Saturday, December 13, 2008

Generali Mboma ajitosa ubunge Mbeya Vijijini

Mkuu Meshi ya ulinzi mstaafu Generali Robert Mboma amechukua fomu kuomba kugombea ubunge wa jimbo la Mbeya vijini huku akikanusha kuwa ametumwa na rais Kikwete kuwnia nafasi hiyo.

Anasema kugombea ubunge ni haki yake na kugombea nafasi hiyo yamekuwa ni maamuzi yake binafsi, hivyo isihesabiwe kuwa ameingia baada ya kushawishiwa na mtu yeyote.

Alisema anagombea nafasi hiyo si kwa ajili ya kutafuta utajiri, bali kuwasaidia wananchi wenzake wa mkoa wa Mbeya kuleta maendeleo.

Alisema kipaumbele chake kitakuwa ni kutatua kero za muda mrefu zinzowakabili wananvhi wa jimbo hilo kama vile ukosefu wa maji na huduma nyingine za jamii.

"Hakuna masilahi yoyote ambayo yamenishawishi kugombea nafasi hii kwani baada ya kustaafu nilipata kiiinua mgongo changu ambacho kinanitosheleza katika kuendesha maisha yangu hivyo nia yangu ni kuwakilisha mawazo, fikra na kero za wananchi ili kuweza kusukuma gurudumu la maendeleo katika jimbo langu la Mbeya vijijini," alisema.

Hadi Ijumaa jioni, jumla ya wanachama tisa walikuwa wameshachukua fomu hizo. Hao ni Mchungaji Luckson Mwanjali, Michael Mponzi,Jjovita Diyami, Flora Mwalyambi, Alaan Mwaigaga, Petro Mwashusa, Maria Mwambanga na Andrew Sayila .

Tuesday, December 9, 2008

Waziri Chibulunje apata ajali

naibu Waziri wa Miundombinu, Ezekia Chibulunje amepata ajali leo mkoani Singida baada ya gari lake kupinduka mara tatu baada ya tairi kupasuka. Walioshuhudia ajali hiyo wanasema Chibulunje, ambaye alipata mshituko wa moyo na majeraha madogo madogo, aliokolewa na mifuko ya hewa (airbags).
Ajakli imetokea eneo la Misugha, yapata kilometa 45 kutoka Singida mjini. Alikuwa ndio kwanza amewasili mkoani humo wka ajili ya ziara ya siku nne ya kukagua barabara akitokea mkoani Manyara. Kwenye gari lake alikuwamo na dereva na Meneja wa tanroads mkoa wa Singida ambao nao wamepata majeraha madogo na kutibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani

Friday, December 5, 2008

Serikali yatangaza mapambano na Mengi

Kauli iliyotolewa na Reginald Mengi siku mbili zilizopita imezua malumbano makali baina yake na serikali ambayo yasipoangaliwa yanaweza kuzusha migogoro isiyo na maana.
katika kile kinachoonekana kujitu tuhuma za Mengi kuwa anatishiwa na 'Wziri kijana' anayeongoza 'wizara nyeti'. Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, leo amempa Mengi siku saba kuthibitisha madai yake kuwa anatishiwa.
Waziri Masha amesema iwapo Mengi atashindwa kuthibitisha hivyo baada ya siku sana "sheria itachukua mkondo wake."
Kwa kauli hiyo, ni dhahiri kuwa serikali inaweza kumfungulia Mengi mashitaka ingawa hadi sasa ni vigumu kutabiri yatakuwa mashitaka gani hasa.
Aidha, masha alisema kuwa ameliagiza Jeshi la Polisi kuchunguza vitisha alivyopatiwa Mengi. Amemtaka mfanyabishara huyo anayemiliki vyombo vingi vya habari kuziwasilisha meseji za vitisho anazodai kutumiwa.
Siku mbili zilizopita, Mengi aliwaeleza waandishi wa habari kuwa kuna waziri alikuwa amekula njama, akitaka yeye (Mengi) amambikiziwe kodi kubwa, ili akishindwa kuilipa afilisiwe kama ilivyotokea kwa tajiri mmoja huko Urusi.
Aidha, mengi aliwaonyesha waandishi wa habari baadhi ya meseji za vitisho alivzotumiwa

Wednesday, December 3, 2008

Abiria ATCL wanusurika

Zaidi ya abiria 50 waliokuwa ndani ya ndege ya Air Tanzania Company Limited iliyokuwa inaelekea kuruka katika uwanja wa Mwanza, wamenusurika baada ya rubani kufanikiwa kuisimamisha ndege hiyo kutokana na moja ya tairi kuanza kuwaka moto.
Moto huo uligunduliwa na mmoja wa abiria aliyekuwa amekaa siti za nyuma ambaye alianza kupiga kelele zilizowashitua abiria wenzake ambao nao walianza kupiga kelele kabla ta rubani kushituka na kuisimamisha ndege hiyo iliyokuwa inashika kasi ili ipae.
Mara moja askari wa zimamoto walifika na kufanmikiwa kuuzima moto huo na kuwashusha abiria wote ambaow alipelekwa kwenye vyumba vya kusubiria uwanjani hapo.
Mmoja wa abiria ameeleza kuwa tanguw awekwe hapo, hakuna ofisa yeyote wa ATCL aliyekwenda kuwaleza chochote zaidi ya kufahamishwa tu kwua safari yao imefutwa kwa leo.
Abiria huyo alisema kuwa ingawa waliripoti uwanjani hapo saa 4 asubuhi kulingana na ratiba ya wali, safari yao ilisogezwa mbele na walipanda kwenye ndege saa 8.
Mkrugenzi wa ATCL, David Mataka, alipotafutwa alisema kuwa ndio kwanza alikuwa amepata taarifa hizo na kuomba apataiwe muda ili akusanye taarifa zaidi. Alitaka apigiwe simu kama baada ya dakika 40.
Ndege iliyopata ajali hiyo ni aina ya dash 8 ambayo ina uawezo wa kubeba abiria wapata 56 na ni moja ya ndege zilizokodiwa na shirika hilo katika harakati zake za kujiimarisha kibiashara

Tuesday, December 2, 2008

NEWS UPDATE: Mramba, Yona nje

Mawaziri wa Zamani, Basil Mramba na Daniel Yona, leo wameachiwa kwa dhamana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kusota gerezani kwa muda wa wiki moja.
Vigogo hao walipata dhamana baada ya kukata rufaa Mahakama Kuu kupinga masharti magumu waliyowekewa na Mahakama ya Kisutu na jaji Njengafibili Mwaikugile alilegeza masharti hayo. Mahakama ya Kisutu iliwataka watuhumiwa hao kutoa dhamana ya fedha taslimu kiasi cha sh bil 3.9 kila mmoja.
Mahakama kuu ilibadili sharti hilo na kupunguza kiwango cha fedha hadi sh bil 2.9 na kuwaruhusu kuweka hati za mali zenye thamani kama hiyo.
Lakini Mahakama Kuu iliachia masharti mengine kama yalivyo. Nayo ni kuwasilisha pasi zao za kusafiria, kutotoka nje ya dar es Salaam bila idhini ya Mahakama na kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika.
Mramba aliwasilisha hat tatu ambazo zilikuwa na thamani ya zaidi ya sh bil 3 zenye majina tofauti, hyuku moja tu ikiwa na jina lake. Yona aliwasilisha hati tatu za thamani ya zaidi ya sh bil 3 zote zikiwa na majina yake.
Katika serikali ya awamu ya Tatu, Mramba alikuwa waziri wa fedha na Yona waziri wa Nishati na Madini. Wanatuhumiwa kutumia madaraka yao vibaya wakiwa mawaziri kwa kuingia mkataba ya kampuni ya ukaguzi wa dhahabu ya Alez Sterwat kinyume na sheria ya manunuzi na kuisababishia serikali hasara ya sh bil 11.7

Monday, December 1, 2008

Mramba na Yona warejeshwa rumande

Habari kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zinasema kuwa Basil Mramba na Daniel Yona, ambao walikuwa na matarajio ya kupata dhamana leo, wamerejeshwa tena Keko.
Mawaziri hao wa zamani, wanaokabiliwa na mashitaka 13 ya kutumia madaraka yao vibaya, walifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kuomba dhamana baada ya Mahakama Kuu kutengua masharti ya awali wiki iliyopita.
Walipofikishwa Mahakamani Kisutu leo, Hakimu anayeisikiliza kesi hiyo, alikataa kuendelea nayo kwa maelezo kuwa alikuwa hajaipanga kusikilizwa leo. Pia, hakimu huyo Hezron Mwankenja, alisema kuwa yeye hakuandika removal order kulitaka jeshi la Magereza liwalete watuhumiwa hao mahakamani leo.
Baada ya kufanya hivyo, aliipangia kesi hiyo kusikilizwa kesho, hivyo kuwalazimua Mramba na Yona kurejea keko hadi hiyo kesho.
Awali, hakimu huyo alipanga dhamana iliyoelezwa kuwa na nasharti magumu, akimtaka kila mtuhumiwa kuweka mahakamani hapo kiasi cha Sk bil 3.9, kuwa na wadhamini wawili, kusalimisha hati zao za kusafiria na kutotoka nje ya dar bila idhini ya mahakama.
mahakama Kuu ilitengua sharti la kwanza na kuwataka watuhumiwa aidha kutoa kiasi cha Sh bil 2.9 au kuwasilisha hati ya mali yenye thamani hiyo.

Saturday, November 29, 2008

JK apangua Makatibu Wakuu

RAIS Kikwete, amefanya mabadiliko ya makatibu wakuu na naibu katibu wakuu wa wizara 13 na Gray Mgonja wa fedha amekwenda likizo ya kustaafu.

Makatibu kadhaa na manaibu wamehamishwa na wengine wapya wameteuliwa baada ya wengine kustaafu.

Mabadiliko hayo yamegusa wizara kadhaa ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Ulinzi, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki na nyingine tisa.

Kikwete amewateua wasaidizi wake wawili wa Ikulu kuwa naibu makatibu wakuu wa wizara.

Alhaj Ramadhan Kijja anakuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Uchumi, Dk Florens Turuka Katibu Mkuu wa Habari Utamaduni na Michezo, Joyce Mapunjo anakuwa Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara na Andrew Nyumayo anakuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Kabla ya uteuzi Kijja alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Uchumi, Dk Turuka alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Joyce Mapunjo alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Miundo Mbinu na Andrew Nyumayo alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu.

Makatibu wakuu waliohamishwa Wizara ya ni pamoja na Paniel Lyimo aliyekuwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Masoko sasa anakwenda Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Ladislaus Komba amehamishiwa Maliasili na Utalii, Kijakazi Mtengwa amepekewa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana na Mohamed Muya amehamishiwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.

Awali Dk Ladislaus Komba alikuwa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Kijakazi Mtengwa alikuwa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo ambapo Mohamed Muya alikuwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Makatibu wakuu wengine waliohamishwa ni Patrick Rutabanzibwa amepangiwa Wizara ya Mambo ya Ndani kutoka Maji na Umwagiliaji, Dk Sergomena Tax - Afrika Mashariki akitokea Viwanda, Biashara na Masoko, Wilson Mukama anakwenda Maji na Umwagiliaji kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, pamoja na Blandina Nyoni anayekwenda Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii akitokea Maliasili na Utalii.

Naibu makatibu wakuu wapya walioteuliwa ni pamoja na Dk. Philip Mpango- Fedha na Uchumi, Celestine Gesimba - Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Seti Kamuhanda - mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Dk Mpango alikuwa msaidizi wa rais (Uchumi) Ikulu, Seti Kamuhanda pia alikuwa msaidizi wa rais (Hotuba) Ikulu na Gesimba alikuwa Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.

Fanuel Mbonde aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Thursday, November 27, 2008

NEWS ALERT: Hatma ya akina Mramba kesho

Hatma ya basil Mramba na mwenzake Daniel Yona kuhusiana na dhamana yao, itajulikana kesho baada ya leo Mahakama Kuu kulikubali ombi lao la kukata rufaa dhidi ya masharti magumu ya dhamana waliyowekewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wanafunzi waigomea serikali

Wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma vilivyofungwa, wamegoma kuyakubali masharti yaliyotolewa na serikali. Serikali iliagiza uongozi wa vyuo vikuu vya umma nchini, kuwabagua wanafunzi kati ya wale wanaokubaliana na mfumo wa uchangiaji wa elimu ya juu na wale wasiokubaliana nao.

Baada ya hapo, wanafunzi hao walitakiwa kuandika barua ya kueleza kukubaliana kwao na mfumo huo na kujaza fomu maalum, ambayo itakuwa kama mkataba baina yao na uongozi wa vyuo kuhusiana na makubaliano hayo.

Akizungumza leo, rais wa serikali ya Wanafunzi wa UDSM, Anthony Machibya, alisema kuwa uongozi wa UDSM ulishawapatia masharti hayo na wao wameyakataa.

Akizungumza kwa niaba ya marais wenzake saba kutoka vyuo sana vya umma vilivyofungwa kutokana na migomo ya wanafunzi, Machibya alisema kuwa hakuna atakayeandika barua wala kujaza fimu kama sharti la kumtaka arejee chuoni.

Alisisitiza kuwa wanafunzi watarejea chuoni iwapo tu serikali itaondoa mfumo wa uchangiaji wa elimu ya juu uliopo.

Alisisitiza kuwa iwapo serikali haitotekeleza madai yao, hawatarejea vyuoni na iwapo watarejea, wataendelea na migomo hadi sera hiyo ya uchangiaji iondolewe.

Lakini, mgawanyiko baina ya wanafunzi hao kwani wale wanaounda umoja wa viongozi wa vyuo vya umma, (Tahliso) wenyewe wameonekana kupingana na wenzao.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Tahliso, Nicholaus Mtindya, alisema kuwa umoja wao haukubaliani na mgomo uliofanywa na wanafunzi hivi karibuni.

Alisema kuwa hawakubaliani na mgomo huo kwa sababu Tahliso tayari ilishaongea na serikali na wakaipatia miezi miwili ili iyashughulikie madai yao.

Anasema kuwa miezi miwili haijapita kwa sababu kikao hicho kilifanyika Oktoba 23 na inashangaza kwa nini wanafunzi waligoma kabla ya kumalizika kwa muda huo.

Aidha, anasema kuwa mgomo uliofanywa na wanafunzi hivi karibuni ulishinikizwa na baadhi ya watu kwa maslahi yao binafsi. Hakufafanmua.

Wednesday, November 26, 2008

Waziri awatembelea akina Mramba gerezani

Waziri wa mambo ya Ndani, Lawrence Masha, jana alifanya ziara ya ghafla katika gereza la Keko ambako mawaziri waandamizi wawili wa zamani wamehifadhiwa baada ya kukosa dhamana katika kesi yao ya kutumia vibaya madaraka yao inayowakabili.
mawaziri hao wa zamani, basili Mramba na Daniel Yona walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana, wakikabiliwa na jumla ya mashitaka 13 ya kutumia vibaya madaraka yao, kuhusiana na mkataba wa kampuni ya Alex Steward Asseyers, iliyoingia mkataba wa kufanya ukaguzi wa biashara ya dhahabu.
Masha alifika gerezani hapo kinyemela kwani alikuwa anatumia gari binafsi, akiwa amevaa mavazi ambayo yanaweza kuhesabiwa kuwa si rasmi kwa kazi kwa mtu mwenye hadhi yake.
Maofisa wa Magereza hiyo walikataa kuzungumzia suala hilo lakini Masha mwenyewe amethibitisha kwua kweli alikwenda katika gereza hilo.
Alipoulizwa ziara yake hiyo ilikuwa na lengo gani, Masha alisema ilikuwa ni ziara ya kikazi, ingawa alipotakiwa kueleza kwa nini anafanya ziara ya kikazi akitumia gari binafsi, alishindwa kufanya hivyo.
Wakati huo huo, Mawakili wa Yona na Mramba walirejea mahakamani hapo wakiwa na barua ya kuomba kupatia mwenendo wa kesi hiyo ili wakate urfaa Mahakama Kuu kupinga masharti magumu ya dhamana waliyowekwa wateja wao.
hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Hezron Mwankenja, amewaamuru makarani kuiabndaa nyaraka hiyo haraka ili mawakili hao watimize dhamira yao.

Tuesday, November 25, 2008

BREAKING NEWS: Mapapa kortini

Mawaziri wawili wa zamani, basil Mramba na Daniel Yona. leo hii wanalala katika gerezz la Keko baada ya kutekeleza matakwa ya dhamana kutokana na kesi ya kutumia vibaya madaraka yao na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Shilingi bilioni 11.752.
Mawaziri hao wa zamani waliburuzwa katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu leo asubuhi na kusomewas jumla na mashitaka 13 yanayohusiana na mkataba wa kampuni ya kufanya ukaguzi wa dhahabu ya Alex Atewart Asseyers.
Wanadai wakuwa walitumia madaraka yao vibaya na kuingia mkataba huo kinyume cha sheria kadhaa na kuisababishia serikali hasara hiyo.
Wakati makosa hayo yanatoka, Mramba alikuwa waziri wa Fedha na Yona alikuwa waziri wa Nishati na Madini katika serikali ya wamu ya tatu.
hali ilikuwa tete mahakamani hapo jana kwani watu wengi walifika baada ya taarifa kuenea mjini kuwa mawaziri hao wamefikishwa mahakamani hapo.
Walifikishwa wakiwa katika shangingi la takukuru na kukaa katika shangingi hilo kwa muda wa takriban saa mbili kabla ya kupandishwa kizimbani.
Ingawa walionekana kuwa watulivu, lakini Yona alikuwa na kazi ya kujifuta jasho katika kipindi chote alichokuwamo ndani ya mahakama.
Wakati wanaondoka, wananchi waliwatolea uvivu na kuwazomea wakiwaita wezi... wezi... wezi...
Katika masharti ya dhamana waliyoshindwa kuyatekeleza, Mawaziri hao wa zamani walitakiwa kuweka kiasi cha shilingi bilioni 3.9 taslim kila mmoja, kuwasilisha pasi zao za kusafiria na kuwa an wadhamini wawili wanaoaminika.
kesi hiyo itatajwa tena mwezi ujao na upelelezi wake bado unaendelea.

Saturday, November 22, 2008

Serikali 'yafukuza' wanafunzi vyuo vikuu

Serikali imesema itawafukuza wanafunzo wote wa vyuo vikuu vya serikali nchini ambao hawakubalini ya sera ya uchangiaji wa elimu ya juu.

Hayo yalitangazwa jana na Naibu waziri wa Elimu ya Juu, Gaudentia Kabaka. Kabaka alisema kuwa serikali imeuagiza uongozi katika vyuo vikuu vya uume kote nchini kuwachanganua wanafunzi wanaokubalina na sera hiyo na wale wanaoipinga.

Alisema baada ya kufanya hivyo, wale wanaokubaliana warudishwe masomoni haraka na wale wanaoipinga sera hiyo wabakie majumbani kwao.

Alisema hivi sasa serikali haina uwezo wa kugharamia ada za wanafunzi wote kwa asilimia 100 kama ambavyo wanafunzi hao wanavyodai.

Alisema bajeti ya kusaidia wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka huu ni Sh bilioni 117 na iwapo serikali ikitekeleza madai ya wanafunzi kuwa serikali ilipie ada kwa asilimia 100, zitahitajika Sh bilioni 163 na serikali haina uwezo wa kupata hiyo ziada ya Sh bilioni 52.

Alisema mpango wa serikali kuwakopesha ada wanafunzi kwa mujibu wa uwezo wao, umewezesha idadi ya wabafunzi wanaonufaika kufikia 60,000 lakini chini ya utaratibu unaodaiwa na wanafunzi, kwa kutumia kiwango cha bajeti iliyopo, idadi ya wanafunzi watakaonufaika haitafikia 40,000.

Tuesday, November 18, 2008

Serikali yakamata wanafunzi

Jumla ta wanafunzi saba wa vyuo vikuu nchini walikuwa wamekamatwa hadi jana mchana kutokana na kuhusishwa na migomo iliyosababisha kufungwa kwa vyuo vikuu kadhaa vya umma.
Kamatakatama hiyo ya Polisi ilianza Jumamosi ambapo wanafunzi wawili, Julius Mtatiro (kiongozi wa zamani wa daruso) na Odong Odwar (mwanafunzi rais wa Uganda ambaye anaelezwa kuwa ni mwanaharakati nzuri), walikamatwa na kuanza kuhojiwa. lakini katika hali ya kushangaza, Polisi bado haitaki kukiri kuwa inawashikilia wanafunzi hao.
Waliokamatwa wote ni viongozi wa serikali za wanafunzi katika vyuo wanavyosoma.
Wengine watano walikamatwa jana. Hao ni Rais wa DARUSO, Anthony Machibya, waziri mkuu Benedicto Raphael na waziri wa elimu wa UDSM, Suleman Ally.
Wengine waliokamatwa ni rais wa serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi za Afya Muhimbili, Godbless Charles na rais wa serikali ya wanafunzi wa Chuo Cha Ardhi, Anthony Massawe.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, amesema kuwa yeye hana taarifa za kukamatwa kwa vijana hao ingawa taarifa za uhakika zimeenea mjini kuwa baadhi yao walikamatwa katika kituo cha cha Channel Ten wakati walipokuwa wanarekodi moja ya vipindi vya mahojiano vinavyoandaliwa na kurushwa na kituo hicho.

Sunday, November 16, 2008

Mgomo wa walimu-Kesho ndio kesho

Juhudi za serikali kuhakikisha mgomo wa walimu hautokeo, zimeshindikana. walimu wamethibitisha kuwa liwake jua inyeshe mvua, kesho lazima watagoma.
rais wa Chama Cha walimu, Gratian Mukoba, amesema kuwa baada ya hukumu ya Mahakama ya Rufaa mapema wiki hii, hakuna tena kunachoweza kuwazuia walimu nchini kugoma.
Aidha, Mukoba anasema vitisho na ahadi zinazotolewa na serikali hivi sasa zinathibitisha kuwa madai ya walimu ni ya kweli na halali.
Kupitia kwa katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, serikali juzi ilitishia kuwa mwalimu atakayegoma hatolipwa mshahara. Pia, waziri wa TAMISEMI, Celina Kombani, naye amepiga mkwara akiwa humo Mwanza kuwa walimu waliowasilisha nyaraka za kughushi katika madai yao watafikishwa mahakamani.
Luhanjo alisema katika taarifa yake kuwa Serikali imekwenda mahakamani kuomba mgomo huo usitishwe na Chama cha walimu kimeshapelekewa wito wa kuitwa mahakamani.
Lakini, Mukoba anasema kuwa wao bado hawajapata wito huo, na hata kama wakiupata hauwezi kuwafanya waahirishe mgomo wao wka sababu vitu hivyo viwili havihusiani.
Anasema kuwa walimu walishajiandaa kugoma tangu siku nyingi na hivi sasa wanaisubiri kesho ifike kwa hamu waonyeshe kile ambacho wana uwezo kukifanya.
Mukoba alisema CWT haiwezi kuvutwa na ahadi ya serikali kuwa fedha zimeanza kusambazwa wilayani kwa ajili ya malipo ya walimu kwa sababu wao madai yao si fedha kusambazwa wilayani, bali walipwe malimbikizo ya madai yao.
Walimu wanasema kuwa wanadai zaidi ya Sh bilioni 16 kama malimbikizo ya posho za likizo, usafiri, matibabu na madai mengineyo lakini serikali inasema karibu nusu ya madai hayo ni feki.

Friday, November 14, 2008

Mahakimu Kesi za EPA 'wagoma'

Mahakimu wanaosikiliza kesiz a watuhumiwa wa wizi wa mabilioni ya fedha za EPA, leo wasitisha kwa muda kusikiliza kesi hizo, na 'kuandamana' hadi Mahakama Kuu kuwasilisha malalamiko yao.
Malalamiko yao yanahusisha usalama mdogo na kupatiwa vitendea kazi. Msajili wa Mahakama Kuu kimsingi alikubaliana na madai hayo na kuahidi kuwa kuanzia sasa mahakimu hao watapatiwa magari kwa ajili ya kuwachukua na kuwarejesha majumbani mwao.
Walipofika asubuhi leo, walisikiliza kesi moja ambapo waliwapatia dhamana Johnson Lukaza na mdogo wake na kisha kuahirisha usikilizaji wa kesi, ili kwenda Mahakama Kuu kuwasilisha malalamiko yao.
Huko walionana na jaji Mfawidhi, ambaye aliwapeleka kwa msajili walikowasilisha malalamiko yao.
Baada ya kurejea, waliskiliza kesi moja inayomkabili jeetu Patel na wenzake na kumkubalia dhamana na kisha wakaingia tena kwenye kikao Mahakamani hapo pamoja na msajili.
baada ya kikao hicho, hivi sasa mahakimu hao wanaendelea kusikiliza kesi nyingine ya Jeetu huku wafanyakazi wa BoT ambao nao wameshitakiwa wakisubiri na wao zamu yao ya kusikiliza maombi yao ya rufaa.
lakini taarifa nyingine zinadai kuwa malalamiko ya mahakimu hao yanahisuska pia mambo ya fedha.
Mahakimu wanadai kuwa waendesha mashitaka katika kesi hizo wanalipwa posho maalum ambayo wao (mahakimu) hawapewi).
Pia wanadai kuwa kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hizo, waendesha mashitaka walipatiwa mafunzo maalum kuhusu kesi hizo wakati wao hawakupatiwa mafunzo yoyote.
lakini kubwa zaidi, habari zimeenea mitaani kuwa wanahusika katiak kesiz a EPA wamekuwa wakihongwa kiasi kikubwa cha fedha. nadhani hatua hii ya mahakimu ni kutaka kujionyesha kuwa wao si baadhi ya hao wanaodaiwa kuhongwa

Kivuko cha Mgogoni chaota mbawa

Serikali leo imeshindwa kuzindua kivuko cha Magogoni. Ingawa waziri wa Miundombinu alishaandaliwa, na kufikishwa kilipo kivuko hicho, lakini shughuli za kukizindua kwa ajili ya safari za majaribio haikufanyika wka maenelezo kuwa bado kuna mambo ya kiufundi hayajakamilika.
nakihusisha habari hii na ile taarifa ya rais Kikwete kupelekwa kuzindua daraja ambalo halijakamilika huko Ruvuma, napata wasi wasi kuhusiana na umakini wa watendaji wetu serikalini

Magogoni yapata kivuko kipya

Kivuko kipya cha Magogoni jijini Dar es Salaam kinazinduliwa leo. Kivuko hicho kikubwa, chenye uwezo wa kubeba watu 2,000 na tani nyingi za mizigo kwa wakati mmoja kinatarajiwa kuwa mkombozi kwa wakazi wa Kigamboni, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisumbuka sana kutokana na matatizo ya usafiri.
Tutawaletea taarifa zaidi baadaye baada ya uzinduzi

Thursday, November 13, 2008

BREAKING NEWS: Jeetu Patel apata dhamana, arudishwa rumande

Mfanyabiashara Jeetu patel amerudishwa rumande katika gereza la Keko licha ya jana kupata dhamana.
Jeetu na wenzake wanashitakiwa katika kesi ya wizi wa fedha za EPA.
Taarifa kutoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zinaeleza kuwa Jeetu alipata dhamana katika kesi moja lakini alirudishwa ndani kwa sababu anakabiliwa na kesi nyingine tatu za wizi wa fedha za EPA ambazo hajapata dhamana.
Wafanyabishara wengine watatu, Bahati mahenge, Manase Mwakale na mke wake, Eddah Mwakale, ambao jana walikosa dhamana, jana walipata bahati na mtende baada ya mahakama kukuzikubali hati walizowasilisha mahakamani hapo hivyo kuachiwa kwa dhamana.
Mfanyabishara mwingine, Johnson Lukaza, pamoja na mmoja wa watumishi wa BoT ambao wanakabiliwa na kesi kama hizo, nao waligonga mwamba katika harakati zao za kusaka dhamana na hivyo kurejeshwa rumande.

NEWS UPDATE: DUCE nacho chafungwa

Habari zilizopatikana mchana huu zimethibitisha kuwa Chuo Kishiriki cha Chuo Kikuu cha dar es Salaam cha Ualimu (DUCE) nacho kimefungwa kwa muda usiojulikana.
hatua hiyo imekuja siku moja tu baada ya kufungwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kutokana na mgomo wa anafunzi.
Habari kutoka katika chuo hicho kilichop maeneo ya Chang'ombe jijini Dar es Salaam, zinaeleza kuwa uongozi wa chuo ulitoa trangazo la kukifunga chuo hicho leo asubuhi, wakati wanafunzi wanaingia katika siku ya pili ya mgomo wao.
Tangazo hilo liliwataka wanafunzi kuwa wameshaondoka chuoni hapo ifikapo saa 7 mchana. Tayari magari ya askari Polisi wa doria na wale wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia, yalionekana katika maeneo ya chuo hicho, wakati wanafunzi wakifungasha mizigo yao tayari kwa kuondoka.
Hata hivyo, wanafunzi hao walisema kuwa kufunga chuo si suluhisho la tatizo hilo kwani watakaporudishwa chuoni hapo wataendelea na mgomo wao hadi wapate haki yao.
Taarifa zaidi kutoka Morogoro zinaeleza pia kuwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) nao wanapanga kugoma kuwaunga mkono wenzao wa UDSM.
Wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu nchini wapo katika mgogoro na serikali wakipinga sera ya uchangiaji wa elimu ya juu, wanayodai kuwa inawanyanyasa na kuwabagua watanzania kutokana na uwezo wao kiuchumi.
hata hivyo, serikali inaitetea sera hiyo, ikisema kuwa inawezesha kwuasaidia wanafunzi kulingana na uwezo wa wazazi wao.

Wednesday, November 12, 2008

Chuo Kikuu chafungwa

Baraza la Chuo Kikuu cha dar es Salaam limekifunga chuo hicho kwa muda usiojulikana baada ya wanafunzi kugoma kwa siku tatu mfululizo.
Tangazo la kufungwa kwa chuo hicho limetolewa leo asubuhi na kubandikwa katika mbao kadhaa za matangazo chuoni hapo.
Jana, waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi, Prof. Jumanne maghembe aliwataka wanafunzi hao kuachana na mgomo huo na kurejea madarasani leo. Kwa upande wake, uongozi wa Chuo Kikuu uliwataka wanafunzi hao kuwa madarasani leo saa moja asubuhi.
Lakini wanafunzi hao waliendelea na mgomo wao ambao walisema hautakuwa na mwisho hadi madai yao yasikilizwe na serikali.
Wanafunzi hao wanataka kuondolewa kwa sera ya kuchangia elimu inayotoa maelekezo kwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutoa mikopo kwa kiwango kulingana na hali za waombaji.
Wanafunzi wanasema kigezo hicho hakitumiki ipasavyo, ni cha unyanyasaji na kinawabagua wanafunzi wasio na uwezo.
Walianza mgomo wao Jumatatu na kwa mujibu wa sheria, Chuo kinalazimika kufungwa iwapo wanafunzi watagoma kwa siku tatu mfululizo.