Thursday, November 13, 2008

BREAKING NEWS: Jeetu Patel apata dhamana, arudishwa rumande

Mfanyabiashara Jeetu patel amerudishwa rumande katika gereza la Keko licha ya jana kupata dhamana.
Jeetu na wenzake wanashitakiwa katika kesi ya wizi wa fedha za EPA.
Taarifa kutoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zinaeleza kuwa Jeetu alipata dhamana katika kesi moja lakini alirudishwa ndani kwa sababu anakabiliwa na kesi nyingine tatu za wizi wa fedha za EPA ambazo hajapata dhamana.
Wafanyabishara wengine watatu, Bahati mahenge, Manase Mwakale na mke wake, Eddah Mwakale, ambao jana walikosa dhamana, jana walipata bahati na mtende baada ya mahakama kukuzikubali hati walizowasilisha mahakamani hapo hivyo kuachiwa kwa dhamana.
Mfanyabishara mwingine, Johnson Lukaza, pamoja na mmoja wa watumishi wa BoT ambao wanakabiliwa na kesi kama hizo, nao waligonga mwamba katika harakati zao za kusaka dhamana na hivyo kurejeshwa rumande.

No comments: