Sunday, April 6, 2008

Meli yazama bahari ya Hindi

MELI isiyofahamika iliyokuwa na abiria na wafanyakazi 14, imezama katika Bahari ya Hindi mwishoni mwa wiki.

Mbali na kuwa na abiria hao, meli hiyo ilikuwa na shehena ya magari matatu ya Idara ya Magereza na lita 90 za mafuta ya mitambo ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco).

Habari zilizopatikana jana zilieleza kuwa meli hiyo ilizama usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita katika Bahari ya Hindi wakati ikiwa njiani kutokea Dar es Salaam kuelekea Mafia.

Habari hizo zinaeleza kati ya abiria hao, mwili mmoja unaosadikiwa kuwa wa nahodha wa meli hiyo umepatikana huku abiria wanane kati ya hao wakipatikana wakia hai katika eneo la Makunduchi, Zanzibar na wengine watano hado hawajulikani walipo.

Miongoni mwa abiria ambao hawajulikani waliko, ni askari magereza ambaye alikuwa akisindikiza shehena ya magari matatu ambayo ni mali ya idara hiyo.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, tayari ametuma salamu za rambirambi kwa ndugu na familia wa marehemu, abiria na wafanyakazi wa meli hiyo.

Aidha, Pinda ameagiza Polisi Wanamaji kwenda eneo la ajali kusaidia kuokoa watu ambao watakuwa bado wako hai na kama wameshakufa waopoe miili yao.

No comments: