Friday, December 5, 2008

Serikali yatangaza mapambano na Mengi

Kauli iliyotolewa na Reginald Mengi siku mbili zilizopita imezua malumbano makali baina yake na serikali ambayo yasipoangaliwa yanaweza kuzusha migogoro isiyo na maana.
katika kile kinachoonekana kujitu tuhuma za Mengi kuwa anatishiwa na 'Wziri kijana' anayeongoza 'wizara nyeti'. Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, leo amempa Mengi siku saba kuthibitisha madai yake kuwa anatishiwa.
Waziri Masha amesema iwapo Mengi atashindwa kuthibitisha hivyo baada ya siku sana "sheria itachukua mkondo wake."
Kwa kauli hiyo, ni dhahiri kuwa serikali inaweza kumfungulia Mengi mashitaka ingawa hadi sasa ni vigumu kutabiri yatakuwa mashitaka gani hasa.
Aidha, masha alisema kuwa ameliagiza Jeshi la Polisi kuchunguza vitisha alivyopatiwa Mengi. Amemtaka mfanyabishara huyo anayemiliki vyombo vingi vya habari kuziwasilisha meseji za vitisho anazodai kutumiwa.
Siku mbili zilizopita, Mengi aliwaeleza waandishi wa habari kuwa kuna waziri alikuwa amekula njama, akitaka yeye (Mengi) amambikiziwe kodi kubwa, ili akishindwa kuilipa afilisiwe kama ilivyotokea kwa tajiri mmoja huko Urusi.
Aidha, mengi aliwaonyesha waandishi wa habari baadhi ya meseji za vitisho alivzotumiwa

No comments: