Monday, November 5, 2007

KARIBUNI

Ninajilaumu sana kwa nini nimechelewa kuingia kwenye tekinolojia hii. Lakini kama walivyotueleza wahenga, kuchelewa si sababu ya kutufanya tusifike safari yetu. Nadhani hata kwa kuchelewa huku, bado tunaweza kuienenda safari hii na kufika. Hivyo waungwana, ningependa kuwakaribisha kwenye uwanja huu kwani sikuuanzisha kwa ajili yangu, bali kwa ajili yetu.
Naamini kuwa mchango wenu wa mawazo, katika kuchambua na kunyambulisha masuala, utatusaidia si tu kupanua uelewa wetu, bali kupanga mikakati ya kuleta mabadiliko yatajkayofanya maisha yetu ya leo yawe bora kuliko yalivyokuwa jan.
KARIBUNI SANA

1 comment:

Simon Kitururu said...

Karibu Mkuu!
Tuko Pamoja!