Thursday, February 7, 2008

BREAKING NEWS: Lowassa Aomba Kujiuzulu

Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ameandika barua kjwa Rais Jakaya Kikwete akiomba kujiuzulu wadhifa huo.
Lowassa alitangaza hayo Bungeni leo wakati alipotakiwa kuchangia ripoti ya Kamati nTeule ya Bunge kuhusu kampuni ya Richmond.
Lowassa amesema kuwa ameamua kujiuzulu ili kuonyesha uwajibikaji ingawa hakubaliani na jinsi kamati hiyo ilivyomhukumu bila kumhoji.
Alisema kuwa baada ya kuisoma taarifa ya kamati hiyo amebaini kuwa kinachotakiwa ni Uwaziri Mkuu, hivyo kwa manufaa ya serikali, chama chake na nchi, ameamua kuuachia wadhifa huo.
Huku akiongea kwa masikitiko makubwa, Lowassa alisema kuwa imemshangaza kuwa wakati ripoti hiyo inamtuhumu yeye, hakuhojiwa wakati yeye alikuwa tayari kutoa maelezo yake. Alisema ahata aliponong'onezwa suala hilo na Spika, samwel Sitta, alimletea ushahidi wa maandishi.
Habari kutoka Ikulu zinaeleza kuwa tayari barua hiyo imeshapokelewa na maamuzi yatakapofanywa yatatangazwa.
Mwandishi wa Habari wa rais, Premmy Kibanga aliiambia tovuti hii kuwa suala hilo litatangazwa hadharani ingawa hakusema lini maamuzi hayo yatafanywa na kutangazwa

No comments: