Saturday, December 1, 2007



Lakini hakuna kizuri kisichokosa kasoro. Huu ni mchanganyiko wa aina yake wa majengo katikati ya jiji la Addis Ababa. Kama unavyoona, jengo la ghorofa kadhaa, ambalo ujenzi wake ni wa thamani kubwa, likiwa limezungukwa na vibanda vya wenzangu na mimi, ambavyo baadhi vimeezekwa kwa makaratasi ya plastiki. Ni utajiri katikati ya umaskini na haya ndiyo aina ya maisha ambayo waafrika wengi tunalazimishwa kuyaishi na viongozi wetu. Picha hii niliipiga siku chache zilizopita nilipokuwa Addis Ababa. Hili ni eneo ambalo lipo meta kama 50 tu kutoka yalipo makao makuu ya Umoja wa Afrika

No comments: