Friday, November 7, 2008

BREAKING NEWS: Neti ya EPA yatanuka

Neti inayowadaka watu wanaotuhumiwa kujipatia fedha kwa njia za ulaghai na wizi kutoka akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) imetanuka na kudaka wanne zaidi leo.
Habari kutoka Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu zinapasha kuwa watumishi wanne wa benki Kuu, ambayo ndiko akaunti hiyo ilikuwepo wakati bilioni 133 zilipochotwa na wajanja, wametinga mahakamani hapo.
kama wengine walioshitakiwa juzi na jana, watumishi hao nao wanashitajkiwa kwa makosa ya wizi wa fedha za EPA. Zikipatikana habari zaidi tutaendelea kuziweka hapa, endelea kutembelea.

No comments: