Thursday, November 15, 2007

Arusha inaangamia?

Jamani bado nipo A town. Baada ya kuzunguka hapa na pale mjini hapa na kuzungumza na wenyeji, nimebaini kuwa mambo si shwaji mjini hapa na mkoani Arusha ka ujumla.
Ni kwamba uchumi wa mji wa Arusha ulikuwa ukitegemea sana madini ya tanzanite huko Mererani. Lakini kwa bahati mbaya sana, upatikanaji wa madini hayo, hasa miongoni mwa wachimbaji wadogo, umeshuka sana, ni kama hakuna kitu kinapatikana hivi sasa.
Matokeo yake, watu wengi wamekosa kazi. Vijana wengi wamelazimika kukimbia kutoka Mererani na kukimbilia katika miji jirani ya Moshi na Arusha. Si ajabu matukio ya uhalifu yanazidi kushika kasi ingawa Polisi hawataki kukiri hivyo (nadhani wanahofia kitumbua chao).
Sasa hivi kampuni ya Tanzanite One pekee ndiyo inayoendelea na uchimbaji na hata madini machache yanayoonekana mitaani inasemekana yanaibwa kutoka Tnzanite One kwa sababu kwenye machimbo ya wachimbaji wadogo hakuna kinachopatikana kabisa!
Hii ni hatari na nadhani mamlaka zinazohusika zinapaswa kuchukua hatua mara moja kunusu maisha ya hao waliokosa kazi pamoja na wananchi wengine ambao wameaza kuwa walengwa wa vijana hao waliokosa kazi. Wanachokijua hivi sasa ni kuvuzia maduka na kuiba, kweli ni hatari.

No comments: