Wednesday, July 30, 2008

Kwa heri Wangwe

(KWA HISANI YA TANZANIA DAIMA)

RAIS Jakaya Kikwete, jana aliwaongoza viongozi mbalimbali wa serikali, wabunge, majaji, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Chacha Wangwe, katika shughuli ya kuaga mwili wake.

Shughuli ya kuuaga mwili wa Chacha, ilifanyika katika maeneo ya Bunge, kuanzia majira ya saa 12:15, jioni.

Rais Kikwete alikuwa Dodoma kuhudhuria mkutano wa Baraza la Mawaziri, uliofanyika katika Ikulu ya Chamwino, mjini hapa, ambapo alitumia fursa hiyo kuuaga mwili wa Wangwe, aliyefariki dunia juzi kutokana na ajali ya gari, iliyotokea katika eneo la Pandambili, wilayani Kongwa, takriban kilometa 20 kutoka Dodoma mjini.

Shughuli ya kuuaga mwili wa Wangwe ambao ulikuwa umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, ilitawaliwa na kwikwi ya vilio vya wabunge, ndugu, jamaa na marafiki na wake wawili wa mbunge huyo, waliokuwa wameongozana na watoto watatu wa marehemu.

Kabla ya kuanza shughuli hiyo, zilitolewa salamu za rambirambi, na wa kwanza alikuwa Kiongozi wa upinzani Bungeni, Hamad Rashad, aliyemwelezea Wangwe kuwa ni kiongozi shupavu na mtetezi mkubwa wa watu wake wa Tarime.

Katika kulithibitisha hilo, Hamad Rashidi, alisema uamuzi wake kutaka kuwasilisha hoja binafsi inayozungumzia mgogoro wa ardhi katika jimbo lake, ni dhamira ya wazi ya namna mbunge huyo alivyokuwa akiwapigania watu wake.

Wa pili kutoa salamu za rambirambi alikuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwa niaba ya serikali.

Pinda alimwelezea Wangwe kuwa ni kiongozi mwenzao na Bunge limepoteza kiongozi stadi, akiwa ni mbunge wa tano kupoteza maisha, tangu Serikali ya Awamu ya Nne iingie madarakani.

Wengine waliopoteza maisha ni pamoja na Juma Akukweti (Tunduru), aliyefariki kutokana na ajali ya ndege, mkoani Mbeya na Salome Mbatia (Viti Maalumu) ambaye pia alifariki dunia kwa ajali ya gari.

Wengine ni Benedict Losurtia (Kiteto) na Amina Chifupa (Viti Maalumu), ambao walifariki dunia kutokana na maradhi.

Wa tatu kutoa salamu za rambirambi, alikuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye alianza kwa kusoma histori fupi ya maisha ya Wangwe.

Alisema Wangwe alizaliwa Julai 15, 1956, huko Tarime. Alimwelezea Wangwe kama kiongozi aliyejiamini na mtu madhubuti aliyetetea hoja zake hata kama hoja hizo zingesababisha kuhitilafiana na watu wengine.

Aidha, Spika alisema kifo cha Wangwe kimesababisha Bunge lipoteze mtu aliyekuwa akihitajika sana katika taifa lake na katika familia.

Alitumia fursa hiyo kuwaeleza kuwa Bunge, lilitoa ubani wa sh milioni tano kama rambirambi yake kutokana na kifo cha mbunge huyo.

Kwa upande wake kaka wa marehemu Wangwe, Profesa Samweli Wangwe, alimwelezea mdogo wake kuwa alikuwa kiungo mhimu katika familia.

Alisema alikuwa jasiri na mtetezi wa haki, hasa katika masuala ya kifamilia na kusisitiza kuwa mdogo wake alikuwa mtu mwenye moyo mweupe hata ilipotokea kukorofishana na kutetea ndugu zake.

Kabla ya shughuli hiyo ya kuaga, katika hali isiyokuwa ya kawaida, Spika Sitta, alishindwa kujizuia na kububujikwa machozi wakati akitoa taarifa za kifo hicho bungeni.

Kutokana na hali hiyo, Waziri Pinda na wabunge wengine waliokuwemo ukumbini humo, baadhi yao walifuta machozi na kusababisha kuwepo utulivu kwa muda kabla ya Bunge hilo kuahirisha shughuli zake jana.

“Waheshimiwa wabunge, kwa mara nyingine tena tumeangukiwa na msiba mzito wa mwenzetu Chacha Wangwe.

“Kifo cha mwenzetu kilitokea jana (juzi) usiku kwenye eneo la Pandambili, baada ya gari lake kupinduka na kugonga miti, hali iliyosababisha kifo chake papo hapo.

“Ndani ya gari hilo alikuwepo kijana mwingine alitwaye Deus Mallya…kwa kweli hali ilivyokuwa pale hatuna maelezo zaidi.

“Natoa pole kwa familia yake, CHADEMA na mwenyekiti wa chama hicho…kwa kuzingatia kanuni ya 149 naliahirisha Bunge, hadi saa sita mchana kwa ajili ya kuangalia namna ya kufanikisha hili.

“Hivyo basi, nawaomba wajumbe wa Kamati ya Uongozi…(kilio), na Tume ya Huduma za Bunge kukutana kwenye Ukumbi wa Spika,” alisema Sitta aliyekuwa akipangusa machozi yake kwa kitambaa cheupe huku akiliahirisha Bunge.

Aidha, kanuni ya 149 ya Bunge toleo la mwaka jana, inaeleza kwamba, endapo mbunge atafariki dunia wakati Bunge likiwa katika shughuli zake, Spika ataahirisha shughuli za Bunge kwa siku hiyo kwa ajili ya maombolezo.

Baada ya kukutana kwa Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge, Spika huyo aliwaeleza wabunge kuhusu utaratibu wa mazishi.

Alisema bungeni hapo kwamba mwili wa marehemu Wangwe utasafirishwa leo kuelekea kijijini kwao kilometa 12 kutoka Tarime mjini kwa mazishi.

Aidha, Ofisi ya Bunge imeshughulikia mazishi hayo ambapo ndege maalumu imekodiwa kwa ajili ya kubeba mwili wa marehemu na ndugu zake akiwemo mjane na watoto.

Alisema, wabunge 20 na maofisa wa Bunge watahudhuria mazishi hayo, ambapo watakwenda kwa ndege ya kukodi kesho asubuhi na kurudi baada ya mazishi.

Spika, alisema hatahudhuria mazishi hayo kwa sababu anasafiri kuelekea Malaysia kwenye uchaguzi wa viongozi wa Commonwealth Parliamentary Association (CPA), kwa kuwa ni miongoni mwa wagombea.

Kuhusu udhuru wa Naibu Spika, Anne Makinda, Sitta alisema naye atashindwa kwenda Tarime kwenye mazishi hayo, kwa kuwa Rais Kikwete atakuwa kwenye ziara ya kikazi wilayani Njombe.

“Kutokana na udhuru wetu, Bunge limemteua Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu inayoshughulikia Nishati na Madini, William Shelukindo, kuwa kiongozi wa msafara huo,” alisema Sitta.

Hata hivyo, alisisitiza uwiano katika uwakilishi huo, ambapo Bunge limezingatia jinsia na uwakilishi wa Bara na Visiwani.

Sitta pia, alisema uchunguzi wa kina utafanyika na taratibu za kipolisi zitafuatwa kuhusu mwili wa mbunge huyo.

Aidha, timu ya uchunguzi iliongozwa na daktari bingwa kuchunguza maiti kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, ndugu mmoja wa marehemu, ofisa wa Bunge na askari polisi.

Baadhi ya wabunge kutoka vyama mbalimbali vya siasa, wameelezea masikitiko yao kuhusu kifo cha Wangwe.

Kifo cha Wangwe, kilitokea juzi usiku baada ya gari alilokuwa akisafiria kuelekea Dar es Salaam kutoka Dodoma, kupinduka kwenye eneo la Pandambili, Kongwa mkoani hapa.

Akizungumza kwa masikitiko, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, alisema kifo hicho ni pigo kwa kambi ya upinzani bungeni.

Dk. Slaa ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, alisema licha ya kushtushwa na msiba huo wa ghafla, chama kimempoteza mtu aliyekuwa na misimamo.

Alisema, baada ya kupokea taarifa hizo kutoka kwa mtu ambaye hakumtaja, alikwenda kwenye eneo la tukio ili kuhakikisha alichosikia.

Alisema, kabla hajafika gari alilokuwamo lilisimamishwa na askari polisi walioweka kizuizi, hali iliyosababisha magari kutoka pande zote kusimama.

Baada ya kusimama kwa muda alifuatilia mazungumzo ya polisi na gari la upande wa pili, ndipo alipogundua kwamba gari lile lilibeba mwili wa Wangwe kwa ajili ya kuupeleka hospitali na kuuhifadhi.

“Nilipogundua hivyo, niliamua kugeuza gari nikaongozana na lile lililobeba maiti hadi Hospitali ya Mkoa hapa Dodoma.

“Hapo sasa ndipo niliamini kwamba aliyekuwa amekufa ni Wangwe…hapo ilikuwa saa saba usiku, kwa kweli hali ya gari lake inasikitisha,” alisema Dk. Slaa na kusisitiza kwamba kifo hicho ni pigo kwa CHADEMA, kambi ya upinzani na Bunge zima.

Alimwelezea Wangwe kuwa mtu mwenye misimamo, jasiri, aliyesimamia kila alichokiamini na kwamba alikuwa changamoto pia kwa wabunge wengine kutokana na hoja zake.

Kwa upande wake, Naibu Spika wa Bunge alisema kifo hicho ni pengo kwa Bunge na wabunge wengine kutokana na kauli zake, misimamo na maamuzi yake.

Hata hivyo alibainisha kwamba juzi ilikuwa awasilishe maelezo yake binafsi kuhusu hali ya wakazi wa Tarime, nguvu inayotumiwa na polisi kuwahamisha kwenye baadhi ya maeneo na tatizo sugu la mapigano ya koo na wizi wa mifugo hasa ng’ombe.

“Ijumaa iliyopita aliniletea maelezo yake nikamwambia ratiba haitamruhusu hadi jana (Jumatatu), ilipofika asubuhi aliniuliza vipi mheshimiwa nitapata nafasi ya kutoa maelezo yangu? Nikamwambia tumsubiri Spika anaweza kukupa muda.

“Kweli Spika akasema muda utapatikana baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, kuhitimisha hoja ya bajeti ya wizara yake. Hapo napo Spika alimpa dakika 20, nikamwambia ‘hang around’ yaani asiende mbali nafasi imepatikana.

“Nadhani kifo chake kilifika kwa kweli maana saa 12, Spika aliwaagiza maofisa wa Bunge kumtafuta Chacha Wangwe ili muda utakapofika wa kutoa maelezo yake, afanye hivyo lakini hakupatikana,” alisema Naibu Spika huyo.

Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Susan Lyimo (CHADEMA), alimwelezea Wangwe kuwa ni mtu aliyesimamia alichokiamini hata kama anapingwa na watu wengi.

“Wangwe namuelezea kama mtu mwenye misimamo, asiyeogopa kupingwa kwa kila alichoamini. Tumempoteza mtu muhimu. Ni pengo kubwa kwa upinzani na Bunge pia,” alisema Lyimo.

Naye Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema amepokea kwa mshituko mkubwa kifo cha Wangwe, na kuongeza kuwa kifo hicho ni pigo kwa chama chake kwani kimempoteza kiongozi mwenye msimamo.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka nchini Afrika Kusini alikokwenda kwenye ziara ya kikazi, Mbowe alisema amelazimika kukatiza ziara hiyo na kurejea nchini ili kuwahi mazishi ya Wangwe.

7 comments:

Anonymous said...

Hi !.
You may , perhaps curious to know how one can reach 2000 per day of income .
There is no need to invest much at first. You may begin to get income with as small sum of money as 20-100 dollars.

AimTrust is what you thought of all the time
The company incorporates an offshore structure with advanced asset management technologies in production and delivery of pipes for oil and gas.

It is based in Panama with affiliates everywhere: In USA, Canada, Cyprus.
Do you want to become an affluent person?
That`s your chance That`s what you desire!

I feel good, I began to take up real money with the help of this company,
and I invite you to do the same. It`s all about how to select a correct companion who uses your funds in a right way - that`s the AimTrust!.
I earn US$2,000 per day, and my first investment was 500 dollars only!
It`s easy to join , just click this link http://firafowevo.the-best-free-web-hosting.com/mewijaw.html
and go! Let`s take our chance together to become rich

Anonymous said...

Hi !.
You may , probably curious to know how one can collect a huge starting capital .
There is no initial capital needed You may begin to get income with as small sum of money as 20-100 dollars.

AimTrust is what you need
The company represents an offshore structure with advanced asset management technologies in production and delivery of pipes for oil and gas.

It is based in Panama with structures around the world.
Do you want to become a happy investor?
That`s your chance That`s what you wish in the long run!

I feel good, I started to get income with the help of this company,
and I invite you to do the same. It`s all about how to choose a correct partner who uses your savings in a right way - that`s the AimTrust!.
I earn US$2,000 per day, and what I started with was a funny sum of 500 bucks!
It`s easy to join , just click this link http://idagodyf.100freemb.com/gapalo.html
and lucky you`re! Let`s take this option together to become rich

Anonymous said...

Hello !.
You re, I guess , probably curious to know how one can reach 2000 per day of income .
There is no need to invest much at first. You may begin to receive yields with as small sum of money as 20-100 dollars.

AimTrust is what you thought of all the time
The firm incorporates an offshore structure with advanced asset management technologies in production and delivery of pipes for oil and gas.

Its head office is in Panama with structures around the world.
Do you want to become really rich in short time?
That`s your choice That`s what you really need!

I feel good, I started to take up income with the help of this company,
and I invite you to do the same. It`s all about how to select a correct partner utilizes your savings in a right way - that`s it!.
I make 2G daily, and my first investment was 500 dollars only!
It`s easy to start , just click this link http://olyhijimiq.s-enterprize.com/paxaxet.html
and lucky you`re! Let`s take this option together to get rid of nastiness of the life

Anonymous said...

Hi there!
I would like to burn a theme at here. There is such a nicey, called HYIP, or High Yield Investment Program. It reminds of ponzy-like structure, but in rare cases one may happen to meet a company that really pays up to 2% daily not on invested money, but from real profits.

For several years , I make money with the help of these programs.
I don't have problems with money now, but there are heights that must be conquered . I get now up to 2G a day , and I started with funny 500 bucks.
Right now, I managed to catch a guaranteed variant to make a sharp rise . Turn to my blog to get additional info.

[url=http://theblogmoney.com] Online investment blog[/url]

Anonymous said...

Glad to materialize here. Good day or night everybody!

We are not acquainted yet? It’s easy to fix,
my parents call me Nikolas.
Generally I’m a social gmabler. for a long time I’m keen on online-casino and poker.
Not long time ago I started my own blog, where I describe my virtual adventures.
Probably, it will be interesting for you to find out how to win not loose.
Please visit my blog. http://allbestcasino.com I’ll be glad would you find time to leave your comments.

Anonymous said...

Отличная статья! большое спасибо автору за интересный материал. Удачи в развитии!!!
http://www.miriadafilms.ru/
nyanje.blogspot.com

Anonymous said...

Почему регистрация не работает ?