni jambo la hatari kwa amani na usalama wa watu wetu.
Ndugu Wananchi,
Mauaji yanayotokana na imani za kishirikina ni tatizo la muda mrefu kabla na wakati wa ukoloni na imeendelea hata baada ya nchi yetu kupata uhuru.
Uzoefu unaonyesha kwamba baadhi ya wahanga wanaoathirika ni akina mama vikongwe ambao hutuhumiwa kuwa ni wachawi, kwamba wanawaroga watu wengine na kuwaua. Mauaji ya namna hii yamejikita sana katika mikoa ya Kanda ya Ziwa mikoa ya Mara, Shinyanga, Mwanza na hata mkoa wa Tabora. Mauaji haya hufanywa na magenge ya watu wanaokodishwa na watu ambao wamepata maelezo potofu kutoka kwa waganga wa jadi baada ya kuuguliwa au kufiwa na jamaa zao, na wao kuamua kulipiza kisasi kwa watu waliotajwa kuwa ndio waliowaroga jamaa zao.
Vilevile, mauaji mengi ya kishirikina hufanyika kutokana na imani potofu walizonazo baadhi ya watu kwamba kwa kutumia viungo vya watu wengine wanaweza kufanikiwa katika biashara wazifanyazo au katika shughuli zao za uchimbaji wa madini na uvuvi.
Kutokana na imani hizo potofu, watu hao wanaowania utajiri wa haraka haraka huenda kwa waganga wa jadi na kupata maelekezo ya viungo vinavyotakiwa kutoka kwenye mwili wa binadamu. Katika mazingira haya, tumeshuhudia baadhi ya watu wakiuawa na kukutwa wamenyofolewa baadhi ya sehemu za miili yao kama vile sehemu za siri, ndimi, viganja, matiti na wengine kuchunwa ngozi.
Katika nyakati zingine, huvumishwa habari za watu wenye maumbile au mapungufu fulani kwenye mwili kama vile watu wenye vipara au maalbino kwamba viungo vyao vina mchango mkubwa katika kufanikisha utajiri wa haraka. Kwa sababu hiyo katika kipindi cha mwezi Julai, 2007 hadi sasa tumeshuhudia ndugu zetu wa jamii ya maalbino wakivamiwa na kuuawa na wengine kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na hadi sasa bado hawajapatikana. Kuanzia mwezi Machi 2007 hadi 01 Aprili, 2008, jumla ya maalbino 19 wameuawa na wengine wawili wametoweka na hadi sasa hawajapatikana, lakini inasadikika kwamba nao wameuawa.
Tatizo hili la mauaji yanayotokana na imani za ushirikina limekuzwa zaidi na baadhi ya watu ambao hawana taaluma ya uganga (waganga pandikizi) kwa kujiingiza kwenye shughuli za uganga wa jadi hivyo kuzidisha upotoshwaji wa watu kwa kupiga ramli chonganishi au maelekezo yasiyosahihi kwa lengo la kujipatia kipato kwa njia ya udanganyifu.
Ndugu Watanzania wenzangu,
Kama nilivyosema, mauaji haya ni ya kusikitisha na ni ukatili usio na mfano. Ni aibu kubwa kwa jamii yetu. Nawasihi wale wanaojihusisha na vitendo hivi, waachane na dhana ya kwamba utajiri unaweza kuja kwa njia ya miujiza bila ya kufanya kazi kwa bidii.. Utajiri unakuja kwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa. Pia unakuja kwa kuwa na nidhamu ya kazi na matumizi ya fedha uzipatazo.
Tiba ya asili na uganga wa jadi ni sehemu ya asili ya Mtanzania, na hiyo Serikali inaitambua na wala haiikatazi. Hata hivyo, nawasihi Watanzania wenzangu tujiepushe na matapeli na wahuni walioingilia fani hii na wao wakiwa na nia ya kuwalaghai wananchi kwamba wanaweza kuwafanya wapate utajiri wa haraka haraka kwa kutumia baadhi ya viungo vya wanadamu.
Hatua za Serikali Kukabiliana na Tatizo Hili
Ndugu Wananchi,
Serikali kwa upande wake itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kudhibiti mauaji haya kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali, wakiwemo wale waganga wa jadi waliosajiliwa Serikali.
Kwa kushirikiana na Chama vya Maalbino nchini, Serikali inaendelea na zoezi la kupata orodha ya maalbino wote nchini na kutambua sehemu wanazoishi ili kwa kushirikiana na Serikali za Mitaa, Manispaa, Kata na Vijiji kubuni kwa pamoja namna ya kutengeneza mazingira ya ulinzi yanayoweza kuwahakikishia usalama wao. Zoezi hili ni muhimu liambatane na matumizi ya Ulinzi-Shirikishi ili kuwashirikisha wananchi katika kuyatambua makundi ya waganga wa jadi wanaopiga ramli chonganishi na makundi yanayoendesha mauaji hayo na wale wanayoyakodisha.
Vilevile, Serikali itaendelea kutoa elimu ya uhamasishaji kwa wananchi wetu ili wasaidie kutoa taarifa kwa vyombo vya dola dhidi ya wahalifu wote wanaofahamika kushiriki katika mauaji yanayotokana na imani za kishirikina.
Ningependa Jeshi la Polisi nalo liharakishe zoezi la kuwaorodhesha waganga wote wa Tiba Asili walioko nchini ili kudhibiti wale wanaotoa maelekezo ya kuua watu. Nina imani waganga wa jadi wa kweli watatoa ushirikiano, kwani wanawajua wenzao wanaotoa maelekezo kinyume na sheria za nchi.
Vilevile, Jeshi la Polisi lijipange upya kuyatambua na kuyakamata magenge ya watu wanaokodishwa kufanya mauaji kwa wanawake vikongwe, au kwa watu wengine ili kunyofoa sehemu zao za mwili au kuchuna ngozi kama inavyotokea kwa maiti zinazopatikana zimeuawa wakiwemo maalbino.
Ndugu Wananchi,
Kila mtu ana imani yake. Na Serikali haiwezi kuingilia imani za watu kwa mambo ya asili na jadi. Hata hivyo, pale imani yako inapoingilia uhuru na haki ya msingi ya mtu mwingine, ikiwemo haki yake ya kuishi, Serikali haiwezi kukaa kimya. Lazima ichukue hatua.
Nina imani kabisa kwamba tukishirikiana kwa pamoja, wananchi, Serikali, asasi za kiraia, vyombo vya habari, waganga wa jadi na wadau mbalimbali, tunaweza kulimaliza kabisa tatizo hili ili lisije likaonekana kama ni sehemu ya maisha na utamaduni wa Mtanzania.
Muafaka Kati ya CUF na CCM
Sasa napenda kulizungumzia suala la tatu nalo ni Mazungumzo ya Muafaka kati ya CCM na CUF. Suala ambalo limetawala vichwa vya habari vya vyombo vya habari nchini na duniani tangu Butiama mpaka sasa. Na sasa, naona inaanza kujitokeza dhana potofu hasa kuhusu nini kilichoamuliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.
Ndugu Wananchi;
Moja ya ajenda katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichokutana Butiama hivi majuzi ilikuwa ni kujadili taarifa ya Kamati ya Mazungumzo baina ya CCM na CUF ya kutafuta ufumbuzi wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
Kwa kweli haikuwa nia yangu kulizungumzia suala hilo katika hotuba yangu ya mwisho wa mwezi. Lakini kutokana na yanayoendelea sasa, nisipolisema sitaeleweka. Nitaongeza maswali mengi yasiyokuwa na majibu na kuishia kuwafanya wanachama wa CCM, wananchi na hata wenzangu wa CUF wachanganyikiwe zaidi.
Ndugu Wananchi,
Nianze kwa kutamka moja kwa moja kwamba, tofauti na yanayosemwa na baadhi ya watu, sisi katika CCM tunaamini kwamba maamuzi yaliyofanywa na Halmashauri Kuu ya Taifa ni ya kujenga na wala siyo ya kubomoa. Kimsingi ni maamuzi yanayotusogeza hatua kubwa sana mbele kwenye kufikia muafaka.
Labda nirudi nyuma kidogo. Chimbuko la mazungumzo yanayoendelea sasa ni ahadi yangu, wakati nikizindua Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 30 Desemba 2005, kwamba nitaanzisha na kuwezesha mjadala wa kisiasa kwa lengo la kumaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
Dhamira yangu ilitokana na kusoneshwa na uhasama, chuki, kejeli, dharau na hata fujo na vurugu, hasa nyakati za uchaguzi, na hata baada ya uchaguzi, baina ya wakazi wa Zanzibar. Kwangu mimi, hali hii, ambayo imefanya hali ya kisiasa na kiusalama kutokuwa ya utulivu, haiendani na taswira ya Tanzania tunayotaka kuijenga na Tanzania tunayoijua sisi na wanaoijua marafiki zetu wote duniani.
Kutokana na uhasama wa kisiasa, ilifika mahali ambapo watu walikuwa hawaoleani, Bibi na Bwana wanapeana talaka, wazazi na watoto wanatengana na hata ndugu kufarakana. Watu wamekuwa wanasusiana misiba, hawasalimiani, wanaachiana safu misikitini, na hawabebani kwenye vyombo vya usafiri na hawauziani bidhaa hadi wawe wa Chama kimoja. Hiyo sio Tanzania ninayoijua mimi, na wala siyo tunayoijua sote. Hiyo sio Tanzania ambayo waasisi wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Abeid Aman Karume waliyokuwa nayo mioyoni mwao walipojitolea muhanga kuongoza harakati za ukombozi wa nchi zetu mbili zilizokuja kuungana na kuwa nchi moja.
Ndugu zangu,
Siku zote nimekuwa natambua kwamba dhamira yangu pekee haitoshi kwenye kuifikia Tanzania tunayoitaka. Kimsingi, kutekelezwa kwa ahadi niliyoitoa Bungeni kulitegemea ridhaa ya Chama changu na Chama cha Wananchi, CUF. Aidha, kulitegemea utayari na ushirikiano wa viongozi wa siasa wa Zanzibar na wananchi wanaowaongoza. Na, nilisema hivyo kwenye hotuba yangu Bungeni.
Bahati nzuri, nilipolipeleka suala hili kwenye vikao vyote vikubwa husika vya Chama chetu (CCM), viongozi wenzangu wa Chama, kutoka Bara na Visiwani, waliunga mkono hoja na haja ya kufanya mazungumzo na Chama cha CUF. Vilevile, sote tulifarijika kwamba wenzetu wa CUF nao walikuwa tayari kufanya mazungumzo nasi. Haya hayakuwa mazungumzo ya kwanza baina ya vyama vyetu lakini safari hii tulikuwa na dhamira ya kutafuta suluhu ya kudumu.
Katika miezi yote kumi na minne, tumeendesha mazungumzo haya katika mazingira ya udugu na kuheshimiana, wote tukiwa na dhamira ya kupata suluhu mapema kadri inavyowezekana. Palipotokea vizingiti vya hapa na pale, wote tulishirikiana kuvimaliza na kuendelea na mazungumzo.
Ndugu Wananchi,
Kama mnavyojua, tuliamua kufanya mazungumzo haya kwa mfumo wa Kamati ya pamoja, kila Chama kikiwa na Wajumbe walioongozwa na Katibu Mkuu wa Chama husika. Kila Chama kilitengeneza hadidu za rejea kwa Wajumbe wake. Lakini, Kamati ya Pamoja ilitengeneza agenda ya pamoja ya mazungumzo yao. Bahati nzuri vikao vya uamuzi vya vyama vyetu kila kimoja kwa wakati wake viliridhia agenda hiyo.
Agenda ya Mazungumzo ilikuwa na mambo matano:
(i) Uchaguzi Mkuu wa 2005 na athari zake.
(ii) Usawa na haki kuendesha siasa.
(iii) Masuala ya Utawala wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
(iv) Njia za kuimarisha maelewano katika uendeshaji wa Uchaguzi Huru na Haki.
(v) Utaratibu wa Utekelezaji na Programu ya Utekelezaji wa makubaliano yatakayofikiwa katika mazungumzo hayo.
Ndugu Wana-CCM;
Kwa miezi kumi na minne, yaani tangu Februari, 2007 mazungumzo yamefanyika baina ya Wajumbe wa vyama vyetu viwili kwenye Kamati hiyo. Pamoja na tofauti au migongano ya hapa na pale, mazungumzo yalifanyika katika mazingira ya uwazi, ukweli na moyo wa udugu. Mara kwa mara Wajumbe wa Vyama vyetu walitoa taarifa kwa uongozi wa juu wa vyama na vikao vyake. Kwa upande wa CCM, Wajumbe wetu walitoa taarifa kwangu na kwa Kamati Kuu, na kila Halmashauri Kuu ya Taifa ilipokutana, taarifa ya maendeleo ya mazungumzo ilitolewa. Maoni yalitolewa na Wajumbe walielekezwa ipasavyo kuhusu yale yaliyofikiwa na yale ambayo walitakiwa kurudi kwa wenzao na kuzungumza nao. Nao walifanya hivyo na kutoa taarifa ipasavyo. Zipo nyakati Wajumbe wetu walilazimika kurudi kwetu kutoa taarifa kuhusu baadhi ya maelekezo tuliyowapa kutoafikiwa na upande wa wenzetu. Pale ilipoonekana kuwa wenzetu wanayo hoja bora zaidi ilikubaliwa.
Ndugu Wananchi;
Nalisema hili kutaka kuwathibitishia kuwa kilichofanywa Butiama na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM si jambo la ajabu, ndiyo utaratibu wetu. Katika vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM vilivyofanyika Musoma, hususan Butiama, wajumbe wetu wa Kamati waliwasilisha taarifa ya mwisho ya mazungumzo yao wa wenzao wa CUF. Hivyo walileta taarifa ya mazungumzo na makubaliano kuhusu agenda zote tano. Wajumbe walijadili agenda moja baada ya nyingine. Kwa jumla Wajumbe wamepokea kwa furaha taarifa hiyo, wameridhika na kazi nzuri iliyofanywa na kuwapongeza wajumbe wake na wenzi wao wa CUF kwa kazi nzuri waliyoifanya. Kazi ambayo waliitambua kuwa ni hatua kubwa katika safari yetu ya pamoja kuutafutia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa uliopo Zanzibar.
Mjadala ulikuwa wa kina, tena mrefu. Ilituchukua saa 6 kwenye Kamati Kuu na karibu saa 8 kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa. Agenda hii siyo tu ilichukua muda mwingi wa mkutano wetu wa Butiama bali ilipunguza hamu ya wajumbe kujadili kwa urefu agenda nyingine. Hii ilikuwa ndiyo ilikuwa ndiyo mama wa agenda zote.
Kuna nyakati mjadala ulikuwa mkali na kuwatisha baadhi, wakidhani kuwa huenda tusifikie makubaliano. Lakini kama ilivyo kawaida ya Chama chetu, mwishowe tulikubaliana na mapendekezo ya Kamati. Kwangu mimi ukali wa baadhi ya wajumbe unaimarisha imani yangu kuhusu umuhimu wa kuhakikisha kuwa juhudi za kupata muafaka zinafanikiwa. Kushindwa hakuna maslahi kwa Zanzibar na kwa nchi yetu kwa jumla.
Pamoja na kukubaliana na mapendekezo ya Kamati, Halmashauri Kuu iliona haja ya kufanya marekebisho fulani fulani katika baadhi ya mapendekezo hasa kuhusu mapendekezo ya muundo wa Serikali Shirikishi. Shabaha ya mapendekezo hayo ni kuboresha na kuimarisha mfumo huo unaopendekezwa. Marekebisho yanapendekezwa kwenye utaratibu wa uteuzi wa Wasaidizi Wakuu wawili wa Rais na Baraza la Mawaziri. Marekebisho mengine yanahusu pendekezo la kuwepo Baraza la Usuluhishi. Mimi naamini marekebisho yote ambayo Halmashauri Kuu imetaka yafanywe kwa nia ya kuboresha mapendekezo ya Kamati yetu yasingekuwa mambo magumu. Naamini wenzetu na wao wangegundua hekima ya Halmashauri Kuu kupendekeza inavyopendekeza. Bahati mbaya wenzetu wanakataa jambo kabla ya kuliona. Hata kabla Katibu Mkuu wa CCM hajawaandikia kuwasilisha kile kinachopendekezwa, wenzetu wamekaa na kukataa, sijui wamekataa nini. Wamekataa Halmashauri Kuu kutoa maoni ya kuboresha kitu ambacho inabidi sote tukubaliane ndipo kitekelezwe. Je, ni sawa hivyo?
Ndugu Wananchi;
Pamoja na marekebisho hayo yahusuyo mapendekezo ya Kamati kuhusu mfumo wa Serikali Shirikishi, katika mjadala, Wajumbe ndani ya Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu walikuja na mawazo mawili mapya. Nia ya mawazo hayo ni kuimarisha na kuboresha huo mfumo mpya unaopendekezwa uwepo. Jambo la kwanza linahusu kuwashirikisha wananchi katika kufanya uamuzi huu mkubwa. Halmashauri Kuu ya Taifa inaamini kuwa mabadiliko yanayopendekezwa ni makubwa sana na ya msingi. Yanahusu kuubadili kabisa mfumo wa sasa wa utawala na uendeshaji wa shughuli za Serikali Zanzibar. Halmashauri Kuu ya Taifa inaona kuwa ipo haja ya msingi ya kuwashirikisha wananchi wa Zanzibar kuamua.
Halmashauri Kuu inaona kuwa sahihi za Maalim Seif na Mzee Makamba au za viongozi tu pekee hazitoshi. Ridhaa ya wananchi ni muhimu na hili ni jambo la msingi na la kawaida katika mifumo yote ya kidemokrasia.. Kama suala ni muda, napenda kuwahakikishia kuwa hata CCM inapenda mambo hayo yaishe mapema iwezekanavyo.
Jambo la pili jipya lililojitokeza kwenye Halmashauri Kuu linahusu haja ya kujipa muda wa kuufanyia mapitio mfumo huu mpya unapendekezwa hapo utakapokubaliwa na kutumika. Tofauti na ilivyo sasa ambapo mshindi anaunda Serikali hata kama ameshinda kwa tofauti ndogo (hata iwe chini ya asilimia moja), mfumo mpya nao unaleta utaratibu ambapo hata kama mshindi kapata ushindi mkubwa lazima awashirikishe wenzake. Halmashauri Kuu inaafiki hoja ya mfumo wa sasa wa kutokidhi haja ya kuwepo utulivu wa kisasa na kiusalama hasa kwa historia yetu tangu 1995 na hivyo kuafiki dhana ya kushirikiana katika Serikali kama jawabu.
Pamoja na hayo, Halmashauri Kuu inasema mahali pote mfumo wa Serikali Shirikishi ulipotumika ilifanyika hivyo kwa muda maalum. Wakati wote lengo kuu likiwa kuivusha nchi katika mazingira magumu ya wakati huo. Baada ya hapo, watu hurejea kwenye mfumo wa kawaida wa mshindi kuunda Serikali akiwa na hiari ya kuwashirikisha wenzake. Hivyo ndivyo ilivyokuwa Afrika ya Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na ndivyo ilivyo hata sasa hapo Kenya. Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM inataka hata kwenye huu mfumo wetu tuweke utaratibu wa kuutazama upya kila baada ya wakati. Kwa jinsi ilivyo sasa dhana hiyo haipo. Ni mfumo utakaokuwepo daima dumu.
Ndugu Wananchi;
Kwa kweli hayo ndiyo yanapendekezwa na CCM. Na ndiyo mambo ambayo Halmashauri Kuu imeagiza Wajumbe wake waende wakazungumze na wenzi wao wa CUF. Tukubaliane ili tuendelee na hatua zinazofuatia. Kwa kweli sikutegemea yale mliyoyasikia ya kusemwa na viongozi wa CUF kuhusu maamuzi hayo. Upande mmoja siwalaumu kwa sababu walitoa matamko kabla ya kupata undani wa kila kilichoamuliwa na CCM. Lakini, upande mwingine nawalaumu kwa kutokusubiri taarifa rasmi kutoka kwa CCM juu ya mapendekezo yetu. Mimi bado naamini kuwa wangeyapata na kuyatafakari huenda wasingesema hayo wanayoyasema au kama wangesema wangefanya hivyo kwa namna na lugha tofauti.
Kwetu sisi katika CCM, tulichotegemea kutoka kwa wenzetu wa CUF, siyo tamko la kujitoa kwenye mazungumzo na kutishia kuvurugika kwa amani. Tulichotegemea ni kwamba hata kama wangekuwa na wazo la kujitoa kwenye mazungumzo, angalau wangetusikiliza ili kujua ni marekebisho gani ambayo wana-CCM wanaona yangeimarisha na kuyapa uhalali zaidi makubaliano ambayo Kamati zetu zilikuwa zinaelekea kuyapata.
Napenda kuwahakikishia wana-CCM wenzangu, wenzetu wa CUF na wananchi kwa jumla kuwa CCM haifanyi, wala haitafanya usanii wa kisiasa kwa jambo kubwa kama hili. CCM ina nia ya dhati ya kupata ufumbuzi wa kudumu wa migogoro inayojirudia ya kisiasa na kiusalama Zanzibar. CCM inaamini kuwa mahali pa kuanzia ni kwenye mazungumzo baina yake na CUF. Ni kutokana na imani hiyo ndiyo maana tarehe 20 – 21 Desemba, 2006, Halmashauri Kuu iliamua kuanzisha mazungumzo na CUF.
Baada ya miezi 14 ya mazungumzo, CCM inaridhika kuwa tumefika mahali pazuri. Kilichobaki ni kukamilisha vizuri ili tupate makubaliano ambayo yatakuwa endelevu kama vile shabaha yetu ilivyo ya kupata suluhisho la kudumu. Kwa ajili hiyo pamoja na yote yaliyotokea na kusemwa CCM itawasilisha mapendekezo yake kwa wabia wetu kwenye mazungumzo haya, yaani CUF. Katibu Mkuu wa CCM, Lt. Yusufu Makamba tayari ameshaandika barua hiyo kwenda kwa Maalim Seif Shariff Hamadi, Katibu Mkuu wa CUF. Ni matumaini yetu kuwa tutapata majibu mazuri na vyama vyetu vitakaa chini baada ya muda si mrefu kukamilisha mazungumzo yetu.
Mimi naamini ni kwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar na wananchi wa Tanzania kwa vyama vya CCM na CUF kukamilisha mazungumzo hayo. Haya shime tufanye hivyo! Inawezekana sote hatuna budi kutimiza wajibu wetu.
Ndugu Wana-CCM, Ndugu Wananchi;
Nawashukuru sana kwa kunisikiliza.
Mungu Ibariki Tanzania!
Mungu Ibariki Afrika!
Kidumu Chama cha Mapinduzi
02 APRILI, 2008
Ndugu Wana-CCM Wenzangu;
Viongozi na Wanachama Jumuiya za CCM;
Ndugu Wananchi;
Kama mjuavyo tumejiwekea utaratibu wa Rais kuzungumza na taifa kila mwisho wa mwezi. Lakini, kwa mwisho wa mwezi wa Machi nilishindwa kufanya hivyo kwa sababu ya kulazimika kwenda Mererani, Mkoani Manyara ambako kumetokea maafa makubwa kwa wachimbaji wa madini. Maafa hayo yalisababishwa na mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa zilizonyesha katika eneo hilo usiku wa tarehe 28 kuamkia tarehe 29. Nilikwenda kuwafariji wenye migodi, wachimbaji na familia zao kwa maafa yaliyowakuta. Pia nilikwenda kuona shughuli za uokoaji na uopoaji wa miili ya wale waliofariki.
Kwenye hotuba yangu ya mwezi Machi, nilikuwa nimepanga kuongea na Watanzania kuhusu mambo mawili. Mambo hayo ni Ushiriki wa Majeshi ya Tanzania kama sehemu ya Jeshi la Umoja wa Afrika nchini Comoro na tatizo la mauaji ya ndugu zetu Maalbino kwa imani za kishirikina. Awali nilikuwa na wazo kuwa maadam tarehe 31 Machi imeshapita basi niache na hotuba ipite. Lakini, baada ya kusikia kueleweka vibaya kwa uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM kuhusu Mazungumzo ya Muafaka baina ya CCM na CUF nikaona ipo haja ya kuzungumza. Niitumie fursa hii kuzungumzia yale mambo mawili niliyoyakusudia, na pia nizungumzie maafa ya Mererani na uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuhusu mazungumzo ya Muafaka baina ya CCM na CUF.
Tanzania Kupeleka Majeshi Comoro
Ndugu Wananchi;
Tanzania imepeleka wanajeshi wake 924 kuungana na wanajeshi wa Sudan, Senegal na Libya katika Jeshi la Umoja wa Afrika lililoundwa kuisaidia Serikali ya Jamhuri ya Shirikisho la Visiwa vya Comoro kurejesha mamlaka yake katika Kisiwa cha Nzuani. Jamhuri ya Shirikisho la Visiwa vya Comoro inaundwa na visiwa vitatu, yaani Ngazija (Grand Comoro), Nzuani (Anjouan) na Mwali (Moeli). Kwa mujibu wa mfumo wao wa utawala, kila kisiwa kina Serikali yake ya ndani inayoongozwa na Rais, na kuna Rais wa Shirikisho anayekaa na kufanyia kazi mjini Moroni, kwenye Makao Makuu ya Taifa la Comoro.
Urais wa Shirikisho unashikiliwa kwa mzunguko baina ya raia wa visiwa hivyo vitatu. Rais wa sasa ni Mheshimiwa Abdallah Sambi ambaye anatokea Kisiwa cha Nzuani. Uchaguzi ujao wa Urais unaenda kwa mtu wa kisiwa kingine.. Kipindi cha Urais wa Shirikisho na wa Visiwa vinavyounda Shirikisho ni miaka mitano.
Mwezi Aprili, 2002 uchaguzi wa Marais wa Visiwa vya Ngazija, Mwali na Anzuan ulifanyika. Kipindi cha miaka mitano cha Marais hao kiliisha rasmi tarehe 13 Aprili, 2007. Kwa mujibu wa utaratibu na Katiba ya Comoro uchaguzi wa Rais hufanyika ndani ya siku 90 baada ya kipindi cha uongozi cha Rais kumalizika. Katika kipindi hicho cha siku 90, Spika wa Bunge huwa Kiongozi wa muda. Kwa mujibu huo wa Katiba, tarehe 14 Aprili, 2007, Marais wa visiwa vya Ngazija na Mwali waliachia madaraka kwa Maspika wa Mabunge ya Visiwa vyao, lakini Bw. Mohamed Bakari, Rais wa Kisiwa cha Nzuan akakataa na kudai kuwa ataendelea kuwepo mpaka baada ya uchaguzi. Akamfukuza Spika ili kutengeneza mazingira ya kutokuwepo mtu anayestahili kuchukua nafasi yake. Rais wa Shirikisho alitumia mamlaka yake ya Kikatiba kuteua mtu mwingine badala ya Spika aliyeondolewa kibabe na Bwana Mohamed Bakari. Lakini naye huyo pia Bwana Bakari akamkataa.
Rais Abdallah Sambi aliamua kwenda Nzuani kumuona na kuzungumza na Bw. Mohamed Bakari na viongozi wengine ili kupata ufumbuzi wa mgogoro huo usiokuwa wa lazima. Bwana Mohamed Bakari akafunga kiwanja cha ndege cha Ouani, Nzuani na kuweka magogo uwanjani hapo hivyo ndege ya Rais wa Shirikisho ikashindwa kutua.
Aidha, Bwana Mohamed Bakari akaamuru kuteremshwa bendera za Shirikisho na kukamatwa kwa askari 30 wa Jeshi la Shirikisho. Mmoja wakamuua, watatu wakawajeruhi, na 26 wakawanyang’anya silaha na kuwafukuza kisiwani humo.
Baada ya hapo, Umoja wa Afrika ukaingilia kati na kufanya mazungumzo na Bwana Mohamed Bakari kumtaka aheshimu Katiba aondoke madarakani na kuruhusu taratibu stahiki zifanyike. Imefanyika mikutano tisa (9) ya namna hiyo; miwili Pretoria, mwili Cape Town, mitatu Addis Ababa na miwili Nzuani. Mikutano yote hiyo haikufanikiwa.
Ndugu Wananchi;
Bwana Mohamed Bakari alikaidi mara zote kuondoka na kufanya mambo kuwa magumu zaidi. Alikaidi uamuzi wa Rais wa Shirikisho ulioungwa mkono na Umoja wa Afrika na kutaka uchaguzi Nzuani usifanyike tarehe 10 Juni, 2007. Sababu ya agizo hilo ni kutaka uchaguzi huo ufanyike siku ambayo Serikali ya Shirikisho na Umoja wa Afrika utakuwepo kusimamia. Bwana Mohamed Bakari akakaidi na kuendelea kufanya uchaguzi huo chini ya usimamizi wake yeye mwenyewe. Kwa kutumia madaftari ya shule, akaendesha uchaguzi na kutangaza kuwa amepata ushindi wa asilimia 85. Mahakama ya Katiba ya Comoro ikakataa kuutambua uchaguzi huo, lakini yeye akaendelea kula kiapo na kuendelea kuwa Rais wa Nzuani kwa kipindi cha pili cha miaka mitano.
Umoja wa Afrika ukaendelea na juhudi za kumtaka aachie madaraka kuruhusu taratibu za Kikatiba zifuatwe na uchaguzi halali ufanyike. Kama nilivyosema hapo awali, mikutano tisa iliyofanywa (wa mwisho ulikuwa mwezi Februari, 2008) haikuzaa matunda.
Kwa sababu ya ukaidi wa dhahiri wa Bw. Mohamed Bakari, ndipo katika kikao kilichopita, Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika walikubali ombi la Rais Abdallah Sambi la kuunda Jeshi la Umoja wa Afrika kusaidia Jeshi la Comoro kurejesha mamlaka ya Serikali ya Shirikisho katika kisiwa cha Nzuani. Iliamuliwa kuwa, Baraza la Amani na Usalama la AU lishirikiane na Kamisheni ya Afrika kutafuta nchi zitakazotoa majeshi ya kufanya kazi hiyo. Kwa kushirikiana na Serikali ya Comoro ndipo zikaombwa nchi nne yaani Libya, Senegal, Sudan na Tanzania kuchangia wanajeshi kwenye Jeshi la UA.
Baada ya kupokea uamuzi huo wa Baraza la Amani na Usalama la UA, tulijadiliana na kufanya mashauriano na wahusika mbalimbali na hatimaye tukakubaliana kuwa tuyakubali maombi hayo. Tumefanya hivyo kwa kutambua wajibu wetu kwa UA na wajibu wetu kwa nchi jirani ya Comoro ambayo wetu wake na wetu wana mahusiano makubwa hata ya kinasaba. Lakini pia kwetu sisi kama Mwenyekiti wa AU tunao wajibu wa kuhakikisha maamuzi muhimu kama haya ya kuhakikisha kuwa nchi ya Comoro haimeguliwi tena kama ilivyofanywa huko nyuma.
Ndugu Wananchi;
Kama mnavyofahamu, operesheni maalum ya kumng’oa Bwana Mohamed Bakari na utawala wake ilianza rasmi alfajiri ya tarehe 24 Machi, 2008 na siku iliyofuata, yaani tarehe 25 Machi, 2008, majeshi ya Umoja wa Afrika yakiongozwa na Tanzania yaliweza kukamilisha zoezi hilo bila umwagaji wa damu au uharibifu wa mali. Hakuna mtu aliyeuawa wakati wa operesheni hiyo. Bwana Mohamed Bakari ametoroka na kiongozi wa muda Nzuani amepatikana kwa mujibu wa Katiba ya Comoro. Ameanza kazi ya kuliongoza taifa kwenye uchaguzi utakaofanyika mwezi Mei, 2008.
Majeshi yetu yataondoka kwa awamu mbili: Awamu ya kwanza yataondoka mwisho wa mwezi huu na ya pili mara baada ya uchaguzi. Umoja wa Afrika una dhamana ya kugharamia operesheni hii. Kiasi cha fedha kimetolewa na UA unaendelea kutoa. Pale ambapo tutalazimika kutumia fedha zetu tumeelewana kuwa UA utatufidia.
Kwanini Tanzania Imeshiriki
Ndugu Wananchi;
Operesheni hii imefanikiwa. Ni heshima kwa UA na ni heshima kwa nchi yetu kuwa sehemu ya mafanikio haya. Kwa niaba yenu napenda kuitumia nafasi hii kuwapongeza Wanajeshi wetu kwa kazi nzuri waliyoifanya. Imeliletea jeshi letu heshima kubwa na sifa kwa nchi yetu. Kabla ya operesheni ile kwanza kulikuwa na hofu kubwa hasa ya kutokea vifo na uharibifu wa mali. Mkuu wa Majeshi yetu Jenerali Davis Mwamunyange alinihakikishia kuwa wameiandaa kisayansi kuepuka hayo yote. Na kweli ndivyo ilivyotokea. Nawashukuru na kumpongeza Mkuu wa Majeshi na Maofisa Wakuu Wanadhimu Makao Makuu ya Jeshi katika operesheni hii huko Comoro kwa kazi nzuri iliyotukuka. Nawapa pole kwa magumu yote waliyokabiliana nayo. Nawapa pole kwa msiba uliowapata wa kumpoteza mwenzao mmoja aliyezama majini pale Kisiwani Mwali siku moja kabla ya majeshi yetu kuondoka kuelekea Nzuani. Ajali haina kinga.. Kila mtu ana siku yake na namna yake ya kuondoka. Tuzidi kumuombea marehemu wetu huyo kwa Mwenyezi Mungu aipokee roho yake na kuiweka mahala pema peponi, Amin.
Tatizo la Mauaji Yanayotokana na Imani za Kishirikina
Ndugu Wananchi;
Jambo la pili ninalotaka kuliongelea ni kuhusu mauaji ya ndugu zetu wa jamii ya albino yanayofanyika hapa nchini. Niseme mapema tu kwamba jambo hili ni la aibu kubwa kwa jamii yetu. Ni jambo la hatari kwa amani na usalama wa watu wetu.
Ndugu Wananchi,
Mauaji yanayotokana na imani za kishirikina ni tatizo la muda mrefu kabla na wakati wa ukoloni na imeendelea hata baada ya nchi yetu kupata uhuru.
Uzoefu unaonyesha kwamba baadhi ya wahanga wanaoathirika ni akina mama vikongwe ambao hutuhumiwa kuwa ni wachawi, kwamba wanawaroga watu wengine na kuwaua. Mauaji ya namna hii yamejikita sana katika mikoa ya Kanda ya Ziwa mikoa ya Mara, Shinyanga, Mwanza na hata mkoa wa Tabora. Mauaji haya hufanywa na magenge ya watu wanaokodishwa na watu ambao wamepata maelezo potofu kutoka kwa waganga wa jadi baada ya kuuguliwa au kufiwa na jamaa zao, na wao kuamua kulipiza kisasi kwa watu waliotajwa kuwa ndio waliowaroga jamaa zao.
Vilevile, mauaji mengi ya kishirikina hufanyika kutokana na imani potofu walizonazo baadhi ya watu kwamba kwa kutumia viungo vya watu wengine wanaweza kufanikiwa katika biashara wazifanyazo au katika shughuli zao za uchimbaji wa madini na uvuvi.
Kutokana na imani hizo potofu, watu hao wanaowania utajiri wa haraka haraka huenda kwa waganga wa jadi na kupata maelekezo ya viungo vinavyotakiwa kutoka kwenye mwili wa binadamu. Katika mazingira haya, tumeshuhudia baadhi ya watu wakiuawa na kukutwa wamenyofolewa baadhi ya sehemu za miili yao kama vile sehemu za siri, ndimi, viganja, matiti na wengine kuchunwa ngozi.
Katika nyakati zingine, huvumishwa habari za watu wenye maumbile au mapungufu fulani kwenye mwili kama vile watu wenye vipara au maalbino kwamba viungo vyao vina mchango mkubwa katika kufanikisha utajiri wa haraka. Kwa sababu hiyo katika kipindi cha mwezi Julai, 2007 hadi sasa tumeshuhudia ndugu zetu wa jamii ya maalbino wakivamiwa na kuuawa na wengine kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na hadi sasa bado hawajapatikana. Kuanzia mwezi Machi 2007 hadi 01 Aprili, 2008, jumla ya maalbino 19 wameuawa na wengine wawili wametoweka na hadi sasa hawajapatikana, lakini inasadikika kwamba nao wameuawa.
Tatizo hili la mauaji yanayotokana na imani za ushirikina limekuzwa zaidi na baadhi ya watu ambao hawana taaluma ya uganga (waganga pandikizi) kwa kujiingiza kwenye shughuli za uganga wa jadi hivyo kuzidisha upotoshwaji wa watu kwa kupiga ramli chonganishi au maelekezo yasiyosahihi kwa lengo la kujipatia kipato kwa njia ya udanganyifu.
Ndugu Watanzania wenzangu,
Kama nilivyosema, mauaji haya ni ya kusikitisha na ni ukatili usio na mfano. Ni aibu kubwa kwa jamii yetu. Nawasihi wale wanaojihusisha na vitendo hivi, waachane na dhana ya kwamba utajiri unaweza kuja kwa njia ya miujiza bila ya kufanya kazi kwa bidii.. Utajiri unakuja kwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa. Pia unakuja kwa kuwa na nidhamu ya kazi na matumizi ya fedha uzipatazo.
Tiba ya asili na uganga wa jadi ni sehemu ya asili ya Mtanzania, na hiyo Serikali inaitambua na wala haiikatazi. Hata hivyo, nawasihi Watanzania wenzangu tujiepushe na matapeli na wahuni walioingilia fani hii na wao wakiwa na nia ya kuwalaghai wananchi kwamba wanaweza kuwafanya wapate utajiri wa haraka haraka kwa kutumia baadhi ya viungo vya wanadamu.
Hatua za Serikali Kukabiliana na Tatizo Hili
Ndugu Wananchi,
Serikali kwa upande wake itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kudhibiti mauaji haya kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali, wakiwemo wale waganga wa jadi waliosajiliwa Serikali.
Kwa kushirikiana na Chama vya Maalbino nchini, Serikali inaendelea na zoezi la kupata orodha ya maalbino wote nchini na kutambua sehemu wanazoishi ili kwa kushirikiana na Serikali za Mitaa, Manispaa, Kata na Vijiji kubuni kwa pamoja namna ya kutengeneza mazingira ya ulinzi yanayoweza kuwahakikishia usalama wao. Zoezi hili ni muhimu liambatane na matumizi ya Ulinzi-Shirikishi ili kuwashirikisha wananchi katika kuyatambua makundi ya waganga wa jadi wanaopiga ramli chonganishi na makundi yanayoendesha mauaji hayo na wale wanayoyakodisha.
Vilevile, Serikali itaendelea kutoa elimu ya uhamasishaji kwa wananchi wetu ili wasaidie kutoa taarifa kwa vyombo vya dola dhidi ya wahalifu wote wanaofahamika kushiriki katika mauaji yanayotokana na imani za kishirikina.
Ningependa Jeshi la Polisi nalo liharakishe zoezi la kuwaorodhesha waganga wote wa Tiba Asili walioko nchini ili kudhibiti wale wanaotoa maelekezo ya kuua watu. Nina imani waganga wa jadi wa kweli watatoa ushirikiano, kwani wanawajua wenzao wanaotoa maelekezo kinyume na sheria za nchi.
Vilevile, Jeshi la Polisi lijipange upya kuyatambua na kuyakamata magenge ya watu wanaokodishwa kufanya mauaji kwa wanawake vikongwe, au kwa watu wengine ili kunyofoa sehemu zao za mwili au kuchuna ngozi kama inavyotokea kwa maiti zinazopatikana zimeuawa wakiwemo maalbino.
Ndugu Wananchi,
Kila mtu ana imani yake. Na Serikali haiwezi kuingilia imani za watu kwa mambo ya asili na jadi. Hata hivyo, pale imani yako inapoingilia uhuru na haki ya msingi ya mtu mwingine, ikiwemo haki yake ya kuishi, Serikali haiwezi kukaa kimya. Lazima ichukue hatua.
Nina imani kabisa kwamba tukishirikiana kwa pamoja, wananchi, Serikali, asasi za kiraia, vyombo vya habari, waganga wa jadi na wadau mbalimbali, tunaweza kulimaliza kabisa tatizo hili ili lisije likaonekana kama ni sehemu ya maisha na utamaduni wa Mtanzania.
Muafaka Kati ya CUF na CCM
Sasa napenda kulizungumzia suala la tatu nalo ni Mazungumzo ya Muafaka kati ya CCM na CUF. Suala ambalo limetawala vichwa vya habari vya vyombo vya habari nchini na duniani tangu Butiama mpaka sasa. Na sasa, naona inaanza kujitokeza dhana potofu hasa kuhusu nini kilichoamuliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.
Ndugu Wananchi;
Moja ya ajenda katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichokutana Butiama hivi majuzi ilikuwa ni kujadili taarifa ya Kamati ya Mazungumzo baina ya CCM na CUF ya kutafuta ufumbuzi wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
Kwa kweli haikuwa nia yangu kulizungumzia suala hilo katika hotuba yangu ya mwisho wa mwezi. Lakini kutokana na yanayoendelea sasa, nisipolisema sitaeleweka. Nitaongeza maswali mengi yasiyokuwa na majibu na kuishia kuwafanya wanachama wa CCM, wananchi na hata wenzangu wa CUF wachanganyikiwe zaidi.
Ndugu Wananchi,
Nianze kwa kutamka moja kwa moja kwamba, tofauti na yanayosemwa na baadhi ya watu, sisi katika CCM tunaamini kwamba maamuzi yaliyofanywa na Halmashauri Kuu ya Taifa ni ya kujenga na wala siyo ya kubomoa. Kimsingi ni maamuzi yanayotusogeza hatua kubwa sana mbele kwenye kufikia muafaka.
Labda nirudi nyuma kidogo. Chimbuko la mazungumzo yanayoendelea sasa ni ahadi yangu, wakati nikizindua Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 30 Desemba 2005, kwamba nitaanzisha na kuwezesha mjadala wa kisiasa kwa lengo la kumaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
Dhamira yangu ilitokana na kusoneshwa na uhasama, chuki, kejeli, dharau na hata fujo na vurugu, hasa nyakati za uchaguzi, na hata baada ya uchaguzi, baina ya wakazi wa Zanzibar. Kwangu mimi, hali hii, ambayo imefanya hali ya kisiasa na kiusalama kutokuwa ya utulivu, haiendani na taswira ya Tanzania tunayotaka kuijenga na Tanzania tunayoijua sisi na wanaoijua marafiki zetu wote duniani.
Kutokana na uhasama wa kisiasa, ilifika mahali ambapo watu walikuwa hawaoleani, Bibi na Bwana wanapeana talaka, wazazi na watoto wanatengana na hata ndugu kufarakana. Watu wamekuwa wanasusiana misiba, hawasalimiani, wanaachiana safu misikitini, na hawabebani kwenye vyombo vya usafiri na hawauziani bidhaa hadi wawe wa Chama kimoja. Hiyo sio Tanzania ninayoijua mimi, na wala siyo tunayoijua sote. Hiyo sio Tanzania ambayo waasisi wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Abeid Aman Karume waliyokuwa nayo mioyoni mwao walipojitolea muhanga kuongoza harakati za ukombozi wa nchi zetu mbili zilizokuja kuungana na kuwa nchi moja.
Ndugu zangu,
Siku zote nimekuwa natambua kwamba dhamira yangu pekee haitoshi kwenye kuifikia Tanzania tunayoitaka. Kimsingi, kutekelezwa kwa ahadi niliyoitoa Bungeni kulitegemea ridhaa ya Chama changu na Chama cha Wananchi, CUF. Aidha, kulitegemea utayari na ushirikiano wa viongozi wa siasa wa Zanzibar na wananchi wanaowaongoza. Na, nilisema hivyo kwenye hotuba yangu Bungeni.
Bahati nzuri, nilipolipeleka suala hili kwenye vikao vyote vikubwa husika vya Chama chetu (CCM), viongozi wenzangu wa Chama, kutoka Bara na Visiwani, waliunga mkono hoja na haja ya kufanya mazungumzo na Chama cha CUF. Vilevile, sote tulifarijika kwamba wenzetu wa CUF nao walikuwa tayari kufanya mazungumzo nasi. Haya hayakuwa mazungumzo ya kwanza baina ya vyama vyetu lakini safari hii tulikuwa na dhamira ya kutafuta suluhu ya kudumu.
Katika miezi yote kumi na minne, tumeendesha mazungumzo haya katika mazingira ya udugu na kuheshimiana, wote tukiwa na dhamira ya kupata suluhu mapema kadri inavyowezekana. Palipotokea vizingiti vya hapa na pale, wote tulishirikiana kuvimaliza na kuendelea na mazungumzo.
Ndugu Wananchi,
Kama mnavyojua, tuliamua kufanya mazungumzo haya kwa mfumo wa Kamati ya pamoja, kila Chama kikiwa na Wajumbe walioongozwa na Katibu Mkuu wa Chama husika. Kila Chama kilitengeneza hadidu za rejea kwa Wajumbe wake. Lakini, Kamati ya Pamoja ilitengeneza agenda ya pamoja ya mazungumzo yao. Bahati nzuri vikao vya uamuzi vya vyama vyetu kila kimoja kwa wakati wake viliridhia agenda hiyo.
Agenda ya Mazungumzo ilikuwa na mambo matano:
(i) Uchaguzi Mkuu wa 2005 na athari zake.
(ii) Usawa na haki kuendesha siasa.
(iii) Masuala ya Utawala wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
(iv) Njia za kuimarisha maelewano katika uendeshaji wa Uchaguzi Huru na Haki.
(v) Utaratibu wa Utekelezaji na Programu ya Utekelezaji wa makubaliano yatakayofikiwa katika mazungumzo hayo.
Ndugu Wana-CCM;
Kwa miezi kumi na minne, yaani tangu Februari, 2007 mazungumzo yamefanyika baina ya Wajumbe wa vyama vyetu viwili kwenye Kamati hiyo. Pamoja na tofauti au migongano ya hapa na pale, mazungumzo yalifanyika katika mazingira ya uwazi, ukweli na moyo wa udugu. Mara kwa mara Wajumbe wa Vyama vyetu walitoa taarifa kwa uongozi wa juu wa vyama na vikao vyake. Kwa upande wa CCM, Wajumbe wetu walitoa taarifa kwangu na kwa Kamati Kuu, na kila Halmashauri Kuu ya Taifa ilipokutana, taarifa ya maendeleo ya mazungumzo ilitolewa. Maoni yalitolewa na Wajumbe walielekezwa ipasavyo kuhusu yale yaliyofikiwa na yale ambayo walitakiwa kurudi kwa wenzao na kuzungumza nao. Nao walifanya hivyo na kutoa taarifa ipasavyo. Zipo nyakati Wajumbe wetu walilazimika kurudi kwetu kutoa taarifa kuhusu baadhi ya maelekezo tuliyowapa kutoafikiwa na upande wa wenzetu. Pale ilipoonekana kuwa wenzetu wanayo hoja bora zaidi ilikubaliwa.
Ndugu Wananchi;
Nalisema hili kutaka kuwathibitishia kuwa kilichofanywa Butiama na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM si jambo la ajabu, ndiyo utaratibu wetu. Katika vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM vilivyofanyika Musoma, hususan Butiama, wajumbe wetu wa Kamati waliwasilisha taarifa ya mwisho ya mazungumzo yao wa wenzao wa CUF. Hivyo walileta taarifa ya mazungumzo na makubaliano kuhusu agenda zote tano. Wajumbe walijadili agenda moja baada ya nyingine. Kwa jumla Wajumbe wamepokea kwa furaha taarifa hiyo, wameridhika na kazi nzuri iliyofanywa na kuwapongeza wajumbe wake na wenzi wao wa CUF kwa kazi nzuri waliyoifanya. Kazi ambayo waliitambua kuwa ni hatua kubwa katika safari yetu ya pamoja kuutafutia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa uliopo Zanzibar.
Mjadala ulikuwa wa kina, tena mrefu. Ilituchukua saa 6 kwenye Kamati Kuu na karibu saa 8 kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa. Agenda hii siyo tu ilichukua muda mwingi wa mkutano wetu wa Butiama bali ilipunguza hamu ya wajumbe kujadili kwa urefu agenda nyingine. Hii ilikuwa ndiyo ilikuwa ndiyo mama wa agenda zote.
Kuna nyakati mjadala ulikuwa mkali na kuwatisha baadhi, wakidhani kuwa huenda tusifikie makubaliano. Lakini kama ilivyo kawaida ya Chama chetu, mwishowe tulikubaliana na mapendekezo ya Kamati. Kwangu mimi ukali wa baadhi ya wajumbe unaimarisha imani yangu kuhusu umuhimu wa kuhakikisha kuwa juhudi za kupata muafaka zinafanikiwa. Kushindwa hakuna maslahi kwa Zanzibar na kwa nchi yetu kwa jumla.
Pamoja na kukubaliana na mapendekezo ya Kamati, Halmashauri Kuu iliona haja ya kufanya marekebisho fulani fulani katika baadhi ya mapendekezo hasa kuhusu mapendekezo ya muundo wa Serikali Shirikishi. Shabaha ya mapendekezo hayo ni kuboresha na kuimarisha mfumo huo unaopendekezwa. Marekebisho yanapendekezwa kwenye utaratibu wa uteuzi wa Wasaidizi Wakuu wawili wa Rais na Baraza la Mawaziri. Marekebisho mengine yanahusu pendekezo la kuwepo Baraza la Usuluhishi. Mimi naamini marekebisho yote ambayo Halmashauri Kuu imetaka yafanywe kwa nia ya kuboresha mapendekezo ya Kamati yetu yasingekuwa mambo magumu. Naamini wenzetu na wao wangegundua hekima ya Halmashauri Kuu kupendekeza inavyopendekeza. Bahati mbaya wenzetu wanakataa jambo kabla ya kuliona. Hata kabla Katibu Mkuu wa CCM hajawaandikia kuwasilisha kile kinachopendekezwa, wenzetu wamekaa na kukataa, sijui wamekataa nini. Wamekataa Halmashauri Kuu kutoa maoni ya kuboresha kitu ambacho inabidi sote tukubaliane ndipo kitekelezwe. Je, ni sawa hivyo?
Ndugu Wananchi;
Pamoja na marekebisho hayo yahusuyo mapendekezo ya Kamati kuhusu mfumo wa Serikali Shirikishi, katika mjadala, Wajumbe ndani ya Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu walikuja na mawazo mawili mapya. Nia ya mawazo hayo ni kuimarisha na kuboresha huo mfumo mpya unaopendekezwa uwepo. Jambo la kwanza linahusu kuwashirikisha wananchi katika kufanya uamuzi huu mkubwa. Halmashauri Kuu ya Taifa inaamini kuwa mabadiliko yanayopendekezwa ni makubwa sana na ya msingi. Yanahusu kuubadili kabisa mfumo wa sasa wa utawala na uendeshaji wa shughuli za Serikali Zanzibar. Halmashauri Kuu ya Taifa inaona kuwa ipo haja ya msingi ya kuwashirikisha wananchi wa Zanzibar kuamua.
Halmashauri Kuu inaona kuwa sahihi za Maalim Seif na Mzee Makamba au za viongozi tu pekee hazitoshi. Ridhaa ya wananchi ni muhimu na hili ni jambo la msingi na la kawaida katika mifumo yote ya kidemokrasia.. Kama suala ni muda, napenda kuwahakikishia kuwa hata CCM inapenda mambo hayo yaishe mapema iwezekanavyo.
Jambo la pili jipya lililojitokeza kwenye Halmashauri Kuu linahusu haja ya kujipa muda wa kuufanyia mapitio mfumo huu mpya unapendekezwa hapo utakapokubaliwa na kutumika. Tofauti na ilivyo sasa ambapo mshindi anaunda Serikali hata kama ameshinda kwa tofauti ndogo (hata iwe chini ya asilimia moja), mfumo mpya nao unaleta utaratibu ambapo hata kama mshindi kapata ushindi mkubwa lazima awashirikishe wenzake. Halmashauri Kuu inaafiki hoja ya mfumo wa sasa wa kutokidhi haja ya kuwepo utulivu wa kisasa na kiusalama hasa kwa historia yetu tangu 1995 na hivyo kuafiki dhana ya kushirikiana katika Serikali kama jawabu.
Pamoja na hayo, Halmashauri Kuu inasema mahali pote mfumo wa Serikali Shirikishi ulipotumika ilifanyika hivyo kwa muda maalum. Wakati wote lengo kuu likiwa kuivusha nchi katika mazingira magumu ya wakati huo. Baada ya hapo, watu hurejea kwenye mfumo wa kawaida wa mshindi kuunda Serikali akiwa na hiari ya kuwashirikisha wenzake. Hivyo ndivyo ilivyokuwa Afrika ya Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na ndivyo ilivyo hata sasa hapo Kenya. Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM inataka hata kwenye huu mfumo wetu tuweke utaratibu wa kuutazama upya kila baada ya wakati. Kwa jinsi ilivyo sasa dhana hiyo haipo. Ni mfumo utakaokuwepo daima dumu.
Ndugu Wananchi;
Kwa kweli hayo ndiyo yanapendekezwa na CCM. Na ndiyo mambo ambayo Halmashauri Kuu imeagiza Wajumbe wake waende wakazungumze na wenzi wao wa CUF. Tukubaliane ili tuendelee na hatua zinazofuatia. Kwa kweli sikutegemea yale mliyoyasikia ya kusemwa na viongozi wa CUF kuhusu maamuzi hayo. Upande mmoja siwalaumu kwa sababu walitoa matamko kabla ya kupata undani wa kila kilichoamuliwa na CCM. Lakini, upande mwingine nawalaumu kwa kutokusubiri taarifa rasmi kutoka kwa CCM juu ya mapendekezo yetu. Mimi bado naamini kuwa wangeyapata na kuyatafakari huenda wasingesema hayo wanayoyasema au kama wangesema wangefanya hivyo kwa namna na lugha tofauti.
Kwetu sisi katika CCM, tulichotegemea kutoka kwa wenzetu wa CUF, siyo tamko la kujitoa kwenye mazungumzo na kutishia kuvurugika kwa amani. Tulichotegemea ni kwamba hata kama wangekuwa na wazo la kujitoa kwenye mazungumzo, angalau wangetusikiliza ili kujua ni marekebisho gani ambayo wana-CCM wanaona yangeimarisha na kuyapa uhalali zaidi makubaliano ambayo Kamati zetu zilikuwa zinaelekea kuyapata.
Napenda kuwahakikishia wana-CCM wenzangu, wenzetu wa CUF na wananchi kwa jumla kuwa CCM haifanyi, wala haitafanya usanii wa kisiasa kwa jambo kubwa kama hili. CCM ina nia ya dhati ya kupata ufumbuzi wa kudumu wa migogoro inayojirudia ya kisiasa na kiusalama Zanzibar. CCM inaamini kuwa mahali pa kuanzia ni kwenye mazungumzo baina yake na CUF. Ni kutokana na imani hiyo ndiyo maana tarehe 20 – 21 Desemba, 2006, Halmashauri Kuu iliamua kuanzisha mazungumzo na CUF.
Baada ya miezi 14 ya mazungumzo, CCM inaridhika kuwa tumefika mahali pazuri. Kilichobaki ni kukamilisha vizuri ili tupate makubaliano ambayo yatakuwa endelevu kama vile shabaha yetu ilivyo ya kupata suluhisho la kudumu. Kwa ajili hiyo pamoja na yote yaliyotokea na kusemwa CCM itawasilisha mapendekezo yake kwa wabia wetu kwenye mazungumzo haya, yaani CUF. Katibu Mkuu wa CCM, Lt. Yusufu Makamba tayari ameshaandika barua hiyo kwenda kwa Maalim Seif Shariff Hamadi, Katibu Mkuu wa CUF. Ni matumaini yetu kuwa tutapata majibu mazuri na vyama vyetu vitakaa chini baada ya muda si mrefu kukamilisha mazungumzo yetu.
Mimi naamini ni kwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar na wananchi wa Tanzania kwa vyama vya CCM na CUF kukamilisha mazungumzo hayo. Haya shime tufanye hivyo! Inawezekana sote hatuna budi kutimiza wajibu wetu.
Ndugu Wana-CCM, Ndugu Wananchi;
Nawashukuru sana kwa kunisikiliza.
Mungu Ibariki Tanzania!
Mungu Ibariki Afrika!
Kidumu Chama cha Mapinduzi
Wednesday, April 2, 2008
Mtego wa Kikwete uliowanasa CUF
ALIPOLIHUTUBIA Bunge wakati analizindua Desemba 30, 2005, rais Jakaya Kikwete alitoa kauli iliyowahakikishia watu wengi kuwa sit u amedhamiria, bali pia atafanya kila lililo katika uwezo wake (kama rais) kumaliza mpasuko wa kisiasa unaokwamisha mambo mengi Zanzibar. Kauli aliyoitoa haikuonyesha mashaka yoyote kuhusu dhamira yake ya kukabiliana na suala hilo.
Kauli hiyo, ilionyesha kwa mara ya kwanza kuwa kiongozi mkuu wa nchyi ametambua matatizo yanayoikabili Zanzibar. Hili lilimpa sifa sana. Hata wakati mazungumzo hayo yaliposuasua, hili lilitumika kama sehemu ya ushawishi kwa Chama cha Wananchi (CUF) kisijitoe katika mazungumzo kama ambavyo kilikuwa kimetishia.
Kwa zaidi ya mwaka mmoja, watanzania walivumilia wakati mazungumzo hayo yakivuta miguu na hatimaye, mwezi uliopita, CUF ilipasua jibu kwa kueleza hadharani kile ambacho kilikubalika katika mazungumzo hayo yaliyokihusisha pia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Lakini kabla ya hapo, itakumbukwa kuwa masuala yaliyokuwa yakijadiliwa katika kamati ya mazungumzo yalikuwa yakivuja na kuufikia umma. Kwa mfano, ilipobainishwa kuwa moja kati ya masuala ambayo yanaelekea kuafikiwa ni kuundwa kwa serikali ya mseto, baadhi ya watu wasiopendelea mfumo huo wa utawala, walijitokeza na kueleza wazi wazi jinsi ambavyo hautokubalika hata kama kamati hiyo ya mazungumzo itaafiki hilo.
Na hivyo ndivyo ilivyotokea.
Lakini hakuna mtu ambaye aliuona mtego alioutega rais Kikwete katyika hotuba yake hiyo ya kihistoria. Katika sehemu ya hotuba hiyo, kwa kutaka kkujivua uwajibikaji katika suala hilo siku za usoni, Kikwete alisema: “Natambua kuwa uamuzi wa mwisho kuhusu hatma ya siasa na utawala Zanzibar ni wa Wazanzibari wenyewe.”
Maana ya kauli hii ni kuwa chochote kitakachoafikiwa katika yale atakayoayaanzisha kuhusiana na mazungumzo hayo, itapaswa kipate baraka za Wazanzibari wenyewe. Kauli hii ni kichaka ambacho CCM wanekitumia kujificha, hasa wale wahafidhina ambao hawapendi kuona CUF ikihusishwa serikalini.
Ilichofanya NEC ya CCM huko Butiama ni kwenda nje kabisa ya yale yaliyoafikiwa katika mazungumzo na kutafuta namna ya kuliingiza hilo la kura ya maoni. Kilichokuwa kinafahamika ni kuwa yaliyokubaliwa kwenye kamati ya mazungumzo ndiyo yafikishwe kwenye vyama husika ili yajadiliwe na kupata baraka. Inavyoelekea, kamati ya mazungumzo haikuweka kipengele chochote kinachohusisha kura ya maoni (ndio maana CUF wameng’aka).
Lakini hata kama itakubalika kuwa kura ya maoni kama ilivyopendekezwa na NEC ya CCM, kitakachotokea kinaweza kujulikana tangu sasa. Mgawanyo wa kura huko Zanzibar tangu 1995 unajulikana. Ni dhahiri kuwa kura hiyo itapigwa kwa kufuata itikadi ya vyama hivyo.
Wale wa CUF, kwa sababu chama chao kimekubali kuingia kwenye serikali ya mseto, wataliunga mkono suala la kuanzishwa kwa serikali hiyo. Kwa upande mwingine, wale wa CCM, ambao wameapa kutoishirikisha CUF kwenye serikali, watalipinga suala hilo.
Kutokana na mgawanyiko uliopo visiwani humo, matokeo ya kura hii hayatatofautiana sana na matokeo ya chaguzi kuu zilizopita. Tofauti ya kura utakuwa chache sana na hili litazusha mabishani upya huku CCM wakishangilia ushindi katika kura ya maoni na CUF ikibishia matokeo hayo kwa sababu wameibiwa kura.
Hapa tutakuwa tuinarudi tena kule kule tulikotoka. Kwa maana hiyo inabidi tujiandae na muafaka mwingine tena wa kupatanisha ugomvi utakaotokana na malumbaano ya kura za maoni. Hivi ndilo lengo letu?
Ilichokifanya CCM ni kutaka kuliingiza taifa katika aibu kubwa. Naamini kuwa kamati ya mazungumzo walijua fika kuwa upo uwezekano wa kupiga kura ya maoni kuhusiana na jambo lakini kwa kutambua ukweli wa hali halisi, waliamua kulikwepesha wakiamini kuwa walikuwa wanawakilisha maslahi ya watu wote. Kumbe huku nyuma kuna genge jingine ambalo lina malengo yake.
Haikuwa na maana kwa Kikwete kuanzisha mazungumzo haya akihusishsa akikundi kidogo cha watu, wakati akijua kuwa suala hilo linahitaji maamuzi ya Wazanzibari wote. Haikuwa na maana kwa Kikwete kuanzisha mazungumzo hayo wakati anafahamu kuwa kitakachokubaliwa kitageuzwa na chama chake kwa maslahi ya nani sijui.
Inavyoonekana, baada ya wawakilishi wa CCM na CUF kukubaliana jambo hili katika mazungumzo yao, CUF katika umoja wao wameamua kulikubali suala hilo wakati wale wa CCM wameamua kulikataa. Je, katika hali kama hiyo suluhisho ni kwenda kwenye kura ya maoni? Na ni nani atatoa uhakikisho leo kuwa kura ya maoni itakuwa ya huru na haki na kuwa matokeo yake yataheshimiwa?
Ieleweke kuwa kinachojadiliwa hapa ni mustakabali wa Zanzibar yote na Tanzania kwa ujumla. Ifahamike kuwa katika mfumo wa utawala ambao tumeamua kuufuata, hakuna maana kuvihusisha vyama viwili tu katika mazungumzo haya hata kama vyama hivyo ndivyo vyenye ushawishi mkubwa visiwani hum oleo hii.
Haipendezi na wala haitosaidia kutengeneza muafaka wa CCM na CUF wakati nchi sit u inafuataa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, bali pia kuna vyamka lukuki ambavyo vinaendesha siasa na vimeshaonyesha upinzani wa kweli katika masuala kadhaa.
Hata kama serikali ya mseto itakubalka Zanzibar, tumepata kujiuliza, iwapo tutafikia muafaka baina ya CUF na CCM leo hii, hivi itakuwaje wakati ambapo NCCR-Mageuzi itafanikiwa kupata nguvu ya kiaisasa Zabnzibar ka kushika nafasi ya pili katika matokeo ya kura? Nayo itahusika na mfumo wa kugawana madaraka au mfumo huu ni kwa ajili ya bCCM na CUF peke yao?
Kama na NCCR au chama kingine chochote kitakuwa kinahusika kutekeleza maamuzi haya, kwa nini nao hawakuhusishwa katika mazungumzo haya aambayo yamezaa mtafaruku mwingine badala ya muafaka?
CCM wanapozungumzia kura ya maoni hivi sasa wanafahamu kuwa suala hilo linahusu pia matumizi ya fedha? Zipo? Au ni namna nyingine ya kukwamisha maafikiano? Kwamba kura ya maoni haitofanyika mapema kwa sababu hakuna fedha na serikali zote mbili zipo katika juhudi ya kutafuta fedha ili kufanikisha suala hilo. Kuna aina fulani ya mchezo unafanyika hapa lakini umeshagunduliwa.
Nani atasimamia kura hii ya maoni? Chombo pekee kinachoweza kusimamia kura hii ni Tume ya Uchaguzi, ambayo inaweza kupewa jukumu hili. Lakini ni tume hii hii ambayo imekuwa ikilalamikiwa mara zote kuwa haitendi haki. Hivi sasa nani ataamini matokeo ya kura ya maoni iwapo mmojawapo wa wahusika atalalamika kuwa haki haikutendeka?
Kuna makosa ambayo kama nchi tumekuwa tukiyafanya kwa muda mrefu sana. Pamoja na kuwa suala hili linaweza lisionekane kuwa na uhusiano wa moja kwa moja, lakini hali ya Zanzibar na uhuru wake kama nchi nalo lina mchango wake humu.
Kwa muda mrefu, Zanzibar inajichukulia na kujiheshimu kama nchi (si taifa kama ilivyoamriwa na Mahakama). Lakini pamoja na mahakama kueleza kuwa hili si taifa, lakini yanayofanyika, jinsi ambavyio Zanzibar imeonekana katika harakati zake za kujiongezea mamlaka na madaraka, inaonekana ni jinsi gani ambavyo inapenda kuwa taifa kamili.
Kosa hapa ni kuwa wakati Zanzibar ikiwa na mwelekeo huo, inaonekana kuwa maamuzi makubwa mengi kuhusiana na nchio hiyo hufanywa aidha na Bara au kuathiriwa sana na Bara. Kwa Wazanzibari wengi, hasa wale wenye msimamo mkali, hili ni tusi.
Katika hili la mpasuko wa kisiasa ilipaswa ieleweke mapema iwapo ni suala lililopo katika malaka ya Zanzibar au la. Kikwete alipaswa kulijua hili kabla hajatoa kauli yake iliyoonyesha dhamira yake ya kulitafutia suala hilo ufumbuzi.
Inaelekea kuwa hata hakupata ushauri wa Wazanzibari kuhusiana na hili kama ambavyo wamemuonyesha juzi huko Butiama kwa kukataa mapendekezo ya kamati aliyoiunda. Kama angekuwa ameshauriana na kukubaliana na Wanzazibari kabla ya kuchukua hatua, ni dhahiri kuwa tusingefikia hali hii.
CCM wasipoanglia wanaweza kuwa wanafanya kosa la kuipa CUF nafasi ya kuendeleza mapambano ya kisiasa bila ya wao wenyewe kujua kuwa wanakipa faida chama hicho. Kwa kuwa kinaonekana kushindwa uchaguzi kila mara, CUF kinapata nafasi ya kuwa chama cha upinzani na kazi yake kubwa kuwa ni kuikosoa serikali iliyopo madarakani. Hili unaweza kulifanya kwa ufanisi iwapo utakuwa na hoja za msingi.
Mchezo unaofanywa na CCM kuhusiana na muafaka unakipa CUF hoja ambazo kwa kutumia uzoefu wake wa upinzani, kinaweza kuisumbua sana CCM hata kama kipo nje ya serikali. Inawezekana CCM wakaona kuwa harakati za CUF ambayo iko nje ya serikali kama keleleza mlango. Huo ni uamuazi wao.
Lakini kuna hatari nyingine kubwa zaidi ambayo inaweza kutokea ndani ya CCM yenyewe. Kwa muda mrefu sana kumekuwa na malalamiko kutoka kwa CUF kuwa wanaonewa, wanadhulumiwa na kunyanyaswa visiwani Zanzibar. Lakini habari kutoka kwenye kikao cha NWEC cha CCM cha Butiama, zinaeleza kuwa hata wana CCM, hasa wale walioko Pemba, nao wameanza kulalamika.
WanaCCM hao wa Pemba wanasema kuwa kutokana na mgawanyo wa kisiasa uliopo, wanafanya kazi kaatika mazingira magumu kisiwani humo, hasa kutokana na CUF kujiimarisha na kuwa hiyo ni ngome yake.
Kwao hawa, serikali ya mseto ilikuwa ni namna fulani ya kuwapunguzia ugumu wa kazi na maumivu wanayoyapata kukitumikia chama chao. Pale ambapo wenzao wa Unguja wameshindwa kusikiliza kilio chao, machozi yao yanaweza yasipotee hivi hivi. Lakini nani anayejua kuwa wanaweza kusikilizwa na kupozwa kwa namna nyingine?
Iwapo hali itaachwa iendelee kuwa hivi, ni dhahiri kwua itafika wakati, kutokana na kuimarika kwa harakati za CUF kutokana na kupatia hoja za msingi kisiasa, hali ya wanaCCM hawa wa Pemba ikawa mbaya zaidi kiasi cha kufikia kubadili msimamo wao.
Wazungu wana msemo kuwa iwapo huwezi kupambana nao basi jiunge nao. Itafika siku ambayo wanaCCM hawa kisiwani pemba wataona dhahiri kuwa hawawezi tena kuhimili vishindo na mikiki ya CUF, hivyo busara pekee watakayobakiwa nayo ni kujiunga nao.
Kauli hiyo, ilionyesha kwa mara ya kwanza kuwa kiongozi mkuu wa nchyi ametambua matatizo yanayoikabili Zanzibar. Hili lilimpa sifa sana. Hata wakati mazungumzo hayo yaliposuasua, hili lilitumika kama sehemu ya ushawishi kwa Chama cha Wananchi (CUF) kisijitoe katika mazungumzo kama ambavyo kilikuwa kimetishia.
Kwa zaidi ya mwaka mmoja, watanzania walivumilia wakati mazungumzo hayo yakivuta miguu na hatimaye, mwezi uliopita, CUF ilipasua jibu kwa kueleza hadharani kile ambacho kilikubalika katika mazungumzo hayo yaliyokihusisha pia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Lakini kabla ya hapo, itakumbukwa kuwa masuala yaliyokuwa yakijadiliwa katika kamati ya mazungumzo yalikuwa yakivuja na kuufikia umma. Kwa mfano, ilipobainishwa kuwa moja kati ya masuala ambayo yanaelekea kuafikiwa ni kuundwa kwa serikali ya mseto, baadhi ya watu wasiopendelea mfumo huo wa utawala, walijitokeza na kueleza wazi wazi jinsi ambavyo hautokubalika hata kama kamati hiyo ya mazungumzo itaafiki hilo.
Na hivyo ndivyo ilivyotokea.
Lakini hakuna mtu ambaye aliuona mtego alioutega rais Kikwete katyika hotuba yake hiyo ya kihistoria. Katika sehemu ya hotuba hiyo, kwa kutaka kkujivua uwajibikaji katika suala hilo siku za usoni, Kikwete alisema: “Natambua kuwa uamuzi wa mwisho kuhusu hatma ya siasa na utawala Zanzibar ni wa Wazanzibari wenyewe.”
Maana ya kauli hii ni kuwa chochote kitakachoafikiwa katika yale atakayoayaanzisha kuhusiana na mazungumzo hayo, itapaswa kipate baraka za Wazanzibari wenyewe. Kauli hii ni kichaka ambacho CCM wanekitumia kujificha, hasa wale wahafidhina ambao hawapendi kuona CUF ikihusishwa serikalini.
Ilichofanya NEC ya CCM huko Butiama ni kwenda nje kabisa ya yale yaliyoafikiwa katika mazungumzo na kutafuta namna ya kuliingiza hilo la kura ya maoni. Kilichokuwa kinafahamika ni kuwa yaliyokubaliwa kwenye kamati ya mazungumzo ndiyo yafikishwe kwenye vyama husika ili yajadiliwe na kupata baraka. Inavyoelekea, kamati ya mazungumzo haikuweka kipengele chochote kinachohusisha kura ya maoni (ndio maana CUF wameng’aka).
Lakini hata kama itakubalika kuwa kura ya maoni kama ilivyopendekezwa na NEC ya CCM, kitakachotokea kinaweza kujulikana tangu sasa. Mgawanyo wa kura huko Zanzibar tangu 1995 unajulikana. Ni dhahiri kuwa kura hiyo itapigwa kwa kufuata itikadi ya vyama hivyo.
Wale wa CUF, kwa sababu chama chao kimekubali kuingia kwenye serikali ya mseto, wataliunga mkono suala la kuanzishwa kwa serikali hiyo. Kwa upande mwingine, wale wa CCM, ambao wameapa kutoishirikisha CUF kwenye serikali, watalipinga suala hilo.
Kutokana na mgawanyiko uliopo visiwani humo, matokeo ya kura hii hayatatofautiana sana na matokeo ya chaguzi kuu zilizopita. Tofauti ya kura utakuwa chache sana na hili litazusha mabishani upya huku CCM wakishangilia ushindi katika kura ya maoni na CUF ikibishia matokeo hayo kwa sababu wameibiwa kura.
Hapa tutakuwa tuinarudi tena kule kule tulikotoka. Kwa maana hiyo inabidi tujiandae na muafaka mwingine tena wa kupatanisha ugomvi utakaotokana na malumbaano ya kura za maoni. Hivi ndilo lengo letu?
Ilichokifanya CCM ni kutaka kuliingiza taifa katika aibu kubwa. Naamini kuwa kamati ya mazungumzo walijua fika kuwa upo uwezekano wa kupiga kura ya maoni kuhusiana na jambo lakini kwa kutambua ukweli wa hali halisi, waliamua kulikwepesha wakiamini kuwa walikuwa wanawakilisha maslahi ya watu wote. Kumbe huku nyuma kuna genge jingine ambalo lina malengo yake.
Haikuwa na maana kwa Kikwete kuanzisha mazungumzo haya akihusishsa akikundi kidogo cha watu, wakati akijua kuwa suala hilo linahitaji maamuzi ya Wazanzibari wote. Haikuwa na maana kwa Kikwete kuanzisha mazungumzo hayo wakati anafahamu kuwa kitakachokubaliwa kitageuzwa na chama chake kwa maslahi ya nani sijui.
Inavyoonekana, baada ya wawakilishi wa CCM na CUF kukubaliana jambo hili katika mazungumzo yao, CUF katika umoja wao wameamua kulikubali suala hilo wakati wale wa CCM wameamua kulikataa. Je, katika hali kama hiyo suluhisho ni kwenda kwenye kura ya maoni? Na ni nani atatoa uhakikisho leo kuwa kura ya maoni itakuwa ya huru na haki na kuwa matokeo yake yataheshimiwa?
Ieleweke kuwa kinachojadiliwa hapa ni mustakabali wa Zanzibar yote na Tanzania kwa ujumla. Ifahamike kuwa katika mfumo wa utawala ambao tumeamua kuufuata, hakuna maana kuvihusisha vyama viwili tu katika mazungumzo haya hata kama vyama hivyo ndivyo vyenye ushawishi mkubwa visiwani hum oleo hii.
Haipendezi na wala haitosaidia kutengeneza muafaka wa CCM na CUF wakati nchi sit u inafuataa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, bali pia kuna vyamka lukuki ambavyo vinaendesha siasa na vimeshaonyesha upinzani wa kweli katika masuala kadhaa.
Hata kama serikali ya mseto itakubalka Zanzibar, tumepata kujiuliza, iwapo tutafikia muafaka baina ya CUF na CCM leo hii, hivi itakuwaje wakati ambapo NCCR-Mageuzi itafanikiwa kupata nguvu ya kiaisasa Zabnzibar ka kushika nafasi ya pili katika matokeo ya kura? Nayo itahusika na mfumo wa kugawana madaraka au mfumo huu ni kwa ajili ya bCCM na CUF peke yao?
Kama na NCCR au chama kingine chochote kitakuwa kinahusika kutekeleza maamuzi haya, kwa nini nao hawakuhusishwa katika mazungumzo haya aambayo yamezaa mtafaruku mwingine badala ya muafaka?
CCM wanapozungumzia kura ya maoni hivi sasa wanafahamu kuwa suala hilo linahusu pia matumizi ya fedha? Zipo? Au ni namna nyingine ya kukwamisha maafikiano? Kwamba kura ya maoni haitofanyika mapema kwa sababu hakuna fedha na serikali zote mbili zipo katika juhudi ya kutafuta fedha ili kufanikisha suala hilo. Kuna aina fulani ya mchezo unafanyika hapa lakini umeshagunduliwa.
Nani atasimamia kura hii ya maoni? Chombo pekee kinachoweza kusimamia kura hii ni Tume ya Uchaguzi, ambayo inaweza kupewa jukumu hili. Lakini ni tume hii hii ambayo imekuwa ikilalamikiwa mara zote kuwa haitendi haki. Hivi sasa nani ataamini matokeo ya kura ya maoni iwapo mmojawapo wa wahusika atalalamika kuwa haki haikutendeka?
Kuna makosa ambayo kama nchi tumekuwa tukiyafanya kwa muda mrefu sana. Pamoja na kuwa suala hili linaweza lisionekane kuwa na uhusiano wa moja kwa moja, lakini hali ya Zanzibar na uhuru wake kama nchi nalo lina mchango wake humu.
Kwa muda mrefu, Zanzibar inajichukulia na kujiheshimu kama nchi (si taifa kama ilivyoamriwa na Mahakama). Lakini pamoja na mahakama kueleza kuwa hili si taifa, lakini yanayofanyika, jinsi ambavyio Zanzibar imeonekana katika harakati zake za kujiongezea mamlaka na madaraka, inaonekana ni jinsi gani ambavyo inapenda kuwa taifa kamili.
Kosa hapa ni kuwa wakati Zanzibar ikiwa na mwelekeo huo, inaonekana kuwa maamuzi makubwa mengi kuhusiana na nchio hiyo hufanywa aidha na Bara au kuathiriwa sana na Bara. Kwa Wazanzibari wengi, hasa wale wenye msimamo mkali, hili ni tusi.
Katika hili la mpasuko wa kisiasa ilipaswa ieleweke mapema iwapo ni suala lililopo katika malaka ya Zanzibar au la. Kikwete alipaswa kulijua hili kabla hajatoa kauli yake iliyoonyesha dhamira yake ya kulitafutia suala hilo ufumbuzi.
Inaelekea kuwa hata hakupata ushauri wa Wazanzibari kuhusiana na hili kama ambavyo wamemuonyesha juzi huko Butiama kwa kukataa mapendekezo ya kamati aliyoiunda. Kama angekuwa ameshauriana na kukubaliana na Wanzazibari kabla ya kuchukua hatua, ni dhahiri kuwa tusingefikia hali hii.
CCM wasipoanglia wanaweza kuwa wanafanya kosa la kuipa CUF nafasi ya kuendeleza mapambano ya kisiasa bila ya wao wenyewe kujua kuwa wanakipa faida chama hicho. Kwa kuwa kinaonekana kushindwa uchaguzi kila mara, CUF kinapata nafasi ya kuwa chama cha upinzani na kazi yake kubwa kuwa ni kuikosoa serikali iliyopo madarakani. Hili unaweza kulifanya kwa ufanisi iwapo utakuwa na hoja za msingi.
Mchezo unaofanywa na CCM kuhusiana na muafaka unakipa CUF hoja ambazo kwa kutumia uzoefu wake wa upinzani, kinaweza kuisumbua sana CCM hata kama kipo nje ya serikali. Inawezekana CCM wakaona kuwa harakati za CUF ambayo iko nje ya serikali kama keleleza mlango. Huo ni uamuazi wao.
Lakini kuna hatari nyingine kubwa zaidi ambayo inaweza kutokea ndani ya CCM yenyewe. Kwa muda mrefu sana kumekuwa na malalamiko kutoka kwa CUF kuwa wanaonewa, wanadhulumiwa na kunyanyaswa visiwani Zanzibar. Lakini habari kutoka kwenye kikao cha NWEC cha CCM cha Butiama, zinaeleza kuwa hata wana CCM, hasa wale walioko Pemba, nao wameanza kulalamika.
WanaCCM hao wa Pemba wanasema kuwa kutokana na mgawanyo wa kisiasa uliopo, wanafanya kazi kaatika mazingira magumu kisiwani humo, hasa kutokana na CUF kujiimarisha na kuwa hiyo ni ngome yake.
Kwao hawa, serikali ya mseto ilikuwa ni namna fulani ya kuwapunguzia ugumu wa kazi na maumivu wanayoyapata kukitumikia chama chao. Pale ambapo wenzao wa Unguja wameshindwa kusikiliza kilio chao, machozi yao yanaweza yasipotee hivi hivi. Lakini nani anayejua kuwa wanaweza kusikilizwa na kupozwa kwa namna nyingine?
Iwapo hali itaachwa iendelee kuwa hivi, ni dhahiri kwua itafika wakati, kutokana na kuimarika kwa harakati za CUF kutokana na kupatia hoja za msingi kisiasa, hali ya wanaCCM hawa wa Pemba ikawa mbaya zaidi kiasi cha kufikia kubadili msimamo wao.
Wazungu wana msemo kuwa iwapo huwezi kupambana nao basi jiunge nao. Itafika siku ambayo wanaCCM hawa kisiwani pemba wataona dhahiri kuwa hawawezi tena kuhimili vishindo na mikiki ya CUF, hivyo busara pekee watakayobakiwa nayo ni kujiunga nao.
Tuesday, April 1, 2008
Tabata Dampo wakataa fidia ya Serikali
Wakazi kadhaa wa eneo la Tabata Dampo katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam, ambao nyumba zao libomolewa hivi karibuni, wamekataa kupokea fidia ya sh milioni 20 kila mmoja, walizoahidiwa na serikali.
Wakazi hao wamesema hawawezi kupokea fedha hizo kwa sababu ni kidogo ukilinganisha na hali halisi inayowakabili hivi sasa baada ya kubomolewa nyumba zao.
Aidha, wakazi hao wamekataa viwanja vya bure walivyopewa na serikali kwa madai kuwa eneo la Buyuni, wakisema kuwa eneo hilo halina huduma zozote za kijamii na hakuna miundombinu kwa sasa.
Tamko la kutaka kuwalipa fuidia wananchi hao lilitolewa na waziri wa Sertikali za Mitaa, Stephen Wassira kama hatua ambazo serikali imezichukua baada ya kukabidhiwa ripoti ya timu iliyochunguza sakata hilo.
Wassira alisema fedha hizo zinalipwa kutokana na uvunjwaji wa haki za binadamu waliofanyiwa wakazi hao kwa kuvunjiwa nyumba zao kinyama.
Timu ya watu wanne ilifanyakazi yake kwa siku 16 na kubaini ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu uliofanywa na watendaji wa Manispaa ya Ilala katika kusimamia zoezi hilo, na kusababisha kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi, Mhandisi na Mwanasheria.
Timu ilibaini kuwa ubomoaji huo haukuzingatia uamuzi wa Baraza la Ardhi ulioisisitiza Halmashauri ya Ilala kuangalia taratibu zilizopo za kuwaondoa wavamizi katika eneo husika.
Aidha, timu hiyo pia iligundua kuwa taratibu za uendeshaji wa Halmashauri hazikuzingatiwa kwa kuwa ilipaswa dhamira ya kubomoa makazi hayo, ilitelewe katika vikao vya menejimenti na baraza la madiwani.
Wassira alisema, timu hiyo ilibaini mambo yaliyojitokeza wakati wa zoezi hilo ambayo ni kunyanyasika na kuteseka kisaikolojia kwa wakazi hao na familia zao na kubainisha kuwa leseni za makazi zilitolewa kimakosa.
Kwa mujibu wa kanuni na sheria kama ilivyoelezwa na Wassira, notisi ya kuondoka katika maeneo hayo ilitakiwa kutolewa siku 30 kabla ya ubomoaji huo kwa vile hilo ni eneo la makazi.
Baraza la ardhi, Februari 27 mwaka huu lilitoa hukumu yenye kueleza kuwa kiwanja namba 52 eneo la viwanda Tabata dampo ni mali ya Kampuni ya Allied Cargo na baada ya siku mbili watendaji wa Manispaa ya Ilala ilibomoa makazi ya watu hao kinyume cha sheria na taratibu.
“Hilo ni kosa, serikali wajibu wetu ni kulinda haki za raia hasa kuishi salama…nataka tuelewane vizuri. Ninachosema hapa ni kwamba tunashughulikia ukiukwaji wa sheria uliofanywa na watendaji wetu.
“Katika hili, kanuni za ubomoaji zimekiukwa na tunachokitoa hapa siyo malipo ya makazi yao, hapana hii ni pole kwa yaliyowakuta. Na mimi kama Waziri wa TAMISEMI, nawashauri kuhamia buyuni kwenye viwanja vya bure.
“We are concerned with human right (tunafuata haki za binadamu) kutokana na makosa ya maofisa wetu wachache, hii watalipwa wenye nyumba tuu,” alisisitiza Wassira.
Alisema, serikali imejifunza kutokana na ukiukwaji huu hivyo imeziagiza mamlaka zote za halmashauri nchini zinazoshughulikia mipango miji kuwawajibisha watendaji wote wanaokiuka sheria, taratibu na kanuni za kuwahamisha wananchi.
Wassira pia, alisema iwapo kuna baadhi ya watendaji wa Manispaa hiyo wanaotuhumiwa kwa ruhwa au uzembe, mamlaka husika ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) itawashighulikia.
Wakazi hao wamesema hawawezi kupokea fedha hizo kwa sababu ni kidogo ukilinganisha na hali halisi inayowakabili hivi sasa baada ya kubomolewa nyumba zao.
Aidha, wakazi hao wamekataa viwanja vya bure walivyopewa na serikali kwa madai kuwa eneo la Buyuni, wakisema kuwa eneo hilo halina huduma zozote za kijamii na hakuna miundombinu kwa sasa.
Tamko la kutaka kuwalipa fuidia wananchi hao lilitolewa na waziri wa Sertikali za Mitaa, Stephen Wassira kama hatua ambazo serikali imezichukua baada ya kukabidhiwa ripoti ya timu iliyochunguza sakata hilo.
Wassira alisema fedha hizo zinalipwa kutokana na uvunjwaji wa haki za binadamu waliofanyiwa wakazi hao kwa kuvunjiwa nyumba zao kinyama.
Timu ya watu wanne ilifanyakazi yake kwa siku 16 na kubaini ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu uliofanywa na watendaji wa Manispaa ya Ilala katika kusimamia zoezi hilo, na kusababisha kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi, Mhandisi na Mwanasheria.
Timu ilibaini kuwa ubomoaji huo haukuzingatia uamuzi wa Baraza la Ardhi ulioisisitiza Halmashauri ya Ilala kuangalia taratibu zilizopo za kuwaondoa wavamizi katika eneo husika.
Aidha, timu hiyo pia iligundua kuwa taratibu za uendeshaji wa Halmashauri hazikuzingatiwa kwa kuwa ilipaswa dhamira ya kubomoa makazi hayo, ilitelewe katika vikao vya menejimenti na baraza la madiwani.
Wassira alisema, timu hiyo ilibaini mambo yaliyojitokeza wakati wa zoezi hilo ambayo ni kunyanyasika na kuteseka kisaikolojia kwa wakazi hao na familia zao na kubainisha kuwa leseni za makazi zilitolewa kimakosa.
Kwa mujibu wa kanuni na sheria kama ilivyoelezwa na Wassira, notisi ya kuondoka katika maeneo hayo ilitakiwa kutolewa siku 30 kabla ya ubomoaji huo kwa vile hilo ni eneo la makazi.
Baraza la ardhi, Februari 27 mwaka huu lilitoa hukumu yenye kueleza kuwa kiwanja namba 52 eneo la viwanda Tabata dampo ni mali ya Kampuni ya Allied Cargo na baada ya siku mbili watendaji wa Manispaa ya Ilala ilibomoa makazi ya watu hao kinyume cha sheria na taratibu.
“Hilo ni kosa, serikali wajibu wetu ni kulinda haki za raia hasa kuishi salama…nataka tuelewane vizuri. Ninachosema hapa ni kwamba tunashughulikia ukiukwaji wa sheria uliofanywa na watendaji wetu.
“Katika hili, kanuni za ubomoaji zimekiukwa na tunachokitoa hapa siyo malipo ya makazi yao, hapana hii ni pole kwa yaliyowakuta. Na mimi kama Waziri wa TAMISEMI, nawashauri kuhamia buyuni kwenye viwanja vya bure.
“We are concerned with human right (tunafuata haki za binadamu) kutokana na makosa ya maofisa wetu wachache, hii watalipwa wenye nyumba tuu,” alisisitiza Wassira.
Alisema, serikali imejifunza kutokana na ukiukwaji huu hivyo imeziagiza mamlaka zote za halmashauri nchini zinazoshughulikia mipango miji kuwawajibisha watendaji wote wanaokiuka sheria, taratibu na kanuni za kuwahamisha wananchi.
Wassira pia, alisema iwapo kuna baadhi ya watendaji wa Manispaa hiyo wanaotuhumiwa kwa ruhwa au uzembe, mamlaka husika ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) itawashighulikia.
TAMKO RASMI LA CUF KUHUSU MAZUNGUMZO YA MUAFAKA
TAMKO LA CHAMA CHA WANANCHI (CUF) KUFUATIA TAMKO LA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM KUHUSIANA NA MAZUNGUMZO YA KUTAFUTA UFUMBUZI WA KUDUMU WA MPASUKO WA KISIASA ZANZIBAR
Tarehe 17 Machi, 2008, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama Cha Wananchi (CUF) lilifanya kikao chake mjini Zanzibar ambapo lilipokea na kuridhia makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Siku hiyo hiyo, CUF iliwatangazia wanachama wake na Watanzania kwa jumla matokeo ya kikao hicho cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Demokrasia, mjini Zanzibar.
Hiyo ilikuwa ni hatua kubwa na muhimu kutekelezwa na upande wa CUF baada ya vyama vyetu viwili kukubaliana kuwa viwasilishe makubaliano hayo kwa vikao vya juu vya maamuzi vya vyama vyetu ili kuyaridhia kabla ya kutiwa saini. Baada ya CUF kutekeleza wajibu wake, yalikuwa matarajio na imani yetu kwamba na upande wa CCM nao ungefanya wajibu wake.
Kwa mshangao na masikitiko makubwa, jana tumepokea Tamko la Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuhusiana na mazungumzo ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar ambalo kimsingi limeyakataa makubaliano yaliyofikiwa na Kamati zetu mbili.
CCM imeamua kufanya usanii wa kisiasa kwa kutumia lugha ya mzunguko, ya ubabaishaji na ya upotoshaji kwa lengo la ama kuendelea kurefusha muda hadi mwaka 2010 au kuyakataa makubaliano ambayo wajumbe wake wameshiriki kuyaandaa katika miezi 14 ya mazungumzo kati ya vyama vyetu viwili.
Hali hiyo iko wazi kwa sababu mbili kuu zifuatazo:
CCM imetamka ‘kuyakubali kimsingi’ mapendekezo yaliyowasilishwa na Kamati ya chama hicho inayoshiriki mazungumzo lakini wakati huo huo inazungumzia marekebisho ambayo inataka yafanywe na hivyo kuiagiza Kamati yake kukutana na wajumbe wa CUF ili kuyajadili marekebisho hayo.
Kwanza, CCM haikutaja ni maeneo gani inataka yafanyiwe marekebisho. Pili, hoja hii inashangaza kwa sababu wajumbe wa Kamati ya Mazungumzo kutoka upande wa CCM walikuwa wakiwaarifu wajumbe wa Kamati kutoka upande wa CUF kwamba wao walikuwa wakiwasilisha taarifa kwa kila hatua inayofikiwa katika vikao vya chama vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa na pia kwa viongozi wao wa juu, Rais Jakaya Kikwete na Mheshimiwa Amani Karume, na kupata maelekezo na miongozo inayohitajika. Hata taarifa ya karibuni kabisa ya CCM iliyokuwa ikikanusha taarifa za vyombo vya habari kwamba Mheshimiwa Amani Karume si kikwazo cha kufikiwa makubaliano ya muafaka iliweka mkazo na msisitizo kwamba katika kila hatua, viongozi hao wameshauriwa ipasavyo. Hatua hii ya mwisho ilikusudiwa kubariki makubaliano hayo yaliyokuwa yakifikiwa hatua kwa hatua na siyo kufungua mjadala mpya kupitia duru mpya ya mazungumzo.
CCM imekuja na hoja mpya kwamba iwapo mapendekezo haya yatakubaliwa, yatakuwa yanaleta mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala katika Zanzibar na hivyo yanapaswa kuridhiwa na wananchi wenyewe kwa njia ya kura ya maoni.
CCM kuleta hoja hii ni kulifanyia mzaha jambo kubwa linalohitaji umakini wa hali ya juu kwani linagusa mustakbali wa taifa letu. Muda wote wa mazungumzo ambayo yamechukua miezi 14 na yakiwa yamehusisha vikao 21, wajumbe wa Kamati ya CCM wanaoshiriki mazungumzo hawakuleta hoja hii ya kura ya maoni. Kinachosikitisha zaidi ni kuwa tofauti na ilivyoelezwa, pendekezo la kutaka kura ya maoni halikuwa limeibuliwa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM bali lilikuwemo katika Taarifa ya Kamati ya CCM inayoshiriki mazungumzo likiwa ni pendekezo walilotaka liridhiwe na Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa. Hivyo, ni wazi liliandaliwa mapema kutokana na kile Kamati hiyo ya CCM ilichokiita “kuipiku CUF katika ubunifu wa kujenga”. Kitendo cha Kamati ya CCM kuwasilisha kitu kipya nje ya makubaliano yaliyofikiwa ni upotoshaji mkubwa wenye lengo la kulifanyia usanii wa kisiasa suala kubwa kama hili linalogusa maslahi ya taifa na watu wake moja kwa moja. Na iwapo pendekezo hilo lina nia njema ya kuwashirikisha wananchi, kwa nini wajumbe wa Kamati ya CCM wasiliwasilishe katika vikao vya mazungumzo na badala yake wakaamua kuliingiza kama mtego wa kisiasa wenye lengo la “kuipiku CUF”?
Hoja nyengine ni kwamba kura ya maoni hiyo itaendeshwa na chombo kipi na kwa utaratibu upi hasa ikitiliwa maanani tayari CCM na CUF wamekubaliana kuwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na Daftari la Kudumu la Wapiga Kura vina matatizo ya msingi ambayo yanahitaji kurekebishwa? Ni vipi basi Tume hiyo chini ya Daftari bovu liliopo itaweza kuendesha kura ya maoni ambayo itakuwa huru na ya haki?
Sisi tunaona suala hilo ni mbinu chafu tu yenye lengo la kuendelea kupoteza muda ili makubaliano yaliyofikiwa yasiweze kutiwa saini na utekelezaji kuanza. Kwa lugha yao CCM waliyoandika katika waraka wao ni njia ya “kuipiku CUF” na kamwe haikusudiwi kupata maoni ya wananchi.
Kwa msingi huo CUF haikubaliani na hoja hizo zote mbili.
Ni lazima tukiri kuwa tumeshtushwa sana na kiwango hiki cha CCM kulifanyia usanii wa kisiasa suala kubwa kama hili. Lakini pia tumepata faraja kuwa Watanzania sasa wameweza kujua ni nani kati ya CCM na CUF asiyeitakia mema nchi hii. Wamejua ni nani kati ya CCM na CUF asiyetaka amani na utulivu katika nchi hii. Wamejua ni nani kati ya CCM na CUF asiyetaka siasa za maelewano na mashirikiano katika nchi hii.
Sasa ni wazi kwamba CCM iliingia katika mazungumzo haya ikiwa haina dhamira ya kweli na ya dhati ya kuupatia ufumbuzi wa kweli mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Inaonekana lengo pekee la CCM katika mazungumzo haya lilikuwa ni kuwahadaa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kwa kujidanganya kwamba wangeweza kuidhibiti kisiasa CUF kupitia utaratibu wa kuwapa matumaini ya uongo (strategic engagement) na kuyarefusha mazungumzo hayo kadiri inavyowezekana hadi kipindi kinachokaribia uchaguzi mkuu ujao pasina kuchukua hatua zozote za maana zenye kulenga kutoa ufumbuzi wa kweli wa mpasuko uliopo. CCM imeonesha wazi wazi kuwa haiitakii mema Tanzania yetu na wala haitaki kuona umoja wa kitaifa na utulivu wa kudumu vinapatikana Zanzibar ambayo ni sehemu moja ya Jamhuri ya Muungano.
Kwa upande mwengine, Watanzania wote na jumuiya ya kimataifa ni mashahidi kuwa CUF imefanya kila liliomo katika uwezo wake kuinusuru hali tete ya kisiasa Zanzibar isichafuke. CUF imechukua kila juhudi kuona mazungumzo haya yanafanikiwa. Imetoa kila ushirikiano unaohitajika kwa CCM na hata kuachia madai yake makuu (kutoa ‘concessions’) ili kuyanusuru mazungumzo hayo na kuyafanikisha.
CUF imeonesha ustahamilivu, ustaarabu na uelewa mkubwa katika mazungumzo haya. Tumeweza kukubaliana na CCM kwa kila hatua tuliyoombwa tuwe na subira ili kupisha mambo kadhaa ya kisiasa yapite. Mara nyengine, hata bila ya kutuomba, sisi wenyewe tumeonyesha uelewa na kuwapa nafasi pale yalipoibuka matukio ya kisiasa ambayo hayakutarajiwa na ambayo tulihisi yanahitaji tuwape muda wenzetu. CCM haionekani kujali au kuthamini juhudi hizo na imeamua kuzipiga teke.
Kama tulivyowahi kusema, hatukufanya hivyo kwa sababu CUF ni dhaifu kisiasa kama ambavyo CCM wangependa kujidanganya. Tulifanya yote hayo kwa sababu tunaongozwa na dhamira njema ya kuhakikisha nchi yetu inabaki katika hali ya amani na utulivu huku tukiamini kwa dhati kwamba mazungumzo ndiyo njia pekee ya kistaarabu ya kumaliza tofauti au migogoro ya kisiasa na kijamii. Lakini ni lazima tusisitize kuwa mazungumzo yenye lengo hilo ni lazima yawe mazungumzo makini yanayoongozwa na utashi wa kweli wa kisiasa uliojengeka juu ya nia njema na kuheshimiana baina ya pande zinazohusika. Hilo limekosekana kwa upande wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Kufuatia misukosuko iliyoyakumba mazungumzo haya mwaka jana, Rais Kikwete, alitoa taarifa kwa umma tarehe 14 Agosti, 2007 akiuomba upande wa CUF ukubali kuendelea na mazungumzo na akiwahakikishia Watanzania kuwa angechukua hatua kuona yanakamilishwa na yanafanikishwa. Wakati akiwahutubia Mabalozi wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa nchini katika sherehe za kuukaribisha mwaka mpya, mapema mwaka huu, Rais Kikwete aliwaeleza kwamba mazungumzo yamefikia ukingoni na kwamba karibu suala la mpasuko wa kisiasa Zanzibar litakuwa historia. Kauli hiyo ilipokewa kwa matumaini makubwa na wananchi ambao wamekuwa wakifuatilia kwa makini kila hatua ya mazungumzo yetu. Ni bahati mbaya kwamba Rais Kikwete ameyaangusha matumaini hayo ya Watanzania kama ambavyo ameyaangusha matumaini yao katika masuala mengine yote aliyowaahidi wakati anaomba kura na anaingia madarakani.
CUF imevunjwa moyo sana na Mheshimiwa Jakaya Kikwete akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM. Imani tuliyokuwa nayo kwake kama kiongozi wa nchi na ambayo tulibaki nayo hadi CCM inaelekea katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa imetetereka sana. Kitendo cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM chini ya Uenyekiti wake kukataa kupitisha makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF na badala yake kuja na hoja mpya za ajabu ajabu zenye lengo la “kuipiku CUF” kisiasa kunamwonyesha Rais Kikwete ama hakuwa mkweli na mwaminifu tokea mwanzoni na kwamba alikuwa akifanya usanii wa kisiasa wakati alipotangaza kuwa anasononeshwa sana na mpasuko wa kisiasa Zanzibar au ni kiongozi dhaifu asiye na udhibiti wa chama anachokiongoza. Yote mawili hayampi sifa za kiongozi ambaye nchi inamhitaji inapopita katika vipindi vigumu.
Kama tulivyofanya mwaka jana, ni vyema tumkumbushe tena Mheshimiwa Jakaya Kikwete kauli yake mwenyewe aliyoitoa wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tarehe 16 Septemba, 2003 wakati anafungua Mkutano wa Kumi na Moja wa Hali ya Siasa Tanzania ambao ulihusu ‘Udhibiti na Utatuzi wa Migogoro’, pale aliposema:
“…[N]aelewa kuwa utaratibu wa kung’amua dalili za migogoro hauwezi kuwa na manufaa kama haukuambatana na vitendo vya haraka. Taarifa za dalili za uendelezaji wa migogoro zinapopatikana zitakuwa hazina manufaa katika uzuiaji wa migogoro hiyo kama zitashughulikiwa kwa njia ya mlolongo wa uamuzi wa kirasimu ambao unaweza kuchelewesha utekelezaji hadi migogoro inapotokea. Kwa hiyo ni wazi kuwa upatikanaji wa taarifa za dalili za migogoro unakuwa wa maana katika uzuiaji wa migogoro kama mara zipatikanapo, zinatafsiriwa kwa vitendo. Mtiririko wa hoja hapa unapaswa kuwa “dalili za mwanzo kujumlisha na vitendo halisi ni sawa sawa na uzuiaji wa migogoro.” Ili haya yatokee unahitaji kuharakisha au kurekebisha utaratibu wa utoaji wa maamuzi ili dalili za mwanzo ziweze kutafsirika kwa vitendo haraka iwezekanavyo.”
Maamuzi ya Chama chake kupitia kikao alichokiongoza yeye mwenyewe akiwa Mwenyekiti wake hayaonyeshi kuwa anayazingatia haya aliyowaasa wenzake mwaka 2003 maana maamuzi ya Halmshauri Kuu ya Taifa yanawakilisha hasa “mlolongo wa maamuzi ya kirasimu” ambayo kama alivyosema hayawezi kuwa msingi wa utatuzi wa mgogoro. Inasikitisha zaidi kwa Rais Kikwete kuwatangazia Watanzania na ulimwengu kuwa amefanikiwa kuwakutanisha Rais Mwai Kibaki na Mheshimiwa Raila Odinga wa Kenya na kufanikisha kufikiwa kwa makubaliano kati ya ODM na PNU nchini humo lakini anashindwa kulifanikisha hilo nchini mwake ndani ya chama anachokiongoza mwenyewe na kati ya CCM na CUF. Rais Kikwete anaona fakhari kuwa Tanzania imeongoza Jeshi la Umoja wa Afrika (AU) katika operesheni ya kijeshi iliyopewa jina la “Operesheni Demokrasia” kisiwani Anjouan, nchini Comoro lakini ameshindwa kuongoza operesheni ya kisiasa ya kusimamisha demokrasia visiwani Zanzibar.
Rais anapaswa ajue kuwa heshima ya ofisi yake na uadilifu wake binafsi ameutia doa kubwa kutokana na kushindwa kusimamia kwa vitendo ahadi yake aliyoitoa kwa Watanzania kupitia hotuba yake ya Desemba 30, 2005 Bungeni na pia ahadi aliyoitoa na kuirejea mara kadhaa kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa katika ziara zake za nje ya nchi kila mara pale alipoulizwa kuhusiana na mgogoro wa muda mrefu wa kisiasa Zanzibar.
MSIMAMO WETU:
Chama Cha Wananchi (CUF) hakiko tayari kushirikiana na CCM kuwafanyia Watanzania usanii wa kisiasa. Huu sio utaratibu wa CUF katika uendeshaji wa siasa. Kwa CUF, siasa si proaganda zilizopitwa na wakati bali ni utumishi wa dhati na uliotukuka kwa umma uliowaamini viongozi wake. Kwa msingi huo, CUF haitakubali kurejea katika mazungumzo kwa utaratibu inaoutaka CCM.
CUF kinakitaka CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya vyama vyetu viwili na endapo kweli Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho “ imeyakubali kimsingi” makubaliano yaliyofikishwa kwake kama ilivyosema taarifa yake, basi kikubali kutia saini makubaliano hayo na utekelezaji wa yaliyokubaliwa uanze mara moja.
Kinyume na hayo, CUF inatoa wito kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti, za uhakika na za haraka kuingilia kati suala hili ili kuhakikisha makubaliano yaliyofikiwa yanatiwa saini. Baada ya Tanzania yenyewe kushindwa katika utatuzi wa mgogoro wake huu wa muda mrefu, sasa ni wakati muafaka kwa Jumuiya ya Kimataifa kuingilia kati kwa kuchagua Mpatanishi wa Kimataifa anayeheshimika kuja kuyasimamia hadi kuyafikisha ukingoni kwa kuhakikisha makubaliano ya dhati yanafikiwa yatakayotoa ufumbuzi wa kweli na wa haki wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
CUF inatoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuepuka fedheha iliyoipata katika nchi nyengine za Kiafrika ambazo iliziachia hadi hali ikachafuka na ndipo ikaingilia kati. Hali ya Zanzibar ni mbaya. Ilitulia kwa sababu ya matumaini ya Wazanzibari na Watanzania kwamba mazungumzo ya CCM na CUF yataleta suluhisho la utulivu na umoja. Makubaliano yaliyofikiwa yanapokosa uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuyakamilisha, yanahitaji kuona jumuiya ya kimataifa inaingilia kati kwa hatua za wazi na madhubuti kuinusuru Zanzibar na Tanzania isitumbukie kule nchi nyengine za Kiafrika zilipotumbukia.
Wakati tunawashukuru kwa dhati viongozi wa vyama vyengine vya siasa, viongozi wa dini, taasisi na jumuiya za kijamii, mabalozi wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania na vyombo vya habari hususan magazeti huru kwa mchango wao mkubwa walioutoa na ambao ulisaidia kuyafikisha mazungumzo hadi hatua ya kukamilishwa, CUF tunatoa wito tena kwao kuendelea kutoa ushirikiano wao na kutimiza wajibu wao kuona mgogoro huu unamalizwa kwa njia za amani na za haki.
CUF inawataka wanachama na wapenzi wake pamoja na Wazanzibari na Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki na siku zote upande wa amani, ukweli na haki utashinda.
Kwa jinsi inavyoyachezea masuala mazito yanayohusu maslahi ya taifa kama ilivyodhihirika kwa mambo yote makubwa yaliyojitokeza hivi karibuni, ni wazi kuwa CCM imepoteza uhalali wa kuongoza nchi na wakati sasa umefika wa Watanzania kuchagua chama makini kitakachoipa Tanzania uongozi makini unaohitajika.
HAKI SAWA KWA WOTE
SEIF SHARIF HAMAD
KATIBU MKUU – CUF
Dar es Salaam
01 Aprili, 2008
Tarehe 17 Machi, 2008, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama Cha Wananchi (CUF) lilifanya kikao chake mjini Zanzibar ambapo lilipokea na kuridhia makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Siku hiyo hiyo, CUF iliwatangazia wanachama wake na Watanzania kwa jumla matokeo ya kikao hicho cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Demokrasia, mjini Zanzibar.
Hiyo ilikuwa ni hatua kubwa na muhimu kutekelezwa na upande wa CUF baada ya vyama vyetu viwili kukubaliana kuwa viwasilishe makubaliano hayo kwa vikao vya juu vya maamuzi vya vyama vyetu ili kuyaridhia kabla ya kutiwa saini. Baada ya CUF kutekeleza wajibu wake, yalikuwa matarajio na imani yetu kwamba na upande wa CCM nao ungefanya wajibu wake.
Kwa mshangao na masikitiko makubwa, jana tumepokea Tamko la Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuhusiana na mazungumzo ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar ambalo kimsingi limeyakataa makubaliano yaliyofikiwa na Kamati zetu mbili.
CCM imeamua kufanya usanii wa kisiasa kwa kutumia lugha ya mzunguko, ya ubabaishaji na ya upotoshaji kwa lengo la ama kuendelea kurefusha muda hadi mwaka 2010 au kuyakataa makubaliano ambayo wajumbe wake wameshiriki kuyaandaa katika miezi 14 ya mazungumzo kati ya vyama vyetu viwili.
Hali hiyo iko wazi kwa sababu mbili kuu zifuatazo:
CCM imetamka ‘kuyakubali kimsingi’ mapendekezo yaliyowasilishwa na Kamati ya chama hicho inayoshiriki mazungumzo lakini wakati huo huo inazungumzia marekebisho ambayo inataka yafanywe na hivyo kuiagiza Kamati yake kukutana na wajumbe wa CUF ili kuyajadili marekebisho hayo.
Kwanza, CCM haikutaja ni maeneo gani inataka yafanyiwe marekebisho. Pili, hoja hii inashangaza kwa sababu wajumbe wa Kamati ya Mazungumzo kutoka upande wa CCM walikuwa wakiwaarifu wajumbe wa Kamati kutoka upande wa CUF kwamba wao walikuwa wakiwasilisha taarifa kwa kila hatua inayofikiwa katika vikao vya chama vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa na pia kwa viongozi wao wa juu, Rais Jakaya Kikwete na Mheshimiwa Amani Karume, na kupata maelekezo na miongozo inayohitajika. Hata taarifa ya karibuni kabisa ya CCM iliyokuwa ikikanusha taarifa za vyombo vya habari kwamba Mheshimiwa Amani Karume si kikwazo cha kufikiwa makubaliano ya muafaka iliweka mkazo na msisitizo kwamba katika kila hatua, viongozi hao wameshauriwa ipasavyo. Hatua hii ya mwisho ilikusudiwa kubariki makubaliano hayo yaliyokuwa yakifikiwa hatua kwa hatua na siyo kufungua mjadala mpya kupitia duru mpya ya mazungumzo.
CCM imekuja na hoja mpya kwamba iwapo mapendekezo haya yatakubaliwa, yatakuwa yanaleta mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala katika Zanzibar na hivyo yanapaswa kuridhiwa na wananchi wenyewe kwa njia ya kura ya maoni.
CCM kuleta hoja hii ni kulifanyia mzaha jambo kubwa linalohitaji umakini wa hali ya juu kwani linagusa mustakbali wa taifa letu. Muda wote wa mazungumzo ambayo yamechukua miezi 14 na yakiwa yamehusisha vikao 21, wajumbe wa Kamati ya CCM wanaoshiriki mazungumzo hawakuleta hoja hii ya kura ya maoni. Kinachosikitisha zaidi ni kuwa tofauti na ilivyoelezwa, pendekezo la kutaka kura ya maoni halikuwa limeibuliwa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM bali lilikuwemo katika Taarifa ya Kamati ya CCM inayoshiriki mazungumzo likiwa ni pendekezo walilotaka liridhiwe na Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa. Hivyo, ni wazi liliandaliwa mapema kutokana na kile Kamati hiyo ya CCM ilichokiita “kuipiku CUF katika ubunifu wa kujenga”. Kitendo cha Kamati ya CCM kuwasilisha kitu kipya nje ya makubaliano yaliyofikiwa ni upotoshaji mkubwa wenye lengo la kulifanyia usanii wa kisiasa suala kubwa kama hili linalogusa maslahi ya taifa na watu wake moja kwa moja. Na iwapo pendekezo hilo lina nia njema ya kuwashirikisha wananchi, kwa nini wajumbe wa Kamati ya CCM wasiliwasilishe katika vikao vya mazungumzo na badala yake wakaamua kuliingiza kama mtego wa kisiasa wenye lengo la “kuipiku CUF”?
Hoja nyengine ni kwamba kura ya maoni hiyo itaendeshwa na chombo kipi na kwa utaratibu upi hasa ikitiliwa maanani tayari CCM na CUF wamekubaliana kuwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na Daftari la Kudumu la Wapiga Kura vina matatizo ya msingi ambayo yanahitaji kurekebishwa? Ni vipi basi Tume hiyo chini ya Daftari bovu liliopo itaweza kuendesha kura ya maoni ambayo itakuwa huru na ya haki?
Sisi tunaona suala hilo ni mbinu chafu tu yenye lengo la kuendelea kupoteza muda ili makubaliano yaliyofikiwa yasiweze kutiwa saini na utekelezaji kuanza. Kwa lugha yao CCM waliyoandika katika waraka wao ni njia ya “kuipiku CUF” na kamwe haikusudiwi kupata maoni ya wananchi.
Kwa msingi huo CUF haikubaliani na hoja hizo zote mbili.
Ni lazima tukiri kuwa tumeshtushwa sana na kiwango hiki cha CCM kulifanyia usanii wa kisiasa suala kubwa kama hili. Lakini pia tumepata faraja kuwa Watanzania sasa wameweza kujua ni nani kati ya CCM na CUF asiyeitakia mema nchi hii. Wamejua ni nani kati ya CCM na CUF asiyetaka amani na utulivu katika nchi hii. Wamejua ni nani kati ya CCM na CUF asiyetaka siasa za maelewano na mashirikiano katika nchi hii.
Sasa ni wazi kwamba CCM iliingia katika mazungumzo haya ikiwa haina dhamira ya kweli na ya dhati ya kuupatia ufumbuzi wa kweli mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Inaonekana lengo pekee la CCM katika mazungumzo haya lilikuwa ni kuwahadaa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kwa kujidanganya kwamba wangeweza kuidhibiti kisiasa CUF kupitia utaratibu wa kuwapa matumaini ya uongo (strategic engagement) na kuyarefusha mazungumzo hayo kadiri inavyowezekana hadi kipindi kinachokaribia uchaguzi mkuu ujao pasina kuchukua hatua zozote za maana zenye kulenga kutoa ufumbuzi wa kweli wa mpasuko uliopo. CCM imeonesha wazi wazi kuwa haiitakii mema Tanzania yetu na wala haitaki kuona umoja wa kitaifa na utulivu wa kudumu vinapatikana Zanzibar ambayo ni sehemu moja ya Jamhuri ya Muungano.
Kwa upande mwengine, Watanzania wote na jumuiya ya kimataifa ni mashahidi kuwa CUF imefanya kila liliomo katika uwezo wake kuinusuru hali tete ya kisiasa Zanzibar isichafuke. CUF imechukua kila juhudi kuona mazungumzo haya yanafanikiwa. Imetoa kila ushirikiano unaohitajika kwa CCM na hata kuachia madai yake makuu (kutoa ‘concessions’) ili kuyanusuru mazungumzo hayo na kuyafanikisha.
CUF imeonesha ustahamilivu, ustaarabu na uelewa mkubwa katika mazungumzo haya. Tumeweza kukubaliana na CCM kwa kila hatua tuliyoombwa tuwe na subira ili kupisha mambo kadhaa ya kisiasa yapite. Mara nyengine, hata bila ya kutuomba, sisi wenyewe tumeonyesha uelewa na kuwapa nafasi pale yalipoibuka matukio ya kisiasa ambayo hayakutarajiwa na ambayo tulihisi yanahitaji tuwape muda wenzetu. CCM haionekani kujali au kuthamini juhudi hizo na imeamua kuzipiga teke.
Kama tulivyowahi kusema, hatukufanya hivyo kwa sababu CUF ni dhaifu kisiasa kama ambavyo CCM wangependa kujidanganya. Tulifanya yote hayo kwa sababu tunaongozwa na dhamira njema ya kuhakikisha nchi yetu inabaki katika hali ya amani na utulivu huku tukiamini kwa dhati kwamba mazungumzo ndiyo njia pekee ya kistaarabu ya kumaliza tofauti au migogoro ya kisiasa na kijamii. Lakini ni lazima tusisitize kuwa mazungumzo yenye lengo hilo ni lazima yawe mazungumzo makini yanayoongozwa na utashi wa kweli wa kisiasa uliojengeka juu ya nia njema na kuheshimiana baina ya pande zinazohusika. Hilo limekosekana kwa upande wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Kufuatia misukosuko iliyoyakumba mazungumzo haya mwaka jana, Rais Kikwete, alitoa taarifa kwa umma tarehe 14 Agosti, 2007 akiuomba upande wa CUF ukubali kuendelea na mazungumzo na akiwahakikishia Watanzania kuwa angechukua hatua kuona yanakamilishwa na yanafanikishwa. Wakati akiwahutubia Mabalozi wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa nchini katika sherehe za kuukaribisha mwaka mpya, mapema mwaka huu, Rais Kikwete aliwaeleza kwamba mazungumzo yamefikia ukingoni na kwamba karibu suala la mpasuko wa kisiasa Zanzibar litakuwa historia. Kauli hiyo ilipokewa kwa matumaini makubwa na wananchi ambao wamekuwa wakifuatilia kwa makini kila hatua ya mazungumzo yetu. Ni bahati mbaya kwamba Rais Kikwete ameyaangusha matumaini hayo ya Watanzania kama ambavyo ameyaangusha matumaini yao katika masuala mengine yote aliyowaahidi wakati anaomba kura na anaingia madarakani.
CUF imevunjwa moyo sana na Mheshimiwa Jakaya Kikwete akiwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM. Imani tuliyokuwa nayo kwake kama kiongozi wa nchi na ambayo tulibaki nayo hadi CCM inaelekea katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa imetetereka sana. Kitendo cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM chini ya Uenyekiti wake kukataa kupitisha makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF na badala yake kuja na hoja mpya za ajabu ajabu zenye lengo la “kuipiku CUF” kisiasa kunamwonyesha Rais Kikwete ama hakuwa mkweli na mwaminifu tokea mwanzoni na kwamba alikuwa akifanya usanii wa kisiasa wakati alipotangaza kuwa anasononeshwa sana na mpasuko wa kisiasa Zanzibar au ni kiongozi dhaifu asiye na udhibiti wa chama anachokiongoza. Yote mawili hayampi sifa za kiongozi ambaye nchi inamhitaji inapopita katika vipindi vigumu.
Kama tulivyofanya mwaka jana, ni vyema tumkumbushe tena Mheshimiwa Jakaya Kikwete kauli yake mwenyewe aliyoitoa wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tarehe 16 Septemba, 2003 wakati anafungua Mkutano wa Kumi na Moja wa Hali ya Siasa Tanzania ambao ulihusu ‘Udhibiti na Utatuzi wa Migogoro’, pale aliposema:
“…[N]aelewa kuwa utaratibu wa kung’amua dalili za migogoro hauwezi kuwa na manufaa kama haukuambatana na vitendo vya haraka. Taarifa za dalili za uendelezaji wa migogoro zinapopatikana zitakuwa hazina manufaa katika uzuiaji wa migogoro hiyo kama zitashughulikiwa kwa njia ya mlolongo wa uamuzi wa kirasimu ambao unaweza kuchelewesha utekelezaji hadi migogoro inapotokea. Kwa hiyo ni wazi kuwa upatikanaji wa taarifa za dalili za migogoro unakuwa wa maana katika uzuiaji wa migogoro kama mara zipatikanapo, zinatafsiriwa kwa vitendo. Mtiririko wa hoja hapa unapaswa kuwa “dalili za mwanzo kujumlisha na vitendo halisi ni sawa sawa na uzuiaji wa migogoro.” Ili haya yatokee unahitaji kuharakisha au kurekebisha utaratibu wa utoaji wa maamuzi ili dalili za mwanzo ziweze kutafsirika kwa vitendo haraka iwezekanavyo.”
Maamuzi ya Chama chake kupitia kikao alichokiongoza yeye mwenyewe akiwa Mwenyekiti wake hayaonyeshi kuwa anayazingatia haya aliyowaasa wenzake mwaka 2003 maana maamuzi ya Halmshauri Kuu ya Taifa yanawakilisha hasa “mlolongo wa maamuzi ya kirasimu” ambayo kama alivyosema hayawezi kuwa msingi wa utatuzi wa mgogoro. Inasikitisha zaidi kwa Rais Kikwete kuwatangazia Watanzania na ulimwengu kuwa amefanikiwa kuwakutanisha Rais Mwai Kibaki na Mheshimiwa Raila Odinga wa Kenya na kufanikisha kufikiwa kwa makubaliano kati ya ODM na PNU nchini humo lakini anashindwa kulifanikisha hilo nchini mwake ndani ya chama anachokiongoza mwenyewe na kati ya CCM na CUF. Rais Kikwete anaona fakhari kuwa Tanzania imeongoza Jeshi la Umoja wa Afrika (AU) katika operesheni ya kijeshi iliyopewa jina la “Operesheni Demokrasia” kisiwani Anjouan, nchini Comoro lakini ameshindwa kuongoza operesheni ya kisiasa ya kusimamisha demokrasia visiwani Zanzibar.
Rais anapaswa ajue kuwa heshima ya ofisi yake na uadilifu wake binafsi ameutia doa kubwa kutokana na kushindwa kusimamia kwa vitendo ahadi yake aliyoitoa kwa Watanzania kupitia hotuba yake ya Desemba 30, 2005 Bungeni na pia ahadi aliyoitoa na kuirejea mara kadhaa kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa katika ziara zake za nje ya nchi kila mara pale alipoulizwa kuhusiana na mgogoro wa muda mrefu wa kisiasa Zanzibar.
MSIMAMO WETU:
Chama Cha Wananchi (CUF) hakiko tayari kushirikiana na CCM kuwafanyia Watanzania usanii wa kisiasa. Huu sio utaratibu wa CUF katika uendeshaji wa siasa. Kwa CUF, siasa si proaganda zilizopitwa na wakati bali ni utumishi wa dhati na uliotukuka kwa umma uliowaamini viongozi wake. Kwa msingi huo, CUF haitakubali kurejea katika mazungumzo kwa utaratibu inaoutaka CCM.
CUF kinakitaka CCM kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na Kamati ya Mazungumzo ya vyama vyetu viwili na endapo kweli Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho “ imeyakubali kimsingi” makubaliano yaliyofikishwa kwake kama ilivyosema taarifa yake, basi kikubali kutia saini makubaliano hayo na utekelezaji wa yaliyokubaliwa uanze mara moja.
Kinyume na hayo, CUF inatoa wito kwa marafiki wa Tanzania na jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti, za uhakika na za haraka kuingilia kati suala hili ili kuhakikisha makubaliano yaliyofikiwa yanatiwa saini. Baada ya Tanzania yenyewe kushindwa katika utatuzi wa mgogoro wake huu wa muda mrefu, sasa ni wakati muafaka kwa Jumuiya ya Kimataifa kuingilia kati kwa kuchagua Mpatanishi wa Kimataifa anayeheshimika kuja kuyasimamia hadi kuyafikisha ukingoni kwa kuhakikisha makubaliano ya dhati yanafikiwa yatakayotoa ufumbuzi wa kweli na wa haki wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
CUF inatoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuepuka fedheha iliyoipata katika nchi nyengine za Kiafrika ambazo iliziachia hadi hali ikachafuka na ndipo ikaingilia kati. Hali ya Zanzibar ni mbaya. Ilitulia kwa sababu ya matumaini ya Wazanzibari na Watanzania kwamba mazungumzo ya CCM na CUF yataleta suluhisho la utulivu na umoja. Makubaliano yaliyofikiwa yanapokosa uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuyakamilisha, yanahitaji kuona jumuiya ya kimataifa inaingilia kati kwa hatua za wazi na madhubuti kuinusuru Zanzibar na Tanzania isitumbukie kule nchi nyengine za Kiafrika zilipotumbukia.
Wakati tunawashukuru kwa dhati viongozi wa vyama vyengine vya siasa, viongozi wa dini, taasisi na jumuiya za kijamii, mabalozi wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania na vyombo vya habari hususan magazeti huru kwa mchango wao mkubwa walioutoa na ambao ulisaidia kuyafikisha mazungumzo hadi hatua ya kukamilishwa, CUF tunatoa wito tena kwao kuendelea kutoa ushirikiano wao na kutimiza wajibu wao kuona mgogoro huu unamalizwa kwa njia za amani na za haki.
CUF inawataka wanachama na wapenzi wake pamoja na Wazanzibari na Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki wakijua kuwa CUF iko upande wa amani, ukweli na haki na siku zote upande wa amani, ukweli na haki utashinda.
Kwa jinsi inavyoyachezea masuala mazito yanayohusu maslahi ya taifa kama ilivyodhihirika kwa mambo yote makubwa yaliyojitokeza hivi karibuni, ni wazi kuwa CCM imepoteza uhalali wa kuongoza nchi na wakati sasa umefika wa Watanzania kuchagua chama makini kitakachoipa Tanzania uongozi makini unaohitajika.
HAKI SAWA KWA WOTE
SEIF SHARIF HAMAD
KATIBU MKUU – CUF
Dar es Salaam
01 Aprili, 2008
BREAKING NEWS: CUF yakataa kura ya maoni
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema kuwa hakitashiriki kuwafanyia wananchi usanii kama ambavyo ilivyopendekezwa na CCM. Katika kikao chake cha NEC hivi karibuni, CCM iliamua kuwa suala la kuundwa kwa serikali ya mseto huko Zanzibar.
Aidha, chama hichio kimesema kuwa imani yake kwa rais Jakaya Kikwete kuhusiana na suala la majadiliano ya kusaka muafaka wa Zanzibar imekwisha. Sasa chama hicho kimeamua kismingi kutoshiriki tena katika mchakato wa harakati hizo zilizoanzishwa na Kikwete na kuitaka jumuiya ya kimtaifa kingilia kati ili kuvinusuru visiwa hivyo kuingia katika machafuko.
Msimamo huo wa CUF umetangazwa hivi punde na katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad. Katika tamko la chama hicho, Hamad amesema kuwa CUF haikubaliani na hoja zilizotolewa na CCM za kutaka kuendeshwa kwa kura ya maoni.
CUF haikubaliani na hoja hiyo kwa sababu: “Sisi tunaona suala hilo ni mbinu chafu tu yenye lengo la kuendelea kupoteza muda ili makubaliano yaliyofikiwa yasiweze kutiwa saini na utekelezaji kuanza.”
CUF inasema kuwa kilichofanywa na CCM ni ghiliba na usanii mkubwa lakini kinafurahi kuwa hatua hiyo ya CCM imesaidia kuwaonyesha wananchi kuwa CCM haina dhamira na kulimaliza suala hilo kubwa.
(more coming later)
Aidha, chama hichio kimesema kuwa imani yake kwa rais Jakaya Kikwete kuhusiana na suala la majadiliano ya kusaka muafaka wa Zanzibar imekwisha. Sasa chama hicho kimeamua kismingi kutoshiriki tena katika mchakato wa harakati hizo zilizoanzishwa na Kikwete na kuitaka jumuiya ya kimtaifa kingilia kati ili kuvinusuru visiwa hivyo kuingia katika machafuko.
Msimamo huo wa CUF umetangazwa hivi punde na katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad. Katika tamko la chama hicho, Hamad amesema kuwa CUF haikubaliani na hoja zilizotolewa na CCM za kutaka kuendeshwa kwa kura ya maoni.
CUF haikubaliani na hoja hiyo kwa sababu: “Sisi tunaona suala hilo ni mbinu chafu tu yenye lengo la kuendelea kupoteza muda ili makubaliano yaliyofikiwa yasiweze kutiwa saini na utekelezaji kuanza.”
CUF inasema kuwa kilichofanywa na CCM ni ghiliba na usanii mkubwa lakini kinafurahi kuwa hatua hiyo ya CCM imesaidia kuwaonyesha wananchi kuwa CCM haina dhamira na kulimaliza suala hilo kubwa.
(more coming later)
Monday, March 31, 2008
Mashaka Yaanza Zanzibar
Kile kilichokuwa kikihofiwa siku zote, sasa kinaweza kutokea. Hali ya mambo kisiwani Zanzibar imeanza kuwa ya wasi wasi kutokana na maamuzi yaliyofikiwa katika kikao cha NEC ya CCM huko Butiama.
Kinachoonekana kikuweka rehani kisiwa hicho ni kukengeuka kwa CCM na kuamua kupindisha kilichokubaliwa katika kamati ya Mazungumzo na kutaka ifanyike kura ya maoni kuhusu kuanzishwa kwa serikali ya Mseto visiwani humo.
Katika kile kinachoashiria kuwa hali ya mambo imeanza kuwa mbaya, wajumbe wa Baraza la wawakilishi wa CUF, waliacha kuendelea na vikao vya baraza na kwenda katika makao makuu ya chama chao ambajko ulifanyika mkutano.
Habari kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa wajumbe hao wametakiwa na wanachama wao kususia vikao vyote vya baraza la wawakilishi.
Aidha, kuna taarifa pia kuwa wanaCUF wamewataka wabunge wao kutohudhuria vikao vya Bunge, linalotarajia kuanza kukutana mjini Dodoma wiki ijayo.
Wajumbe hao wa CUF walitoka Barazani wakiongozwa na Mnadhimu wa kambi ya upinzani, Soud Yussuf Mgeni, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika.
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma na Haki za Binaadamu wa CUF, Salum Bimani alisema kwamba kikao hicho kiliitishwa baada ya viongozi wa chama na wajumbe wa Baraza hilo kupewa ujumbe wa simu kutoka kwa wanachama kuwataka wasusie mara moja vikao vya Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Tayari watu kadhaa wameshaanza kuonyesha wasi wasi wao kutokana na maamuzi yaliyofikiwa na CCM , ambayo yabnaonekana kurudisha nyuma hatua iliyokubaliwa na Kamatio ya Mazungumzo ambayo iliwashirikisha wajumbe kutoka CCM na CUF.
Katika mazungumzo hayop, ilikubaliwa kuwa iundwe serikali ya mseto Zanzibar, ambapo chaka kitakachoshinda uchagzui kitatoa rais na kile kinachofuatia kitatoa waziri Kiongozi.
Lakini suala hili limekuwa likipingwa miaka yote ya wahafidhina walio ndani ya CCM Zanzibat na wamejiapiza kuwa kamwe hawatoiruhusu CUF katika serikali yao.
Biomani alisema kuwa CUF kimepokea maamuzi ya NEC lakini kitatoa maamuzi yake Jumanne kupitia mkutano na waandishi wa habari, ambao utahutubiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad.
Wakati huo huo, uamuzi wa NEC ya CCM kuwa suala hilo liamuriwe kupitia kura ya maobni, limezua mjadala visiwani hapa, huku baadhi ya watu wakipinga wazo hilo.
Katibu wa TADEA, Juma Ali Khatib, alisema suala la kuitisha kura ya maoni juu ya serikali ya pamoja visiwani humu si muafaka kwa sasa kwa sababu muda uliobakia ni mdogo.
Alieleza kwamba Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ilipaswa kulitambua hilo mapema, kwa vile linagusa katiba na sheria za uchaguzi.
Naye Mkurugenzi wa Habari wa NCCR-Mageuzi, Ali Omar, alisema kwamba wakati muafaka umefika kwa Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa ameshindwa kutatua mpasuko wa kisiasa wa Zanzibar.
Alisema kwamba kwa kuzingatia kuwa suala la serikali ya mseto linahusu maslahi ya taifa halikupaswa kurejeshwa kwa wananchi kwa vile hatua hiyo ni sawa na kupoteza muda.
“NCCR-Mageuzi tunavyoona Rais Kikwete ameshindwa kutekeleza ahadi yake ya kumaliza mpasuko wa kisiasa kama alivyoahdi katika Bunge,” alisema kiongozi huyo.
mwisho
Kinachoonekana kikuweka rehani kisiwa hicho ni kukengeuka kwa CCM na kuamua kupindisha kilichokubaliwa katika kamati ya Mazungumzo na kutaka ifanyike kura ya maoni kuhusu kuanzishwa kwa serikali ya Mseto visiwani humo.
Katika kile kinachoashiria kuwa hali ya mambo imeanza kuwa mbaya, wajumbe wa Baraza la wawakilishi wa CUF, waliacha kuendelea na vikao vya baraza na kwenda katika makao makuu ya chama chao ambajko ulifanyika mkutano.
Habari kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa wajumbe hao wametakiwa na wanachama wao kususia vikao vyote vya baraza la wawakilishi.
Aidha, kuna taarifa pia kuwa wanaCUF wamewataka wabunge wao kutohudhuria vikao vya Bunge, linalotarajia kuanza kukutana mjini Dodoma wiki ijayo.
Wajumbe hao wa CUF walitoka Barazani wakiongozwa na Mnadhimu wa kambi ya upinzani, Soud Yussuf Mgeni, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika.
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma na Haki za Binaadamu wa CUF, Salum Bimani alisema kwamba kikao hicho kiliitishwa baada ya viongozi wa chama na wajumbe wa Baraza hilo kupewa ujumbe wa simu kutoka kwa wanachama kuwataka wasusie mara moja vikao vya Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Tayari watu kadhaa wameshaanza kuonyesha wasi wasi wao kutokana na maamuzi yaliyofikiwa na CCM , ambayo yabnaonekana kurudisha nyuma hatua iliyokubaliwa na Kamatio ya Mazungumzo ambayo iliwashirikisha wajumbe kutoka CCM na CUF.
Katika mazungumzo hayop, ilikubaliwa kuwa iundwe serikali ya mseto Zanzibar, ambapo chaka kitakachoshinda uchagzui kitatoa rais na kile kinachofuatia kitatoa waziri Kiongozi.
Lakini suala hili limekuwa likipingwa miaka yote ya wahafidhina walio ndani ya CCM Zanzibat na wamejiapiza kuwa kamwe hawatoiruhusu CUF katika serikali yao.
Biomani alisema kuwa CUF kimepokea maamuzi ya NEC lakini kitatoa maamuzi yake Jumanne kupitia mkutano na waandishi wa habari, ambao utahutubiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad.
Wakati huo huo, uamuzi wa NEC ya CCM kuwa suala hilo liamuriwe kupitia kura ya maobni, limezua mjadala visiwani hapa, huku baadhi ya watu wakipinga wazo hilo.
Katibu wa TADEA, Juma Ali Khatib, alisema suala la kuitisha kura ya maoni juu ya serikali ya pamoja visiwani humu si muafaka kwa sasa kwa sababu muda uliobakia ni mdogo.
Alieleza kwamba Kamati ya Mazungumzo ya CCM na CUF ilipaswa kulitambua hilo mapema, kwa vile linagusa katiba na sheria za uchaguzi.
Naye Mkurugenzi wa Habari wa NCCR-Mageuzi, Ali Omar, alisema kwamba wakati muafaka umefika kwa Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa ameshindwa kutatua mpasuko wa kisiasa wa Zanzibar.
Alisema kwamba kwa kuzingatia kuwa suala la serikali ya mseto linahusu maslahi ya taifa halikupaswa kurejeshwa kwa wananchi kwa vile hatua hiyo ni sawa na kupoteza muda.
“NCCR-Mageuzi tunavyoona Rais Kikwete ameshindwa kutekeleza ahadi yake ya kumaliza mpasuko wa kisiasa kama alivyoahdi katika Bunge,” alisema kiongozi huyo.
mwisho
Wednesday, March 19, 2008
Timu ya Pinda Yakamilisha Kazi
Timu iliyoteuliwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kupitia kwa kina mapendekezo yaliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wa Richmond, imemaliza kazi yake na kukabidhi ripoti.
Pinda amesema kuwa hivi sasa, serikali inaipitia ripoti hiyo kabla ya kutoa maamuzi kutokana na mapendekezo ya Timu hiyo.
Katika ripoti yake, Kamati teule ya Bunge iliyokuwa na wajumbe watano chini ya uenyekiti wa Dk. Harison Mwakyembe, ilipendekeza watumishi kadhaa wa umma, walio katika ngazi za juu serikalini, wachukuliwe hatua kutokana na uzembe uliosababisha taifa kupata hasara kupitia mkatana huow a Richmond.
Mtumishi mmojawapo mkubwa wa umma ambaye kamati hiyo imependekeza awajibishwe ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, John Mwanyika, kutokana na kile kilichoelezwa na kamati kuwa ni kushindwa kwa ofisi anayoiongoza kuishauri vema serikali katika suala hilo.
Pia, pamoja na kushauri hatua zichukuliwe dhidi ya Mkurugenzi wa Takukuru, kamati hiyo inapendekeza pia taasisi hiyo imulikwe baada ya kutoa taarifa iliyoonyesha kuwa kimsingi hakukuwa na tatizo lolote la ufisadi katika mkataba wa Richmond.
Tayari aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wawili, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, walishajiuzulu nyadhfa zao baada ya kuwasilishwa kwa ripoti hiyo Bungeni.
Kukamilika kwa ripoti hiyo kunafanya idadi ya ripoti kuhusiana na sakata la Richmond kufikia tatu baada ya timu nyingine iliyohusisha wanasheria wa Bunge kuipitia mikataba baina ya Tanesco na makamopuni binafsi ya kzualisha umeme, ukiwemo wa Richmond.
Wataalam hao wa washeria walibaini kwua mikataba na makampuni matano baina ya sita ilikuwa inafanana kwa kiasi kikubwa na kuleta wasi wasi wa umahiri wa watu walioandika au kuidhinisha mikataba hiyo.
Pinda amesema kuwa hivi sasa, serikali inaipitia ripoti hiyo kabla ya kutoa maamuzi kutokana na mapendekezo ya Timu hiyo.
Katika ripoti yake, Kamati teule ya Bunge iliyokuwa na wajumbe watano chini ya uenyekiti wa Dk. Harison Mwakyembe, ilipendekeza watumishi kadhaa wa umma, walio katika ngazi za juu serikalini, wachukuliwe hatua kutokana na uzembe uliosababisha taifa kupata hasara kupitia mkatana huow a Richmond.
Mtumishi mmojawapo mkubwa wa umma ambaye kamati hiyo imependekeza awajibishwe ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, John Mwanyika, kutokana na kile kilichoelezwa na kamati kuwa ni kushindwa kwa ofisi anayoiongoza kuishauri vema serikali katika suala hilo.
Pia, pamoja na kushauri hatua zichukuliwe dhidi ya Mkurugenzi wa Takukuru, kamati hiyo inapendekeza pia taasisi hiyo imulikwe baada ya kutoa taarifa iliyoonyesha kuwa kimsingi hakukuwa na tatizo lolote la ufisadi katika mkataba wa Richmond.
Tayari aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wawili, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, walishajiuzulu nyadhfa zao baada ya kuwasilishwa kwa ripoti hiyo Bungeni.
Kukamilika kwa ripoti hiyo kunafanya idadi ya ripoti kuhusiana na sakata la Richmond kufikia tatu baada ya timu nyingine iliyohusisha wanasheria wa Bunge kuipitia mikataba baina ya Tanesco na makamopuni binafsi ya kzualisha umeme, ukiwemo wa Richmond.
Wataalam hao wa washeria walibaini kwua mikataba na makampuni matano baina ya sita ilikuwa inafanana kwa kiasi kikubwa na kuleta wasi wasi wa umahiri wa watu walioandika au kuidhinisha mikataba hiyo.
Friday, March 14, 2008
BOT sasa yaiogopa EPA!
Baada ya moto uliowaka sasa inaonekana kuwa akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) ni moto kweli kweli na Benki Kuu imeonyesha dhamira ya kutaka kujitoe kuendesha akaunti hiyo.
Gavana wa BoT, Benno Ndulu amesema leo kuwa tayari BoT imeshawasiliana na mtaalamu, ambaye ni kampuni moja kutoka nchini kutoka nchini Ufaransa, ili aje kufanya tathmini itakayosaidia kuamua iwapo akaunti hiyo iendelee kubaki BoT au la.
Lakini Ndulu amesema kuwa kimsingi, EPA si sehemu ya shughuli za BoT na ndio maana wanataka kuiondoa akaunti hiyo chini yao.
Gavana Ndulu amesema kuwa kampuni hiyo itatakiwa kukamilisha kazi yake kabla ya katikati ya mwaka huu ili uamuzi wa wapi akaunti hiyo iwekwe ufanywe. Inaonekana kuwa lengo lake ni kuhakikisha kuwa unapoanza mwaka mpya wa fedha mwezi Julai, shughuli za akaunti hiyo zikabidhiwe kwa taasisi inayostahili kuiendesha.
Awali, kabla ya kuhamishiwa BoT, akaunto hiyo ilikuwa ikiendeshwa na NBC.
Baada ya kuhamishiwa BoT, wajanja wachache, kwa kutumia nyaraka za kughushi na ulaghai, walichota kisi cha sh bilioni 133 kutoka katika akaunti hiyo.
Wizi huo ulibainishwa na wanasiasa, hasa wa upinzani walipozungumza bungeni, ingawa viongozi wa serikali walijipanga kukanusha.
Hata hivyo, mbinyo wa wapinzani uliendelea hadi serikali kulazimika kuialika kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu wa Ernst & Young ambayo mwishoni mwa mwaka jana ilithibitisha kuwa kweli wajanja wamejichotea mabilioni kutoka katika akaunti hiyo.
Gavana wa BoT, Benno Ndulu amesema leo kuwa tayari BoT imeshawasiliana na mtaalamu, ambaye ni kampuni moja kutoka nchini kutoka nchini Ufaransa, ili aje kufanya tathmini itakayosaidia kuamua iwapo akaunti hiyo iendelee kubaki BoT au la.
Lakini Ndulu amesema kuwa kimsingi, EPA si sehemu ya shughuli za BoT na ndio maana wanataka kuiondoa akaunti hiyo chini yao.
Gavana Ndulu amesema kuwa kampuni hiyo itatakiwa kukamilisha kazi yake kabla ya katikati ya mwaka huu ili uamuzi wa wapi akaunti hiyo iwekwe ufanywe. Inaonekana kuwa lengo lake ni kuhakikisha kuwa unapoanza mwaka mpya wa fedha mwezi Julai, shughuli za akaunti hiyo zikabidhiwe kwa taasisi inayostahili kuiendesha.
Awali, kabla ya kuhamishiwa BoT, akaunto hiyo ilikuwa ikiendeshwa na NBC.
Baada ya kuhamishiwa BoT, wajanja wachache, kwa kutumia nyaraka za kughushi na ulaghai, walichota kisi cha sh bilioni 133 kutoka katika akaunti hiyo.
Wizi huo ulibainishwa na wanasiasa, hasa wa upinzani walipozungumza bungeni, ingawa viongozi wa serikali walijipanga kukanusha.
Hata hivyo, mbinyo wa wapinzani uliendelea hadi serikali kulazimika kuialika kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu wa Ernst & Young ambayo mwishoni mwa mwaka jana ilithibitisha kuwa kweli wajanja wamejichotea mabilioni kutoka katika akaunti hiyo.
Thursday, March 13, 2008
BREAKING NEWS: Mwekezaji TRL asalimu amri
Mwekezaji katika Kampuni ya Reli nchini (TRL) amesalimu amri na kukubali kutekeleza madai ya watumishi ambao jana walianza mgomo kushinikiza waongezewe mishahara.
Habari zinaeleza kuwa mwekezaji huyo (Shirika la Rites na India na Serikali ya Tanzania) amekubali kuwaongezea mishahara ya kima cha chini wafanyakazi hao kutoka kima wanacholipwa hivi sasa cha sh 86,000 hadi sh 160,000 kwa mwezi.
Aidha, mwekezaji huyo ameahidi kuwa ifikapo Agosti mwaka huu, ataongeza kima hicho cha chini na kufikia sh 200,000. watumishi hao waligoma wakitaka nyongeza ya mishahara wakidai kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakiahidiwa nyongeza hiyo lakini hawajaipata.
Msimamo huo uliomaliza rasmi mgomo, ulifikiwa leo katika kikao baina ya wafanyakazi hao, mwekezaji pamoja na serikali kupitia Wizara ya Miundombinu.
Hali ilianza kuwa mbaya katyika reli hiyo kwani mgomo huo ulisitisha shughuli zote za safari za treni. Moja ya treni ambayo iliondoka juzi dare s Salaam ikielekea mikoa ya Dodoma, tabora, Kigoma na Mwanza, ilikwama ilipofika mjini Dodoma, baada ya watumishi waliokuwa wakiiendesha kugoma kuendelea na safari.
Hali hiyo ilisababisha mtafaruku mkubwa baada ya baadhi ya wabiria kuandamana hadi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambaye alipojadiliana na wafanyakazi hao, alishindwa kuwashawishi waendelee na safari baada ya wenzao wa tabora kueleza kuwa hawapo tayari kuipokea treni hiyo.
Jambo hilo liliwafnay abiria waliokuwa na hasira kuanza kurusha mawe wakiwalenga watumishi wa treni hiyo waliokuwa katika injini na kuwalazimisha askari walioitwa kulinda usalama kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya.
Habari zinaeleza kuwa mwekezaji huyo (Shirika la Rites na India na Serikali ya Tanzania) amekubali kuwaongezea mishahara ya kima cha chini wafanyakazi hao kutoka kima wanacholipwa hivi sasa cha sh 86,000 hadi sh 160,000 kwa mwezi.
Aidha, mwekezaji huyo ameahidi kuwa ifikapo Agosti mwaka huu, ataongeza kima hicho cha chini na kufikia sh 200,000. watumishi hao waligoma wakitaka nyongeza ya mishahara wakidai kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakiahidiwa nyongeza hiyo lakini hawajaipata.
Msimamo huo uliomaliza rasmi mgomo, ulifikiwa leo katika kikao baina ya wafanyakazi hao, mwekezaji pamoja na serikali kupitia Wizara ya Miundombinu.
Hali ilianza kuwa mbaya katyika reli hiyo kwani mgomo huo ulisitisha shughuli zote za safari za treni. Moja ya treni ambayo iliondoka juzi dare s Salaam ikielekea mikoa ya Dodoma, tabora, Kigoma na Mwanza, ilikwama ilipofika mjini Dodoma, baada ya watumishi waliokuwa wakiiendesha kugoma kuendelea na safari.
Hali hiyo ilisababisha mtafaruku mkubwa baada ya baadhi ya wabiria kuandamana hadi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambaye alipojadiliana na wafanyakazi hao, alishindwa kuwashawishi waendelee na safari baada ya wenzao wa tabora kueleza kuwa hawapo tayari kuipokea treni hiyo.
Jambo hilo liliwafnay abiria waliokuwa na hasira kuanza kurusha mawe wakiwalenga watumishi wa treni hiyo waliokuwa katika injini na kuwalazimisha askari walioitwa kulinda usalama kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya.
Monday, March 10, 2008
BREAKING NEWS: TRL kwafukuta
Jitihada za kuwazuia wafanyakazi wa Kampuni ya reli nchini kufanya mgomo zimegonga mwamba. Muda mfupi uliopita, wafanyakazi wa kampuni hiyo ambayo ilikodishwa na serikali mwaka huu, wametoa notisi ya saa 48 kwa mwajiri wao, awaongezee mshahara.
Iwapo mwajiri atashindwa kutekeleza ombi hilo, wafanyakazi hao wamejiandaa kufanya mgomo nchi nzima na madhara ya mgomo huo yanaweza kuhatarisha hali ya uchumi wa nchi na kusababisha mvugano katika jamii.
Hii ni kwa sababu Reli hiyo ndiyo tegemeo la usafiri kwa mikoa mingi ya bara hivyo iwapo itashindwa kufanya kazi kutokana na mgomo huo, kuna uwezekano mkubwa bidhaa nyingi zikakosekana katika mikoa kadhaa.
Sakata la wafanyakazi hao lilianza mara tu baada ya mkodishaji, kampuni ya rites ya India, alipoingia kuanza kazi mwanzoni mwa mwaka huu.
Baada ya kuja kwa mkodishaji huyo anayemiliki sehemu kubwa ya hisa za kampuni hiyo, wafanyakazi walitaka kulipwa mafao yaao ya miaka iliyopita na kuanza mkataba upya na mwajiri huyo.
Lakini madai hayo yalitawaliwa na mizengwe na kabla halijapatiwa ufumbuzi unaoeleweka, wafanyakazi walikuja na dai jingine wakitaka nyonmgeza ya mishahara.
Dai hilo la pili ndilo lililozaa notisi iliyotolewa jana na iwapo haitatekelezwa hadi Jumatano, wafanyakazi hao wamesema kuwa watagoma.
Iwapo mwajiri atashindwa kutekeleza ombi hilo, wafanyakazi hao wamejiandaa kufanya mgomo nchi nzima na madhara ya mgomo huo yanaweza kuhatarisha hali ya uchumi wa nchi na kusababisha mvugano katika jamii.
Hii ni kwa sababu Reli hiyo ndiyo tegemeo la usafiri kwa mikoa mingi ya bara hivyo iwapo itashindwa kufanya kazi kutokana na mgomo huo, kuna uwezekano mkubwa bidhaa nyingi zikakosekana katika mikoa kadhaa.
Sakata la wafanyakazi hao lilianza mara tu baada ya mkodishaji, kampuni ya rites ya India, alipoingia kuanza kazi mwanzoni mwa mwaka huu.
Baada ya kuja kwa mkodishaji huyo anayemiliki sehemu kubwa ya hisa za kampuni hiyo, wafanyakazi walitaka kulipwa mafao yaao ya miaka iliyopita na kuanza mkataba upya na mwajiri huyo.
Lakini madai hayo yalitawaliwa na mizengwe na kabla halijapatiwa ufumbuzi unaoeleweka, wafanyakazi walikuja na dai jingine wakitaka nyonmgeza ya mishahara.
Dai hilo la pili ndilo lililozaa notisi iliyotolewa jana na iwapo haitatekelezwa hadi Jumatano, wafanyakazi hao wamesema kuwa watagoma.
Sunday, March 9, 2008
Mwanyika azusha maswali mapya kashfa ya EPA
Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Kiongozi wa Timu iliyoteuliwa na Rais Kikwete kuchunguza wizi wa mabilioni ya EPA, Johnsom Mwanyika ametoa taarifa ambayo inaibua maswali mengi bila kujibu maswali yaliyoibuliwa awali.
Katika taarifa hiyo, ambayo kimsingi haina kipya, Mwanyika amewataka watanzania na wanahabari kuwa na uvumilivu wakati Timu yake ikiendelea na kazi ya uchunguzi.
Kwa kudhihirisha kuwa hataki kutoa taarifa mpya, Mwanyika amejificha chini ya kivuli cha kuogopa kuharibu wa upelelezi unaoendelea.
Anasema: “Timu inaona ni vyema kutotoa taarifa ambazo zitaathiri kazi ya uchunguzi inayoendelea. Tunapenda kuusihi Umma na Wanahabari kuwa na subira wakati kazi hii inaendelea.”
Aidha, alishindwa kutaja majina ya watuhumiwa ambao tayari wamerejesha sh bil 50 walizoiba. Mwanyika anasema hawezi kuwataja kwa sababu wao ni makampuni na utu wao unatambuliwa kisheria tu.
Taarifa kamili ya Mwanyika hi hii hapa:
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TIMU YA RAIS YA UCHUNGUZI WA FEDHA ZA EPA
TAARIFA KWA UMMA
Kama mnavyofahamu tarehe 08 Januari, 2008 Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete aliunda Timu inayojumuisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili, pamoja na mambo mengine, kuchunguza na kuchukua hatua za kisheria kwa makampuni na watuhumiwa wa upotevu wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Mheshimiwa Rais alituagiza kuwa tuwe tumekamilisha kazi hiyo katika kipindi cha miezi sita.
Taarifa hii ya tatu inatolewa kufafanua na kutoa taarifa ya namna kazi inavyoendelea kama alivyoagiza Mheshimiwa Rais takriban miezi miwili iliyopita.
Timu inapenda kuufahamisha umma kuwa pamoja na majukumu mengi iliyopewa, kwa sasa Timu imejikita katika kufanya uchunguzi wa kitaalam na wa kina. Kwa msingi huo, pamoja na fedha zinazorudishwa, ni vyema Umma na Wanahabari wakafahamu kuwa kazi ya uchunguzi haijafika mwisho na kwa sasa Timu inaona ni vyema kutotoa taarifa ambazo zitaathiri kazi ya uchunguzi inayoendelea. Tunapenda kuusihi Umma na Wanahabari kuwa na subira wakati kazi hii inaendelea.
Hata hivyo, Timu inapenda kuuhakikishia Umma na Vyombo vya Habari kuwa kazi hii ya uchunguzi inaendelea vizuri na Timu inapata ushirikiano mzuri kutoka kwa makampuni na wamiliki wanaohusika na upotevu wa fedha za EPA.
Vilevile tunapenda kuukumbusha Umma na Wanahabari kuwa Timu imepewa miezi sita ya kufanya kazi na hatimaye kuwasilisha Taarifa kwa Mheshimiwa Rais. Huu ni mwezi wa pili tangu Timu ianze kazi yake. Kwa msingi huo, Timu inawasihi Umma na Wanahabari kuwa na subira kwani Wahenga walisema SUBIRA YAVUTA HERI. Tunawahakakishia kuwa kazi inaendelea vizuri na heri yaja kwani tulichonacho hadi sasa katika uchunguzi si haba.
Vilevile Timu inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu maswali na malalamiko ya kutokamatwa kwa waliohusika. Tunapenda kuueleza umma kwamba uchunguzi wetu hadi hivi sasa unaonyesha kwamba wahusika wakuu ni makampuni. Kisheria, makampuni hayo ni mtu yaani ‘Legal Person’. Hata hivyo, makampuni hayo ni tofauti na mtu wa kawaida. Kampuni katika maana hii, inajitegemea yenyewe.
Kwa msingi huo, ikiwa kampuni imefanya kosa, kuna utaratibu wa kufuata kisheria. Kazi inayofanyika hivi sasa, ni uchunguzi wa kina kuhusu maafisa wa makampuni hayo ili kufahamu ni kitu gani kilichosababisha hali hiyo kutokea. Uchunguzi huu unaendelea na ndiyo utakaotuwezesha kujua hatua za kisheria zitakazochukuliwa.
Timu inapenda kuutarifu Umma na Wanahabari kuwa itaendelea kutoa taarifa ambazo inaamini hazitaathiri uchunguzi unaoendelea mara kwa mara.
Imetolewa na Johnson P.M Mwanyika,
Mwenyekiti wa Timu
9 Machi, 2008
Katika taarifa hiyo, ambayo kimsingi haina kipya, Mwanyika amewataka watanzania na wanahabari kuwa na uvumilivu wakati Timu yake ikiendelea na kazi ya uchunguzi.
Kwa kudhihirisha kuwa hataki kutoa taarifa mpya, Mwanyika amejificha chini ya kivuli cha kuogopa kuharibu wa upelelezi unaoendelea.
Anasema: “Timu inaona ni vyema kutotoa taarifa ambazo zitaathiri kazi ya uchunguzi inayoendelea. Tunapenda kuusihi Umma na Wanahabari kuwa na subira wakati kazi hii inaendelea.”
Aidha, alishindwa kutaja majina ya watuhumiwa ambao tayari wamerejesha sh bil 50 walizoiba. Mwanyika anasema hawezi kuwataja kwa sababu wao ni makampuni na utu wao unatambuliwa kisheria tu.
Taarifa kamili ya Mwanyika hi hii hapa:
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TIMU YA RAIS YA UCHUNGUZI WA FEDHA ZA EPA
TAARIFA KWA UMMA
Kama mnavyofahamu tarehe 08 Januari, 2008 Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete aliunda Timu inayojumuisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili, pamoja na mambo mengine, kuchunguza na kuchukua hatua za kisheria kwa makampuni na watuhumiwa wa upotevu wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Mheshimiwa Rais alituagiza kuwa tuwe tumekamilisha kazi hiyo katika kipindi cha miezi sita.
Taarifa hii ya tatu inatolewa kufafanua na kutoa taarifa ya namna kazi inavyoendelea kama alivyoagiza Mheshimiwa Rais takriban miezi miwili iliyopita.
Timu inapenda kuufahamisha umma kuwa pamoja na majukumu mengi iliyopewa, kwa sasa Timu imejikita katika kufanya uchunguzi wa kitaalam na wa kina. Kwa msingi huo, pamoja na fedha zinazorudishwa, ni vyema Umma na Wanahabari wakafahamu kuwa kazi ya uchunguzi haijafika mwisho na kwa sasa Timu inaona ni vyema kutotoa taarifa ambazo zitaathiri kazi ya uchunguzi inayoendelea. Tunapenda kuusihi Umma na Wanahabari kuwa na subira wakati kazi hii inaendelea.
Hata hivyo, Timu inapenda kuuhakikishia Umma na Vyombo vya Habari kuwa kazi hii ya uchunguzi inaendelea vizuri na Timu inapata ushirikiano mzuri kutoka kwa makampuni na wamiliki wanaohusika na upotevu wa fedha za EPA.
Vilevile tunapenda kuukumbusha Umma na Wanahabari kuwa Timu imepewa miezi sita ya kufanya kazi na hatimaye kuwasilisha Taarifa kwa Mheshimiwa Rais. Huu ni mwezi wa pili tangu Timu ianze kazi yake. Kwa msingi huo, Timu inawasihi Umma na Wanahabari kuwa na subira kwani Wahenga walisema SUBIRA YAVUTA HERI. Tunawahakakishia kuwa kazi inaendelea vizuri na heri yaja kwani tulichonacho hadi sasa katika uchunguzi si haba.
Vilevile Timu inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu maswali na malalamiko ya kutokamatwa kwa waliohusika. Tunapenda kuueleza umma kwamba uchunguzi wetu hadi hivi sasa unaonyesha kwamba wahusika wakuu ni makampuni. Kisheria, makampuni hayo ni mtu yaani ‘Legal Person’. Hata hivyo, makampuni hayo ni tofauti na mtu wa kawaida. Kampuni katika maana hii, inajitegemea yenyewe.
Kwa msingi huo, ikiwa kampuni imefanya kosa, kuna utaratibu wa kufuata kisheria. Kazi inayofanyika hivi sasa, ni uchunguzi wa kina kuhusu maafisa wa makampuni hayo ili kufahamu ni kitu gani kilichosababisha hali hiyo kutokea. Uchunguzi huu unaendelea na ndiyo utakaotuwezesha kujua hatua za kisheria zitakazochukuliwa.
Timu inapenda kuutarifu Umma na Wanahabari kuwa itaendelea kutoa taarifa ambazo inaamini hazitaathiri uchunguzi unaoendelea mara kwa mara.
Imetolewa na Johnson P.M Mwanyika,
Mwenyekiti wa Timu
9 Machi, 2008
Tuesday, March 4, 2008
Butiama Kuitikisa CCM
HALI ya kisiasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) si shwari na taarifa za hivi karibuni zinaonyesha kuwa, makundi ya kisiasa ndani ya chama hicho yameshaanza kujipanga kwa ajili ya kushtakiana ndani ya vikao vikubwa viwili vitakavyoitishwa baadaye mwezi huu.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kwamba, wajumbe wanaounda makundi hayo ambayo yamechipua kutokana na Kashfa ya Richmond wameshaanza kufanya mashauriano ya namna ya kukabiliana wakati wa vikao vya Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.
Maandalizi ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kinatarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu huko Butiama ambako ndiko nyumbani na mahali alikozikwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya makundi hayo mawili, moja likiwa ni lile lililofanikisha kuanguka kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na jingine linalojaribu kumsafisha yeye na wenzake wengine kadhaa tayari yanaonyesha mwelekeo wa kujipanga, tayari kukabiliana na mwenendo huo wa mambo.
Mmoja wa makada maarufu wa chama hicho anayetoka katika kundi linaloshangilia kuanguka kwa Lowassa, Nazir Karamagi na kusakamwa kwa mfanyabiashara Rostam Aziz anasemakuwa tayari walikuwa wameshajipanga kwa ajili ya kukamilisha kazi hiyo.
Mwana CCM huyo ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho, alisema tayari wameshaanza kufuatilia kile walichokiita nyendo za Lowassa na wana CCM wenzake wengine wanaomuunga mkono ili kuweza kupata msingi imara wa kujenga hoja zao dhidi ya kundi hilo.
Kada huyo machachari wa CCM alisema miongoni mwa hadidu za rejea ambazo watazitumia kummaliza Lowassa, Rostam, Karamagi na wanasiasa wenzao wa kundi hilo ni kauli walizozitoa nje ya Bunge dhidi ya ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.
Kwa mujibu wa kada huyo, watu kadhaa wenye msimamo kama wake tayari wameshaanza kukusanya vielelezo na kujenga hoja ambazo wanaamini wakizitumia zitasaidia kuzima jitihada zozote zinazoonekana kuanza za Lowassa na wana CCM wenzake kujisafisha.
Mbali ya Lowassa, kundi hilo linataka pia chama hicho kitoe karipio kali dhidi ya Rostam na Karamagi kutokana na kile wanachokieleza kuwa ni kukitia doa chama na serikali kwa sababu tu ya kuweka kwao mbele maslahi ya kibiashara kuliko ya umma.
Habari zaidi kutoka ndani ya kundi hilo la kwanza zinaeleza kwamba, iwapo mkakati wao huo utakwama ndani ya chama, basi hatua itakayofuata itakuwa ni kuupeleka bungeni ambako wataitumia Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuwachukulia hatua Lowassa na wenzake kadhaa wanaodaiwa kutoa kauli ambazo zinaonyesha dharau kwa Bunge.
Wakati kundi hilo la kwanza likijipanga kwa ajili ya kupigilia msumari wa mwisho katika kile wanachokiona kuwa ni ‘jeneza la kisiasa’ la akina Lowassa, Rostam na Karamagi upande wa pili nao unaonekana kujipanga kwa ajili ya kulikabili kundi hilo la kwanza.
Habari zinaonyesha kuwa, nalo limeanza kukusanya vielelezo kadhaa ambavyo wanataka kuvitumia kwa lengo la kukishawishi chama chao kuwa Kashfa ya Richmond ilikuwa na lengo la kuwadhalilisha, kuwaumiza na kuwamaliza kisiasa.
“We will definitely hit back (Ni wazi kwamba tutajibu mapigo). Hatuwezi tukakaa kimya wakati tukijua waziwazi kwamba watu hawa wameazimia kutuumiza kwa malengo ya kisiasa.
“Hii si haki hata kidogo, mtu unazushiwa uongo wa wazi halafu watu wanakuwa washangiliaji. Ni jambo baya kwamba taasisi za kisheria zimefanya ‘mob justice’ (zinachukua sheria mikononi).
“Hili hatuwezi kukubali liendelee. You wait and see,” alisema mmoja wa wanasiasa hao waliotajwa katika sakata la Richmond ambalo lilisababisha Lowassa ajiuzulu uwaziri mkuu huku Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha wakijiuzulu nyadhifa zao za uwaziri.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kwamba, wajumbe wanaounda makundi hayo ambayo yamechipua kutokana na Kashfa ya Richmond wameshaanza kufanya mashauriano ya namna ya kukabiliana wakati wa vikao vya Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.
Maandalizi ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kinatarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu huko Butiama ambako ndiko nyumbani na mahali alikozikwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya makundi hayo mawili, moja likiwa ni lile lililofanikisha kuanguka kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na jingine linalojaribu kumsafisha yeye na wenzake wengine kadhaa tayari yanaonyesha mwelekeo wa kujipanga, tayari kukabiliana na mwenendo huo wa mambo.
Mmoja wa makada maarufu wa chama hicho anayetoka katika kundi linaloshangilia kuanguka kwa Lowassa, Nazir Karamagi na kusakamwa kwa mfanyabiashara Rostam Aziz anasemakuwa tayari walikuwa wameshajipanga kwa ajili ya kukamilisha kazi hiyo.
Mwana CCM huyo ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho, alisema tayari wameshaanza kufuatilia kile walichokiita nyendo za Lowassa na wana CCM wenzake wengine wanaomuunga mkono ili kuweza kupata msingi imara wa kujenga hoja zao dhidi ya kundi hilo.
Kada huyo machachari wa CCM alisema miongoni mwa hadidu za rejea ambazo watazitumia kummaliza Lowassa, Rostam, Karamagi na wanasiasa wenzao wa kundi hilo ni kauli walizozitoa nje ya Bunge dhidi ya ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.
Kwa mujibu wa kada huyo, watu kadhaa wenye msimamo kama wake tayari wameshaanza kukusanya vielelezo na kujenga hoja ambazo wanaamini wakizitumia zitasaidia kuzima jitihada zozote zinazoonekana kuanza za Lowassa na wana CCM wenzake kujisafisha.
Mbali ya Lowassa, kundi hilo linataka pia chama hicho kitoe karipio kali dhidi ya Rostam na Karamagi kutokana na kile wanachokieleza kuwa ni kukitia doa chama na serikali kwa sababu tu ya kuweka kwao mbele maslahi ya kibiashara kuliko ya umma.
Habari zaidi kutoka ndani ya kundi hilo la kwanza zinaeleza kwamba, iwapo mkakati wao huo utakwama ndani ya chama, basi hatua itakayofuata itakuwa ni kuupeleka bungeni ambako wataitumia Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuwachukulia hatua Lowassa na wenzake kadhaa wanaodaiwa kutoa kauli ambazo zinaonyesha dharau kwa Bunge.
Wakati kundi hilo la kwanza likijipanga kwa ajili ya kupigilia msumari wa mwisho katika kile wanachokiona kuwa ni ‘jeneza la kisiasa’ la akina Lowassa, Rostam na Karamagi upande wa pili nao unaonekana kujipanga kwa ajili ya kulikabili kundi hilo la kwanza.
Habari zinaonyesha kuwa, nalo limeanza kukusanya vielelezo kadhaa ambavyo wanataka kuvitumia kwa lengo la kukishawishi chama chao kuwa Kashfa ya Richmond ilikuwa na lengo la kuwadhalilisha, kuwaumiza na kuwamaliza kisiasa.
“We will definitely hit back (Ni wazi kwamba tutajibu mapigo). Hatuwezi tukakaa kimya wakati tukijua waziwazi kwamba watu hawa wameazimia kutuumiza kwa malengo ya kisiasa.
“Hii si haki hata kidogo, mtu unazushiwa uongo wa wazi halafu watu wanakuwa washangiliaji. Ni jambo baya kwamba taasisi za kisheria zimefanya ‘mob justice’ (zinachukua sheria mikononi).
“Hili hatuwezi kukubali liendelee. You wait and see,” alisema mmoja wa wanasiasa hao waliotajwa katika sakata la Richmond ambalo lilisababisha Lowassa ajiuzulu uwaziri mkuu huku Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha wakijiuzulu nyadhifa zao za uwaziri.
Monday, March 3, 2008
BREAKING NEWS: JENGO LA USHIRIKA LAUNGUA
Sehemu ya jengo maarufu la ushirika, zilimo ofisi mbalimbali imeungua kwa moto usiku wa kuamkia leo. Habari zinapasha kuwa ingawa haijathibitishwa na mamlaka husika, chanzo cha moto huo kinaweza kuwa umeme.
Mashuhuda wanapasha kuwa usiku umeme ulikatika katika jengo hilo na uliporejea baadaye, waliona cheche za moto kana kwamba kuna mtu alikuwa anachomelea vyuma . baada ya muda kidogo waliona moshi mzito ukifuka sehemu hiyo na moto mkubwa kuzuka.
Takriban ofisi 15 zimeungua na mojawapo ni ofisi ya Prince bagenda, ambaye alikuwa katika harakati za kuanzisha gazeti jipya lililotarajiwa kuwa mitaani kwa mara ya kwanza Ijumaa ijayo (bado haijaelezwa kuwa mipango ya kulitoa Ijumaa imefuitwa).
Akizungumza eneo la tukio, Bagenda alisema kuwa vitu vilivyokuwa katika ofisi yake vina thamani ya zaidi y ash milioni 250. vuti hivyo vinajumuisha na kompyuta na vifaa vingine vinavyohusiana na uandaaji wa gazeti.
Aidha, alisema kuwa ndani ya ofisi hiyo ndimo ilimokuwa inaendeshwa mipango ya kuanzisha TV na radio.
Wamiliki wa ofisi zilizoungua wamesema kuwa watatoa taarifa hapo baadaye.
Waziri wa Mambo ya ndani, Lawarence Masha, alifika eneo la tukio leo asubuhi lakini hakutaka kuzungumza chochote bkwa maelezo kuwa hajapatiwa taarifa za kutosha kuhusiana na ajali hiyo.
Mashuhuda wanapasha kuwa usiku umeme ulikatika katika jengo hilo na uliporejea baadaye, waliona cheche za moto kana kwamba kuna mtu alikuwa anachomelea vyuma . baada ya muda kidogo waliona moshi mzito ukifuka sehemu hiyo na moto mkubwa kuzuka.
Takriban ofisi 15 zimeungua na mojawapo ni ofisi ya Prince bagenda, ambaye alikuwa katika harakati za kuanzisha gazeti jipya lililotarajiwa kuwa mitaani kwa mara ya kwanza Ijumaa ijayo (bado haijaelezwa kuwa mipango ya kulitoa Ijumaa imefuitwa).
Akizungumza eneo la tukio, Bagenda alisema kuwa vitu vilivyokuwa katika ofisi yake vina thamani ya zaidi y ash milioni 250. vuti hivyo vinajumuisha na kompyuta na vifaa vingine vinavyohusiana na uandaaji wa gazeti.
Aidha, alisema kuwa ndani ya ofisi hiyo ndimo ilimokuwa inaendeshwa mipango ya kuanzisha TV na radio.
Wamiliki wa ofisi zilizoungua wamesema kuwa watatoa taarifa hapo baadaye.
Waziri wa Mambo ya ndani, Lawarence Masha, alifika eneo la tukio leo asubuhi lakini hakutaka kuzungumza chochote bkwa maelezo kuwa hajapatiwa taarifa za kutosha kuhusiana na ajali hiyo.
Thursday, February 14, 2008
JESHI KATIKA KASHFA
Hospitali ya Jeshi la Lugalo Jijini Dar es Salaam imeingia katika kashfa ya kuwageuza watanzania kuwa nguruwe wa majaribio kwa kuruhusu kufanyika kwa utafiti kwa kutumia dawa iliyopigwa marufuku.
Kashfa hiyo imebainishwa Bunbgeni jana kufuatia swali lililoulizwa na Mbunge machachari wa Karatu, Dk. Wilnrod Slaa na Naibu waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda kukiri kutokea kwa jambo hilo.
Dk. Aisha Kigoda alisema kuwa licha ya taasisi ya serikali, Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupiga marufuku kufanyika kwa utafiti huo, Jeshi, huku likionyesha kiburi, liliiruhusu kampuni moja ya Afrika Kusini, sit u kuleta dawa hizo ziitwazo virodene PO 58 kuzifanyia utafiti kwa kuwatumia watanzania, bali pia kampuni hioyo ilianza kuziuza dawa hizo kiholela mitaani.
Taarifa zilizotolewa na Dk. Slaa akilinukuu gazeti la Washington Post la Marekani, zinaonyesha kuwa watanzania 64 wamefanyiwa majaribio ya dawa hiyo ya ukimwi iliyotengenezwa Afrika Kusini lakini meshapigwa marufuku nchini humo.
Dk. Slaa aliitaka serikali kueleza ni chombo gani cha sheria kilitoa kibali cha watanzania kufanyiwa majaribio ya dawa ambayo imeshapigwa marufuku.
Dk. Slaa alisema kuwa pamoja na Hospitali ya Lugalo, kuna taarifa kuwa majaribio hayo yalifanywa pia katika zahanati binafsi inayomilikiwa na Mkuu wa Jshi la Polisi mstaafu ambaye hakumtaja jina.
Kwa kawaifda, vyombo vya serikali vinavyohusika na utoaji wa vibali vya utafiti wa kisayansi ni Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) pamoja na COSTECH.
Hata hivyo, hakuna hata moja ya taasisi nilizozitaja iliyowahi kutoa kibali kwa ajili ya utafiti huo na kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kuwa ombi la kibali cha kufanya utafiti liliwasilishwa NIMR Julai 2000.
Baada ya NIMR kufanya tathimini ya utafiti huo, ililikataa ombi hilo kwa kuwa andiko kuhusu utafiti wa dawa hiyo lilikuwa na upungufu mkubwa kisayansi na kimaadili.
Lakini katika hali ya kushangaza, hata baada ya kukataliwa kwa ombi la kufanya utafiti, wanasayansi hao waliingiza dawa bila kibali cha serikali na kuanza kufanya utafiti katika hospitali ya Lugalo.
Alipopewa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, Dk. Slaa alimtaka Naibu waziri huyo kueleza hatua zilizochukuliwa kwa watanzania ambao walishirikiana na watafiti hao kutoka nje kufanya uhalifu huo.
Dk. Slaa alisema anazo taarifa kuwa ombi la utafiti lilipokataliwa na NIMR, viongozi wa Jeshi walisema wazi wazi kuwa Wizara ya asfya haihusiki kutoa vibali vya utafiti.
Dk. Kigoda hakulijibu swali hilo ipasavyo kwani hakueleza viongozi wa jeshi walioshiriki kuwaleta watafiti hao walichukuliwa hatua gani.
Badala yake, alilieleza Bunge kuwa Wizara ilikaa na Jeshi la kukubaliana kuwa utafiti huo usiendelee na kuwa iwapo wanataka utafiti huo unedelee basi wafuate sheria na taratibu zilizopo.
Kashfa hiyo imebainishwa Bunbgeni jana kufuatia swali lililoulizwa na Mbunge machachari wa Karatu, Dk. Wilnrod Slaa na Naibu waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda kukiri kutokea kwa jambo hilo.
Dk. Aisha Kigoda alisema kuwa licha ya taasisi ya serikali, Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupiga marufuku kufanyika kwa utafiti huo, Jeshi, huku likionyesha kiburi, liliiruhusu kampuni moja ya Afrika Kusini, sit u kuleta dawa hizo ziitwazo virodene PO 58 kuzifanyia utafiti kwa kuwatumia watanzania, bali pia kampuni hioyo ilianza kuziuza dawa hizo kiholela mitaani.
Taarifa zilizotolewa na Dk. Slaa akilinukuu gazeti la Washington Post la Marekani, zinaonyesha kuwa watanzania 64 wamefanyiwa majaribio ya dawa hiyo ya ukimwi iliyotengenezwa Afrika Kusini lakini meshapigwa marufuku nchini humo.
Dk. Slaa aliitaka serikali kueleza ni chombo gani cha sheria kilitoa kibali cha watanzania kufanyiwa majaribio ya dawa ambayo imeshapigwa marufuku.
Dk. Slaa alisema kuwa pamoja na Hospitali ya Lugalo, kuna taarifa kuwa majaribio hayo yalifanywa pia katika zahanati binafsi inayomilikiwa na Mkuu wa Jshi la Polisi mstaafu ambaye hakumtaja jina.
Kwa kawaifda, vyombo vya serikali vinavyohusika na utoaji wa vibali vya utafiti wa kisayansi ni Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) pamoja na COSTECH.
Hata hivyo, hakuna hata moja ya taasisi nilizozitaja iliyowahi kutoa kibali kwa ajili ya utafiti huo na kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kuwa ombi la kibali cha kufanya utafiti liliwasilishwa NIMR Julai 2000.
Baada ya NIMR kufanya tathimini ya utafiti huo, ililikataa ombi hilo kwa kuwa andiko kuhusu utafiti wa dawa hiyo lilikuwa na upungufu mkubwa kisayansi na kimaadili.
Lakini katika hali ya kushangaza, hata baada ya kukataliwa kwa ombi la kufanya utafiti, wanasayansi hao waliingiza dawa bila kibali cha serikali na kuanza kufanya utafiti katika hospitali ya Lugalo.
Alipopewa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, Dk. Slaa alimtaka Naibu waziri huyo kueleza hatua zilizochukuliwa kwa watanzania ambao walishirikiana na watafiti hao kutoka nje kufanya uhalifu huo.
Dk. Slaa alisema anazo taarifa kuwa ombi la utafiti lilipokataliwa na NIMR, viongozi wa Jeshi walisema wazi wazi kuwa Wizara ya asfya haihusiki kutoa vibali vya utafiti.
Dk. Kigoda hakulijibu swali hilo ipasavyo kwani hakueleza viongozi wa jeshi walioshiriki kuwaleta watafiti hao walichukuliwa hatua gani.
Badala yake, alilieleza Bunge kuwa Wizara ilikaa na Jeshi la kukubaliana kuwa utafiti huo usiendelee na kuwa iwapo wanataka utafiti huo unedelee basi wafuate sheria na taratibu zilizopo.
Thursday, February 7, 2008
BREAKING NEWS: Lowassa Aomba Kujiuzulu
Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ameandika barua kjwa Rais Jakaya Kikwete akiomba kujiuzulu wadhifa huo.
Lowassa alitangaza hayo Bungeni leo wakati alipotakiwa kuchangia ripoti ya Kamati nTeule ya Bunge kuhusu kampuni ya Richmond.
Lowassa amesema kuwa ameamua kujiuzulu ili kuonyesha uwajibikaji ingawa hakubaliani na jinsi kamati hiyo ilivyomhukumu bila kumhoji.
Alisema kuwa baada ya kuisoma taarifa ya kamati hiyo amebaini kuwa kinachotakiwa ni Uwaziri Mkuu, hivyo kwa manufaa ya serikali, chama chake na nchi, ameamua kuuachia wadhifa huo.
Huku akiongea kwa masikitiko makubwa, Lowassa alisema kuwa imemshangaza kuwa wakati ripoti hiyo inamtuhumu yeye, hakuhojiwa wakati yeye alikuwa tayari kutoa maelezo yake. Alisema ahata aliponong'onezwa suala hilo na Spika, samwel Sitta, alimletea ushahidi wa maandishi.
Habari kutoka Ikulu zinaeleza kuwa tayari barua hiyo imeshapokelewa na maamuzi yatakapofanywa yatatangazwa.
Mwandishi wa Habari wa rais, Premmy Kibanga aliiambia tovuti hii kuwa suala hilo litatangazwa hadharani ingawa hakusema lini maamuzi hayo yatafanywa na kutangazwa
Lowassa alitangaza hayo Bungeni leo wakati alipotakiwa kuchangia ripoti ya Kamati nTeule ya Bunge kuhusu kampuni ya Richmond.
Lowassa amesema kuwa ameamua kujiuzulu ili kuonyesha uwajibikaji ingawa hakubaliani na jinsi kamati hiyo ilivyomhukumu bila kumhoji.
Alisema kuwa baada ya kuisoma taarifa ya kamati hiyo amebaini kuwa kinachotakiwa ni Uwaziri Mkuu, hivyo kwa manufaa ya serikali, chama chake na nchi, ameamua kuuachia wadhifa huo.
Huku akiongea kwa masikitiko makubwa, Lowassa alisema kuwa imemshangaza kuwa wakati ripoti hiyo inamtuhumu yeye, hakuhojiwa wakati yeye alikuwa tayari kutoa maelezo yake. Alisema ahata aliponong'onezwa suala hilo na Spika, samwel Sitta, alimletea ushahidi wa maandishi.
Habari kutoka Ikulu zinaeleza kuwa tayari barua hiyo imeshapokelewa na maamuzi yatakapofanywa yatatangazwa.
Mwandishi wa Habari wa rais, Premmy Kibanga aliiambia tovuti hii kuwa suala hilo litatangazwa hadharani ingawa hakusema lini maamuzi hayo yatafanywa na kutangazwa
Wednesday, February 6, 2008
BREAKING NEWS: Lowassa ananuka Richmond
Kamati teule ya Bunge, iliyopewa kazi ya kuangalia mkataba wa uzalishaji umeme wa dharura kati ya kampuni ya Richmond Development ya Marekani na serikali, imemkuta waziri Mkuu, Edward Lowassa, akiwa mchafu kimaadili na kumshauri kujiuzulu.
Kwa maneno yake, kamati hiyo inahitimisha: “Kamati teule haikufurahishwa hata kidogo na taarifa zinazomgusa moja kwa mowa moja Mhe waziri Mkuu katika kuipendelea Richmond Development Company LLC. Hata hivyo, Kamati teule imetimiza wajibu wake kwa uwazi na ukweli kama ilivyoagizwa na Bunge letu tukufu.
“Kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi aliyonayo Mhe. Waziri Mkuu katika uendeshaji wa shughuli za serikali na uongozi wan chi kwa ujumla, ni wajibu wake yeye mwenyewe kupima uzito wa matokeo ya uchunguzi huu na wajibu wake kikatiba ndani na nje ya Bunge.
“Vile vile ni wajibu wa Bunge ambalo linathibitisha uteuzi wake kwa mujibu wa Ibara ya 51 inayothibitisha uteuzi wake, kuangalia ikiwa matokeo ya uchunguzi huu hayajaathiri hadhi na uzito wake ndani ya Bunge.”
Kwa maneno mengine, Kamati hiyo iliyokuwa inaongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe (Kyela-CCM) ilikuwa inamtaka waziri Mkuu kujiuzulu kutokana na kuhusika kwake na kashfa hiyo.
Aidha, iwapo Lowassa angeshindwa kuchukua uamuzi wa kumwajibisha kwa kumpigia kura ya kutokwua na imani naye.
Kwa ujumla, Kamati hiyo imebaini kuwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha, na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wanahusishwa moja kwa moja na kuipatia kampuni hiyo kazi ya kuzalisha umeme wa dharura wakati ikiwa haina sifa.
Aidha, wengine wanaotajwa katika ripoti hiyo na kushauri wawajibishwe kutokana na ushiriki wao katika sakata hilo ni waziri wa sasa wa Nishati na Madini, nazir Karamagi, katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Ather Mwakapugi pamoja na Kamishna wa Madini, Bashir Mrindoko.
Wengine ni Mwanassheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye kwa mujibuw a ripoti hiyo ameonekana kutojua alichokuwa anakifanya wakati baadhi ya viongozi wakiwa wanatekjeleza njama za kupindisha sheria na taratibu ili kuhakikisha kuwa Richmond inapatiwa kazi hiyo.
Uchunguzi wa Kamati pia ulibaini kuhusika kwa aliyekuwa waziri katika serikali ya awamu ya tatu, Daniel Yona, jinsi ambavyio naye alishiriki katika kuhakikisha kuwa Richmond inapata kazi hiyo.
Inaelezwa katika ripoti hiyo kuwa Dk. Msabaha aliamua kukiuka maagizo ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na mchakato wa kuipata kampuni itakayozalisha umeme wa dharura, na kuilazimisha Tanesco kupindisha taratibu na kuikumbatia Richmond ingawa ilidhihirika wazi kuwa haikuwa na sifa ya kupata kazi hiyo.
Hata hivyo, Msabaha anakaririwa na ripoti hiyo akisema kuwa katika suala hilo, yeye amefanywa kuwa kondoo wa kafara tu.
Mtiririko wa ripoti hiyo unaonyesha kuwepo kwa maelekezo na maagizo kutoka kwa Lowassa, kwenda kwa Dk. Msabaha kuhakikisha kuwa Richmond inapatiwa kazi hiyo kwa njia yoyote ile.
Pia ripoti hiyo imeonyesha jinsi Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Nchini (Takukuru), kwa jinsi ambavyo ilitumia mamlaka yake kuficha ukweli wa mambo na kuisafisha Richmond pamoja na viongozi wasio waadilifu walioileta kampuni hiyo.
Kwa msingi huo, Kamati hiyo imependekeza kuwa uongozi wa Takukuru ufanyiwe mabadiliko makubwa ili kulinda hadhi ya taasisi hiyo muhimu katika mapamvbano dhidi ya rushwa.
Kwa maneno yake, kamati hiyo inahitimisha: “Kamati teule haikufurahishwa hata kidogo na taarifa zinazomgusa moja kwa mowa moja Mhe waziri Mkuu katika kuipendelea Richmond Development Company LLC. Hata hivyo, Kamati teule imetimiza wajibu wake kwa uwazi na ukweli kama ilivyoagizwa na Bunge letu tukufu.
“Kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi aliyonayo Mhe. Waziri Mkuu katika uendeshaji wa shughuli za serikali na uongozi wan chi kwa ujumla, ni wajibu wake yeye mwenyewe kupima uzito wa matokeo ya uchunguzi huu na wajibu wake kikatiba ndani na nje ya Bunge.
“Vile vile ni wajibu wa Bunge ambalo linathibitisha uteuzi wake kwa mujibu wa Ibara ya 51 inayothibitisha uteuzi wake, kuangalia ikiwa matokeo ya uchunguzi huu hayajaathiri hadhi na uzito wake ndani ya Bunge.”
Kwa maneno mengine, Kamati hiyo iliyokuwa inaongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe (Kyela-CCM) ilikuwa inamtaka waziri Mkuu kujiuzulu kutokana na kuhusika kwake na kashfa hiyo.
Aidha, iwapo Lowassa angeshindwa kuchukua uamuzi wa kumwajibisha kwa kumpigia kura ya kutokwua na imani naye.
Kwa ujumla, Kamati hiyo imebaini kuwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha, na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wanahusishwa moja kwa moja na kuipatia kampuni hiyo kazi ya kuzalisha umeme wa dharura wakati ikiwa haina sifa.
Aidha, wengine wanaotajwa katika ripoti hiyo na kushauri wawajibishwe kutokana na ushiriki wao katika sakata hilo ni waziri wa sasa wa Nishati na Madini, nazir Karamagi, katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Ather Mwakapugi pamoja na Kamishna wa Madini, Bashir Mrindoko.
Wengine ni Mwanassheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye kwa mujibuw a ripoti hiyo ameonekana kutojua alichokuwa anakifanya wakati baadhi ya viongozi wakiwa wanatekjeleza njama za kupindisha sheria na taratibu ili kuhakikisha kuwa Richmond inapatiwa kazi hiyo.
Uchunguzi wa Kamati pia ulibaini kuhusika kwa aliyekuwa waziri katika serikali ya awamu ya tatu, Daniel Yona, jinsi ambavyio naye alishiriki katika kuhakikisha kuwa Richmond inapata kazi hiyo.
Inaelezwa katika ripoti hiyo kuwa Dk. Msabaha aliamua kukiuka maagizo ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na mchakato wa kuipata kampuni itakayozalisha umeme wa dharura, na kuilazimisha Tanesco kupindisha taratibu na kuikumbatia Richmond ingawa ilidhihirika wazi kuwa haikuwa na sifa ya kupata kazi hiyo.
Hata hivyo, Msabaha anakaririwa na ripoti hiyo akisema kuwa katika suala hilo, yeye amefanywa kuwa kondoo wa kafara tu.
Mtiririko wa ripoti hiyo unaonyesha kuwepo kwa maelekezo na maagizo kutoka kwa Lowassa, kwenda kwa Dk. Msabaha kuhakikisha kuwa Richmond inapatiwa kazi hiyo kwa njia yoyote ile.
Pia ripoti hiyo imeonyesha jinsi Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Nchini (Takukuru), kwa jinsi ambavyo ilitumia mamlaka yake kuficha ukweli wa mambo na kuisafisha Richmond pamoja na viongozi wasio waadilifu walioileta kampuni hiyo.
Kwa msingi huo, Kamati hiyo imependekeza kuwa uongozi wa Takukuru ufanyiwe mabadiliko makubwa ili kulinda hadhi ya taasisi hiyo muhimu katika mapamvbano dhidi ya rushwa.
Friday, February 1, 2008
Masuala Nyeti Yapigwa Danadana Bungeni
KIU ya watanzania kufahamu hatma ya hoja nyeti zinazosubiri maamuzi ya Bunge itabidi kusubiri kwa wiki moja zaidi.
Hii ni kutokana na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kutangaza kuwa masuala hayo nyeti, hayatajadiliwa Bungeni wiki hii hadi atakaporejea kutoka Marekani.
Spika Sitta alitangaza kuwa atakuwa na ziara ya wiki moja nchini Marekani alikoalikwa na Baraza la Wawakilishi na kutoa maelekezo kuwa katika muda ambao hatokuwepo, masuala nyeti yaliyo Bungeni yatapaswa kusubiri.
Alisema kuwa anatarajia kuondoka Jumatatu na kurejea Alhamisi hivyo Naibu Spika, Anne Makinda, atakaimu nafasi yake lakini kati ya majukumu yake hayatahusisha kushughulikia masuala hayo nyeti.
Sitta aliyataja masuala hayo kuwa ni pamoja na suala la ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoangalia mchakato wakuipata kampuni ya Richmond Development (RDC) ya Marekani, iliyopewa kandarasi ya kuzalisha umeme za dharura wakati taifa lilipokabiliwa na upungufu wa nishati hiyo mwaka juzi.
Pia aliitaja hoja nyingine nzito kuwa ni lile linalohusiana na sakata la kashfa ya akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) ya Benki Kuu (BoT).
“Sikutaka Naibu Spika akurupuke na kuvamia masuala haya nyeti, itabidi yasubiri mpaka pale nitakaporejea… tunayo wiki nzima ya kuyaangalia haya,” alisema.
Hata hivyo, dalili za kupigwa danadana kwa suala la EPA zilianza kuonekana mapema Bungeni jana wakati wa kipindi cha maswali na majibu, pale ambapo masuali kuhusiana na suala hilo yalipozuiliwa na Spika, kwa maelezo kuwa suala hilo bado linajadiliwa.
Wakati fulani, Spika alizima swali la nyongeza lililoulizwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed (Wawi-CUF), ambaye baada ya Naibu Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo kubainisha kuwa suala la EPA linafanyiwa kazi kutokana na maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
Aliposimama kuuliza swali la nyongeza, Hamad Rashid alikumbusha kwua kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, taasisi hiyo ambayo ni moja ya mihimili ya utawala, haizuiliwi kujadili suala ambalo linachunguzwa na taasisi nyingine, ukiacha masuala ambayo yapo mahakamani.
Lakini Spika badala ya kumwita Mkulo kujibu suala hilo, alisimama na kutoa maelezo kuwa alishatoa maelezo awali kuwa majadiliano kuhusu suala hilo yanaendelea na atalitaarifu Bunge hatma ya majadiliano hayo.
Baada ya jitihada za Hamad Rashid kugonga mwamba, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema) alisimama kwa lengo la kuuliza swali la nyongeza, na kwa kudhani kuwa anakusudiakuuliza swali kuhusiana na suala hilo, Spika alimzuia akisema kuwa maelezo aliyoyatoa yameizima hoja hiyo kuendelea kuhojiwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa mapema wiki hii, Spika aliliambia Bunge kuwa ndani ya wiki huii angetoa taarifa kuhusiana na matokeo ya mashauriano kati ya ofisi yake na serikali kuhusiana na suala la kuwasilishwa Bungeni kwa ripoti kamili iliyoandaliwa na kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu ya Ernst & Young kuhusiana na EPA.
Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili nje ya Bunge baada ya kipindi cha maswali na najibu, Zitto alisema kuwa lengo lake la kusimama halikuwa kuulizia masuala ya EPA.
“Inaonekana mzimu wa EPA umevawaa serikalini, kila kitu wao wanaona kama EPA… mimi sikutaka kuulizia kuhusu EPA, hoja yangu ilikuwa ni kuwa Naibu Waziri hakujibu swali lililoulizwa.
“Swali liliuliza kuhusu Debt Conversion Scheme, hizi ni fedha ilizoliwa na wafanyabishara waliouziwa madeni, hilo ndilo lililoulizwa lakini waziri alikwepa kulijibu hilo,” alisema Zitto.
Hii ni kutokana na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kutangaza kuwa masuala hayo nyeti, hayatajadiliwa Bungeni wiki hii hadi atakaporejea kutoka Marekani.
Spika Sitta alitangaza kuwa atakuwa na ziara ya wiki moja nchini Marekani alikoalikwa na Baraza la Wawakilishi na kutoa maelekezo kuwa katika muda ambao hatokuwepo, masuala nyeti yaliyo Bungeni yatapaswa kusubiri.
Alisema kuwa anatarajia kuondoka Jumatatu na kurejea Alhamisi hivyo Naibu Spika, Anne Makinda, atakaimu nafasi yake lakini kati ya majukumu yake hayatahusisha kushughulikia masuala hayo nyeti.
Sitta aliyataja masuala hayo kuwa ni pamoja na suala la ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoangalia mchakato wakuipata kampuni ya Richmond Development (RDC) ya Marekani, iliyopewa kandarasi ya kuzalisha umeme za dharura wakati taifa lilipokabiliwa na upungufu wa nishati hiyo mwaka juzi.
Pia aliitaja hoja nyingine nzito kuwa ni lile linalohusiana na sakata la kashfa ya akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) ya Benki Kuu (BoT).
“Sikutaka Naibu Spika akurupuke na kuvamia masuala haya nyeti, itabidi yasubiri mpaka pale nitakaporejea… tunayo wiki nzima ya kuyaangalia haya,” alisema.
Hata hivyo, dalili za kupigwa danadana kwa suala la EPA zilianza kuonekana mapema Bungeni jana wakati wa kipindi cha maswali na majibu, pale ambapo masuali kuhusiana na suala hilo yalipozuiliwa na Spika, kwa maelezo kuwa suala hilo bado linajadiliwa.
Wakati fulani, Spika alizima swali la nyongeza lililoulizwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed (Wawi-CUF), ambaye baada ya Naibu Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo kubainisha kuwa suala la EPA linafanyiwa kazi kutokana na maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
Aliposimama kuuliza swali la nyongeza, Hamad Rashid alikumbusha kwua kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, taasisi hiyo ambayo ni moja ya mihimili ya utawala, haizuiliwi kujadili suala ambalo linachunguzwa na taasisi nyingine, ukiacha masuala ambayo yapo mahakamani.
Lakini Spika badala ya kumwita Mkulo kujibu suala hilo, alisimama na kutoa maelezo kuwa alishatoa maelezo awali kuwa majadiliano kuhusu suala hilo yanaendelea na atalitaarifu Bunge hatma ya majadiliano hayo.
Baada ya jitihada za Hamad Rashid kugonga mwamba, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema) alisimama kwa lengo la kuuliza swali la nyongeza, na kwa kudhani kuwa anakusudiakuuliza swali kuhusiana na suala hilo, Spika alimzuia akisema kuwa maelezo aliyoyatoa yameizima hoja hiyo kuendelea kuhojiwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa mapema wiki hii, Spika aliliambia Bunge kuwa ndani ya wiki huii angetoa taarifa kuhusiana na matokeo ya mashauriano kati ya ofisi yake na serikali kuhusiana na suala la kuwasilishwa Bungeni kwa ripoti kamili iliyoandaliwa na kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu ya Ernst & Young kuhusiana na EPA.
Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili nje ya Bunge baada ya kipindi cha maswali na najibu, Zitto alisema kuwa lengo lake la kusimama halikuwa kuulizia masuala ya EPA.
“Inaonekana mzimu wa EPA umevawaa serikalini, kila kitu wao wanaona kama EPA… mimi sikutaka kuulizia kuhusu EPA, hoja yangu ilikuwa ni kuwa Naibu Waziri hakujibu swali lililoulizwa.
“Swali liliuliza kuhusu Debt Conversion Scheme, hizi ni fedha ilizoliwa na wafanyabishara waliouziwa madeni, hilo ndilo lililoulizwa lakini waziri alikwepa kulijibu hilo,” alisema Zitto.
Subscribe to:
Posts (Atom)