Tuesday, April 22, 2008

Ditopile azikwa Dar

Rais Jakaya Kikwete ameongoza mazishi ya aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Ukiwaona Ramadhan Mwinshehe Ditopile Mzuzuri, aliyefariki Jumapili iliyopita katika hoteli ya Hikux mjini Morogorogo.
Mazishi hayo yamefanyika leo katika shamba la marehemu huko Kinyerezi,nje kidogo ya Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi wengine maarufu akiwemo Waziri Mkuu, Mizengi Pinga na mtangulizi wake aliyejiuzulu, Edward Lowassa.
Mazishi hayoyalifanyika saa 10jioni bada ya maiti hiyo kuswaliwa katika msikiti wa Tambaza na salamu za rambirambi kutolewa nyumbani kwa marehemu, Upanga.

No comments: