Saturday, December 29, 2007

MATOKEO KENYA

Mpaka asubuhi ya leo (Desemba 29), raila odinga alikuwa anaongoza kwa takribani kura milioni moja katika kinyang’anyiro cha urais wa Kenya.

Matokeo kutoka katika majimbo 112 kati ya majimbo 210, ambayo ni zaidi ya nusu ya majimbo yote, yanaonyesha kuwa Raila anaongoza kwa kupata kura 3, 268,571 dhidi ya kura 2,278,355 za rais Kibaki. Kalonzo Musyoka wa ODM-Kenya yeye amejipatia kura 356,632.

Inavyoonekana hata kama muujiza utatokea na Kibaki akashinda, serikali yake haiwezi kufanya kazi ipasavyo kwani matokeo yanaonyesha kuwa Raila na ODM yake watakuwa na viti vingi Bungeni.

Mkapa wakati huu, Raila na chama chake walikuwa wanakaribia kupata viti 80 wakati PNU ikijikongoja kwa viti ambayo haviki hata 20. Mbaya zaidi timu kubwa ya mawaziri ambao Kibaki alikuwa akiwategemea kuwa watarudi Bungeni imeshindwa akiwemo makamu wake, Moody Awori.

KANU ndiyo inaelekea kufa kwani hata watoto wa Moi waliokuwa wakitarajiwa kuwa ndio wangekuwa wakombozi, wote wamepigwa chini.

Endelea kufuatilia matokeo hayo kupitia hapa kwani nitakuwa nikiyahuisha kila taarifa mpya zitakapotolewa.

No comments: