Tuesday, November 10, 2009

Rostam aendeleza mjadala wa Richmond

Mbunge wa Igunga bado hajakubaliana na ripoti ya Richmond na sasa anataka iundwe tume maalum ya majaji kulichunguza suala hilo upya. Anasema iwapo tume hiyo ya majaji itabaini kuwa amehusika wka namna yoyote katika kashfa hiyo, basi afukuzwe kwenye nyadhifa zote alizonazo ndani ya chama na kisha kuchukuliwa hatua za kisheria.
Rostam amezidi kusisiza kuwa ripoti ya Richmond iliyowasilishwa bungeni ya mwenyektii wake Dk Mwakyembe kuwa ilijaa uongo dhidi yake.
Je, atafanikiwa katika jitihada hizi mpya za kutaka kujitakasa?

No comments: