Friday, October 9, 2009

Ajali yaua wanane Geita

Taarifa kutoka Geita mkoani Mwanza zinasema kuwa watu wanane wamefariki baada ya magari mawili (saloon) kugongana uso kwa uso. Magari hayo, ambayo huko Geitwa ni maarufu kama vipanya (na si Toyota Hiace kama ilivyozoeleka kuitwa mijini hasa Dar), yanatumika kama mabasi ya abiria.
Inadaiwa kuwa chanzo cha ajali ni mwendo kasi. Kati ya waliofariki ni deremo wa mmoja wa magari hayo. Dereva mwingine ameshakimbia

No comments: