Monday, April 14, 2008

CUF-CHENGE AKAMATWE

Chama cha Wananchi (CUF) kimetaka Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, akamatwe na kuwekwa chini ya ulinzi mara moja, wakati uchunguzi dhidi yake kuhusiana na kumiliki na akaunti yenye zaidi ya sh bilioni moja nje ya nchi, ukifanywa.

Mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahim Lipumba, amemtaka Rais Jakaya Kikwete amsimamishe kazi Chenge haraka, ili kuwezesha uchunguzi dhidi ya waziri huyo, ambaye alipata kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa zaidi ya muongo mmoja, kufanyika bila kuingiliwa.

Akiishadidia hoja yake ya kutaka Chenge awajibishwe, Prof Lipumba alinukuu sehemu ya sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Kifungu cha 29 cha sheria hiyo, ambacho kiongozi huyo wa CUF alikinuu kinasema kuwa kiongozi wa umma atahesabika kuwa amefanya kosa iwapo;
(a) atakuwa na hali ya maisha ya juu kuliko kipato chake cha sasa au awali na
(b) atakuwa anamiliki mali zisizolingana na kipato chake cha sasa au cha awali.

Kutokana na kifungu hicho, Lipumba anadai kuwa kiasi alichokutwa nacho Chenge katika akaunti yake ni kikubwa kuliko kipato chake hivyo ametenda kosa kwa mujibu wa kifungu hicho.

“Sheria na maadili ya viongozi wa umma inawataka wabunge kutoa taarifa za mali walizonazo kila mwaka. Taarifa hizi zinapaswa kufanyiwa uchunguzi wa kina na TAKUKURU. Ikiwa Mhe. Chenge ametoa taarifa ya akaunti zake za Jersey, je? TAKUKURU imefanya uchunguzi fedha hizo amezipataje? Kama hajatoa taarifa hizo basi amevunja sheria,” amesema Lipumba.

Lipumba ameonyesha wasi wasi wake kuhusiana na Chenge kuwa fedha hizo zote na kurejea historia yake inayoonyesha kuwa alimaliza masomo UDS< 1972 na kuajiriwa na serikali kama mwanasheria.

Alisoma shahada ya pili havard University 1975 na akarejea nchini kuendelea na kazi serikalini. Alipanda vyo hadi kuteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu mwanzoni mwa miaka ya tisini hadi 2005 kabla ya kuteuliwa kuwa waziri baada ya kupata ubunge huko bariadi.

Lipumba anasema kuwa ni jambo linaloshangaza kwa mtumishiw a umma kwa hali ya Tanzania kuwa na fedha zote hizo katika benki ya nje.

Gazeti la Guardian la Uingereza liliripoti mwishoni mwa wiki kuwa Cheneg alikutwa akiwa na kiasi cha dola za Marekani milioni moja katika akaunti yake iliyo katika benki moja katika kisiwa cha Jersey.

Chenge mwenyewe amekiri kuwa na kiasi hicho cha fedha katika akaungti hiyo, lakini amekanusha kuwa fedha hizo zimetokana na malipo ta rushwa kutokana na mpango wa shirika la BAE la Uingereza kuiuzia Tanzania rada ya kijeshi.

No comments: