Wednesday, January 9, 2008

BREAKING NEWS: JK AMTIMUA BALALI

Sasa Kikwete anaweza kuwa ameamua kukifanya kile ambacho watanzania wengi walitaka akifanye tangu alipoingia madarakani. Habari zinazosambaa sasa hivi ni kuwa amemfukuza kazi Gavana wa benki Kuu na kuagiza watu wote ambao wametuhumiwa katika ripoti ya uchunguzi wa benki Kuu washughulikiwe.
Kama hatua hii haitakuwa na maana ya kuwatoa mbuzi wa kafara (ili kundi kubwa lipone) sasa tutarajie kupanda kwa chati ya rais Kikwete.
lakini ametoa mtihani kwa Mwanasheria mkuu kwa sababu iwapo watalaamu waliochunguza wamebaini ubadhirifu kiasi cha rais kufikia uamuzi wa kumfukuza mtu, itashangaza sana wao watakaposhindwa kuja na kesi ya kumfunga mtu kifungo kirefu

No comments: