Friday, January 11, 2008

Kenya Kuchemka Upya

Mambio yanazidi kuwa mabaya huko Kenya. Baada ya kushindwa kwa juhudi za kidiplomasia kumaliza mgogoro uliokuwepo, sasa chama cha ODM kimeamua kurudi kwa wananchi. Hivi punde kimetoa tangazo kikiwataka wafuasi wake wajiandae kwa maadamano makubwa nchi nzima kupinga ushindi wa Kibaki. Hakuna anayejua ni nini kitatokea, hasa ukizingatia uzoefu wa maandamano ya kwanza ambapo mamia ya watu waliuawa na mali kuharibiwa.
Hali hii inatishia sana usalama hata wa Tanzania kwa sababu upo uwezekano kuwa madhara yake yakawa makubwa, hasa baada ya kuonyeshwa kuwa Tanzania inapoteza mapato mengi kutokana na vurugu nchini Kenya.

No comments: