Friday, January 1, 2010

Hotuba ya Rais Kikwete ya Mwaka Mpya

SALAMU ZA MWAKA MPYA ZA RAIS WA JAMHURI YA
MUUNGANO WA TAN ZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA
MRISHO KIKWETE, KWA WATANZANIA,
TAREHE 31 DESEMBA, 2009

Utangulizi

Ndugu Wananchi;
Kama ilivyo ada naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na kutuwezesha kufika siku ya leo ya kuuaga mwaka 2009 na kuukaribisha mwaka 2010. Wapo wenzetu wengi tulioanza nao mwaka lakini hawakujaaliwa kuwa nasi siku hii ya leo kwa kuwa wametutangulia mbele ya haki. Tunamuomba Mwenyezi Mungu awape mapumziko mema. Kwa wenzetu wanaougua tuwaombee awape nafuu ya haraka ili waendelee kutoa mchango wao katika maendeleo yao, jamii zao na taifa zima kwa jumla. Aidha, tuendelee kuomba rehema za Mola wetu atujaalie afya njema na umri mrefu ili tuweze kuushuhudia mwaka wote wa 2010 na miaka mingine mingi ijayo.