Tuesday, December 9, 2008

Waziri Chibulunje apata ajali

naibu Waziri wa Miundombinu, Ezekia Chibulunje amepata ajali leo mkoani Singida baada ya gari lake kupinduka mara tatu baada ya tairi kupasuka. Walioshuhudia ajali hiyo wanasema Chibulunje, ambaye alipata mshituko wa moyo na majeraha madogo madogo, aliokolewa na mifuko ya hewa (airbags).
Ajakli imetokea eneo la Misugha, yapata kilometa 45 kutoka Singida mjini. Alikuwa ndio kwanza amewasili mkoani humo wka ajili ya ziara ya siku nne ya kukagua barabara akitokea mkoani Manyara. Kwenye gari lake alikuwamo na dereva na Meneja wa tanroads mkoa wa Singida ambao nao wamepata majeraha madogo na kutibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani

No comments: