Tuesday, January 27, 2009

Twin Tower za BoT zazaa kesi

maofisa wawili wa Benki Kuu (BoT), Amatus Joachim Liyumba na Deogratius Dawson Kweka wamefikishwa katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na shitaka la kutumia madaraka yao vibaya katika mradi wa ujenzi wa mirana pacha ya BoT na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya shilini bnilioni 221.
INgawa walikana mashitaka na upande wa mashitaka kutoweka pingamizi ya dhamana, lakini walishindwa kutekeleza masharti ya dhamana na hivyo kepelekwa katyika mahabusu ya keko hadi Februari 10 kesi hiyo itakapotajwa tena.
Liyumba na mwenzake wanadaiwa kutumia madaraka yao vibaya katika mkataba wa ujenzi huo na kuidanganya Bodi ya Wakurugenzi wa BoT ambayo ilifanya maamuzi yanayopingana na sheria ya manunuzi ya umma, wakati wa kuamua kuhusu mradi huo.
Upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika lakini watuhumiwa walitakiwa kuleta mahakamani nusu ya kiasi cha fedha zilizotajwa (yaani sh bilioni 221). Kwa wastani, kila mmoja alitakiwa kuweka mahakamani si chini ya shilingi bilioni 50 au kutoa hati za mali zisizohamishika zenye thamani kama hiyo.
Wakili wa Liumba, Alexander Kyaruzi, aliiambia mahakama kuwa mteja wake ana hati tatu za nyumba ambay kila moja ina thamani ya sh milioni 600 lakini upande wa mashitaka waliomba muda ili kuzipitia hati hizo ilim kuthibitisha kuwa ni halali.
Thamani ya ujenzi wa majengo hayo imekuwa ikilalamikiwa na wananchi wengi, wakiwamo wabunge wa upinzani na vyombo vya habari, huku seriakli ikitoa majibu yasiyojitosheleza kuhalalisha ujenzi huo.
Suala hilo lilikuwa chini ya uchunguizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa muda mrefu.

1 comment:

Simon Kitururu said...

Mkuu mbona umepotea sana hapa kijiweni?
Nakusabahi tu Mkuu!
Tuko Pamoja!