Friday, April 11, 2008

Uchaguzi wa rais DARUSO wasimamishwa

Uchaguzi wa rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (DARUSO) uliopangwa kufanyika leo umeahirishwa. Hata hivyo, hadi wakati huu sijafahamu sababu za kuahirishwa kwa uchaguzi huo ingawa ninaendelea kulifuatilia suala hilo na nitawajulisha baadaye.
Uchaguzi unaoendelea ni ule wa makamu wa Rais pamoja na wakuu wa mabweni.
Kampeni za uchaguzi huo zilitawaliwa na itikadi za vyama vya siasa na uzawa, huku baadhi ya wagombea wa nafasi ya rais wakituhumiwa kupokea fedha kutoka kwa viongozi wa vyama vya siasa kusaidia kampeni zao.
Aidha, mgombea mmoja alilalamika kufanyiwa kampeni chafu dhidi yake kwa kuwa yeye si raia wa Tanzania. Hata hivyo, mgombea huyo Mganda alisema hilo halimsumbui na ana uhakika wa kushinda kinyang’anyiro hicho.

No comments: