Wednesday, March 19, 2008

Timu ya Pinda Yakamilisha Kazi

Timu iliyoteuliwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kupitia kwa kina mapendekezo yaliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wa Richmond, imemaliza kazi yake na kukabidhi ripoti.
Pinda amesema kuwa hivi sasa, serikali inaipitia ripoti hiyo kabla ya kutoa maamuzi kutokana na mapendekezo ya Timu hiyo.
Katika ripoti yake, Kamati teule ya Bunge iliyokuwa na wajumbe watano chini ya uenyekiti wa Dk. Harison Mwakyembe, ilipendekeza watumishi kadhaa wa umma, walio katika ngazi za juu serikalini, wachukuliwe hatua kutokana na uzembe uliosababisha taifa kupata hasara kupitia mkatana huow a Richmond.
Mtumishi mmojawapo mkubwa wa umma ambaye kamati hiyo imependekeza awajibishwe ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, John Mwanyika, kutokana na kile kilichoelezwa na kamati kuwa ni kushindwa kwa ofisi anayoiongoza kuishauri vema serikali katika suala hilo.
Pia, pamoja na kushauri hatua zichukuliwe dhidi ya Mkurugenzi wa Takukuru, kamati hiyo inapendekeza pia taasisi hiyo imulikwe baada ya kutoa taarifa iliyoonyesha kuwa kimsingi hakukuwa na tatizo lolote la ufisadi katika mkataba wa Richmond.
Tayari aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wawili, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, walishajiuzulu nyadhfa zao baada ya kuwasilishwa kwa ripoti hiyo Bungeni.
Kukamilika kwa ripoti hiyo kunafanya idadi ya ripoti kuhusiana na sakata la Richmond kufikia tatu baada ya timu nyingine iliyohusisha wanasheria wa Bunge kuipitia mikataba baina ya Tanesco na makamopuni binafsi ya kzualisha umeme, ukiwemo wa Richmond.
Wataalam hao wa washeria walibaini kwua mikataba na makampuni matano baina ya sita ilikuwa inafanana kwa kiasi kikubwa na kuleta wasi wasi wa umahiri wa watu walioandika au kuidhinisha mikataba hiyo.

No comments: