Saturday, December 1, 2007

Huu ni mchoro wa kisanii wa Jengo jipya la Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU), ambalo wachina wamekubali kulijenga jijini Addis Ababa. Wachina walitoa ahadi hiyo wakati wa mkutano wa China/Afrika (SinoAfrika) uliopita, kama zawadi yao kwa AU. Kwa kuitikia wito huo, na labda kwa kutaka makao makuu hayo yaendelee kuwa nchini mwao, Ethiopia imetoa eneo kubwa tu, ambalo lipo kando ya makao makuu ya sasa, kwa ajili ya ujenzi huo.
Niliipata picha hii hivi karibuni nilipozuru Makao Makuu ya AU.

No comments: