Friday, May 16, 2008

Serikali Kudhibiti Bei ya Mafuta

Kuendlea kupanda kwa bei ya mafuta kumeilazimisha serikali kutekeleza kilio cha muda mrefu cha wananchi, walioiyaka kuhakikisha inaweka mfumo utakaosaidia kudhibiti bei ya mafuta. Kwa muda mrefu serikali imekwua ikikataa kufanya hivyo, kwa madai kwua inaogopa kuonekana kuwa inaingilia biashara iliyo katika mfumo wa soko huria.
Lakini sasa serikali imeshtuka kwua nkuna uwezekano na yenyewe 'inaliwa' katika soko la mafuta. hivyo, Wizara ya Nishati na Madini iliamua kuchukua uamuzi wa kuwakutanisha wadau wote katika sekta ndogo ya mafuta ili kupanga mikakati ya kudhibiti bei ya bidhaa hizo.
Kilichoamriwa na kutangazwa na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, ni mpango utakaohakikisha kuwa kunakuwa na utaratibu wa kupanga bei ya mafuta.
Ngeleja amesema kuwa chini ya utaratibu huo,wafanyabiashara wote wanaoagiza mafuta kutoka nje ya nchi,wanatakiwa kupeleka taarifa zao zote kwa Malmaka ya Udhibiti wa Nsiahti na Maji (EWURA).
Alisema kwua EWURA ikishapokea taarifa hizo, zitakazohusisha gharama za ununuzi wa mafuta, usafirishaji, upakuaji na kuhifadhi, itakuwa katika nafasi ya kukadiria bei inayofaa ya mafuta itakayotumika kwa wauzaji wote.
Ngeleja alisema kwua utaratibu huo uemshakubaliwa rasmi na atakayekuwa anakiuka atakuwa anatenda kosa hivyo kustahili kuchukuliwa hatua.

No comments: