Monday, December 10, 2007

SUALA LA MADINI; Tatizo ni Sheria au Uwezo wa TRA?

RIPOTI ya Kamati ya kupitia mikataba ya madini iliyoongozwa na aliyepata kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Lawrence Masha, imeanika udhaifu wa kitengo cha madini katika wizara hiyo pamoja na Mamlaka ya Mapato nchini katika kusimamia na kuratibu sekta ya madini nchini.

Ripoti ya Kamati ya Masha inasema ushahidi uliotolewa na Alex Stewart (Assayers) Government Corporation unaonyesha dhahiri kuwa uwezo wa TRA kuwa ni mdogo katika masuala ya madini kwa kuwa haina wafanyakazi wa kutosha na wenye ujuzi mpana wa kunyambulisha taarifa za fedha za makampuni ya madini.

Aidha, kwa mujibu wa ripoti hiyo, ambayo Tanzania imenasa nakala yake, suala la udhaifu wa Kitengo cha Madini katika wazara, lilishabainishwa katika ripoti ya kamati ya Dk Kipokola.

Kamati ya Dk Kipokola ilianisha udhaifu wa kitengo hicho katika masuala ya muundo wake, uwezo pamoja uratibu na mawasilaino na idara nyingine za serikali.

“Ripoti )ya Dk Kipokola) inabainisha kuwa muundo wa kitengo cha madini uliopitishwa mwaka 2001 hauendani na matakwa ya sekta hii ambayo inakuwa kwa kasi,” inasema sehemu ya ripoti ya Kamati ya Masha, ambaye sasa ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Ripoti hiyo inarejea uzoefu ulioonekana katika nchi za Botswana na Ghana na kueleza mathani kuwa nchini Botswana, kuna kitengo cha uchumi wa madini, ambacho jukumu lakwe kubwa ni kulinda maslahi ya nchi kwa kuratibu kwa karibu shughuli za uchimbaji madini.

Nchini Ghana, kipo kitengo ambacho kazi yake kubwa ni kufuatilia kwa karibu gharama za miradi mikubwa ya uchimbaji madini, inasema ripoti hiyo.

Kutokana na masomo hayo, tayari mapanedekezo yalishafikishwa serikalini kuhusiana na umuhimu wa kukifanyia kitengo hicho mabadiliko, lakini kwa mujibu wa ripoti ya Kamati ya Masaha, utekelezaji wa mapendekezo hayo unategemea sana mafunzo kutoka Botswana.

Kuhusu TRA, ripoti hiyo inasema kuwa ripoti iliytoandaliwa na Alex Stewart (Assayers) Government Corporation, mannuzi kutoka nje yaliyofanywa na makampuni ya madini hayakuchunguzwa ipasavyo na Idara ya Ushuru wa Forodha kuhusu idadi, aina na thamani ya vifaa vilivyoagizwa ambavyo vinastahili kusamehewa ushuru.

Inabainishwa pia katika ripoti hiyo kuwa ukaguzi wa kina katika maeneo ya amchimbo ulifanyika mara chache sana kabla masuala ya makampuni ya madini hayajahamishwa kutoka idaya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na Kodi ya Mapato na kupelekwa Idara ya Walipoa Kodi Wakubwa.

“Kodi zilikadiriwa kutokana na ukagusi uliofanyika ofisini tu. Ziara ya maeneo ya machimbo zilifanywa kwa ajili ya marejesho ya VAT na kodi ya zuio,” inabainisha ripoti hiyo.

Ripoti hiyo inasema kuwa Alex Stewart ilibaini kuwepo kwa uwezo mdogo katika ngazi mbalimbali ndani ya TRA kuratibu shughuli za kampuni za kuchimba madini.

“Kwanza TRA ilitakiwa iwe na udadisi wa hali ya juu kuhusu biashara na taarifa za fedha zinazowasilishwa na kampuni za madini… kuna uwezekano kuwa TRA haina watu wenye maarifa maalum kunyambulisha shughuli za kampuni za madini,” inasema ripoti hiyo.

Ripoti hiyo inabainisha kuwa kuna masuala ambayo TRA ilitakiwa iyabaini mapema kama vile muendelezo wa kukosekana kwa nyaraka kadhaa.

“Kuna ushahidi wa dhahiri wa dhamira ya ku[potosha pale madau wawili katika mradi wanapotoa taarifa mbili tofauti za fedha kuhusiana na shehena moja ya dhahabu iliyosafirishwa nje,” inasma ripoti hiyo.

Ikiweka wazi, ripoti inataja tukio ambalo kampuni mbili zilizoungana katika mradi mmoja wa madini, zilidanganya kuhusu mapato ya mauzo ya dhahabu kwa pungufu ya dola za Marekani 2,340,000 kati ya 2001 na 2003.

1 comment:

Anonymous said...

Huyo masha anataka kujifanya mtakatifu miongoni mwa wenye dhambi au ndio sura yake ya kweli?