Monday, March 3, 2008

BREAKING NEWS: JENGO LA USHIRIKA LAUNGUA

Sehemu ya jengo maarufu la ushirika, zilimo ofisi mbalimbali imeungua kwa moto usiku wa kuamkia leo. Habari zinapasha kuwa ingawa haijathibitishwa na mamlaka husika, chanzo cha moto huo kinaweza kuwa umeme.
Mashuhuda wanapasha kuwa usiku umeme ulikatika katika jengo hilo na uliporejea baadaye, waliona cheche za moto kana kwamba kuna mtu alikuwa anachomelea vyuma . baada ya muda kidogo waliona moshi mzito ukifuka sehemu hiyo na moto mkubwa kuzuka.
Takriban ofisi 15 zimeungua na mojawapo ni ofisi ya Prince bagenda, ambaye alikuwa katika harakati za kuanzisha gazeti jipya lililotarajiwa kuwa mitaani kwa mara ya kwanza Ijumaa ijayo (bado haijaelezwa kuwa mipango ya kulitoa Ijumaa imefuitwa).
Akizungumza eneo la tukio, Bagenda alisema kuwa vitu vilivyokuwa katika ofisi yake vina thamani ya zaidi y ash milioni 250. vuti hivyo vinajumuisha na kompyuta na vifaa vingine vinavyohusiana na uandaaji wa gazeti.
Aidha, alisema kuwa ndani ya ofisi hiyo ndimo ilimokuwa inaendeshwa mipango ya kuanzisha TV na radio.
Wamiliki wa ofisi zilizoungua wamesema kuwa watatoa taarifa hapo baadaye.
Waziri wa Mambo ya ndani, Lawarence Masha, alifika eneo la tukio leo asubuhi lakini hakutaka kuzungumza chochote bkwa maelezo kuwa hajapatiwa taarifa za kutosha kuhusiana na ajali hiyo.

No comments: