Saturday, November 29, 2008

JK apangua Makatibu Wakuu

RAIS Kikwete, amefanya mabadiliko ya makatibu wakuu na naibu katibu wakuu wa wizara 13 na Gray Mgonja wa fedha amekwenda likizo ya kustaafu.

Makatibu kadhaa na manaibu wamehamishwa na wengine wapya wameteuliwa baada ya wengine kustaafu.

Mabadiliko hayo yamegusa wizara kadhaa ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Ulinzi, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki na nyingine tisa.

Kikwete amewateua wasaidizi wake wawili wa Ikulu kuwa naibu makatibu wakuu wa wizara.

Alhaj Ramadhan Kijja anakuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Uchumi, Dk Florens Turuka Katibu Mkuu wa Habari Utamaduni na Michezo, Joyce Mapunjo anakuwa Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara na Andrew Nyumayo anakuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Kabla ya uteuzi Kijja alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Uchumi, Dk Turuka alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Joyce Mapunjo alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Miundo Mbinu na Andrew Nyumayo alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu.

Makatibu wakuu waliohamishwa Wizara ya ni pamoja na Paniel Lyimo aliyekuwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Masoko sasa anakwenda Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Ladislaus Komba amehamishiwa Maliasili na Utalii, Kijakazi Mtengwa amepekewa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana na Mohamed Muya amehamishiwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.

Awali Dk Ladislaus Komba alikuwa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Kijakazi Mtengwa alikuwa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo ambapo Mohamed Muya alikuwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Makatibu wakuu wengine waliohamishwa ni Patrick Rutabanzibwa amepangiwa Wizara ya Mambo ya Ndani kutoka Maji na Umwagiliaji, Dk Sergomena Tax - Afrika Mashariki akitokea Viwanda, Biashara na Masoko, Wilson Mukama anakwenda Maji na Umwagiliaji kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, pamoja na Blandina Nyoni anayekwenda Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii akitokea Maliasili na Utalii.

Naibu makatibu wakuu wapya walioteuliwa ni pamoja na Dk. Philip Mpango- Fedha na Uchumi, Celestine Gesimba - Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Seti Kamuhanda - mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Dk Mpango alikuwa msaidizi wa rais (Uchumi) Ikulu, Seti Kamuhanda pia alikuwa msaidizi wa rais (Hotuba) Ikulu na Gesimba alikuwa Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.

Fanuel Mbonde aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Thursday, November 27, 2008

NEWS ALERT: Hatma ya akina Mramba kesho

Hatma ya basil Mramba na mwenzake Daniel Yona kuhusiana na dhamana yao, itajulikana kesho baada ya leo Mahakama Kuu kulikubali ombi lao la kukata rufaa dhidi ya masharti magumu ya dhamana waliyowekewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wanafunzi waigomea serikali

Wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma vilivyofungwa, wamegoma kuyakubali masharti yaliyotolewa na serikali. Serikali iliagiza uongozi wa vyuo vikuu vya umma nchini, kuwabagua wanafunzi kati ya wale wanaokubaliana na mfumo wa uchangiaji wa elimu ya juu na wale wasiokubaliana nao.

Baada ya hapo, wanafunzi hao walitakiwa kuandika barua ya kueleza kukubaliana kwao na mfumo huo na kujaza fomu maalum, ambayo itakuwa kama mkataba baina yao na uongozi wa vyuo kuhusiana na makubaliano hayo.

Akizungumza leo, rais wa serikali ya Wanafunzi wa UDSM, Anthony Machibya, alisema kuwa uongozi wa UDSM ulishawapatia masharti hayo na wao wameyakataa.

Akizungumza kwa niaba ya marais wenzake saba kutoka vyuo sana vya umma vilivyofungwa kutokana na migomo ya wanafunzi, Machibya alisema kuwa hakuna atakayeandika barua wala kujaza fimu kama sharti la kumtaka arejee chuoni.

Alisisitiza kuwa wanafunzi watarejea chuoni iwapo tu serikali itaondoa mfumo wa uchangiaji wa elimu ya juu uliopo.

Alisisitiza kuwa iwapo serikali haitotekeleza madai yao, hawatarejea vyuoni na iwapo watarejea, wataendelea na migomo hadi sera hiyo ya uchangiaji iondolewe.

Lakini, mgawanyiko baina ya wanafunzi hao kwani wale wanaounda umoja wa viongozi wa vyuo vya umma, (Tahliso) wenyewe wameonekana kupingana na wenzao.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Tahliso, Nicholaus Mtindya, alisema kuwa umoja wao haukubaliani na mgomo uliofanywa na wanafunzi hivi karibuni.

Alisema kuwa hawakubaliani na mgomo huo kwa sababu Tahliso tayari ilishaongea na serikali na wakaipatia miezi miwili ili iyashughulikie madai yao.

Anasema kuwa miezi miwili haijapita kwa sababu kikao hicho kilifanyika Oktoba 23 na inashangaza kwa nini wanafunzi waligoma kabla ya kumalizika kwa muda huo.

Aidha, anasema kuwa mgomo uliofanywa na wanafunzi hivi karibuni ulishinikizwa na baadhi ya watu kwa maslahi yao binafsi. Hakufafanmua.

Wednesday, November 26, 2008

Waziri awatembelea akina Mramba gerezani

Waziri wa mambo ya Ndani, Lawrence Masha, jana alifanya ziara ya ghafla katika gereza la Keko ambako mawaziri waandamizi wawili wa zamani wamehifadhiwa baada ya kukosa dhamana katika kesi yao ya kutumia vibaya madaraka yao inayowakabili.
mawaziri hao wa zamani, basili Mramba na Daniel Yona walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana, wakikabiliwa na jumla ya mashitaka 13 ya kutumia vibaya madaraka yao, kuhusiana na mkataba wa kampuni ya Alex Steward Asseyers, iliyoingia mkataba wa kufanya ukaguzi wa biashara ya dhahabu.
Masha alifika gerezani hapo kinyemela kwani alikuwa anatumia gari binafsi, akiwa amevaa mavazi ambayo yanaweza kuhesabiwa kuwa si rasmi kwa kazi kwa mtu mwenye hadhi yake.
Maofisa wa Magereza hiyo walikataa kuzungumzia suala hilo lakini Masha mwenyewe amethibitisha kwua kweli alikwenda katika gereza hilo.
Alipoulizwa ziara yake hiyo ilikuwa na lengo gani, Masha alisema ilikuwa ni ziara ya kikazi, ingawa alipotakiwa kueleza kwa nini anafanya ziara ya kikazi akitumia gari binafsi, alishindwa kufanya hivyo.
Wakati huo huo, Mawakili wa Yona na Mramba walirejea mahakamani hapo wakiwa na barua ya kuomba kupatia mwenendo wa kesi hiyo ili wakate urfaa Mahakama Kuu kupinga masharti magumu ya dhamana waliyowekwa wateja wao.
hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Hezron Mwankenja, amewaamuru makarani kuiabndaa nyaraka hiyo haraka ili mawakili hao watimize dhamira yao.

Tuesday, November 25, 2008

BREAKING NEWS: Mapapa kortini

Mawaziri wawili wa zamani, basil Mramba na Daniel Yona. leo hii wanalala katika gerezz la Keko baada ya kutekeleza matakwa ya dhamana kutokana na kesi ya kutumia vibaya madaraka yao na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Shilingi bilioni 11.752.
Mawaziri hao wa zamani waliburuzwa katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu leo asubuhi na kusomewas jumla na mashitaka 13 yanayohusiana na mkataba wa kampuni ya kufanya ukaguzi wa dhahabu ya Alex Atewart Asseyers.
Wanadai wakuwa walitumia madaraka yao vibaya na kuingia mkataba huo kinyume cha sheria kadhaa na kuisababishia serikali hasara hiyo.
Wakati makosa hayo yanatoka, Mramba alikuwa waziri wa Fedha na Yona alikuwa waziri wa Nishati na Madini katika serikali ya wamu ya tatu.
hali ilikuwa tete mahakamani hapo jana kwani watu wengi walifika baada ya taarifa kuenea mjini kuwa mawaziri hao wamefikishwa mahakamani hapo.
Walifikishwa wakiwa katika shangingi la takukuru na kukaa katika shangingi hilo kwa muda wa takriban saa mbili kabla ya kupandishwa kizimbani.
Ingawa walionekana kuwa watulivu, lakini Yona alikuwa na kazi ya kujifuta jasho katika kipindi chote alichokuwamo ndani ya mahakama.
Wakati wanaondoka, wananchi waliwatolea uvivu na kuwazomea wakiwaita wezi... wezi... wezi...
Katika masharti ya dhamana waliyoshindwa kuyatekeleza, Mawaziri hao wa zamani walitakiwa kuweka kiasi cha shilingi bilioni 3.9 taslim kila mmoja, kuwasilisha pasi zao za kusafiria na kuwa an wadhamini wawili wanaoaminika.
kesi hiyo itatajwa tena mwezi ujao na upelelezi wake bado unaendelea.

Saturday, November 22, 2008

Serikali 'yafukuza' wanafunzi vyuo vikuu

Serikali imesema itawafukuza wanafunzo wote wa vyuo vikuu vya serikali nchini ambao hawakubalini ya sera ya uchangiaji wa elimu ya juu.

Hayo yalitangazwa jana na Naibu waziri wa Elimu ya Juu, Gaudentia Kabaka. Kabaka alisema kuwa serikali imeuagiza uongozi katika vyuo vikuu vya uume kote nchini kuwachanganua wanafunzi wanaokubalina na sera hiyo na wale wanaoipinga.

Alisema baada ya kufanya hivyo, wale wanaokubaliana warudishwe masomoni haraka na wale wanaoipinga sera hiyo wabakie majumbani kwao.

Alisema hivi sasa serikali haina uwezo wa kugharamia ada za wanafunzi wote kwa asilimia 100 kama ambavyo wanafunzi hao wanavyodai.

Alisema bajeti ya kusaidia wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka huu ni Sh bilioni 117 na iwapo serikali ikitekeleza madai ya wanafunzi kuwa serikali ilipie ada kwa asilimia 100, zitahitajika Sh bilioni 163 na serikali haina uwezo wa kupata hiyo ziada ya Sh bilioni 52.

Alisema mpango wa serikali kuwakopesha ada wanafunzi kwa mujibu wa uwezo wao, umewezesha idadi ya wabafunzi wanaonufaika kufikia 60,000 lakini chini ya utaratibu unaodaiwa na wanafunzi, kwa kutumia kiwango cha bajeti iliyopo, idadi ya wanafunzi watakaonufaika haitafikia 40,000.

Tuesday, November 18, 2008

Serikali yakamata wanafunzi

Jumla ta wanafunzi saba wa vyuo vikuu nchini walikuwa wamekamatwa hadi jana mchana kutokana na kuhusishwa na migomo iliyosababisha kufungwa kwa vyuo vikuu kadhaa vya umma.
Kamatakatama hiyo ya Polisi ilianza Jumamosi ambapo wanafunzi wawili, Julius Mtatiro (kiongozi wa zamani wa daruso) na Odong Odwar (mwanafunzi rais wa Uganda ambaye anaelezwa kuwa ni mwanaharakati nzuri), walikamatwa na kuanza kuhojiwa. lakini katika hali ya kushangaza, Polisi bado haitaki kukiri kuwa inawashikilia wanafunzi hao.
Waliokamatwa wote ni viongozi wa serikali za wanafunzi katika vyuo wanavyosoma.
Wengine watano walikamatwa jana. Hao ni Rais wa DARUSO, Anthony Machibya, waziri mkuu Benedicto Raphael na waziri wa elimu wa UDSM, Suleman Ally.
Wengine waliokamatwa ni rais wa serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi za Afya Muhimbili, Godbless Charles na rais wa serikali ya wanafunzi wa Chuo Cha Ardhi, Anthony Massawe.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, amesema kuwa yeye hana taarifa za kukamatwa kwa vijana hao ingawa taarifa za uhakika zimeenea mjini kuwa baadhi yao walikamatwa katika kituo cha cha Channel Ten wakati walipokuwa wanarekodi moja ya vipindi vya mahojiano vinavyoandaliwa na kurushwa na kituo hicho.

Sunday, November 16, 2008

Mgomo wa walimu-Kesho ndio kesho

Juhudi za serikali kuhakikisha mgomo wa walimu hautokeo, zimeshindikana. walimu wamethibitisha kuwa liwake jua inyeshe mvua, kesho lazima watagoma.
rais wa Chama Cha walimu, Gratian Mukoba, amesema kuwa baada ya hukumu ya Mahakama ya Rufaa mapema wiki hii, hakuna tena kunachoweza kuwazuia walimu nchini kugoma.
Aidha, Mukoba anasema vitisho na ahadi zinazotolewa na serikali hivi sasa zinathibitisha kuwa madai ya walimu ni ya kweli na halali.
Kupitia kwa katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, serikali juzi ilitishia kuwa mwalimu atakayegoma hatolipwa mshahara. Pia, waziri wa TAMISEMI, Celina Kombani, naye amepiga mkwara akiwa humo Mwanza kuwa walimu waliowasilisha nyaraka za kughushi katika madai yao watafikishwa mahakamani.
Luhanjo alisema katika taarifa yake kuwa Serikali imekwenda mahakamani kuomba mgomo huo usitishwe na Chama cha walimu kimeshapelekewa wito wa kuitwa mahakamani.
Lakini, Mukoba anasema kuwa wao bado hawajapata wito huo, na hata kama wakiupata hauwezi kuwafanya waahirishe mgomo wao wka sababu vitu hivyo viwili havihusiani.
Anasema kuwa walimu walishajiandaa kugoma tangu siku nyingi na hivi sasa wanaisubiri kesho ifike kwa hamu waonyeshe kile ambacho wana uwezo kukifanya.
Mukoba alisema CWT haiwezi kuvutwa na ahadi ya serikali kuwa fedha zimeanza kusambazwa wilayani kwa ajili ya malipo ya walimu kwa sababu wao madai yao si fedha kusambazwa wilayani, bali walipwe malimbikizo ya madai yao.
Walimu wanasema kuwa wanadai zaidi ya Sh bilioni 16 kama malimbikizo ya posho za likizo, usafiri, matibabu na madai mengineyo lakini serikali inasema karibu nusu ya madai hayo ni feki.

Friday, November 14, 2008

Mahakimu Kesi za EPA 'wagoma'

Mahakimu wanaosikiliza kesiz a watuhumiwa wa wizi wa mabilioni ya fedha za EPA, leo wasitisha kwa muda kusikiliza kesi hizo, na 'kuandamana' hadi Mahakama Kuu kuwasilisha malalamiko yao.
Malalamiko yao yanahusisha usalama mdogo na kupatiwa vitendea kazi. Msajili wa Mahakama Kuu kimsingi alikubaliana na madai hayo na kuahidi kuwa kuanzia sasa mahakimu hao watapatiwa magari kwa ajili ya kuwachukua na kuwarejesha majumbani mwao.
Walipofika asubuhi leo, walisikiliza kesi moja ambapo waliwapatia dhamana Johnson Lukaza na mdogo wake na kisha kuahirisha usikilizaji wa kesi, ili kwenda Mahakama Kuu kuwasilisha malalamiko yao.
Huko walionana na jaji Mfawidhi, ambaye aliwapeleka kwa msajili walikowasilisha malalamiko yao.
Baada ya kurejea, waliskiliza kesi moja inayomkabili jeetu Patel na wenzake na kumkubalia dhamana na kisha wakaingia tena kwenye kikao Mahakamani hapo pamoja na msajili.
baada ya kikao hicho, hivi sasa mahakimu hao wanaendelea kusikiliza kesi nyingine ya Jeetu huku wafanyakazi wa BoT ambao nao wameshitakiwa wakisubiri na wao zamu yao ya kusikiliza maombi yao ya rufaa.
lakini taarifa nyingine zinadai kuwa malalamiko ya mahakimu hao yanahisuska pia mambo ya fedha.
Mahakimu wanadai kuwa waendesha mashitaka katika kesi hizo wanalipwa posho maalum ambayo wao (mahakimu) hawapewi).
Pia wanadai kuwa kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hizo, waendesha mashitaka walipatiwa mafunzo maalum kuhusu kesi hizo wakati wao hawakupatiwa mafunzo yoyote.
lakini kubwa zaidi, habari zimeenea mitaani kuwa wanahusika katiak kesiz a EPA wamekuwa wakihongwa kiasi kikubwa cha fedha. nadhani hatua hii ya mahakimu ni kutaka kujionyesha kuwa wao si baadhi ya hao wanaodaiwa kuhongwa

Kivuko cha Mgogoni chaota mbawa

Serikali leo imeshindwa kuzindua kivuko cha Magogoni. Ingawa waziri wa Miundombinu alishaandaliwa, na kufikishwa kilipo kivuko hicho, lakini shughuli za kukizindua kwa ajili ya safari za majaribio haikufanyika wka maenelezo kuwa bado kuna mambo ya kiufundi hayajakamilika.
nakihusisha habari hii na ile taarifa ya rais Kikwete kupelekwa kuzindua daraja ambalo halijakamilika huko Ruvuma, napata wasi wasi kuhusiana na umakini wa watendaji wetu serikalini

Magogoni yapata kivuko kipya

Kivuko kipya cha Magogoni jijini Dar es Salaam kinazinduliwa leo. Kivuko hicho kikubwa, chenye uwezo wa kubeba watu 2,000 na tani nyingi za mizigo kwa wakati mmoja kinatarajiwa kuwa mkombozi kwa wakazi wa Kigamboni, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisumbuka sana kutokana na matatizo ya usafiri.
Tutawaletea taarifa zaidi baadaye baada ya uzinduzi

Thursday, November 13, 2008

BREAKING NEWS: Jeetu Patel apata dhamana, arudishwa rumande

Mfanyabiashara Jeetu patel amerudishwa rumande katika gereza la Keko licha ya jana kupata dhamana.
Jeetu na wenzake wanashitakiwa katika kesi ya wizi wa fedha za EPA.
Taarifa kutoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zinaeleza kuwa Jeetu alipata dhamana katika kesi moja lakini alirudishwa ndani kwa sababu anakabiliwa na kesi nyingine tatu za wizi wa fedha za EPA ambazo hajapata dhamana.
Wafanyabishara wengine watatu, Bahati mahenge, Manase Mwakale na mke wake, Eddah Mwakale, ambao jana walikosa dhamana, jana walipata bahati na mtende baada ya mahakama kukuzikubali hati walizowasilisha mahakamani hapo hivyo kuachiwa kwa dhamana.
Mfanyabishara mwingine, Johnson Lukaza, pamoja na mmoja wa watumishi wa BoT ambao wanakabiliwa na kesi kama hizo, nao waligonga mwamba katika harakati zao za kusaka dhamana na hivyo kurejeshwa rumande.

NEWS UPDATE: DUCE nacho chafungwa

Habari zilizopatikana mchana huu zimethibitisha kuwa Chuo Kishiriki cha Chuo Kikuu cha dar es Salaam cha Ualimu (DUCE) nacho kimefungwa kwa muda usiojulikana.
hatua hiyo imekuja siku moja tu baada ya kufungwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kutokana na mgomo wa anafunzi.
Habari kutoka katika chuo hicho kilichop maeneo ya Chang'ombe jijini Dar es Salaam, zinaeleza kuwa uongozi wa chuo ulitoa trangazo la kukifunga chuo hicho leo asubuhi, wakati wanafunzi wanaingia katika siku ya pili ya mgomo wao.
Tangazo hilo liliwataka wanafunzi kuwa wameshaondoka chuoni hapo ifikapo saa 7 mchana. Tayari magari ya askari Polisi wa doria na wale wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia, yalionekana katika maeneo ya chuo hicho, wakati wanafunzi wakifungasha mizigo yao tayari kwa kuondoka.
Hata hivyo, wanafunzi hao walisema kuwa kufunga chuo si suluhisho la tatizo hilo kwani watakaporudishwa chuoni hapo wataendelea na mgomo wao hadi wapate haki yao.
Taarifa zaidi kutoka Morogoro zinaeleza pia kuwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) nao wanapanga kugoma kuwaunga mkono wenzao wa UDSM.
Wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu nchini wapo katika mgogoro na serikali wakipinga sera ya uchangiaji wa elimu ya juu, wanayodai kuwa inawanyanyasa na kuwabagua watanzania kutokana na uwezo wao kiuchumi.
hata hivyo, serikali inaitetea sera hiyo, ikisema kuwa inawezesha kwuasaidia wanafunzi kulingana na uwezo wa wazazi wao.

Wednesday, November 12, 2008

Chuo Kikuu chafungwa

Baraza la Chuo Kikuu cha dar es Salaam limekifunga chuo hicho kwa muda usiojulikana baada ya wanafunzi kugoma kwa siku tatu mfululizo.
Tangazo la kufungwa kwa chuo hicho limetolewa leo asubuhi na kubandikwa katika mbao kadhaa za matangazo chuoni hapo.
Jana, waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi, Prof. Jumanne maghembe aliwataka wanafunzi hao kuachana na mgomo huo na kurejea madarasani leo. Kwa upande wake, uongozi wa Chuo Kikuu uliwataka wanafunzi hao kuwa madarasani leo saa moja asubuhi.
Lakini wanafunzi hao waliendelea na mgomo wao ambao walisema hautakuwa na mwisho hadi madai yao yasikilizwe na serikali.
Wanafunzi hao wanataka kuondolewa kwa sera ya kuchangia elimu inayotoa maelekezo kwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutoa mikopo kwa kiwango kulingana na hali za waombaji.
Wanafunzi wanasema kigezo hicho hakitumiki ipasavyo, ni cha unyanyasaji na kinawabagua wanafunzi wasio na uwezo.
Walianza mgomo wao Jumatatu na kwa mujibu wa sheria, Chuo kinalazimika kufungwa iwapo wanafunzi watagoma kwa siku tatu mfululizo.

Tuesday, November 11, 2008

NSSF yamshitaki Dk. Masau

Mfuko wa hifadhi ya Jamii (NSSF) umemburuza mahakamani Mkurugenzi wa Taasisi ya Tiba ya Moyo Tanzania (THI), Dk. Ferdinand Masau kwa madai kuwa kushindwa kulipa michango ya wafanyakazi wake.

Kwa mujibu wa hatu ya mashitaka ya kesi hiyo iliyofunguliwa katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu, dar es salaam, Dk. Masau ameshindwa kwuasilisha michango ya wafanyakazi wake inayofikia zaidi ya sh milioni 79.

Kesi hiyo, iliyofunguliwa na wakili wa NSSF, Crispine Meela, ipo mbele y Hakimu Mkazi Richard Kabate.

Hata hivyo, Dk masau hajapelekewa wito wa kuitwa shaurini ingawa kesi hiyo inajulikana kama ya jinai kwa mujibu wa sheria ya NSSF.

Hati ya mashitaka inaeleza kuwa Dk masau amekiuka kifungu cha 72 (1) (d) cha sheria ya NSSF namba 28 ya 1997. Inadaiwa kuwa Dk. Masau, akiwa kama kiongozi wa taasisi iliyosajiliwa na NSSF na kupewa namba ya uanachama 678171, alishindwa kuwasilisha michango ya watumishi wake kati ya Mei 2004 na November 2007.

Kwa mujibu wa sheria hiyo, mtu anayepatikana na hatia ya kukiuka kifungu hicho anaweza kuhukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka miwili au faini ya sh 100,000.

Monday, November 10, 2008

Wengi zaidi washitakiwa kwa EPA

WATU walioshitakiwa kwa makosa yanayohusiana na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu (BoT) sasa wamefikia 20 baada ya watuhumiwa wengine watatu kufikishwa katika Mahakaha ya hakimu Mkazi Kisutu leo.

Waliofikishwa mahakamani hapo ni wafanyabiashara ndugu; Ajar Sryakant Somani na Jai Chhotalal Somani. Pamoja nao alikuwemo pia Mwesiga Lukaza, ambaye aliunganishwa kwenye kesi ya ndugu yake, Jonson Lukaza. Katika kesi hiyo wanatuhumiwa kujipatia kwa njia ya udanganyifu kiasi cha sh. Bil 6.3 kutoka katika akaunti hiyo.

Kama kawaida, watu walikuwa wengi mahakamani hapo. Watu wengine walifika mapema sana saa 1 asubuhi baada ya taarifa kuenea jijini Dar es Salaam kuwa mmoja wa wafanyabiashara maarufu jijini, leo angefikishwa mahakamani hapo kuhusiana na kesi hizo.

Ndugu hao, Ajar Sryakant Somani na Jai Chhotalal Somani) wanatuhumiwa kujipatia kwa njia ya udanganyifu kiasi cha sh bil 5.91.

Katika moja ya matukio ya jana katika kesi hiyo, Chhotalal Somani alishindwa kujizuia na kububujikwa na machozi ndani ya mahakama wakati akisubiri kusomewa mashitaka.

Akiwasomea mashitaka, Wakili wa Serikali, Fredrick Manyanda aliiambia mahakama hiyo iliyokuwa mbele ya hakimu mkazi Victoria Nongwa kuwa ndugu hao, Sryakant na Chhotalal, waliiba fedha hizo mnamo Septemba 2, 2005.

Manyanda alidai kuwa walijipatia fedha hizo baada ya kughushi nyaraka wakionyesha kuwa wamenunua deni la kampuni ya nje iitwayo Society Alsacienne Construction de Machines Textiles. Watu hao wana kampuni yao iliyosajiliwa nchini ya Liquidity Service Limited, ambayo waliitumia kama iliyonunua deni hilo.

Mwesiga Lukaza yeye alifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Euphemia Mingi na kuunganishwa kwenye kesi ya ndugu yake.

Wanadaiwa kuwa nao waliwasilisha nyaraka za kughushi, wakidai kuwa kampuni ya Kernel Limited Company of Tanzania, imenunua deni la kampuni ya Marubeni Corporation ya Japan.

Watuhumiwa wote watatu walipelekwa mahabusu baada ya kushindwa kutekeleza masharti ya dhamana ambayo yalihusisha kuweka kiasi cha fedha ambacho ni nusu ya kiasi wanachodaiwa kuibaau kutoa hati za mali zisizohamishika zenye thamani hiyo.

Watuhumiwa hao wanatetewa na wakili maarufu, Majura Magafu, ambaye anawatetea pia watuhumiwa wengine wawili wanaokabiliwa na kesi za EPA. Kesi hizo zitatajwa tena Novemba 21.

Watuhumiwa wengine walioshitakiwa kwa makosa hayo wafanyabiashara na watumishi wa BoT.

NEWS UPDATE: Nyaulawa kuzikwa Alhamisi

Mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa, utaagwa Jumatatno jijini Dar es Salaam na kusafirishwa siku ya Alhamisi kwa ndege mbili za kukodi. Ukiwasili jijini Mbeya, mwili huo utapelekwa kijijini kwa marehemu, Inyara, ambako mazishi yatafanyika siku hiyohiyo.
Msemajiw a familia, Aga Mbughuni, amesema marehemu alipelekwa nchini India kwa ajili ya matibabu ya saratani ya ini mwezi Julai mwaka huu na alirejea nyumbani wiki iliyopita.
Marehemu amecha mjane, watoto wanne na wajukuu wanne.
Nyaulawa anakuwa ni Mbunge wa sita kufariki katika Bunge hili. Wabunge wengine waliofariki ni aliyekuwa Mbunge wa Tunduru, Juma Akukweti, ambaye alifariki nchini Afrika Kusini, alikopelekwa kwa ajili ya matibabu baada ya kupata ajali ya ndege jijini Mbeya.
Wengine ni wabunge wa viti maalum, Amina Chifupa na salome Mbatia. Chifupa alifariki kwa maradhi na Mbatia katika ajali ya gari.
Baadaye alifariki Benedict Losurutia (Kiteto) kutokana na maradhi na wa mwisho kufariki kabla ya Nyaulawa ni Chacha Wangwe (Chadema-tarime) aliyefariki kwa ajali ya gari katika eneo la Pandambili mkoani Dodoma.

Sunday, November 9, 2008

Nyaulawa afariki

Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa, amefariki dunia. Kifo cha Mbunge huyo kimethibitishwa na Spika wa Bunge, Samuel Sitta.
Nyaulawa amefariki dunia kutokana na ugonjwa wa kansa ya utumbo uliokuwa unamsumbua kwa muda mrefu.
Wakati fulani alipelekwa nchini India kwa matibabu lakini tangu aliporejea hali yake hakurudia kuwa ya kawaida. Kutokana na hali hiyo, uamuzi ulifikiwa kuwa arudishwe tena India kwa matibabu lakini kabla uamuzi huo haujatekelezwa Mungu ameamua kumchukua.
Fikra Jadidi inamuombea marehemu Nyaulawa apumzike mahali pema peponi na tutaendelea kumkumbuka kwa kazi zake njema alizozifanya duniani, Amen

Friday, November 7, 2008

NEWS UPDATE: Kesi za EPA Kisutu

Taarifa za hivi punde kutoka Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu zinapasha kuwa wafanyakazi wanne wa BOT wamepandishwa kizimbani kujibu mashtaka yanayohusiana na wizi wa pesa za EPA wa zaidi ya shilingi bilioni 207 mali ya BOT.
Waliopandishwa kzizimbani ni:
1. Bi. Esther Komu, ambaye ni Kaimu mkurugenzi wa Idara ya Madai.
2. Bosco Kimela ambaye ni Kaimu Katibu wa BoT.
3. Imani Mwakyosa, anayetajwa kuwa ni Mwanasheria na
4. Sophia Joseph (kutoka Idara ya Fedha) ambao nyadhifa zao tunaendelea kuzitafuta.
Kuna baadhi ambao waliunganishwa katika ksi nyingine zilizofunguliwa jana na juzi na wengine wamesomewa mashitaka mapya peke yao. Bado kesi zinaendelea Kisutu
Wakati hayo yakitokea, taarifa za hivi punde zinapasha kuwa Johnson Lukaza, ambaye alipandishwa mahakamani juzi, amefanikiwa kupata dhamana na ameachiwa

BREAKING NEWS: Neti ya EPA yatanuka

Neti inayowadaka watu wanaotuhumiwa kujipatia fedha kwa njia za ulaghai na wizi kutoka akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) imetanuka na kudaka wanne zaidi leo.
Habari kutoka Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu zinapasha kuwa watumishi wanne wa benki Kuu, ambayo ndiko akaunti hiyo ilikuwepo wakati bilioni 133 zilipochotwa na wajanja, wametinga mahakamani hapo.
kama wengine walioshitakiwa juzi na jana, watumishi hao nao wanashitajkiwa kwa makosa ya wizi wa fedha za EPA. Zikipatikana habari zaidi tutaendelea kuziweka hapa, endelea kutembelea.

Thursday, November 6, 2008

Serikali yaanza kuikana TRL

Serikali imeaonyesha dalili za kuitosa Kampuni ya Reli nchini (TRL). Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akizungumza Bungeni wakati akijibu maswali ya papo kwa papo leo, ameitaka kampuni hiyo kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa mkataba ulioingia.
Alisema kuwa si wajibu wa serikali kutoa fedha kila mara kampuni hiyo inapopatwa na matatizo. Serikali imewahi kutoa fedha mara mbili kulipia mishahara ya wafanyakazi wa kampuni hiyo, ambao walitishia kugoma baada ya mwajiri wao kushindwa kuwalipa nyongeza za mishahara kama walivyokubaliana.
Aidha, Pinda amesema yanayojitokeza hivi sasa ndani ya TRL ni funzo kubwa kwa serikali, ambayo inatakiwa kuwa makini wakati mwingine itajkapokuwa inatafuta mwekezaji.
Maneno hayo ya Pinda yanadhihirisha kiburi cha serikali, ambayo licha ya kuonywa wakati wa mchakato wa kumpata mwekezaji ambaye ni kampuni ya RITES kutoka India, ilikataa kusikiliza ushauri.
Matokeo yake, mwekezaji huyo ameshindwa kukifanya kile ambacho watumiaji wa reli hiyo walikitarajia kutokana na ahadi zake na serikali yenyewe, ambayo ilitamba kuwa imempata mwekezaji makini atakayelifufua lililokuwa Shirika la Reli nchini (TRC).
Tangu mwekezaji huyo alingie nchini, TRL imekuwa ikikumbwa na migogoro ya kazi mara kwa mara na hali ya usaifiri imezorota sana. Mara baada ya kuingia, mwekezaji alifunga baadhi ya njia (kama ile ya Tanga) na kuzusha malalamiko kutoka kwa wadau ambao walisema kuwa matarajio yao ni kuona mwekezaji akifufua na si kufunga reli.

Makazi Mapya

Napenda kuwataarifu wapenzi kuwa nimeacha kazi Freemedia Limited tangu jana. Kuanzia leo nimeanza kazi hapa Mwananchi Communications Limited. Hapa nimeajiriwa kama News Editor wa The Citizen.

Wednesday, November 5, 2008

BREAKING NEWS: Jeetu patel Mahakamani

Taarifa kutoka Mahakama ya Kisutu ni kuwa Jeetu patel, na watu wengine saba wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na kesi mbili zenye mashitaka ya wizi na kughushi.
Dhamana katika kesi hizo zote mbili ziko wazi lakini hakimu amesema kwa kuwa muda ulikuwa umeisha, uamuzi kuhusu dhamana atautoa kesho. Hivyo, watuhumiwa wote wamepelekwa Segerea kupumzika.
Tinafanya jitihada za kupata hati ya mashitaka ili tuiweke hapa

BREAKING NEWS: Mafisadi Kisutu

Kuna taarifa kuwa watu kadhaa, akiwamo Jeetu Patel, wamefikishwa katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, wakikabiliwa na kesi inayohusiana na ufisadi. Habari kamili baadaye

Tuesday, November 4, 2008

Umafia waingia nchini?

Katika kile kinachoweza kuelezewa kama aina fulani ya kuchafuana, watu kadhaa, walikubali kupoeka fedha kutoka kwa mfanyabiashara Yusuf Manji kwa ajili ya kuandaa kampeni za kumchafua mfanyabishara hasimu wake, Reginald mengi.
Lakini, Mengi inaelekea alikuwa na 'inteligence' ya nguvu kwani aliweza kupenyeza watu wake katika kikao cha timu hiyo na kufanikiwa kupata picha za video za mkutano huo na sehemu kubwa ya majadiliano.
Mkanda huo wa video ulionyeshwa katika kituo cha ITV kuanzia jana jioni na taarifa hiyo kurudiwa leo asubuhi.
Katika kampeni hizo, watu hao walikuwa wakipanga kueneza taarifa kuwa Mengi, ameamua kutumia fedha zake, kupiga vita utawala wa Rais Jakaya Kikwete. Inadaiwa kuwa lengo la uzushi huo ni kumgombanisha Mengi ya rais Kikwete.
Kuna taarifa pia kuwa Mengi amefikisha nakala ya mkanda huo kwa Rais.

Monday, November 3, 2008

Mbwa aliyeuawa Tarime aibukia Bungeni

Wabunge wawili, Ibrahim Sanya (Mji Mkongwe-CUF) na Susan Lyimo (Viti Maalum-Chadema) wamehoji bungeni kuhusiana na mbwa aliyeuawa huko Tarime wakati wa kampeni.
Wakichangia muswada wa hali bora za wanyama uliowasilishwa leo asubuhi na John Magufuli (Waziri wa Uvuvi), wabunge hao walitaka kujua hatua zilizochukuliwa dhidi ya watu waliosika na tukio hilo.
Kwa upande wake, Sanya alisema kuwa kitendo cha kumvika mbwa huyo bendera ya CCM ni ujinga. Lakini aliongeza kuwa mtu aliyemuua mbwa huyo kutokana na kuvikwa bendera hiyo, ni mjinga mkubwa zaidi.
Suzan Lyimo, yeye ameitaka serikali kutoa mawelezo ya kina kuhusiana na tukio hilo.
Lakini wakati akihitimisha mjadala wa muswada huo, Magufuli alikataa kulizungumzia suala hilo kwa undani kwa maelezo kuwa hivi sasa hajui iwapo ilifunguliwa kesi mahakamani kuhusiana na tukio hilo au la.