Friday, July 18, 2008

Ndege ya rais yagongwa

Gari la usalama la Ikulu linaelezwa kuigonga ndege ya rais iliyokuwa imepaki katika hangar katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere.

Haijaelezwa tukio hilo limetokea lini lakini Rubani Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali amebainisha kuwa ndege hiyo iliyogongwa haijaharibika sana.

Taarifa zilizopatikana hata hivyo, hazijaeleza gari hilo lilikuwa linatafuta nini karibu na ndege hiyo ya rais iliyonunuliwa kwa bei mbaya, ambayo haitumiki kwenye safari nyingi za rais ingawa wakati inanunuliwa ilidaiwa ni kwa ajili ya kumuondolea rais aibu ya kusafiri na ndege za abiria.

No comments: