Monday, December 3, 2007

Niliyoyakuta Addis Ababa

WAKATI Tanzania ilipoamua kuachana na sera za siasa ya ujamaa (na kujitegemea?), zilitolewa sababu zilizolenga kutuaminisha kuwa mfumo huo ulikuwa umefeli kuijenga nchi na kuipeleka katika mstari tulioutaka.

Lakini nchi nyingine ya Kiafrika, Ethiopia, inaonyesha uzoefu tofauti, kwamba ujamaa, iwapo utatekelezwa ipasavyo, bado una nafasi ya kuijenga nchi.

Ingawa maisha ya Waethiopia si tofauti sana na watu wengine wa bara la Afrika, lakini kung’ang’ania kwake sera za ujamaa, kwa kiasi fulani kumewasaidia baadhi ya wananchi ambao ni maskini na wale wa daraja la kati.

Kama unaingia kwa ndege, unapowasili Uwanja wa Ndege wa Dole tu, unaanza kuona tofauti iliyopo kati ya Ethiopia na nchi nyingi za Kiafrika.

Uwanja wake ni mkubwa na unapendeza sana kwa jengo lake kuwa lenye madirisha makubwa ya vioo, ingawa hauna pilika sana sana. Labda haukuwa na pilika kwa sababu tulifika usiku, na safari nyingi zilikuwa zimeshafanyika.

Kitu kimoja ambacho kitakushangaza, kama umetokea mahali ambako muda unathaminiwa sana, ni ufanyaji kazi wa taratibu wa wafanyakazi hawa wa uwanja wa ndege wa Dole.

Nilipata uzoefu huo mara baada ya kutua kwani ilichukua muda wa zaidi ya saa moja kupata visa ambayo maombi yake tayari yalishafanywa wiki kadhaa zilizopita.

Taarifa kuhusu maombi hayo ya visa zilikuwepo katika mafaili machache ambayo yalikuwepo katika meza za watoa visa wapatao watano niliowakuta baada ya kuteremka kwenye ndege.

Lakini cha kustaajabisha ni kuwa mfanyakazi wa kwanza alichukua faili moja na kutazama makaratasi yote hadi mwisho na kunifahamisha kuwa jina langu, pamoja na mwandishi mwenzangu ambaye nilikuwa naye pamoja, hayakuwemo katika faili hilo.

Alituelekeza kwa ofisa wa pili ambaye alikuwa na hati kadhaa za kusafiria ambazo alikuwa anazishughulikia. Tulimsubiri na alipomaliza alichukua hati zetu na kurudi tena kwenye lile faili.

Alilipitia taratibu, lakini hadi mwisho hakufanikiwa kuyaoona majina yetu. Walianza kutuuliza iwapo tuna barua za mwaliko wa mkutano ambao tulikuwa tumekwenda kuhudhuria.

Niliwajibu kuwa sikuwa na barua hiyo katika karatasi, lakini ipo kwenye kompyuta yangu ya mkononi, hawakuonyesha kuwa na nia ya kutaka kuiona hata humo kwenye kompyuta na wakawa wakijibishana wenyewe kwa lugha yao ambayo sisi hatukuielewa.

Inaelekea hawakupata suluhu kwani walirejea tena kwetu na kutuuliza tena kuhusu taasisi ambayo ilikuwa imetualika.

Hii ilikuwa baada ya kufuatilia jina la taasisi kwa zaidi ya mara kumi na wao kuangalia faili lao zaidi ya mara nne.

Nikaamua kufungua kompyuta yangu na kufungua barua ya mwaliko, nikawaonyesha. Mmoja wao akaisoma alipofika katikati akaacha kuisoma akaitisha tena faili na kuanza kupitia upya.

Hakufanikiwa kuona majina yetu. Baada ya kushughulikia watu wengine kadhaa, ofisa yule wa mwanzo alilichukua tena lile faili na safari hii akawa analipitia jirani na aliposimama mwenzangu ambaye nilikuwa nimefuatana naye akiwa umbali wa mita moja na nusu.
Alipopekua ukurasa kama wa nne, aliupitia taratibu na wakati anataka kufungua ukurasa wa tano, yule mwenzangu akamuonyesha majina yetu ambayo alikuwa ameshayapita. Tulishangaa sana iweje wayapite majina hayo kwa zaidi ya mara saba walipoliangalia faili, lakini tukaweza kuyaona, tena kwa mbali!

Hapo ndipo tukapatiwa visa. Shughuli za uhamiaji zilichukua zaidi ya dakika 15 ingawa tulipofika kwenye mstari sisi ndio tulikuwa wageni pekee tunaohitaji huduma hiyo.

Spidi yao kwa kweli inakatisha tamaa na hadi wakati tunafanikiwa kutoka nje ya uwanja, dereva aliyekuwa ametumwa kutufuata alikuwa amesubiri na kukata tamaa kuwa hatukuwepo katika ndege hiyo na akaamua kuondoka. Ilitupasa kukodi teksi hadi hotelini.

Nilianza kupata wasiwasi kuhusu nchi hii ambayo hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufika. Lakini wasiwasi huo uliondoka na kuingiwa na mshangao wakati ‘shanta’ alipokuwa anatupeleka kwenye teksi.

Nilipokuwa katika ndege nilipitia jarida ambalo moja kati ya taarifa zilizokuwepo ni kwa mgeni kuhakikisha kuwa iwapo unakodi teksi za watu binafsi, ambazo zina rangi za bluu, ni kupatana bei kwanza kwani hazina bei maalum.

Hivyo tulipoamua kukodi teksi, kitu cha kwanza nilichokifanya ni kupatana bei na wakati tunapatana, kwanza ‘shanta’ alitaka kujua iwapo tutamlipa kwa dola za Marekani au kwa Birr, ambayo ni fedha za Ethiopia.

Nilipomueleza kuwa sikuwa na fedha za nchi yao, aliniambia kuwa itakuwa ni dola 10. Nikamuuliza kama ningekuwa na fedha zao ingekuwa kiasi gani kwa safari hiyo, akaniambia ingekuwa Birr 90 kwani dola moja hubadilishwa kwa Birr tisa.

Hapo ndipo nilipoanza kushangaa jinsi fedha ya nchi hii ilivyo na nguvu! Tulipoingia kwenye taxi na kutoka uwanja wa ndege, dereva alituomba radhi kuwa anapaswa kuongeza mafuta, akaingia katika kituo cha mafuta. Yaani kama madereva teksi wa Dar es Salaam!
Nilipatwa na mshangao zaidi nilipogundua kuwa kwa bei niliyoizoea Dar esSalaam, lita moja ya petroli inauzwa kwa zaidi ya dola moja, jijini Addis Ababa bei ya lita ya petroli ilikuwa haijafikia hata nusu dola.

Lita moja ya petroli inauzwa Birr 7.7, ambayo ni chini kabisa ya dola moja ya Marekani wakati nilitarajia kuwa bei ya mafuta hapa ingekuwa kubwa sana kwa sababu Ethiopia inapata mafuta yake yote kupitia barabara kwa sababu haijapakana na bahari.

Lakini unapoingia mitaani, unakutana na ombaomba kama ilivyo Dar es Salaam, inaonekana wana mitaa yao maalum kwa ajili ya kazi hiyo.

Na wapo wengi sana ingawa kuna mgawanyiko wa tabaka hilo unaoonyesha kuwa ni watu wa jamii fulani tu ambao wengi wao ni ombaomba.

Nilipokutana na Mengesha Melekot, ambaye ni raia wa Ethiopia anayefanya kazi katika taasisi ya Friedrich Ebert Stiftung (FES) katika ofisi ya Addis Ababa, ambaye ana uelewa mkubwa kuhusu masuala ya uchumi na siasa za nchi hii, alinifahamisha kuwa pamoja na kuwa Ethiopia haina vitu vingi sana vya kuuza nje, lakini kwa miaka mingi limebakia kuwa ni taifa ambalo lilijitosheleza na mahitaji yake kutokana na vitu vinavyozalishwa ndani.

“Hapa hatuagizi vitu vingi kutoka nje. Watu wengi wanakula chakula wanacholima wenyewe, wanajifumia nguo zao wenyewe… hawahitaji nguo kutoka nje, wengi hawategemei vitu kutoka nje,” alisema.

Melekot aliniambia kuwa ni asilimia kumi tu ya mahitaji yanaagizwa kutoka nje na hii inahusisha vitu ambavyo vinatakiwa sana maeneo ya mijini.

Akizungumzia bei ya mafuta, alisema serikali bado inafuata sera za kijamaa na inadhibiti bei ya mafuta. Licha ya kudhibiti, serikali pia inatoa ruzuku kwa bidhaa hiyo muhimu katika uchumi wa nchi na maisha ya watu ili kuhakikisha kuwa inawalinda wananchi wake.

“Pia serikali inadhibiti baadhi ya bei ya vitu, hasa vile muhimu katika maisha ya binadamu. Hii inasaidia kuhakikisha kuwa watu hawapati matatizo makubwa kutoka kwa wafanyabishara ambao mara zote lengo lao ni kupata faida kubwa,” alisema na kuongeza kuwa serikali bado haina nia ya kubadili mfumo wa uchumi wa nchi hiyo.

Ethiopia ni nchi pekee barani Afrika ambayo haikutawaliwa. Ni nchi pekee ambayo ina alfabeti zake na imeshikilia lugha yake ya asili kama lugha ya taifa. Ni nchi ambayo ina kituo kimoja tu cha televisheni, kinachomilikiwa na serikali.

Katika wiki moja niliyokuwapo hapa, sikupata kuona muziki wa magharibi ukipigwa kupitia kituo hiki. Hata kusikia matangazo kwa lugha nyingine tofauti na Hamharik, ambayo ndiyo lugha ya taifa.

Ni nchi pekee ya Kiafrika ambayo ambayo historia yake imefikia milenia mbili. Ni nchi ambayo licha ya matatizo makubwa ya ukame yaliyoifanya dunia iamke, bado uchumi wake unakwenda vizuri licha ya kuwa ina wananchi wengi ambao ni masikini.

Lakini hali hii inabadilika kwa kasi kutokana na utandawazi. Maingiliano na nchi nyingine yanabadilisha mambo Ethiopia kwa kasi.

Na madhara ya mchanganyiko huu unaotokana na utandawazi yanaanza kuonekana wazi miongoni mwa wananchi wa Ethiopia.

Leo hii si ajabu kukuta ghorofa la kisasa lililojengwa kati ya vibanda vilivyojengwa kwa makaratasi ya plastiki katika Jiji la Addis Ababa. Wakati wanaofanya kazi katika majengo hayo ya kisasa wakifika kazini hapo kwa magari yao ya kifahari, watu kutoka katika mabanda hayo, hushinda kando ya barabara karibu na jengo hilo wakiomba chochote kutoka kwa wapita njia.

Mbaya zaidi, wale wanaofanya kazi ndani ya jengo hilo wanawaona hawa kama wanaowaharibia mandhari ya jengo lao wakati wao ndio waliwavamia, wakajipatia ardhi kati yao na kuonyesha utajiri wao bila kukumbuka kuwasaidia wenyeji waliowakuta hapo.

Tayari kampuni kubwa za kigeni zimeshaanza kuingia kwa uwekezaji nchini humu na wananchi wanaanza kuona tofauti ya maisha kwani wageni hawa wanakuja na athari nyingi za kiuchumi, kisiasa na kijamii.

12 comments:

Anonymous said...

...please where can I buy a unicorn?

Anonymous said...

eso es!! http://nuevascarreras.com/tag/cialis-online/ cialis 20 mg 8 comprimidos Magnifico messaggio, interessante per me:) cialis generico comprar ibomqxozlo [url=http://www.mister-wong.es/user/COMPRARCIALIS/comprar-viagra/]comprar cialis[/url]

Anonymous said...

Sie sind absolut recht. Darin ist etwas auch mich ich denke, dass es der gute Gedanke ist. viagra preis cialis rezeptfrei kaufen [url=http//t7-isis.org]viagra ohne rezept apotheke[/url]

Anonymous said...

Ok so I have a bunch if key loggers and Trojans as of 1 hour ago and I need to know weather I should system restore or something help

___________________
[url=http://www.youtube.com/watch?v=n1BvVfaTQsI]stop sweating[/url]

Anonymous said...

natasha gregson wagner sex scene Really? amazing. Hmm ... well, it pamoymu have extreme ... I like your posts STUDY theme! Yeah, sure, that there still might say. super original Yes, but it's not all ... I hope it will still Really? amazing.

Anonymous said...

minature pony sex Well of course tin ... Thanks to a huge, super article. Content is interesting, learned a lot. I recommend everyone to read. IMHO, the author is wrong So engrossed that I missed a football Super! Everything is very clear and competently, and at the same time without philosophising and narcissism, and in accessible language. Rare case when a person is divided into topical and interesting infoy. Thanks to author! Cool Thank you great!

Anonymous said...

fillipino porn This unrivaled Just do not believe and how difficult it is to your own blog? cool .. took almost all)) You know now who rarely writes on the subject, very pleasant to read, I would advise to add more pictures! All read satisfy my interest but "No matter how cursed himself, others certainly will do it better.") Well of course tin ... Well without untoward happens - even a schoolboy on holiday give job. - Charles Lamb

Anonymous said...

Masturbation Content is interesting, learned a lot. I recommend everyone to read. Wine and women bring to us Blog super, everything would be different! Really? amazing. You normally happy about us with the best phrases thanks, take! Laugh not a sin, but admit it when you read this information at least surprised me:)) decided to help and sent out a post in the soc. bookmarks. hope to rise in popularity In my opinion you stole this article and placed on another site. I had already seen.

Anonymous said...

sex searcher STUDY theme! I read a similar article on this subject, but you have quite a different opinion, thanks, it was interesting to compare I do not know about you, but I like it! There is. Well without untoward happens - even a schoolboy on holiday give job. - Charles Lamb blog in my favorites class) I ponra) especially! while I'm alive, I will remember your resource zanoshu in bukmarki .... Quite strange material you provide to us

Anonymous said...

adult mastiffs available Added to your bookmarks. Now will you read much more often! You normally happy about us with the best phrases thanks, take! Content is interesting, learned a lot. I recommend everyone to read. You read this and think .... A salary of between 5% per day Indeed ... super creative! I thank you - for the warm welcome) The site just super, I will recommend to friends! All read satisfy my interest but "No matter how cursed himself, others certainly will do it better.")

Anonymous said...

free adult webcams they were more You read this and think .... read with pleasure very nice, so we would have done so Really? amazing. Just do not believe Thank you! In quotations! Yes, but it's not all ... I hope it will still

Anonymous said...

adult punch buggy blog in my favorites Interestingly, and cognitive, and will have something on this subject? Blog just super, I will recommend to friends! zabavno Well done! So engrossed that I missed a football Happiness - not a reward for virtue, but virtue itself, not because we enjoy the happiness that curb their passions, but rather enjoy the happiness makes us able to curb them. - Spinoza Indeed ... super creative!