Wednesday, January 16, 2008

BREAKING NEWS- Balali anyang'anywa Visa na Marekani

Habari za uhakika nilizozipata hivi punde zinaeleza kuwa aliyekuwa Gavana wa BoT, Daudi ballali, amenyang'anywa visa na serikali ya Marekani.
taarifa hizo zinaeleza kuwa Marekani imefikia uamuzi huo baada ya kuthibitishiwa na serikali ya Tanzania kuwa Ballali si mwakilishi tena wa serikali.
Marekani tayari imeshaitaarifu serikali ya Tanzania kuwa inabatilisha viza ya Balali kwa sababu haiwakilishi tena Tanzania.
Kwa mujibu wa vyanzo vyangu, Balali alipewa viza hiyo kutokana na wadhifa wake kama Gavana, akiiwakilisha Tanzania katika nchi mbalibali ikiwamo Marekani.
Lakini kwa sababu ajira yake imekoma, Marekani imeona kuwa hana sifa za kuwa na visa hiyo ambayo inaitwa kwa kimombo non-immigrant visa.

No comments: