Monday, August 25, 2008

Hotuba ya Kikwete Bungeni yaota mbawa


Ule mpango wa Bunge kuijadili hotuba ya rais jakaya Kikwete, aliyoitoa Alhamisi iliyopita, umefutwa. Mpango huo mumefutwa kutokana na kile kilichoelezwa kuwa hotuba hiyo bado haijakamilika kutengenezwa.
Taarufa zinasema kwua wakati rais anahutubia, aliongeza maneno mengi sana ambayo hayakuwamo kwenye nakala ya hotuba iliyokuwa imechapishwa. Kwa hiyo, kilichofanyika ni kuongeza maneno hayo aliyoyasema, ambayo yapo nje ya hotuba na kuipeleka Ikulu ili ikahakikiwe.
Lakini habari nyingine zinasema kwua hotuba hiyo imezuiliwa baada ya serikali kuona msimamo wa wananchi uko kinyume na kilichosemwa na rais. Pia inadaiwa kuwa maneno ya Spika Sitta, aliyoyatoa baada ya Kikwete kumakliza hotuba yake, yaliyokuwa na mwelekeo wa kuisema serikali, nayo yamechangia kwa serikali kuweka shinikizo la kuzuia hotuba hiyo kujadiliwa na wabunge.
Inaelekea pia serikali imetishwa na msimamo na maoni ya wananchi kuhusisna na hotuba hiyo, na kuhofia kuwa iwapo wabunge watapata nafasi ya kuijadili, hiyo itakuwa ni fursa kwa wabunge ‘mafyatu’ kuilipukia serikali bila hofu

No comments: