Tuesday, April 22, 2008

Chenge na siri yake ya vijisent

Aliyewahi kuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, aliyejiuzulu Jumapili iliyopita, sasa amewaomba waandishi wa habari wamwache ili kumpatia muda wa kutafakari matatizoyanayomkabili.
Chenge anasema kuwa matatizo yanayomkabili ni makubwa na angependa kupata muda wa kuyatafakari bila bughudha. Alisema kuwa kwa sasa hana mpango wa kuzungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tuhuma zinazomkabili.
Hata hivyo, kuna taarifa kuwa Chenge amepanga kutoa taarifa ndefu ya kufafanua jinsi ambavyo fedha kiasi cha dola milioni moja zilivyoingia kwenye akaunti yakeiliyopo katika benki moja huko katika kisiwa cha Jersey, Uingereza.
Lakini kauli hiyo inaweza kumtia Chenge au mtu au watu wengine katika matatizo zaidi kutokana na uchunguzi unaofanywa na Serious Fraud Ofice (SFO) ya Uingereza kwani anawezakutoa taarifa ambazo wachunguzi hao hawana na wakaanza kuzifuatilia na kuibua mambo mengine mengi.

No comments: