Saturday, October 24, 2009

Makali ya mgao wa umeme yaanza kupungua?

Baada ya kuhangaika na pilikapilika, hatimaye Waziri wa Nishati, William Ngeleja, alitangaza juzi kuwa umeme katika mitambo ya IPTL unaweza kuanza kupatikana Novemba Mosi. Siku hiyo hiyo kuna uwezekano pia kuwa mitambo mipya ya tanesco iliyopo Tegeta nayo itaanza kufanya kazi.
Tulitarajia kuwa jana Ijumaa, mtambo wa Songas uliokuwa umeharibika ungeanza kuingiza katika gridi ya taid kama Megawati 20 hivi. Lakini kabla haya hayajafanyika naona kama kuna nafuu fulani (au labda ni kwa upendeleo) kwa maana watu tunaoishi tangu bovu hatujakatiwa umeme tangu juzi. Ndio maana najiuliza iwapo makali ya mgawo yameanza kupungua au ni Tanesco walisahau kukata umeme katika eneo letu!

No comments: