Friday, July 18, 2008

Mtikila amtisha Rostam

Wakati mfanyabiashara na mwanasiasa, Rostam Aziz amefungua kesi dhidi ya Mchungaji Chritopher Mtikila, akimtaka athibitishe madai yake kuwa yeye (Rostam) ni raia wa Iran, Mtikila naye amempelekea barua Rostam, akimtaka amwombe radhi kwa kumdhalilisha.

Katika Demand Note hiyo, Mtikila ametoa siku 14 kwa Rostam kumwomba radhi na kumlipa fidia y ash bilioni tatu. Pia Demand Note hiyo inavihusu vyombo vya habari kadhaa, ambavyo viliripoti hayo maneno ya Rostam ambayo Mtikila anadai kuwa yamemdhalilisha.

Maneno anayoyalalamikia ni yale yaliyotolewa na Rostam alipokutana na waandishi wa habari hivi karibuni kuwa ‘Mtikili hastahili heshima ya kujibiwa na mimi (Rostam).

Pia Mtikila analalamikia maneno ya Rostam yanayobainisha kuwa kauli za Mtikila ni za kinyaa na zinachochea machafuko nchini.

No comments: